(Docs): Siri ya Kesi ya Mahalu: Ununuzi wa Jengo la Ubalozi Italia

Nimepitia attachments zilizowasilishwa, nyingi ni communication za kawaida kiofisi juu ya jambo hilo. Inaonekana wahusika ni wengi na walijulishwa kuwa bei halisi ni euro 3,098,741.40. Lakini attachment ya 10 'to chief secretary' ndiyo inashtua. Inaonekana kuwepo kwa mikataba miwili mmoja wa official price ya euro 1,032,913.80 na real price ya euro 3,098,741.40. Maana yake kuna bei iliyoonyeshwa rasmi kule italy (official price) na bei iliyoonyeshwa huku TZ (real price); ipi ni halali?
Hapa ndipo serikali ya italy ilipostuka, inaonekana muuzaji alienda kulipa kodi ya serikali ya italy kwa kutumia official price; na baadae (hata kupitia hansard za bunge) ikajulikana kuwa jamaa aliuza kwa real price na hivyo kukwepa kodi. Serikali ya TZ iliafiki ukwepaji huo na ndipo italy walipoibana serikali ya tz kumchukulia hatua Mahalu vinginevyo wao wataichukulia hatua serikali kwa kusaidia ukwepaji kodi. Sakata lilianzia hapo.
Martin Lumbanga baada ya kupewa kimaandishi mikataba miwili tofauti alichukua hatua gani? Kumbuka huyu alikuwa katibu mkuu kiongozi yaani ofisi ya rais wakati huo Mkapa.
Mkapa anaposema mahakamani kuwa hajui kitu hicho cha mabilioni ya pesa wakati katibu wake mkuu alijulishwa, tumweleweje? Nakumbuka kulikuwa na mjadala mkali sana bungeni juu suala hili - ni kwanini Mkapa hakustuka na kumuuliza katibu mkuu wake? au waziri wa mambo ya nje? Nadhani watu wanajaribu kufichiana siri!
Pia ukijikumbusha ushahidi uliokwisha tolewa ofisa wa italy (legal counsel father Marco Papi) anasema alisaini mkataba mmoja tu wa euro 1,032,913.80, (na siyo mikataba miwili) soma hapa: ZoomInfo Cached Page
 
Kwa wsaioweza kufungua hiyo zoominfo cached page: Mjadala mahakamani ulikuwa kama ufuatavyo:
Italian priest testifies against Mahalu

2008-03-15 09:36:28
By Rosemary Mirondo

A legal counsel from Italy, Father Marco Papi, yesterday testified against immediate former Tanzanian ambassador to Italy, Costa Mahalu, in a corruption case he faces alongside former counsellor Grace Alfred Martin.

Papi told the Kisutu Resident Magistrate`s Court in Dar es Salaam that he signed only one contract worth euros 1, 032,913.80 between Prof.

Mahalu and the seller of the building that was acquired by the Tanzanian ambassador in Italy.

Prof Mahalu and Grace Martin are accused of occasioning the government of Tanzania a loss of euros 2, 065, 827.20.

He told the court that because the agreement of sale involved an individual person and a government, they had to seek authority from Tanzania through the Minister for Foreign Affairs and International Cooperation so as to make the contract legally binding.

There was a heated exchange between the prosecution led by an officer from the Prevention and Combating or Corruption Bureau, Tabu Mzee, and State Attorney Ponziano Lukosi and the defence led by counsel Alex Mgongolwa, Mabere Marando and Cuthbert Tenga over the admission of an interpreter.

Tabu: We have one witness from Italy but he can speak neither English nor Kiswahili, so we have brought an interpreter.

Marando: We submit that according to law, an interpreter is for the court and not the prosecution, and anyway, they should tell us how they got him.
Court: Prosecution.

Tabu: The defence alleged that an interpreter is supposed to be brought by the court, but even the witness is for the court and the interpreter is trustworthy because he is a Catholic priest.

