PMNBuko
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 967
- 154
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Col. Issa Njiku, amechakachua maoni ya wananchi wa Missenyi kwa kuanzia na kata za Kyaka na Kilimililie ambako wananchi walipaswa kutoa maoni yao jana 16.7.2012.
Mkuu huyo kwa kushirikiana na makatibu wenezi wa CCM wa kata hizo, waliandaa karatasi maalumu zenye maoni ya kiserikali/CCM na kuzigawa kama njugu kwa wananchi na hayo ndiyo maoni yaliyowasilishwa kwa wajumbe wa katiba. Utaratibu wa kutoa maoni ulikuwa na mfumo wa aina mbili. 1. Kuwasilisha karatasi yenye maoni 2. kuzungumza moja kwa moja mbele ya hadhara.
Utaratibu wa 1, umetumika sana kwa maslahi ya CCM. Maoni hayo ya CCM/Serikali ya Njiku Missenyi yalisisitiza:
1. Uwepo wa serikali mbili- serikali ya Jamhuri na Serikali ya zanzibar
2. Rais aendelee kuwa na madaraka aliyonayo
3. wakuu wa wilaya na mikoa na watendaji wengine waendelee kuteuliwa na Rais
4.N.k.
Fomu yenyewe nitaiweka hapa baadaye.
Je, hali hii ni sawa? Huu utaratibu utawezesha tupate Katiba Mpya kweli?
Wajumbe wa Katiba wanahitaji kuchambua kwa makini na kuona kuwa fomu zaidi ya 2000 zina maoni yanayofanana, kitendo ambacho kinafanya zoezi zima kuwa hopeless.
Nawasilisha
Mkuu huyo kwa kushirikiana na makatibu wenezi wa CCM wa kata hizo, waliandaa karatasi maalumu zenye maoni ya kiserikali/CCM na kuzigawa kama njugu kwa wananchi na hayo ndiyo maoni yaliyowasilishwa kwa wajumbe wa katiba. Utaratibu wa kutoa maoni ulikuwa na mfumo wa aina mbili. 1. Kuwasilisha karatasi yenye maoni 2. kuzungumza moja kwa moja mbele ya hadhara.
Utaratibu wa 1, umetumika sana kwa maslahi ya CCM. Maoni hayo ya CCM/Serikali ya Njiku Missenyi yalisisitiza:
1. Uwepo wa serikali mbili- serikali ya Jamhuri na Serikali ya zanzibar
2. Rais aendelee kuwa na madaraka aliyonayo
3. wakuu wa wilaya na mikoa na watendaji wengine waendelee kuteuliwa na Rais
4.N.k.
Fomu yenyewe nitaiweka hapa baadaye.
Je, hali hii ni sawa? Huu utaratibu utawezesha tupate Katiba Mpya kweli?
Wajumbe wa Katiba wanahitaji kuchambua kwa makini na kuona kuwa fomu zaidi ya 2000 zina maoni yanayofanana, kitendo ambacho kinafanya zoezi zima kuwa hopeless.
Nawasilisha