Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,340
- 9,767
Ndugu zangu Watanzania,
Kwa hakika Dr Slaa anapitia wakati Mgumu Sana, wakati wa majuto, mateso ya moyo na nafsi na upweke wa hali ya juu sana. Kwa sasa haaminiki na yeyote wala kukubalika na kundi lolote lile, hasikilizwi na yeyote wala kupewa muda na yeyote. Amepuuzwa na kila mtu na kudharaulika na kila mtu. Haaminiki kwa yeyote wala kupewa faraja na yeyote.
Hakuna anayetaka kusimama na Dr Slaa kwa sasa, wala kuzungumza na Dr Slaa wala kupanga mipango au mikakati au ajenda au kuandaa sera na Dr Slaa, kwa sasa kila mtu na kila kundi au kila Taasisi au jumuiya inamuona Dr Slaa Kama mtu msaliti na mwenye ndimi mbili, Anaonekana kama mtu mwenye kujali maslahi yake binafsi, mtu mwenye uchu wa madaraka na mroho wa mamlaka,mtu mwenye chuki na mnafiki.
Hakuna anayetaka kujishughulisha na habari za Dr. Slaa wala kufuatilia habari zake wala kumtetea kwa lolote.Amekatalika na vijana, wazee,akina mama, wajane na watu wa makundi yote. Dr Slaa aliyekuwa akisimama mahali anaitwa Rais Rais kwa mbwembwe na madoido sasa Hakuna anayetaka hata kumuona mbele yake wala kusikia maneno yake. Ufalme wake umedondoka na kuvunjika vunjika,haelewi ashike wapi au asimame wapi maana hakuna anapoaminika wala kupokeleka.
Vijana waliokuwa wakimpa jeuri ,kumuamini,kumpenda,kumpigania,kujitoa mhanga kwa ajili yake,kupoteza masomo na kufukuzwa vyuo kwa ajili yake,kukosana na watu kwa ajili yake kwa sasa hawana habari naye wala kutaka hata kumsikia wala kumuona machoni pao,hawataki kusikia sauti yake wala maneno yake,wanamuona kama msaliti na asiyefaa kabisa hapa Duniani.
wanajuta kumfahamu,wanajuta kupoteza na kupotezewa muda wao na Dr Slaa hasa wakikumbuka walivyopigwa mabomu ya machozi kwa ajili yake,kulala mahabusu kwa ajili yake,kupigwa mijeledi kwa ajili yake,kufilisiwa mali kwa ajili ya kumuunga mkono yeye,kutengwa na ndugu kwa ajili yake na kupoteza ndoto zao kwa ajili yake.kwa hakika wakikumbuka haya madhira wanamlaani sana Sana Dr Slaa,wanaona uchungu sana mioyoni mwao ,hawataki hata kumsikia na wanafurahi sana kwa uamuzi wa kijasiri na kishujaa aliouchukua mh Rais wetu mama Samia Suluhu Hasssan wa kumvua hadhi ya Ubalozi.
Kwa sasa Dr Slaa Hakuna anapokaribishwa kuweka hata miguu yake. Haelewi arudi nyuma au aende mbele,haelewi amuombe nani msamaha na ampigie nani magoti maana kila mahali anaona alishaharibu na kusaliti, kila mahali alishapoteza heshima yake,kila mahali alishapoteza uaminifu,kila mahali alishapoteza nguvu yake ,kila mahali alishaoonyesha kuwa siyo wa kuaminika wala kuaminiwa na kila mahali alishawaumiza na kuwajeruhi watu na mioyo yao inatiririka machozi na Damu ya mateso aliyoyawapatia na kuwasababishia .
Anamaliza uzee kwa majuto na maumivu ya hali ya juu sana,anamaliza kwa masononeko,anamaliza kwa kuiona Hadithi yake ikiwa mbaya na kitabu chake cha matendo yake kikitupwa chini na kusiginwa na kila mtu. Alioanza nao wote hawamtaki maana wote wanaona amekiuka viapo vyote alivyoapa na kuwasaliti.
Mtu na kiongozi pekee aliyekuwa amemsitiri na kumtunzia heshima alikuwa ni Amiri jeshi mkuu wetu wa majeshi ya ulinzi na usalama mh Rais wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hasssan.sasa Dr Slaa kwa chuki zake Binafsi akajiona kuwa yeye ni mwamba,Jemedari na komandoo.akaanza vituko hadi vya kuwaza habari za kutaka kumpindua Rais wetu na Serikali yake. Akaanza kuhamasisha machafuko na lugha za kuhatarisha usalama wa Taifa letu na umoja na mshikamano wetu kama Taifa,akaanza kuleta dharau na ubaguzi kwa mh Rais.Akaanza kutaka kuleta utani na mchezo na mboni na Nembo ya Taifa letu .
sasa amepigiwa baada ya kubipu.Simu moja tu imempa pigo la maisha ambalo hata lisahau,kwa kuwa alidhani watanzania wapo upande wake kumbe walishamtoa katika mioyo yao na kumpuuza siku nyingi sana.Sasa amekatalika kila sehemu na kuzomewa kila mahali, na kila mtu hayupo Tayari kumsemea wala kumtetea wala kumuunga mkono wala kusimama upande wake.
