JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,356
- 5,602
Kwa sasa Halima anaendelea na matibabu kwenye hospitali ya rufaa ya St. Benedict iliyopo Ndanda Mtwara baada ya ajali hiyo iliyotokea Mei 22, 2022.
“Wakati natokea Songea kwenda Dar es Salaam kupitia Lindi, sehemu zote hatarishi nilikuwa nimeshazivuka, kuna sehemu ina kona ya kawaida sana, nikaona kuna mtu anavuka kutoka kulia kwenda kushoto na nina mfahamu, ilikuwa ghafla sana.
“Nilishtuka sana, nikawa namkwepa, kushtuka gari likawa limeshalalia upande mmoja, lakini baadaye nilibaini kuwa hakukuwa na huyo mtu, ni miujiza tu ya barabarani, hivyo vitu vipo.
“Wakati gari linalala mkono wangu ulikuwa nje, lilivyoanguka mkono wangu ulikatika palepale nauona, nikakumbuka kuwa gari bado linawaka na inaweza kulipuka, nikatumia mkono wangu wa kushoto kulizima kwa usalama wa kuondoa moto.
“Namshukuru Mungu, nilihudumiwa vizuri hospitali, ndoto yangu ilikuwa kuendesha gari zaidi ili baadaye nisomee urubani, lakini sijakata tamaa kuwa maisha yangu yameishia hapa,” – Halima.
Source: Azam TV
Pia soma: Basi la Super Feo Songea-Dar via Lindi limepata ajali. Dereva mwanamke avunjika mkono