Dakika 45 ITV: Jobu Ndugai apasua siri jinsi nchi inavyofilisiwa na serikali iliyoko madarakani

Kwa bahati mbaya mimi sikuona hayo majadiliano na Mh. Ndugai.

Swali kubwa ninalojiuliza ni kwa nini mambo ya posho na maslahi ya wafanyakazi wa serikali yamewekwa siri? Miaka ya zamani, enzi za JKN niliwahi kufanya kazi serikalini. Mishahara na marupurupu yote ya wafanyakazi serikalini yalikuwa bayana. Leo ni siri kubwa. Nadhani usiri huu umeandamana pamoja na wizi/uporaji. Nchi nyingi duniani zinaweka wazi mishahara na marupurupu ya wafanyakazi wa serikali, na sisi lazima tulazimishe iwe hivyo. Tuone madudu yanayofanyika huko.

Matumizi ya serikali ya Tanzania ni ya kifahari sana. Posho zao za safari za nje za USD600 kwa siku ni kubwa kupita nchi nyingi duniani, na nadhani ni kupita hata wafanyakazi wa UN. Wakati mawaziri wa nchi kadhaa duniani wanapanda ndege daraja la tatu (tourist) ikiwa safari ni chini ya masaa fulani wafanyakazi wengi wa serikali ya Tanzania wanasafiri daraja la kwanza au business. Hivi kweli tuna akili?

Serikali inabidi ituondolee uchafu huu.
 
Makida makida "Kifungu na 215 kinaafikiwa"
Wabunge wa magamba "Ndioooooooooooooooooooooooo!"

Hilo fungu waliloitikia ndiooo Posho za kufa mtu

Mgogo wa Kongwa "Serikali inajilipa posho nyingi kuliko zetu"

Kashasahau kama kabariki mwenyewe.
 
Huu ni uthibitisho tosha kwamba asilimia kubwa ya viongozi wamepoteza sifa na uhalali wa kuendelea kuongoza.
Kuna haja kabisa ya kuwaondoa viongozi walio madarakani kwa njia yoyote na kwa gharama yoyote. Haikubaliki kulipana posho kubwa kiasi hicho na kutaka kujiongezea zaidi wakati huohuo wananchi walipa kodi zaidi ya milioni arobaini wakiishi katika ufukara wa kutisha.
Hii ni dharau ya hali ya juu na ni muhimu kuungana kupambana na kuwaondolea mbali hawa wanyonyaji wasiozidi elfu tano dhidi ya milioni zaidi ya 40.
Serikali, wabunge pamoja na viongozi wa mahakama wanaoshiriki kutunyonya lazima wasafishwe bila kuchelewa kwa faida ya wengi!
Tutakuwa tunatenda dhambi kubwa tukiacha uovu huu dhidi ya uma uendelee.
 
Ndugai bana... Mtindo anaotumia kujustify posho zao silubaliani nao hata kidogo..

Wee trachomatis usishangae huu mtindo kwani hawa jamaa ni wabunifu kwa kwenda na wakati, formula hii inafanana na iliyowahi kutumika kumtoa six uspika kwa kumweleza kuwa safari hii ni ya wanawake wakijua wazi atafeli kwani six hanaga ile......in btwn

Nawasifu CCM kwa ubunifu yakinifu, kufuata kanuni na taratibu za chama chao bila kujifunza lolote toka TUnisia, Misri, Zambia, Libya, Malawi, etc

Mie binafsi naamini kuwa ukombozi wa kweli unazidi kukaribia na kibaya zaidi wao wanauharakisha
 
Trachomatis hebu angalia signature yangu

SEMINA ELEKEZI, Mie ntakula mpaka kulee, wewe palee na nyie paleee, angalieni msiingiliane mpaka tutakapokutana 2015


Ndio maana walilipana kabla ya kuidhinishwa

 
Job Ndugai kanisikitisha.
Nae anaingia kwenye orodha ya magamba yasiyofaa kuwa viongozi wa uma.
How the hell did he become a deputy speaker?
OTIS

Mapepo yasikurudie tena, tunamshukuru muombaji aliyekuombea. Lakini ukijichanganya na Magamba mapepo yatakurudia.
 
Ndugai asifananishe majaji na wabunge, majaji ni proffesional wakati wabunge ni siasa tu mdomoni. kweli ccm imekuwa kila kiongozi ni kambale, mtoto ana ndevu, mama ana mdevu na baba ana ndevu. hakuna kuheshimiana.
Wacongo wanasema mutu nyoso mandevu!!!
 
