Dowans: Another Richmond in making?

Who are these shameless, merciless bloodthirst criminals behind these bogus Companies? I will cast the first stone....
 
Mkataba wa Richmond wafutwa
Mwandishi Wetu
Daily News; Tuesday,July 01, 2008 @00:01

Ni baada ya ushauri wa kisheria
Tanesco yasema haukuwa halali

SERIKALI imefuta mkataba kati yake na kampuni ya kutoa huduma ya umeme ya Dowans Tanzania Ltd kuanzia Agosti mosi mwaka huu. Hatua hiyo imechukuliwa baada ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kupata ushauri wa kisheria kwamba mkataba kati ya shirika hilo na Kampuni ya Richmond ambayo mkataba wake ulihamishiwa Dowans, haukuwa halali wala haukuwa na nguvu kisheria.


Kama mkataba haukuwa halali kwa nini isiwe immediate contract termination...kwa nini mpaka agosti mosi?
je wanaendelea kulipwa mapaka siku hiyo?



Dk. Rashid alisema kutokana na mkataba kati ya Richmond na Tanesco kuwa na utata, shirika hilo liliajiri kampuni ya sheria kutoa ushauri wa uhalali wa utaratibu mzima wa mkataba huo. Hakuitaja kampuni gani. Alisema kampuni hiyo ilibaini kuwa utaratibu mzima wa ununuzi wa huduma hiyo ya umeme na kuingia mkataba na Richmond Development Company LLC, ulikiuka sheria ya ununuzi namba 21 ya 2004.

Siri siri again and again

Kutokana na mapendekezo ya ripoti hiyo, serikali iliahidi kuyafanyia kazi mapendekezo ya ripoti hiyo, na juzi Waziri Mkuu Mizengo Pinda, aliahidi kuwa yuko tayari kutoa taarifa ya serikali kuhusu ilivyofanyia kazi mapendekezo ya Bunge.

Tusikate mbeleko kabla mtoto hajazaliwa...nina wasiwasi na Mzee Mizengwe (m)Pinda(shaji)...kama atakuja na concrete taarifa
 
Mkataba unaisha 30 july 08 ...je wataendelea kulipwa mpaka tarehe hio?....kwa nini wasivunje mkataba palepale kama imejulikana ni batili?...je fedha walizochukua wanazirudisha?...isiwe tunazugwa hapa...

...hivi hakuna media TZ kumbana huyu Idrissa Rashid ili kumwaibisha maana wanaona sisi ni wajiiinga sana ...wamwambie wazi wazi mkataba unaisha 30 July kwa hiyo story za kuvunjwa 1st Agost ni mkataba gani anaongelea hapo...kazi kweli kweli yaani mafisadi yamejisahau mpaka hawajui wanaongea nini? lingine kule limekurupuka na kusema EPA sio pesa za serikali,tuna wendawazimu watupu pale,dawa ni kuwaonyesha njia 2010
 
huu sasa wizi.... yaani wameajiri kampuni ya sheria kuwashauri kwa mambo ambayo tumeyaandika magazetini? Nadhani it is about time watugawie hiyo fee waliyowalipa hao jamaa.

Tangu siku ya kwanza tuliwaambia mkataba wa Dowans hauna msingi wa sheria na tukasema ni kwanini kweli wanaenda kuajiri mtu mwingine kuwaambia kitu ambacho kiko dhahiri?

Hii inaudhi kweli!!

I'm kinda of disillusioned with the way my country is ruled, hivi tutafika kweli?
 
Ama Kweli Uungwana Ni Vitendo.
Yani sasa nchi ni kama hata haina Rais.
Na mwenyewe sasa yuko wapi?
Hao mambo ya ZIMBABWE SI YASHAISHA?
VIPI KUHUSU ZILE HOTUBA ZAKE SIJUI NI ZA KILA MWISHO WA MWEZI?
SALVA NAYE MBONA KIMYA?
MBONA HAKUNA ANAYEKAMATWA?
KUNA WANAOSUBIRIWA WAFE?
 
Kama mkataba haukuwa halali kwa nini isiwe immediate contract termination...kwa nini mpaka agosti mosi?
je wanaendelea kulipwa mapaka siku hiyo?

