Pagoda Hunter
Senior Member
- Apr 15, 2020
- 138
- 172
CORONA:
TUOMBE, TUSIOMBEOMBE
Vita dhidi ya Corona haiepukiki. Napendekeza haya:
1. Mungu haongei nasi kutumia Corona. Tunaalikwa kuongea na Mungu kwa tishio la Corona.
2. Katika vita kuna kujilinda na kushambulia adui. Tumesikia mbinu nyingi za kujilinda na chache za kushambulia Corona. Tuanze kushambulia. Kinachohitajika ni mikakati, vifaa, umoja wa kitaifa na makamanda imara.
3. Tutangaze tunapofunga goli na tunapofungwa. Hofu ya kufungwa inaongeza mbinu za kujilinda. Watu wakiona na kusikia habari za watu wanaowajua, wataelewa kirahisi hatari inayotukabili. TUSIFICHE CHOCHOTE.
4. Tuwalinde wachezaji wetu kwa gharama. Watumishi wa afya nchini kote, wapewe vifaa vya kujilinda na watengewe maeneo ya kukaa. Wasirudi majumbani.
5. Vifaa vipatikane na vijulikane viko wapi. Wenye uwezo wajinunulie na wawanunulie wasio na uwezo.
6. Visivyopatikana nchini viagizwe. Msamaha wa kodi utangazwe na ukiritimba wa kuviingiza uondolewe haraka. Mashirika yahanasishwe kuagiza haraka.
7. Tusitishe vyombo vya usafiri kutoka mkoa kwenda mkoa. Hivi sasa kirusi chaweza kuwa Ubungo asubuhi na jioni kikawa Kahama. Barabara nzuri na Bombadier hazisafirishi bidhaa tu. Hata virusi vinapata lifti.
8. Mashine za kupima virusi zipelekwe kila mkoa. Kupeleka sample DsM ni usumbufu na inaongeza uwezekano wa kuharakisha maambukizi wakati wa kusubiri matokeo. Tumejifunza kwa NIDA na Passport mpya.
9. Elimu isisitizwe kuliko adhabu. Usugu wa adhabu utaongeza kasi ya maambukizi. Polisi wapige virusi, wasipige watu.
10. Tufunge na kuomba lakini tukumbuke CORONA NI TATIZO LA KISAYANSI ZAIDI KULIKO KUWA TATIZO LA KIROHO. Tuombe, tusiombeombe
TUOMBE, TUSIOMBEOMBE
Vita dhidi ya Corona haiepukiki. Napendekeza haya:
1. Mungu haongei nasi kutumia Corona. Tunaalikwa kuongea na Mungu kwa tishio la Corona.
2. Katika vita kuna kujilinda na kushambulia adui. Tumesikia mbinu nyingi za kujilinda na chache za kushambulia Corona. Tuanze kushambulia. Kinachohitajika ni mikakati, vifaa, umoja wa kitaifa na makamanda imara.
3. Tutangaze tunapofunga goli na tunapofungwa. Hofu ya kufungwa inaongeza mbinu za kujilinda. Watu wakiona na kusikia habari za watu wanaowajua, wataelewa kirahisi hatari inayotukabili. TUSIFICHE CHOCHOTE.
4. Tuwalinde wachezaji wetu kwa gharama. Watumishi wa afya nchini kote, wapewe vifaa vya kujilinda na watengewe maeneo ya kukaa. Wasirudi majumbani.
5. Vifaa vipatikane na vijulikane viko wapi. Wenye uwezo wajinunulie na wawanunulie wasio na uwezo.
6. Visivyopatikana nchini viagizwe. Msamaha wa kodi utangazwe na ukiritimba wa kuviingiza uondolewe haraka. Mashirika yahanasishwe kuagiza haraka.
7. Tusitishe vyombo vya usafiri kutoka mkoa kwenda mkoa. Hivi sasa kirusi chaweza kuwa Ubungo asubuhi na jioni kikawa Kahama. Barabara nzuri na Bombadier hazisafirishi bidhaa tu. Hata virusi vinapata lifti.
8. Mashine za kupima virusi zipelekwe kila mkoa. Kupeleka sample DsM ni usumbufu na inaongeza uwezekano wa kuharakisha maambukizi wakati wa kusubiri matokeo. Tumejifunza kwa NIDA na Passport mpya.
9. Elimu isisitizwe kuliko adhabu. Usugu wa adhabu utaongeza kasi ya maambukizi. Polisi wapige virusi, wasipige watu.
10. Tufunge na kuomba lakini tukumbuke CORONA NI TATIZO LA KISAYANSI ZAIDI KULIKO KUWA TATIZO LA KIROHO. Tuombe, tusiombeombe