Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,338
- 9,766
Ndugu zangu Watanzania,
Dkt Tulia Acksoni Mwansasu amefanya wananchi katika mitaa mbalimbali ya jiji la mbeya kububujikwa na kutokwa na machozi utafikiri watu waliowekewa vitunguu machoni. Hii ni baada ya kumsikiliza dkt Tulia akizungumza kupitia kituo cha CAPITAL RADIO, ambapo katika mazungumzo yake na kituo hicho cha redio amezungumza ya kuwa anatoa bima za afya takribani elfu sita bure kabisaa kwa watu wenye shida na wasio jiweza pamoja na wazee ambao bado hawajaingia na kufikia kukidhi vile vigezo vya kuingizwa katika ule mfumo wa kupata matibabu bure. Lakini pia dkt Tulia kupitia taasisi yake amemjengea mtu mmoja aitwae Hosea nyumba bora kabisa na ya kisasa pamoja na kumnunulia vitu mbalimbali kama vile magodoro pamoja na vitanda kwa ajili ya familia yake.
Dkt Tulia ameeleza ya kuwa ataendelea kuwasaidia bima za afya watu wote wenye mahitaji na wasio jiwezi.ambapo mwaka jana pia alifanya hivi kwa kutoa bima za afya takribani elfu tatu.
Hii maana yake nini ndugu zangu? Hii inamaanisha kuwa dkt Tulia amewapa cash ya mitaji maelfu ya wana mbeya na kuwapatia tabasamu katika mioyo yao.amewapa mitaji kwa kuwa afya ndio mtaji,ndio nguvu ,ndio rasilimali iwezayo kumpatia mtu utajiri mkubwa.maana pasipo afya huwezi kufanya kazi wala kupiga hatua bali utateketeza mali na kila kitu kilicho ndani ya kaya yako kwa ajili ya kugharamia matibabu .lakini leo dkt Tulia ameamua kubeba mzigo huo wa gharama za matibabu kwa watu maskini na wasio jiweza kwa kuwapatia bima za afya bure kabisa ,ili wapatapo changamoto za afya waende hospitali na kupata matibabu bila shida ya aina yoyote ile.
Dkt Tulia kwa hisia kali na uchungu ameongeza kusema kuwa atajitahidi kuwafikia watu wengi sana kila mwaka katika kuwasaidia na kugusa maisha ya watu ,ambapo asipokufikia kupitia bima ya afya basi utafikiwa na kuguswa kupitia pesa anazotoa kwa watu kama mitaji au kupitia kujengewa nyumba bora na ya kisasa au kwa namna yoyote ile itakayo gusa maisha yako.amesema kuwa Watanzania tupendane , tusaidiane na tuoneane huruma.amesema ya kuwa usijisikie fahari kula chakula hapo pako pekee yako wakati kwa jirani yako watu wanalala na njaa.hivyo kama unauwezo basi msaidie jirani yako hata kwa chakula au mavazi au chochote kile kwa kadri ulivyo jaliwa na Mungu. Amesema kuwa tuguse maisha ya watu ili siku moja hata tukiondoka Duniani basi tukumbukwe kwa namna tulivyogusa na kuleta Tabasamu katika maisha ya watu.
Ameongeza ya kuwa kufikia June mwaka huu atakuwa amejenga nyumba zingine zaidi ya tatu kwa watu wasio jiweza.
Sasa dkt Tulia anafanya haya yote makubwa katika kugusa maisha ya watu na kuleta Tabasamu katika mioyo ya watu akiwa hajamaliza hata miaka mitano tu ya ubunge wake Mbeya mjini ,lakini cha ajabu SUGU wa CHADEMA alikaa Mbeya mjini ka ma mbunge kwa miaka kumi mfululizo bila kufanya lolote lile wala kugusa maisha ya yoyote yule .sugu alishindwa hata kumsaidia mjane mmoja tu ndani ya jimbo zima kupata hata hela ya mtaji wa nyanya na vitunguu.sugu alishindwa kwa miaka yake yote kumsaidia hata yatima mmoja tu madaftari ya shule pamoja na begi la madaftari.