Court: So what is your position Marando?
Marando: If the prosecution knew that they were bringing a witness who could not understand either of our official languages, they should have informed the court instead of bringing the interpreter on their own, because the court has to satisfy itself that he is not biased.

Due to that, we pray for two things - a short adjournment of the case so that the court can talk with the interpreter and understand his position here in court or the court can satisfy itself by interrogating him.

This is because the defence wants an interpreter who understands the seriousness of the case and not to interpret what the court wants.

Court: But the prosecution told me that they were bringing an interpreter and I allowed them to do so, but if you have doubts

Marando: I was not aware that you had given the go ahead.
Court: But you also have the privilege to decide.
Marando: Some of us don
�t trust anyone, even priests (laughter)

Court: Please can we continue? My ruling is: the interpreter was brought by the prosecution after they had consulted me. In this case, I reject the objection raised by the defence.

Court: Prosecution, please bring your interpreter because I have faith in him.

The interpreter is brought forward and says he is a priest of the Roman Catholic Church.

Tabu: Witness, please tell us your name.
Witness: Marco Papi.

Tabu: Witness, can you please tell the court where you are from and your position there?

Witness: From Italy and I am a notary public.
Tabu: What are your duties?

Witness: I go through all the contracts and register them so that they can be legally binding.

Tabu: Do you know the accused in this case?
Witness: I know the former Tanzanian ambassador to Italy, Ricky Mahalu, because he came to my office.

Court: You say that he came to your office to do what?
Witness: To sign a contract.
Tabu: What contract?

Witness: A contract between Cheres Company under Froeella Pagliuca and Mahalu on behalf of the government of Tanzania. It was concluded after I had signed on it.

Tabu: What did the contract contain?
Witness: Property that was being transferred from Cheres to the embassy of Tanzania in Italy.
Court: What property is that?

Witness: According to laws of ownership, it was a house that is now the embassy of Tanzania in Italy.
Tabu: According to that contract, how much was the house sold for?

Witness: As a notary public, I normally don
�t know the prices. I only know the procedures of obtaining the contract.

Tabu: If you see the contract will you know it?
Witness: The contracts that I go through are many, so it is hard to remember all of them.

Tabu: Is this the contract?

The contract is given to the witness. He goes through it.
Witness: Yes, this is the one, because it bears my signature and my firm`s stamp. I also remember the cost of the house was euros 1, 032,913.80 as indicated in this contract.

The hearing, which started on February 27, this year, will continue again on April 13.


  • SOURCE: Guardian
 
Duhh JF ni balaa. I real appreciate kwa uzi huu. Hakuna kinachoshindikana JF. Big up Great Thinkers
 
Mleta mada ni muongo wa kutupwa jalalani, unaijuwa wewe Euro billioni au unajiandikia tu? Hata barua ulizoweka zinaonesha Euro "million" na si "billion" kama unavyozuwa? unanini weye?

2: Kwamba Balozi Mahalu alikataa kushiriki katika njama za kuiba pesa ya Watanzania Euro billioni 2.4 kwani katika tathmini iliyofanywa na Wizara ya Ujenzi kuhusu Jengo la Ubalozi, bei ya Jengo hilo lingegharimu Euro billioni 5.5 na siyo Euro billioni 3.1 bei ambayo ndio bei ya Jengo iliyokubaliwa chini ya usimamizi wa Balozi katika mchakato wa ununuzi.

Hii ni billion moja tu, diplomatic begi lipi itabeba hizi? wacha kudanganya watu:

And $1 BILLION dollars... now we're really getting somewhere...
pallet_x_10.jpg

 
That is very cheap and no body is prepared to stoop too low ans succumb to your propaganda. The guy has been found to have a case to answer in court and he has been tinkering from one court to another, thinking that he would get a reprieve but to no avail. This is a simple case of theft without any element of religion as you want people to believe. Does this explain or justify why a professor of law had to prepare two sets of contract in respect of the same subject matter and what would be the motive? The Seller has testified and stated in no uncertain terms that the price in one of the contracts was unduly inflated. The evidecne has found that the professor stashed some funds, believed to be proceeds of this illegal business in an account in Monaco or some where in Europe. If you thought people here are so stupid as to suport what you are saying then try somewhere else not in this country where people have all the details at finger tips. You can find another way of diverting attention but using religion as an impediment to a fight against impunity will never be acceptable.


