Chenge, StarTV na Utaalam wa kisasa

Inakuaje unajenga hoja ya kupinga kabla haijathibitishwa kuwa kweli nakala za mkanda huo zipo au la iwe ni za Star au usalama wa bunge tusubiri tuhakikishiwe kuwa kweli tukio hilo limetokea, ushahidi upo n.k, then tuanze kumwaga hoja zetu hapa vinginevyo twaweza kuwa tunaangalia Ze Commedy ya kina Masanja bila kujua!
 
samahani natoka nje ya mada kidogo




...na ninamuomba aelewe kuwa jina langu la FMES ni pamoja na biashara behind it sasa sio jina tu ni signature kubwa sana na I have worked so hard kulifikisha lilipo, hapa JF huwa ninajitolea bure, lakini sio nje ya hapa, nilitaka tu hilo lieleweke wazi kwa wakuu wote hapa maana naona ndio kwanza ana post moja, ni vyema kufahamishana mapema, na ninamtakia mafankio mema hapa ndani ya JF!

Ahsante Wakuu!

mkuu natumai utakuwa umeliorodhesha (register) jina hilo brela na nchi nyingine ilipo na mawasiliano ya kibiashara. vinginevyo mkuu utakuta wenzio wamekuwahi na utapata tabu sana kufaidika nalo kibiashara. ni maoni tu mkuu
 
Uchawi, Unga, Leso - weka chochote - watu wasife moyo. Kazi bado ipo kubwa na huu ni mtapakanyo tuu - yaani ni pumba tupu kama hizi taarifa ni za kweli.

Alafu huyo ndio alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali yetu?? Kazi kweli tunayo
 
mkuu natumai utakuwa umeliorodhesha (register) jina hilo brela na nchi nyingine ilipo na mawasiliano ya kibiashara. vinginevyo mkuu utakuta wenzio wamekuwahi na utapata tabu sana kufaidika nalo kibiashara. ni maoni tu mkuu

Mkuu Heshima yako, ni kweli huyu mtu amekuwa akilitumia hili jina sehemu nyingi huko kwenye forum zingine, ninafahamu sana, lakini haijanipa taabu sana kwa sababu biashara ninazofanya hawezi pata anything bila ya mimi mwenyewe personally kusema, kwa sababu no matter what ni lazima wanaohusika watanitwangia, ndio maana alipoanza tu kulitumia walikuwa wa kwanza kunishitua, ingawa hapa amelifupisha huko kwengie analitumia in full anyway ninashukuru tu kuwa hapa JF ambako ndio nyumbani kwangu kama inavyofahamika na wadau hii imeeleweka,

Pia naomba kuongeza kidogo kuwa hivi karibuni kwa kushirikiana na ndugu yangu mmoja, tumefungua Bar moja nzito sana mjini Dodoma, ni majuzi tu nimemamliza kufunga vyombo vizito toka nga'mbo vya Disco, na bado kuna marekebisho machache ya kumalizia, itakuwa Bar, nyama choma, na I mean socialization kwa ujumla hasa kwa wageni wanaokuja pale kwa kufuata siasa za Dodoma, na pia nitaweka sehemu ya Internet the goal ni kuigeuza kuwa a biog hotel in the next three years, itakapokuwa tayari 100%nitasema rasmi, sasa hivi iko 75% tu, na ninategmea Mkulu kuja kuifungua rasmi, kwa hiyo wazee wote wa JF na wengine mnakaribishwa! hasa waandishi maana sasa itakuwa ni kurusha maneno moja kwa moja hapa kutoka kwenye internet cafe!

Samahani kwa kutoka nje ya mada! Ahsante Wakuu!
 
Uchawi, Unga, Leso - weka chochote - watu wasife moyo. Kazi bado ipo kubwa na huu ni mtapakanyo tuu - yaani ni pumba tupu kama hizi taarifa ni za kweli.

Alafu huyo ndio alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali yetu?? Kazi kweli tunayo

Basi angetumia na uchawi kuhakikisha anawaroga wawekezaji ili wasaini mikataba in favor of Wadanganyika....

%&%^*&^ kabisa.