Jaji Kiongozi atishia kurejesha kesi za uchaguzi bungeni Send to a friend
Monday, 16 January 2012 20:47
0diggsdigg

James Magai
JAJI Kiongozi, Fakihi Jundu amesema Mahakama imelemewa na mzigo wa kesi za uchaguzi ambazo imeshindwa kuziendesha kutokana na kupewa bajeti finyu na kusema kwamba ikiwa hadi kufikia Mei mwaka huu haitakuwa imepewa fedha ilizoomba, itarejesha kesi hizo bungeni.Amesema hadi sasa Serikali imetoa Sh300 milioni kati ya Sh2.3 bilioni zilizoombwa na mhimili huo wa dola na kuonya kuwa kama fedha hizo hazitapatikana watazirudisha kesi hizo bungeni. Mahakama Kuu imeshapokea kesi 43 zilizofunguliwa kupinga matokeo baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2010.



Source: Mwananchi

No wonder majaji wanahitaji mabillion kwa ajili ya kesi za wabunge!!!
 
Kila mara ninapomsikia huyu jamaa huwa napata hasira sana huwa sipendi hoja zake kabisaa!!! Yani kama ni gamba huyu jamaa ni gamba la mamba!
 
Ndugai kama anachosema ni kweli ebu abainishe posho hizo wanalipwa akina nani na ni kiasi gani. Pia ajue kuwa wabunge ndo watetezi wetu ambao tumewatuma mjengoni watutetee ili tuondokane na dhuluma. Wao kama wawakilishi wetu walipaswa kukemea na kuinyoshea kidole serikali ili hujuma hizo zisiendelee kuwepo badala yake nao wanaungana na serikali kuhakikisha mwananchi malala hoi ananyonywa mpaka tone la mwisho. Hivyo kwakuwa wafanyakazi wengine wanalipwa posho kubwa na hali ni mbaya hivo inabidi na wao wajiongezee posho ili mlala hoi akome kisha akomae? Ebu kama ninyi wabunge kweli mpo ili kumsaidia mwananchi wa nchi hii hasa mlala hoi tetea masilahi ya nchi na upolaji huo unaofanywa na viongozi wetu kwa kuanika uovu huo hadharani kwa wananchi ili kuleta ukombozi wa nchi hii, badala ya kutaka posho kubwa ilihali mkijua yule mwananchi mpigakula wako aliyekuchagua wewe kama mwakilishi wake amekalia kuti kavu ambalo linaweza kumdondosha wakati wowote kutokana na ugumu wa maisha unaomkabili. Kama si hivo au kama hamuwezi basi hakuna haja ya kuwa na Bunge kwani kazi yenu hatuioni ama mmeshindwa, zaidi nanyi mnatuongezea ugumu wa maisha, ebu Wabunge simamieni kama mmeshindwa mjiuzuru wote wananchi waamue nini kifanyike.
 
Naibu Spika Jobu Ndugai amedai kuwa watanzania inabidi wasilaumu sana wabunge kuongezewa posho, Ndugai kasema kuwa kuna muhimili mitatu ya nchi ambayo niBUNGE, SERIKALI NAMAHAKAMA, Ndugai kasema kama watanzania wangejua ni kiasi cha posho kubwa wanacholipwa viongozi wa seikali na mahakama basi watanzania wangejinyonga kabisa badala ya kulaumu hizi wabunge ambacho ambacho kadai kuwa ni kidogo kuliko wananchi wanavyofikilia,


Hapo kwenye red: Kama kweli Ndugai ametamka hayo maneno basi Tanzania hatuna viongozi wa bunge. Ndugai ni naibu wa Spika wa Bunge la Tanzania. Bunge ndio chombo cha kutunga sheria, na wabunge kama wawakilishi wa wananchi wanatakiwa siku zote kuhakikisha serikali inafanya mambo kwa mujibu wa sheria na pale mapungufu yanapojitokeza basi wawakilishi hawa (wabunge) wana jukumu la kutafuta suluhu i.e kupitisha sheria mpya.

Sasa Kama Ndugai anajua kuwa kuna watu wanafilisi hii nchi kwa mgongo wa 'posho' kwa nini asitafute solution? Yaani yeye anajuwa watu wanakwapua hela za walipa kodi, badala ya kutafuta namna ya kuondoa huu udhaifu yeye Ndugai anaona dawa ni kwa wabunge nao kukwapua? Kwa maneno mengine ni mchezo wa kuiba kadri ya uwezo wako maana kila mtu anafanya hivyo? Kuna umuhimu gani wa kuwa na kiongozi kama Ndugai ambaye anakuwa na kiguguzi kusimamia maslahi ya walalahoi?
 
Ndugai kama mbunge aliye kwenye muhimili mkuu wa serikali ambao kazi yake kubwa ni kuinyooshea serikali vidole na yeye kama Naibu speaker huu siujinga inamaana hajui hata kazi ya Bunge .............