100% YOU ARE SENT TO THIS, YOU ARE THIS, be either part of...
 
Ukweli ****** anajulikana kwa visasi??? Kila ambaye amefanya naye kazi kwa karibu anajua hili bila kupinga. Na kama contract hela ni ndogo inaelekea ni deal kati ya aliyeuza ili asilipe kodi kubwa na seriakali ikalipa hizo over 3 billion. Kama ni hivyo serikali yetu inakubali uongo so hakuna good governance. Na ili ifanyike hivyo ni lazima Mahalu alishirikisha viongozi waandamizi wa serikali yetu na ndiyo maana ile contract iko ikulu!!!! Na pia mahalu ni mkatoliki wa uhakika na jamaa na wakristu ni paka na mbwa (msinishambulie ndivyo alivyo) maana kuna mambo mengine ya siri kuwa kwa issues za vetting kama ni watu watatu basi wawili wawe ni waislam. Kwa ajira siku hizi pia inatekelezwa!!!! usishangae ndo mambo yalivyo!!! But ushahidi wa jana wa mheshimiwa B.W Mkapa una nguvu? Alijibu to the extent that prosecution waliduwaaaa!!!! Tusubiri hakimu, ni nani zaidi JK au Mkapa? Match kali ya Man u na Real Madrid!!!
 
Jamani mbona sielewi kinachoendela hapa..

Naposoma hapo juu Kamakabuzi #102 kilitokea mahakamani inaonyesha kwamba contract ya ununuzi wa nyumba hiyo ya Ubalozi inaonyesha Euro 1,032,913.80 na hivyo madai ni kwamba serikali imepoteza kiasi cha Euro 2,065,827.20, na ukizijumlisha hizi pamoja inakuja 3, 098,741.00, Gharama ambayo tunaiona ktk nyaraka nyingi za Mahalu kuonyesha kwamba ndio iikuwa gharama ya jengo kumbe zilizolipwa haswa kwa mwenye nyumba ni 1,032,913.80.

Haya nikirudi kwa mleta mada anaonyesha barua zinazodhirisha gharama ya nyuma ile ilikuwa euro 3.1 mil, na kwamba serikali ilitaka kununua kwa euro 5.5 mil lakini sioni nyaraka yoyote inayoonyesha serikali kupendekeza wala kukubali kununua jengo lile kwa bei ya 5.5. Hivyo pengine wenzetu mnaielewa vizuri kesi hii lakini kutokana na kesi hii navyoisoma sioni mahala wanazungumzia hizo 5.5 isipokuwa hiyo 3.1 yenyewe ni kubwa kuliko bei alolipwa mwenye nyumba.

Naomba mwelekezo..
 