Mimi nilisoma hicho kitu nika kaa chini.

Mimi nilidhani watasema hivi, waturudishie pesa zetu toka day one. Si mkataba haukuwa halali, au?

Mi nadhani kuna usanii hapa.

Ukisoma vizuri taarifa zote mbili - tena Bubu amekuwa very trenchant kuweka taarifa ya Habari Leo na ya Daily News - ukisoma ile ya Kiingereza inasema Serikali imekubali pendekezo la Tanesco kufuta Mkataba. Hawa wanasikilizia pumzi ya Dowans. Hawana uhakika. Remember Pinda alisema eti ni vigumu kufuta mikataba, mpaka waende mahakamani, blah blah blah.

Kwa hiyo inawezekana Serikali ina testi zali tu.
 
Unajua nini, angalau safari hii wameajiri law firm ya Kibongo. Huwa nachukia sana ma contract wakipewa wageni.

kama ni hivyo, mbona wameshindwa kuitaja?........

Originally Posted by Bubu ataka kusema
Dk. Rashid alisema kutokana na mkataba kati ya Richmond na Tanesco kuwa na utata, shirika hilo liliajiri kampuni ya sheria kutoa ushauri wa uhalali wa utaratibu mzima wa mkataba huo. Hakuitaja kampuni gani. Alisema kampuni hiyo ilibaini kuwa utaratibu mzima wa ununuzi wa huduma hiyo ya umeme na kuingia mkataba na Richmond Development Company LLC, ulikiuka sheria ya ununuzi namba 21 ya 2004.

But then again ndio unakuta ma law firm hayo hayo ya Wabunge wa CCM.

Yale yale!

Labda ndio maana wanaficha kuitaja?
 
.....kuna mtu aliwahi kuniambia thamani ya magari ya wakurugenzi,mameneja na ofisi za TANESCO yana thamani kuliko mitambo ya kuzalisha umeme!
 
...hivi hakuna media TZ kumbana huyu Idrissa Rashid ili kumwaibisha maana wanaona sisi ni wajiiinga sana ...wamwambie wazi wazi mkataba unaisha 30 July kwa hiyo story za kuvunjwa 1st Agost ni mkataba gani anaongelea hapo...kazi kweli kweli yaani mafisadi yamejisahau mpaka hawajui wanaongea nini? lingine kule limekurupuka na kusema EPA sio pesa za serikali,tuna wendawazimu watupu pale,dawa ni kuwaonyesha njia 2010

Media itoke wapi Bongo.

Mkataba usio halali unatakiwa uishe siku uliposemekana umeanza.

Tuwadai Dowans waturudishie hela yetu.
 
huu sasa wizi.... yaani wameajiri kampuni ya sheria kuwashauri kwa mambo ambayo tumeyaandika magazetini? Nadhani it is about time watugawie hiyo fee waliyowalipa hao jamaa.

Tangu siku ya kwanza tuliwaambia mkataba wa Dowans hauna msingi wa sheria na tukasema ni kwanini kweli wanaenda kuajiri mtu mwingine kuwaambia kitu ambacho kiko dhahiri?

Hii inaudhi kweli!!
Mkuu I feel you!

Nilitaka kuandika the same sentiments...kuwa walikuwa na guts za kuajiri 'kajikamati' ka sheria kuangalia suala lile lile ambalo lilishasemwa kuwa ni batili

kwani Mwakyembe si mwanasheria na ndo maana akawa mwenyekiti wa ile kamati? wanadicredit taaluma yake!
 
Who are these shameless, merciless bloodthirst criminals behind these bogus Companies? I will cast the first stone....

...hii yote ni kwa sababu tuna Raisi ambaye ni mtupu kichwani,huyu jamaa ametucost sana na huu upuuzi wao tutaulipia for the next 50 yrs!
 
Watafuta vipi mkataba ambao ume-expire? kama mkataba ulikuwa wa miaka miwili tangu June 2006 si miaka miwili imetimia, kama walikuwa na kiburi cha kuufuta mkataba mbona wasiufute mwezi wa pili wakati akina Lowassa wamejiuzuru?
 