Muda wote sugu alikuwa ni kuleta usera na mambo ya kihuni huni tu kama ambavyo alitudhaliliisha wana Mbeya kule bungeni kwa kuonyesha kidole kilicho ashiria matusi. Na hivyo kutufanya wana mbeya kuonekana sote ni wahuni wahuni tunaowakilishwa na mhuni mwenzetu tuliye mpeleka bungeni kuwakilisha uhuni wetu na kukosa adabu mbele za watu utafikiri watoto waliokosa malezi bora ya wazazi wao na kukulia mitaani.
Lakini tangia dkt Tulia aingie bungeni imekuwa nuru kwa wana Mbeya ,ameleta faraja na tabasamu kwa watu wengi sana.maana kupitia yeye kuna wengi sana Wamepata mitaji, wengine wamepata nyumba,wengine bima za afya ,wengine kusomeshwa na kulipiwa ada na mengine mengi sana. Wana mbeya tulikuwa kama tumepigwa na laana kwa kumchagua Sugu. Maana hakuna kilichokuwa kinakwenda wala kufanikiwa ,hakuna miradi iliyokuwa inafanyika wala kufanikiwa ,muda wote ukawa ni wa mavurugu tu . CHADEMA wakaweka jiji kama uwanja wa fujo na mazoezi ya kutolea maneno machafu utafikiri walevi wa gongo waliokunywa wakiwa na njaa ya chakula matumboni mwao.
Sasa ni nani mwenye akili Timamu anayeweza kumpa tena kura ya ndio sugu na kumuacha dkt Tulia? Yaani umuache dkt Tulia anayekupa uhakika wa kupata matibabu hospitalini baada ya kuwa umepewa bima ya afya bure halafu upoteze kura yako ukampe sugu anayekwenda kunyoosha vidole vinavyoashiria matusi ndani ya bunge? Huo hautakuwa ukichaa kweli?
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
Dkt Tulia Acksoni Mwansasu amefanya wananchi katika mitaa mbalimbali ya jiji la mbeya kububujikwa na kutokwa na machozi utafikiri watu waliowekewa vitunguu machoni. Hii ni baada ya kumsikiliza dkt Tulia akizungumza kupitia kituo cha CAPITAL RADIO, ambapo katika mazungumzo yake na kituo hicho cha redio amezungumza ya kuwa anatoa bima za afya takribani elfu sita bure kabisaa kwa watu wenye shida na wasio jiweza pamoja na wazee ambao bado hawajaingia na kufikia kukidhi vile vigezo vya kuingizwa katika ule mfumo wa kupata matibabu bure. Lakini pia dkt Tulia kupitia taasisi yake amemjengea mtu mmoja aitwae Hosea nyumba bora kabisa na ya kisasa pamoja na kumnunulia vitu mbalimbali kama vile magodoro pamoja na vitanda kwa ajili ya familia yake.
Dkt Tulia ameeleza ya kuwa ataendelea kuwasaidia bima za afya watu wote wenye mahitaji na wasio jiwezi.ambapo mwaka jana pia alifanya hivi kwa kutoa bima za afya takribani elfu tatu.
Hii maana yake nini ndugu zangu? Hii inamaanisha kuwa dkt Tulia amewapa cash ya mitaji maelfu ya wana mbeya na kuwapatia tabasamu katika mioyo yao.amewapa mitaji kwa kuwa afya ndio mtaji,ndio nguvu ,ndio rasilimali iwezayo kumpatia mtu utajiri mkubwa.maana pasipo afya huwezi kufanya kazi wala kupiga hatua bali utateketeza mali na kila kitu kilicho ndani ya kaya yako kwa ajili ya kugharamia matibabu .lakini leo dkt Tulia ameamua kubeba mzigo huo wa gharama za matibabu kwa watu maskini na wasio jiweza kwa kuwapatia bima za afya bure kabisa ,ili wapatapo changamoto za afya waende hospitali na kupata matibabu bila shida ya aina yoyote ile.