RAIS mstaafu, Benjamin Mkapa, jana aliikaanga serikali ya Jakaya Kikwete mahakamani akidai kuwa hakuna ubadhirifu wowote uliofanywa na aliyekuwa Balozi wa Italia, Prof. Costa Mahalu, katika ununuzi wa jengo la ubalozi nchini humo. Akiongozwa na wakili wa utetezi, Alex Mgongolwa, baada ya kuapa alieleza kuwa kati ya mwaka 1995-2005 akiwa Rais alifahamu ununuzi wa jengo la ubalozi nchini Italia kwa euro 3,098,741.40, na kuwa hata aliyekuwa Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambaye ni Rais wa sasa, Jakaya Kikwete alikubaliana na ununuzi huo. Mkapa ambaye ni shahidi wa Mahalu katika kesi hiyo alisema mwaka 2003 yeye ndiye aliyekwenda mjini Rome-Italia kulizindua jengo hilo la kisasa, Profesa Mahalu akiwa balozi. “Serikali yangu iliarifiwa bei na taratibu za kulinunua na mimi kama Rais wa nchi nilitaarifiwa kuwa muuzaji alitaka malipo yafanywe mara mbili tofauti katika akanti zake …na mimi kwa niaba ya serikali yangu nikatoa idhini linunuliwe kwa mtindo huo nilioutaja hapo juu,” alidai Rais Mkapa. Mahalu anatuhumiwa kuidhinisha kwa niaba ya serikali ununua wa jengo la ubalozi kwa thamani ya euro milioni 3 kwa njia ya mikataba miwili na kwa akaunti mbili. Mawakili: Wewe au serikali ya awamu ya tatu iliwahi kupokea malalamiko toka serikali ya Italia kuwa ubalozi wetu nchini humo ulivunja sheria kuhusu mchakato mzima wa ununuzi wa jengo hilo? Mkapa: Hapana, sijawahi kupokea malalamiko. Mawakili: Ukiwa Rais hujawahi kupokea malalamiko kuwa fedha za serikali yetu zilizotumwa kwa ajili ya kumlipa muuzaji wa jengo hilo kuwa hazijamfikia? Mkapa: Hadi leo hii natoa ushahidi hapa mahakamani sijawahi kupokea malalamiko ya aina hiyo. Mawakili: Uliwahi kupata malalamiko toka kwa CAG, Wizara ya Mambo ya Nje, Katibu Mkuu Kiongozi, Waziri wa Mambo ya Nje, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wala Ofisi ya DPP kuhusu ubadhirifu wa ununuzi wa jengo hilo? KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPA NA HIKI NDICHO ALICHOKISEMA MKAPA NDANI YA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU JANAGUMZO LA JIJI
 
Mleta mada ni muongo wa kutupwa jalalani, unaijuwa wewe Euro billioni au unajiandikia tu? Hata barua ulizoweka zinaonesha Euro "million" na si "billion" kama unavyozuwa? unanini weye?



Hii ni billion moja tu, diplomatic begi lipi itabeba hizi? wacha kudanganya watu:

And $1 BILLION dollars... now we're really getting somewhere...
pallet_x_10.jpg

Mimi naona kawaida ya wabongo ni kuingizwa mjini kila siku, hivi kweli hilo bag la diplomatic lingeweza vipi beba kama serikali ingetaka ziletwe kwa ajili ya campain walishindwa vipi kufanya utaratibu wa Kibenk ambao unajulikana ni salama na ndivyo utaratibu wa kubeba fedha nyingi hutokana au fedha hizo zilikuwa za Unga? na zilikuwa wapi fedha hizo.. Ama kweli wadanganyika tuna safari ndefu sana..
 
Inavyoelekea JK alikuwa anarukwa katika mawasiliano ndiyo sababu akaamua kumshikisha Prof. adabu!

Yawezekana akafikiri anamshikisha adabu lakini mwisho wa siku akajitia kitanzini kwa mwenendo wa kesi na kwa upepo ulivyo Tanzania itafika mahali urais usiwe kigezo cha kutoshtakiwa.
 