Hii ni aibu kubwa kwa taaluma ya Sheria Tanzania. Nina uhakika kwamba Baraza la wanasheria lazima wana kipengere kinachoelekeza hatua ambazo registrant anaweza kuchukuliwa in case atakuwa ame-breach vitu kama moral behavior. What this guy has done ni breach kubwa katika moral behavior, na ina-make sense kwa Baraza la wanasheria, ama chombo chochote kinacho-register wanasheria Tanzania kumchukulia hatua za kum-suspend ama kumfuta kwenye register kwa tendo lake hili. Hili litakuwa ni fundisho kubwa kwa wanasheria wa kesho, na kitendo hiki (cha kumchukulia hatua mwanasheria huyu) kinaweza tumika kama reference huko chuo kikuu katika kuwafundisha wanasheria wa kesho..

Lets get serious jamani. Viongozi wa Baraza la wanasheria mnawajibika kwa hili. Hakuna kuogopa mtu... Sheria ni msumeno. Kama hamtamchukulia hatua huyu jamaa basi the next move hapa JF itakuwa kwenu. We are not here to teach you how to do your job. Futeni huyu mtu kwenye register. We want him to "learn the lesson" wakati akiwa bado ni hai
 
Angalau sasa watu watakoma kidogo kumfuata fuata Chenge. Kila siku makelele tu ambayo hayana msingi wowote. Tulieni tujenge nchi ndugu zangu na kuacha majungu. CCM hakuna mafisadi wowote na huyu Chenge anasingiziwa tu.

MASAKA...Are you serious or simply playing the devil's advocate with a light touch?

Makelele yasiyo na msingi indeed..ina maana vita vya wazalendo dhidi ya ufisadi wewe havikuhusu..au wewe ni mmoja wao? YOU DESERVE TO BE STONED TO.........................................
 
MASAKA...Are you serious or simply playing the devil's advocate with a light touch?

Makelele yasiyo na msingi indeed..ina maana vita vya wazalendo dhidi ya ufisadi wewe havikuhusu..au wewe ni mmoja wao? YOU DESERVE TO BE STONED TO.........................................

womenofsubstanc

Sintoshangaa nikija ambiwa kwamba huyu ndugu yetu alikuwa mmojawapo wa waandamaji na wapiga makofi kule Kiteto - (kwa Lowassa), kijijini kwa Chenge, na kule Ntwara alikopigiwa makofi Nkapa.

It makes no sense kwa mtu mzima mwenye uwezo wa kubonyeza keyboard ya computer akasema maneno haya. Nisingeshangaa kama ningeyasikia maneno haya kwa mtu wa kijijini ambaye hata pesa ya kununua kandambili hana.

Binadamu ni tofauti na wanyama. Tumepewa "utashi" ambao kama tunautumia vyema hatuwezi kuwa na fikra za dizaini hizo.
 
womenofsubstanc

Sintoshangaa nikija ambiwa kwamba huyu ndugu yetu alikuwa mmojawapo wa waandamaji na wapiga makofi kule Kiteto - (kwa Lowassa), kijijini kwa Chenge, na kule Ntwara alikopigiwa makofi Nkapa.

It makes no sense kwa mtu mzima mwenye uwezo wa kubonyeza keyboard ya computer akasema maneno haya. Nisingeshangaa kama ningeyasikia maneno haya kwa mtu wa kijijini ambaye hata pesa ya kununua kandambili hana.

Binadamu ni tofauti na wanyama. Tumepewa "utashi" ambao kama tunautumia vyema hatuwezi kuwa na fikra za dizaini hizo.

usifufuke Yet mkuu maana kweli the likes of MASAKA watakwisha.Give them time to repent..so that they get saved.
 
mhh yatasemwa mengi tutumie akili kama ukumbi ulikuwa ushafungwa ina maana hata hao StarTV walikuwa nje na kamera zao.Zilitegwa vipi au zilikuwa nyuma yake zikimfata Andrea??

haya makubwa kama tv nazo zinaamini mambo ya ushirikina ambao unapigwa vita tanzania na afrika nzima.

UDAKU......

muda mfupi kabla ya mafundi wa StarTV kuondoka; haikutokea usiku wa manane. Na anayedhania ni udaku akalaghe bao.... hivi sasa kuna uchunguzi mkali unaendelea hapa. Kwenye kichwa cha habari sikusema utaalamu wa jadi a.k.a ushirikina. Mimi ni nzi sina imani za kishirikina, nafuata uchafu popote ulipo, naishi kwenye uchafu, nakula uchafu.. lakini mwenyewe nina afya. Hili ni kubwa mno hasa mkitoa imani za kishirikina pembeni.

ina maana hata huko bungeni, hawana wasaidizi ?? hii kitu nashindwa kuielewa, story nzima imekuwa badly staged, hivyo kuamini kwangu itakuwa vigumu ! Maelezo ya mtoa mada yanachanginyi !