Mara nyingi Kampuni za kihuni uwa wanaanzisha hizo kampuni kwenye nchi ambako hakuna sheria na kama zipo basi hazina nguvu sana,

1)kwa kukwepa kodi kwenye nchi zao
2)Money Laundering (kama Meremeta),
3)Kukwepa legal system kwenye nchi ambazo wanafanya biashara mfano kampuni za Madini (Geita, Kahama) hapo Tanzania utakuta zote ziko registered (kwenye visiwa vya Bermuda na siyo Canada) kwa maana wanaogopa sheria za nchi zao kama Canada or USA, kama mambo yakienda vibaya wao utimuka mara moja uwezi jua wako wapi. Huko Bermuda utakuta kuna kiofisi cha chumba kimoja na makaratasi tu ambazo zote uwa na anwani ya P.O.BOX na siyo physical address.
 
...hii yote ni kwa sababu tuna Raisi ambaye ni mtupu kichwani,huyu jamaa ametucost sana na huu upuuzi wao tutaulipia for the next 50 yrs!

Mwanakijiji, Koba,

Dowans ilikuwa ni kama gari la zimamoto la JIJI linalojikuta halina maji baada ya kufika kwenye tukio. Moto huo sasa unaenea kwa kasi ya ajabu pamoja na juhudi kubwa za kutaka kuuzima kwa kuumwagia mchanga.
 
huu sasa wizi.... yaani wameajiri kampuni ya sheria kuwashauri kwa mambo ambayo tumeyaandika magazetini? Nadhani it is about time watugawie hiyo fee waliyowalipa hao jamaa.

Tangu siku ya kwanza tuliwaambia mkataba wa Dowans hauna msingi wa sheria na tukasema ni kwanini kweli wanaenda kuajiri mtu mwingine kuwaambia kitu ambacho kiko dhahiri?

Hii inaudhi kweli!!

... watugawie hiyo fee ... kwi kwi kwi wao wanakuona wewe mchokozi na kwamba ulia-access classified documents halafu wakufikirie kukupongeza? Kazi buti Mzee, wanao toa jasho hawali.
 
na waziri Ngeleja kadhibitisha ulikuwa ni mkataba batili na wanatakiwa waondoe mitambo yao ifikapo agust mosi.Hongera kamati ya Mwakyembe

Na wahusika wanasafishwa bungeni na kwenye vikao vya Chama cha Mapinduzi
 
kampuni iliyoanzishwa kwa mtaji wa dola 100 ikapewa mkataba wa kuleta umeme kwa nchi ya watu milioni 40? Kwa dola mia moja unaweza kunua hata kompyuta ya ofisi?
 
Why all this long? au ndo washakula wameshiba sasa wananawa mikono? Kwa maana hii pamoja na kazi nzuri ya Mwakyembe na Kamati yake bado serekali inauona mkataba wa mwanzo wa Richmond ulikuwa safi lakini ufeki umekuja pale ulipohamishiwa Dowans?- This is a joke an astonishing waste of taxpayers money, kama ni hela kurudishwa zirudishwe zote kwa kuwa mikataba yote ilikuwa feki. Na what will it take kwa mwanasheria mkuu kujiuzulu kama sio serekali kumuwajibisha? serekali ikiingizwa mkenge ina maana yeye hafanyi kazi yake kwa makini so he has got to go too.
 
Hivi jamani huyu Ngeleja si alikuwa wizara hii hii (wakati wa kusaini mkataba)!! sasa nini tena leo anasema "wamegundua" mkataba ulikuwa "fake", jamani huyu Ngeleja si ni yule mtaalamu wa masuala ya sheria!? Jamani hii imekaaje!

Mi binafsi sikubaliani na maelezo mepesi namna hii, ninachotaka bunge litengue kile kipengele cha sheria kisha mjadala ya Richmond urudiwe tena kujadiliwa!! Mpaka mchawi apatikane!!

Think Big unachokisema ni kweli.

Hapa kinachoendelea ni kama mwanamazingaombwe akifanya mavituzz yake jukwaani wakati watazamaji wote wakiwa wameshikilia ndimu.... Tunamwona waziwazi ndugu ngeleja akituletea hadithi ambazo hakupaswa kuja kutuhadithia leo kama angeifanya kazi yake vizuri miezi kadhaa iliyopita.
 
Back
Top Bottom