RAIS mstaafu, Benjamin Mkapa, jana aliikaanga serikali ya Jakaya Kikwete mahakamani akidai kuwa hakuna ubadhirifu wowote uliofanywa na aliyekuwa Balozi wa Italia, Prof. Costa Mahalu, katika ununuzi wa jengo la ubalozi nchini humo. Akiongozwa na wakili wa utetezi, Alex Mgongolwa, baada ya kuapa alieleza kuwa kati ya mwaka 1995-2005 akiwa Rais alifahamu ununuzi wa jengo la ubalozi nchini Italia kwa euro 3,098,741.40, na kuwa hata aliyekuwa Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambaye ni Rais wa sasa, Jakaya Kikwete alikubaliana na ununuzi huo. Mkapa ambaye ni shahidi wa Mahalu katika kesi hiyo alisema mwaka 2003 yeye ndiye aliyekwenda mjini Rome-Italia kulizindua jengo hilo la kisasa, Profesa Mahalu akiwa balozi. “Serikali yangu iliarifiwa bei na taratibu za kulinunua na mimi kama Rais wa nchi nilitaarifiwa kuwa muuzaji alitaka malipo yafanywe mara mbili tofauti katika akanti zake …na mimi kwa niaba ya serikali yangu nikatoa idhini linunuliwe kwa mtindo huo nilioutaja hapo juu,” alidai Rais Mkapa. Mahalu anatuhumiwa kuidhinisha kwa niaba ya serikali ununua wa jengo la ubalozi kwa thamani ya euro milioni 3 kwa njia ya mikataba miwili na kwa akaunti mbili. Mawakili: Wewe au serikali ya awamu ya tatu iliwahi kupokea malalamiko toka serikali ya Italia kuwa ubalozi wetu nchini humo ulivunja sheria kuhusu mchakato mzima wa ununuzi wa jengo hilo? Mkapa: Hapana, sijawahi kupokea malalamiko. Mawakili: Ukiwa Rais hujawahi kupokea malalamiko kuwa fedha za serikali yetu zilizotumwa kwa ajili ya kumlipa muuzaji wa jengo hilo kuwa hazijamfikia? Mkapa: Hadi leo hii natoa ushahidi hapa mahakamani sijawahi kupokea malalamiko ya aina hiyo. Mawakili: Uliwahi kupata malalamiko toka kwa CAG, Wizara ya Mambo ya Nje, Katibu Mkuu Kiongozi, Waziri wa Mambo ya Nje, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wala Ofisi ya DPP kuhusu ubadhirifu wa ununuzi wa jengo hilo? KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPA NA HIKI NDICHO ALICHOKISEMA MKAPA NDANI YA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU JANAGUMZO LA JIJI
Mkuu wangu soma vizuri utaona Mkapa mwenyewe alijikanyaga kanyaga tu.. Aliulizwa kwa nini risiti za ununuzi wa nyumba unaonyesha euro mil tatu wakati Hansard ya Bunge inaonyesha Tsh bil 2.9 naye akajibu ati sio kazi yake kujua thamani ya fedha za kigeni - kama hizo euro million 3 zilikuwa sawa na Tsh sdhilingi ngapi?... Haya majibu kweli? unataka kunambia rais mzima wa nchi yetu alikuwa hajui hata thamani ya Shilingi kwa euro? - Makubwa haya!
 
Kwani kukata mzizi wa fitina si wamlete na muuzaji aseme alipewa shng ngapi.. Nadhani itasaidia mwenendo wa kesi.
 
Jamani mbona sielewi kinachoendela hapa..

Naposoma hapo juu Kamakabuzi #102 kilitokea mahakamani inaonyesha kwamba contract ya ununuzi wa nyumba hiyo ya Ubalozi inaonyesha Euro 1,032,913.80 na hivyo madai ni kwamba serikali imepoteza kiasi cha Euro 2,065,827.20, na ukizijumlisha hizi pamoja inakuja 3, 098,741.00, Gharama ambayo tunaiona ktk nyaraka nyingi za Mahalu kuonyesha kwamba ndio iikuwa gharama ya jengo kumbe zilizolipwa haswa kwa mwenye nyumba ni 1,032,913.80.

Haya nikirudi kwa mleta mada anaonyesha barua zinazodhirisha gharama ya nyuma ile ilikuwa euro 3.1 mil, na kwamba serikali ilitaka kununua kwa euro 5.5 mil lakini sioni nyaraka yoyote inayoonyesha serikali kupendekeza wala kukubali kununua jengo lile kwa bei ya 5.5. Hivyo pengine wenzetu mnaielewa vizuri kesi hii lakini kutokana na kesi hii navyoisoma sioni mahala wanazungumzia hizo 5.5 isipokuwa hiyo 3.1 yenyewe ni kubwa kuliko bei alolipwa mwenye nyumba.

