Kuna Mtu kanipa theory hii, sikupenda kuiamini. Please take it as a Quizz:
Kuna wapiga kura makundi mawili: Kund A na Kundi B
Kuna vyama vitatu vyenye ushawishi: Chama A, Chama B na Chama C:
Inaaminika kuwa kura za Kundi A: Zitagawanyika kwa Chama A na Chama B na Chama C
Where as kura za Kundi A: Zitaenda Chama A na Chache Chama B
Kundi A ni nani na Kundi B ni nani?
Chama A, B na C ni nani?
Why?
According to hiyo nadharia yako, aliyekupa hiyo theory alikuwa anamaanisha kwamba:
Kundi A - ni wale ambao wanataka ku-maintain status quo, yaani wanaogopa upinzani kuingia madarakani kwa kudanganywa, kutishiwa au kupewa ahadi hewa.
Kundi B - Hili ni la wapiga kura ambao wanataka upinzani uingie madarakani wakitarajia kwamba yatakuja mabadiliko mara chama kutoka upinzani kikishinda.
So far kuna vyama vitatu ambavyo vina ushawishi kwenye nafasi za wagombea wa Urais, navyo ni CCM, CHADEMA na CUF.
From this point onward, naomba nitofautiane na theory yako. Kama assumptions zangu hapo juu ziko sahihi, kinachogombewa kwa sasa ni kuongeza kura za vyama upinzani. Kwa hiyo kura za kundi A, ni kama ulivyosema zitaganywa kwenye vyama vitatu. Kwa maneno mengine wapiga kura walioipigia CCM mwaka 2005, wapo ambao watapigia kura CHADEMA na CUF kwenye nafasi za urais. Practically, hicho ndicho kilichotokea kwenye chaguzi ndogo za Kiteto, Busanda na Bihalamuro. Chadema ilipata asilimia kubwa kuliko walizopata kwenye uchaguzi wa 2005 [hapo bado hujapiga factor ya uchakachuaji].
Kura za kundi B zitagawanywa kwa vyama B na C, ambavyo ni CHADEMA na CUF. Nimefuatilia kampeni za CHADEMA na CUF, base yao ya wapiga kura iko solid, sasa hivi wanajaribu kushawishi walioipigia kura CCM mwaka 2005, wapigie vyama vyao. Hapa naogopa kutaja kwamba chama fulani kitapata nyingi na chama fulani kitapata chache kwa sababu ya conflict of interest.
Lakini, angalizo, ukiangalia kampeni za CCM pamoja na siasa za maji taka zinazoendeshwa kwa sasa, you can easily guess which party is a threat to CCM, kazi kwako.