Namshauri tu kuwa Aende kanisani akapige magoti na kunyenyekea mbele za mwenyezi Mungu na kuomba msamaha Hadharani kwa Taifa letu.Bila kufanya hivyo kwa hakika Dr Slaa ataishi kwa mawazo na msongo wa mawazo mkubwa sana maana Hakuna kitu kibaya Duniani kama kukosa Amani ya moyo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Kwa hakika Dr Slaa anapitia wakati Mgumu Sana, wakati wa majuto, mateso ya moyo na nafsi na upweke wa hali ya juu sana. Kwa sasa haaminiki na yeyote wala kukubalika na kundi lolote lile, hasikilizwi na yeyote wala kupewa muda na yeyote. Amepuuzwa na kila mtu na kudharaulika na kila mtu. Haaminiki kwa yeyote wala kupewa faraja na yeyote.
Hakuna anayetaka kusimama na Dr Slaa kwa sasa, wala kuzungumza na Dr Slaa wala kupanga mipango au mikakati au ajenda au kuandaa sera na Dr Slaa, kwa sasa kila mtu na kila kundi au kila Taasisi au jumuiya inamuona Dr Slaa Kama mtu msaliti na mwenye ndimi mbili, Anaonekana kama mtu mwenye kujali maslahi yake binafsi, mtu mwenye uchu wa madaraka na mroho wa mamlaka,mtu mwenye chuki na mnafiki.
Hakuna anayetaka kujishughulisha na habari za Dr. Slaa wala kufuatilia habari zake wala kumtetea kwa lolote.Amekatalika na vijana, wazee,akina mama, wajane na watu wa makundi yote. Dr Slaa aliyekuwa akisimama mahali anaitwa Rais Rais kwa mbwembwe na madoido sasa Hakuna anayetaka hata kumuona mbele yake wala kusikia maneno yake. Ufalme wake umedondoka na kuvunjika vunjika,haelewi ashike wapi au asimame wapi maana hakuna anapoaminika wala kupokeleka.
Vijana waliokuwa wakimpa jeuri ,kumuamini,kumpenda,kumpigania,kujitoa mhanga kwa ajili yake,kupoteza masomo na kufukuzwa vyuo kwa ajili yake,kukosana na watu kwa ajili yake kwa sasa hawana habari naye wala kutaka hata kumsikia wala kumuona machoni pao,hawataki kusikia sauti yake wala maneno yake,wanamuona kama msaliti na asiyefaa kabisa hapa Duniani.
wanajuta kumfahamu,wanajuta kupoteza na kupotezewa muda wao na Dr Slaa hasa wakikumbuka walivyopigwa mabomu ya machozi kwa ajili yake,kulala mahabusu kwa ajili yake,kupigwa mijeledi kwa ajili yake,kufilisiwa mali kwa ajili ya kumuunga mkono yeye,kutengwa na ndugu kwa ajili yake na kupoteza ndoto zao kwa ajili yake.kwa hakika wakikumbuka haya madhira wanamlaani sana Sana Dr Slaa,wanaona uchungu sana mioyoni mwao ,hawataki hata kumsikia na wanafurahi sana kwa uamuzi wa kijasiri na kishujaa aliouchukua mh Rais wetu mama Samia Suluhu Hasssan wa kumvua hadhi ya Ubalozi.
Kwa sasa Dr Slaa Hakuna anapokaribishwa kuweka hata miguu yake. Haelewi arudi nyuma au aende mbele,haelewi amuombe nani msamaha na ampigie nani magoti maana kila mahali anaona alishaharibu na kusaliti, kila mahali alishapoteza heshima yake,kila mahali alishapoteza uaminifu,kila mahali alishapoteza nguvu yake ,kila mahali alishaoonyesha kuwa siyo wa kuaminika wala kuaminiwa na kila mahali alishawaumiza na kuwajeruhi watu na mioyo yao inatiririka machozi na Damu ya mateso aliyoyawapatia na kuwasababishia .
Anamaliza uzee kwa majuto na maumivu ya hali ya juu sana,anamaliza kwa masononeko,anamaliza kwa kuiona Hadithi yake ikiwa mbaya na kitabu chake cha matendo yake kikitupwa chini na kusiginwa na kila mtu. Alioanza nao wote hawamtaki maana wote wanaona amekiuka viapo vyote alivyoapa na kuwasaliti.
Mtu na kiongozi pekee aliyekuwa amemsitiri na kumtunzia heshima alikuwa ni Amiri jeshi mkuu wetu wa majeshi ya ulinzi na usalama mh Rais wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hasssan.sasa Dr Slaa kwa chuki zake Binafsi akajiona kuwa yeye ni mwamba,Jemedari na komandoo.akaanza vituko hadi vya kuwaza habari za kutaka kumpindua Rais wetu na Serikali yake. Akaanza kuhamasisha machafuko na lugha za kuhatarisha usalama wa Taifa letu na umoja na mshikamano wetu kama Taifa,akaanza kuleta dharau na ubaguzi kwa mh Rais.Akaanza kutaka kuleta utani na mchezo na mboni na Nembo ya Taifa letu .
sasa amepigiwa baada ya kubipu.Simu moja tu imempa pigo la maisha ambalo hata lisahau,kwa kuwa alidhani watanzania wapo upande wake kumbe walishamtoa katika mioyo yao na kumpuuza siku nyingi sana.Sasa amekatalika kila sehemu na kuzomewa kila mahali, na kila mtu hayupo Tayari kumsemea wala kumtetea wala kumuunga mkono wala kusimama upande wake.
Namshauri tu kuwa Aende kanisani akapige magoti na kunyenyekea mbele za mwenyezi Mungu na kuomba msamaha Hadharani kwa Taifa letu.Bila kufanya hivyo kwa hakika Dr Slaa ataishi kwa mawazo na msongo wa mawazo mkubwa sana maana Hakuna kitu kibaya Duniani kama kukosa Amani ya moyo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.