Naomba mwelekezo..

Huyu mleta mada ni mwongo na ana exaggerate kila kitu, Serikali ilifanya tathmini na kuona kuwa jengo hilo lina thamani ya Euro 5.5 wakati wa kulitathmini lakini si kuwa Serikali walitaka linunuliwe kwa bei hiyo. Na tathmini hiyo ndiyo iliyopelekea maamuzi ya kulinunuwa yafanyike.

Kama kuna wajanja wakalipata kwa chini ya 3M sishangai kwani Watanzania wanajulikana kwa wizi. Hakuna cha professor wala lecturer. Halafu anaingiza udini ili apate sympathy ya watu.

Huyu ni simply mwongo!
 
Mkuu wangu soma vizuri utaona MNkapa mwenyewe anajikanyaga.. Aliulizwa kwa nini risiti za ununuzi wa nyumba unaonyesha euro mil tatu wakati Hansard ya Bunge inaonyesha Tsh bil 2.9 naye akajibu ati sio kazi yake kujua thamani ya fedha za kigeni kama hizo euro million 3 zilikuwa sawa na Tsh sdhilingi ngapi?... Haya majibu kweli? unataka kunambia rais mzima wa nchi yetu alikuwa hajui hata thamani ya Shilingi kwa euro? - Makubwa haya!

Hili swali halikuwa appropriate kwa Mkapa, ndiyo maana Mkapa the policy wonk kalipangua kirahisi.

Huwezi kutegemea rais aende kwenye detail level ya kukumbuka exchange rate ya euro to Tanzanian shillings at the time. Actually hili swali hata lingekuwa kwa business ya kawaida tu, CEO yeyote angeweza kusema "I can't give you that off the top of my head" which is perfectly understandable. Ni nani anaweza kukupa exchange rate ya euro to dollar on a specific date ten years ago?

Kitu ambacho mimi nina matatizo nacho hapa ni jinsi Mkapa anavyotetea ma deal makubwa kama haya kufanyika bila "paper trail". Kwamba watu wanapeana ahadi na amri kwa mdomo tu eti kwa sababu ya "usalama wa taifa".

Hili likikubalika lina maana rais anaweza kumpigia simu gavana wa benki kuu akamwambia ahamishe hela kutoka Tanzania's coffers kwenda kwenye a personal Swiss account, in the name of "national security".

Kama Mahalu alikuwa msafi sana kwa nini kakubali amri za mdomo zisizo na "paper trail"?

Hii habari ya kwamba rais au waziri anaweza kutoa amri kwa mdomo katika dili kama hili bila kuhitaji written records iko katika sheria gani?

Mkapa mwenyewe ndiye aliye institutionalize "Usalama wa Taifa", katika sheria ya Usalama wa Taifa ndiyo tuna madudu haya ya rais na waziri kutoa amri kwa mdomo katika procurement process?

CAG ataziona vipi records? Au hizi procurements hazipo subject to CAG?

Usalama wa taifa uliokuwa unaongelewa hapa ni upi? Kukata cha juu cha kampeni za CCM?
 
Hii haimtoi Mahalu kwenye wizi.

Kifupi Mahalu ni Mwizi wa mali ya umma, kaiba na sasa anajitetea. kama si mwizi aweke hapa fedha za akaunti za nje baada ya hayo malipo, tuone kiasi gani kiliingia.

Hachomoki huyo. Akichomoka mahakamani watu wataleta hesabu za akaunti zake, ajieleze Euro zaidi ya million 1.5 alipata wapi?
 