Kiungani,

Bandiko linasema ukumbi ulishafungwa how comes waandishi wa Startv wabaki ndani ya ukumbi uliofungwa? ina maana walifungiwa ndani? Kwani hata Mh Chenge "aliposahau" kitu ilibidi "afunguliwe"

i cant afford to agree with this, cha msingi weka tapes ambazo zinadaiwa kuwepo ! other wise, this will be another ball rolling, huku watu wasidiscuss alichosema zitto ! maelezo yooote haya is nothing compared to a five second movie clio, tuonyesheni hata kidogo na tujudge wenyewe, lakini kujudge kutokana na maneno yanayotungwa, is like playing with our heads !


Pollonium 210 - Inabebwa vipi?


Polonium (pronounced /pəˈloʊniəm/) is a chemical element that has the symbol Po and atomic number 84. A rare and highly radioactive metalloid,[1] polonium is chemically similar to tellurium and bismuth, and it occurs in uranium ores. Polonium has been studied for possible use in heating spacecraft. It is unstable; all isotopes of polonium are radioactive.
 
Wewe Kitila, utakuwa kiongozi wa Tanzania bila ya kwenda Bagamoyo? Vipi mkuu unafikiri ni bure? Wakuu kina Zitto wanahitaji kukufunda mkuu,

Yaani bila sangoma na songi songi itakuwaje huwezi kuwa hata katibu tarafa vipi mkuu chi yako unakuwa kama mgeni?

mzee mbona wanivua nguo hadharani
 
bado hii inajadiliwa kwa kufikiria ushirikina. Tangu mwanzo mada hii haikutajwa kuhusika na ushirikina... lakinin sijui kwanini tumeelemea kwenye teknolojia ya ushirikina? I kenti bilivu zisi...
 
Posted Date::6/14/2008
Tuhuma za ushirikina Bungeni zafikishwa polisi
Na Midraji Ibrahim, Dodoma

SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta amesema suala la mbunge na afisa mmoja wa bunge kuzunguka na kunyunyiza vitu vinavyohisiwa vya kushirikiana kwenye kiti viti vya wabunge limekabidhiwa kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma (RPC) na Idara ya Usalama wa Taifa.


Akizungumza baada ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi

(NEC-CCM) jana, Sitta alisema Kaimu Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah amekabidhi suala hilo kwa RPC na usalama wa taifa kwa ajili ya upelelezi.


''Tukio lipo na kamera sita zilikuwa zimezimwa, lakini moja ililinasa ingawa picha imefifia, sasa tumekabidhi kwa RPC na usalama wa taifa watachezesha kuanzia mwanzo wa tukio mpaka mwisho baadaye tutapata taarifa,'' alisema.


Sitta alisema, sio vizuri hivi sasa kuzungumzia kwa undani tukio hilo kwa sababu, linahitaji upelelezi na kwamba, picha hiyo inaonyesha watu wawili wakipita kwenye viti vya wabunge.


Aliongeza tukio hilo limeshtua bunge kama taasisi na kuangalia uwezekano wa kuweka ulinzi kwa saa 24, huku akisema pia sio suluhisho kwa sababu waliongia ndani ya ukumbi kwa tukio hilo wanaruhusiwa kutokana na nafasi zao.


''Nayo inakuwa vigumu kwa sababu huyu ni mbunge na mwingine ni katibu wa bunge, huwezi kuwazuia inawezekana wameacha makabrasha yao ndani utawazuiaje?'' alihoji Sitta.


Kuhusu tukio hilo kuhusishwa na kuugua ghafla kwa Mbunge wa Kyela (CCM), Dk Harrison Mwakyembe, alisema ni fikira tu na kuongeza kuwa, inawezekana watu wanahusisha matukio hayo kutokana na watu hao kuonekana kwenye kiti cha mbunge huyo.


Spika alisema, uvumi wa juzi kuwa mbunge huyo alikuwa amefariki dunia,

unashangaza kwa sababu muda huo walikuwa pamoja nyumbani kwake akimwelezea jinsi alivyoanza kujisikia vibaya.


''Jana (juzi) wakati uvumi ukienea, nilikuwa na Dk Mwakyembe nyumbani kwangu akinielezea kuwa jinsi alivyoanza kujisikia kabla ya kuzidiwa. Aliniambia alikuwa akiniandikia ujumbe kuniuliza jana yake (Jumatano) hakuniona, lakini kabla ya kumalizia akaishiwa nguvu,'' alisema Sitta.