Dkt Tulia kwa hisia kali na uchungu ameongeza kusema kuwa atajitahidi kuwafikia watu wengi sana kila mwaka katika kuwasaidia na kugusa maisha ya watu ,ambapo asipokufikia kupitia bima ya afya basi utafikiwa na kuguswa kupitia pesa anazotoa kwa watu kama mitaji au kupitia kujengewa nyumba bora na ya kisasa au kwa namna yoyote ile itakayo gusa maisha yako.amesema kuwa Watanzania tupendane , tusaidiane na tuoneane huruma.amesema ya kuwa usijisikie fahari kula chakula hapo pako pekee yako wakati kwa jirani yako watu wanalala na njaa.hivyo kama unauwezo basi msaidie jirani yako hata kwa chakula au mavazi au chochote kile kwa kadri ulivyo jaliwa na Mungu. Amesema kuwa tuguse maisha ya watu ili siku moja hata tukiondoka Duniani basi tukumbukwe kwa namna tulivyogusa na kuleta Tabasamu katika maisha ya watu.
Ameongeza ya kuwa kufikia June mwaka huu atakuwa amejenga nyumba zingine zaidi ya tatu kwa watu wasio jiweza.
Sasa dkt Tulia anafanya haya yote makubwa katika kugusa maisha ya watu na kuleta Tabasamu katika mioyo ya watu akiwa hajamaliza hata miaka mitano tu ya ubunge wake Mbeya mjini ,lakini cha ajabu SUGU wa CHADEMA alikaa Mbeya mjini ka ma mbunge kwa miaka kumi mfululizo bila kufanya lolote lile wala kugusa maisha ya yoyote yule .sugu alishindwa hata kumsaidia mjane mmoja tu ndani ya jimbo zima kupata hata hela ya mtaji wa nyanya na vitunguu.sugu alishindwa kwa miaka yake yote kumsaidia hata yatima mmoja tu madaftari ya shule pamoja na begi la madaftari.
Muda wote sugu alikuwa ni kuleta usera na mambo ya kihuni huni tu kama ambavyo alitudhaliliisha wana Mbeya kule bungeni kwa kuonyesha kidole kilicho ashiria matusi. Na hivyo kutufanya wana mbeya kuonekana sote ni wahuni wahuni tunaowakilishwa na mhuni mwenzetu tuliye mpeleka bungeni kuwakilisha uhuni wetu na kukosa adabu mbele za watu utafikiri watoto waliokosa malezi bora ya wazazi wao na kukulia mitaani.
Lakini tangia dkt Tulia aingie bungeni imekuwa nuru kwa wana Mbeya ,ameleta faraja na tabasamu kwa watu wengi sana.maana kupitia yeye kuna wengi sana Wamepata mitaji, wengine wamepata nyumba,wengine bima za afya ,wengine kusomeshwa na kulipiwa ada na mengine mengi sana. Wana mbeya tulikuwa kama tumepigwa na laana kwa kumchagua Sugu. Maana hakuna kilichokuwa kinakwenda wala kufanikiwa ,hakuna miradi iliyokuwa inafanyika wala kufanikiwa ,muda wote ukawa ni wa mavurugu tu . CHADEMA wakaweka jiji kama uwanja wa fujo na mazoezi ya kutolea maneno machafu utafikiri walevi wa gongo waliokunywa wakiwa na njaa ya chakula matumboni mwao.
Sasa ni nani mwenye akili Timamu anayeweza kumpa tena kura ya ndio sugu na kumuacha dkt Tulia? Yaani umuache dkt Tulia anayekupa uhakika wa kupata matibabu hospitalini baada ya kuwa umepewa bima ya afya bure halafu upoteze kura yako ukampe sugu anayekwenda kunyoosha vidole vinavyoashiria matusi ndani ya bunge? Huo hautakuwa ukichaa kweli?
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.