Nape ni jembe la CCM. Mimi naona anachofanikiwa mara zote anapotoa matamko ni kuwafanya wapinzani wake wamjadili yeye badala ya kujikita kwenye adui yao mkuu ambaye ni chama anachokiwakilisha.
nape ni ubao wa shabaha kila mtu anajilengea tuu
nchi hii wakichukua wachagga watauza kila kitu. na hilo halitatokea hata watembee uch. na mik.nd. juu.
Hata jk nae mchaga ndo mana anajua sana fedha.Wewe nawe eti ndo gamba mbona mtupu hivi !Hueleweki nini waandika?ubaguzi utakusaidia nini kijana zaidi ya kujaza pumba kichwa.Ee Mchungaji Msigwa maneno yako yatakumbukwa daima yaani akili ndogo kuongoza akili kubwa.
Sikubaliani na msemaji hapo kwenye RED kwakuwa hapo kwenye YELLOW sisi tunapapiga vita sana. Hofu yangu kwa msemaji huyu ni kuwa"ANAONEKANA KUENDELEZA PUMBA ZA NAPE KWA NJIA MBADALA"16 AUGUST 2012
Na Grace Ndossa
CHAMA cha Wananchi (CUF), kimedai kushangazwa na kauli iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Bw. Nape Nnauye kwa vyombo vya habari kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeingia mikataba ya kifisadi na wafadhili wa nje ili kupora rasilimali za nchi.
Taarifa iliyotolewa Dar es Salaama jana na Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF, Bw. Abdul Kambaya, alisema Bw. Nnauye hakupaswa kuishtaki CHADEMA kwa wananchi bali kupitia Serikali yao walipaswa kuzuia fedha hizo na kuwataja wafadhili hao.
CUF kimeshangazwa na kauli hii ambayo imetolewa na msemaji wa CCM, ambacho ndio chama kinachoongoza nchi, tulitarajia Bw. Nnauye angewataja hao wafadhili wa CHADEMA ambao dhamira yao ni kupora rasilimali za nchi, alisema Bw. Kambaya.
Aliongeza kuwa, chama hicho kinaamini CCM na CHADEMA ni watoto wa familia moja ambapo wafadhili wao ndani na nje ya nchi pia wa aina moja.
Kama CHADEMA imeingia mikataba ya kupewa mabilioni ili baadae wataposhika madaraka waweze kulipa mabilioni hayo kupitia rasilimali za nchi basi watakuwa wanaendeleza utaratibu wa CCM kuingia mikataba mibovu isiyo na tija kwa Watanzania, alisema.
Alisema CUF inaamini kuwa, tatizo lililopo nchini ni mifumo mibovu inayoendesha Serikali, nchi, kukithiri kwa wizi, matumizi mabaya ya fedha za umma na ukiukwaji wa haki za binaadamu.
Bw. Kambaya alisema, sababu ya Watanzania wengi kuwa maskini wa kutupwa, ukosefu wa huduma bora kwa jamii, kudumaa kwa maendeleo ya nchi na ukosefu wa ajira ni matokeo ya muda mrefu yanayosababishwa na mfumo mbovu uliopo.
Alisema njia sahihi ya kulinda rasilimali zilizopo na zinazoendelea kugunduliwa nchini Serikali ya Umoja wa Kitafa ambayo itashirikisha vyama vyote vyenye wabunge.
Aliongeza kuwa, kwa kuzingatia utaratibu huo hakuna chama ambacho kitakuwa na maamuzi yake katika matumizi ya rasilimali na Maliasili za nchi.
Sisi tunataka Watanzania waelewe kuwa, mazingira yanaonesha CHADEMA kimeizidi kete chama tawala kwa kuwa na wafadhili wa nje ndio maana CCM Inapiga kelele, alisema.
Sikubaliani na msemaji hapo kwenye RED kwakuwa hapo kwenye YELLOW sisi tunapapiga vita sana. Hofu yangu kwa msemaji huyu ni kuwa"ANAONEKANA KUENDELEZA PUMBA ZA NAPE KWA NJIA MBADALA"