Hata hivyo hawa tunaowachagua hawajitambui ndio maana anaamua kusema haya .....ni mwezi uliopita Waziri alijitosa kwenye vyombo vya habari na kusemaangekuwa na uwezi angewafunga wauza mafuta wakati yeye ndio waziri wa wizara husika....

Ama kweli mwenye nchi hii kafa! Enzi za mwalimu kiongozi kuchemka kama hivi alikuwa anamchomoa madarakani fasta! Kamuulizeni Prof.Machunda,Mungai, sio leo hii mchovu mwishoni ana siliba kwa kumsifia Kikwete!!
 
Tanzania eeeh, Tanzania eeeh,Nchi yangu eeeh, Nchi yangu eeeh- Nakupenda sana.
 
Haki ya Mungu Job anakotupeleka siyo.nilishangaa sana alipojitokeza na kuanza kutetea suala la Wabunge kujiongezea posho wakati kuna mambo ya msingi ambayo kama kiongozi wa ngazi ile anatakiwa kuyasema na kuyasimamia.Hivi kweli atasema watu wana chuki naye kwa kauli zake za namna hii?hivi cv yake ikoje?mbona ana hoja hafifu sana.It is embalacing!poleni Watanzania,poleni Wananchi wa Kongwa.
 
Huyu ndugai ni mbunge na posho anazozunguzia wanazolipwa hawa wafanyakazi wa ngazi za juu serikalini hupitishwa na bunge. kama si unafiki ni nini? kama analifahamu hilo kwa nini asizipinge hukohuko bungeni?
 
Hii ni kweli mbona watu wanpiga hela nyingi hata mishahara; mfano director wa tanroads anapiga ngapi! Ukijua utazimia.
 
Kwa mtindo huu tusahau maisha bora kwa kila mtanzania badala yake ni maisha bora kwa kila kigogo,nchi ya tanznia sio ,sikini ila watanzania wengi ndio masikini na wanaofanya kuwa masikini ni haohao wanawachagua eti wakawatetee bungeni.Wabunge ni wengi sana kuliko hao ma ofisa wengine wanaolipwa mapesa mengi ndio maana watu wanalalamikia wateule wao ,kingine wanaccholalamikia wa tz ni kwamba tulitegemea wao wakaisimamie serikali iache kulipana maposho kumbe wanashindana kulipana posho nyingi
 
Ndugai funguka zaidi tutakulinda, tunajua unaongelea posho hasa za maofisa wa majeshi kuanzia makamishina hadi Generali inaonekana kule ndiko kwenye kitu kinaitwa POSHO's. ingawa hujajibu hoja ya msingi ya sisi wananchi kwa nini mjiongezee posho kinyemela, ila kwa jinsi ulivyokuja- kuja kweli umegonga katikati a.k.a penyewe. kuna kiharufu tunakisikia kwa mbali ngoja tusubiri majibu upande wa pili.
 
Ninachokiona mimi mpaka sasa ni kwamba uwezo wa kujieleza na kujenga hoja wa hyu mnayemuita mheshimiwa ni duni sana,kwamba wengne wengi wanatenda kosa haijustify hilo kosa.Yeye amekuwepo bungeni kitambo,hizi posho za serikalini na mahakamani kama ni kuzifahamualizifahamu zamani na ilikuwa ni wajibu wake kama mbunge kuhakikisha zinasitishwa.Sasa yeye kwa uelewa wake anaamini tutakubaliana na posho zao kwa vile tu mijizi mingine serikalini na mahakamani inachukua posho kubwa?Basi kila Mtanzania apewe hiyo posho,I guess hii nchi ina hela nyingi kuliko mambo ya msingi tunayoweza kufanya otherwise sielewi watu bila huruma mnagawana tu kodi zetu and you are not even ashamed to stand and justify it!Hii kodi ninayolipa inaniuma saaaaaana,kiungwana ilibidi hawa watu waone aibu washindwe hata kusimama kwenye media kutetea hili ila wao waaaaaala...f**&@K them all
Asante sana kakapeter,umesema yale yote niliyotaka kusema kwa bahati nzuri nilibahatiaka kuangalia dakika 45.sijui kama

ni mimi sikusikia au ndiyo ilivyokuwa,nikimaanisha sikusikia huyu jamaa akijibu hata swali moja kazi ni kujikanyaga kanyaga tuu

unajiuliza huyu kapataje hii nafasi au hakujua kama ataulizwa maswali.!!.mimi naona aibu kuwa na mtu kama huyu katika nafasi

nyeti kama ile ukizingatia na bosi wake(mama)ndiyo kabisa hajui kitu..kaingilia kazi za katibu wa bunge kwa kutangaza kwamba posho zitalipwa wakati si kazi yake na ameishia kujiabisha na kutuaibisha na sisi kwa kuonyesha udhaifu mkubwa alionao.
 
Back
Top Bottom