Mkapa.... Basil Mramba... Gray Mgonja..... Ndege ya Rais.... Radar.. Saileshi Vithlani....Majengo ya Balozi 3.... Gavana Balali (RIP if really Dead).. . .BOT Twin Towers..EPA and more is Ufisadi Super Highway!!!!! All in the name of National Security...
 
I am hitting the ground while running.
Ndugu zangu salamu zangu hizi hapa. Hebu someni attachments hizi muone nani mwongo.
Regards

na hii pia:
Re: Yanayozungumzwa Ministry of Foreign and International Affairs (MFAIC) na mitaani kuhusu FITNA zilizofanywa dhidi ya Professor Mahalu na kesi anayokabiliwa nayo mahakamani Tanzania.
1: Kwamba Balozi Mahalu alikataa begi lile la “diplomatic bag” lisitumike katika ubebaji wa PESA toka nchi za Ulaya Mashariki zilizopelekwa Ubalozini Roma ili zisafirishwe kwenda Dar es Salaam kwa ajili ya kampeni ya URAIS ya mwaka 2005.
Inasemekana kwamba Balozi Mahalu alikataa utumiaji huo wa diplomatic bag kwani haukuwa sahihi. Kwa kuzingatia utaratibu na kanuni yeye alikomolewa kwa kufukuzwa kazi

2: Kwamba Balozi Mahalu alikataa kushiriki katika njama za kuiba pesa ya Watanzania Euro billioni 2.4 kwani katika tathmini iliyofanywa na Wizara ya Ujenzi kuhusu Jengo la Ubalozi, bei ya Jengo hilo lingegharimu Euro billioni 5.5 na siyo Euro billioni 3.1 bei ambayo ndio bei ya Jengo iliyokubaliwa chini ya usimamizi wa Balozi katika mchakato wa ununuzi.

Wapo maofisa wa Wizara ya Nje walioshinikiza serikali inunue jingo lile kwa Euro billioni 5.5 kwa kushirikiana na aliyekuwa Honorary Consul, Tanzania Consulate ya Milano, marehemu Avvocato Georgio. Uadui na chuki dhidi ya Balozi Mahalu ulitokana na hilo pia.

3: Kitendo chake cha kuwakirimu Ubalozini Maaskofu wa Kanisa la Katoliki waliotembelea Italia kilionekana kama kurasimisha UKRISTO wa Ubalozi pale Roma. Tuhuma hizi zipo sambamba na kile alichozusha Shehe na Mnajimu mmoja kwamba Balozi Mahalu ni adui wa Uislamu kwani Balozi Mahalu ndiye aliyetayarisha Memorandum of Understanding (MOU) kati ya Serikali na Kanisa ili Taasisi za Kikristo zilizokuwa chini ya Serikali zirudishwe na kuwa chini ya Kanisa kama ilivyokuwa awali.

4: Umiliki wa Balozi Mahalu wa shamba la hekta 500 kandokando ya barabara iendayo Bagamoyo haukumfurahisha aliyekuwa Bosi wake enzi zile kama Waziri wa MFAIC. Sasa hivi shamba lote limemegwa na kuwa sehemu ya EPZ ya Bagamoyo.

5: Kama michezo michafu iliyochezwa kwenye majengo ya Ubalozi wetu Burundi, Khartoum na nchi nyingine, Balozi Mahalu alishitulia NJAMA za kuuzwa kwa jengo la makazi ya Balozi pale Roma. Njama hizi zilibuniwa na maofisa wa MFAIC.

Balozi Mahalu alihakikisha kwamba suala la uuzwaji huo kiholela limefikishwa kwenye vyombo vya sheria kule Italia na kufanikiwa kurudisha umiliki wa hilo jengo kwa serikali ya Tanzania.

Na hapo pia balozi Mahalu alijiongezea MAADUI ambao wamedumu hadi leo.


Kwa hiyo unamnyang'anya adui unampa rafiki! Maan siku zote najiuliza huu upendo kwa 'wawekezaji' mbona unazidi?
 
Back
Top Bottom