Alisema baada ya kuishiwa nguvu, Mbunge wa Lupa (CCM), Victor Mwambalaswa alimuona na kumsaidia.


Hata hivyo, Sitta alisema, alizungumza na daktari aliyemhudumia na kumweleza kwamba, Dk Mwakyembe alikuwa na msongo wa mawazo (stress) na kuongeza kuwa, inawezekana alikuwa amefanya kazi kwa muda mrefu bila kupumzika.
 
Kwenye darubini ya daktari inaweza kuonekana kuwa msongo wa mawazo lakini in reality ikawa ni kitu tofauti kabisa.
 
13New.JPG


Yule ni kama Muungwana anaingia pale au? Na mzungu mbele ya Muungwana nani yule ,au ni shemeji yake, Mrs. Sinclair? Jim aangalie!

Halafu hivi kwa nini Wangwana wa Bongo wanatembea na wa-Mura badala ya makachero wa kiraia?

Hamna kibaya sana, isipokuwa ila tu nadhani Vasco anapoenda sehemu sehemu kazungukwa na wa-Mura, anapoteza image of a civilian president.

Huyo mbele ya Muungana na Mama Sinclair, Kwi kwi kwi...
 
Aliyeingia bungeni usiku atajwa

na Martin Malera, Dodoma
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kapteni John Chiligati, jana alimtaja mbele ya waandishi wa habari mbunge ambaye aliingia katika ukumbi wa Bunge jioni ya Jumatatu.

Tukio hilo linahusishwa na ushirikina kwa mujibu wa taarifa zisizo rasmi, ambazo zimekuwa zikisambaa kwa muda wa siku tatu zilizopita.

Ingawa hakumtaja kwa jina, Chiligati alisema kuwa mbunge huyo alikuwa waziri lakini sasa hana tena wadhifa huo.

Akifafanua, Chiligati alikiri kuwa mbunge huyo aliomba na kupewa ruhusa kuingia ndani ya ukumbi huo wa Bunge, ili kukagua na kuangalia nafasi atakayokuwa anaketi.

Alisema kuwa mbunge huyo alilazimika kufanya hivyo kutokana na kutokuwa na kiti maalumu cha kukalia ndani ya Bunge kutokana na kuondoka kwake kutoka katika wadhifa wa uwaziri.

Chiligati alisema kwamba, kwa kuwa Bunge lilikuwa linaanza vikao vyake siku inayofuata, mbunge huyo aliona ni busara kutafuta mahali pa kukaa jioni hiyo, ili asisumbuke asubuhi.

Alikiri kuwa ni kweli aliingia ndani ya ukumbi wa Bunge na kupita katika kila kiti, akiangalia majina kwa lengo la kutafuta kiti kilichokuwa wazi.

Alisema wakati akifanya hivyo, hakuweka uchawi wowote kama ambavyo inadaiwa na watu hivi sasa.

Kwa taratibu za Bunge, kila kundi ndani ya Bunge hilo lina mahali pake maalumu pa kukaa kwa mpangilio unaoeleweka. Makundi hayo ni pamoja na mawaziri, ambao huketi upande wa kuume kwa Spika, wapinzani, ambao huketi upande wa kushoto wa Spika na wabunge wengine ambao hukaa katika nafasi zilizosalia.

Chini ya utaratibu huo, mpangilio wa kukaa hupangwa mwanzoni mwa Bunge, ambapo kila mbunge hupangiwa kiti chake cha kukaa. Hata hivyo, wabunge wanaruhusiwa kuhama kwa muda kwenda eneo jingine na wanapomaliza dharura hiyo hurejea kwenye viti vyao.

Spika Samuel Sitta, naye alishathibitisha kuwa, zipo picha zinazomuonyesha mbunge huyo akiwa ameandamana na mtumishi mmoja wa Bunge, akipita katika viti kadhaa ndani ya ukumbi huo wakati ukiwa umefungwa.

Ingawa Sitta na Chiligati waliepuka kumtaja mbunge huyo kwa jina, lakini kiongozi ambaye alikuwa waziri na kujiuzulu katika siku za hivi karibuni ni Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge.

Chenge alijiuzulu kutokana na kuhusishwa kwake kwenye uchunguzi unaoendeshwa na Taasisi ya Kuchunguza makosa ya rushwa ya Uingereza (SFO).

Makachero wa SFO walivutika kumchunguza Chenge katika uchunguzi wao dhidi ya Kampuni ya Bae Systems ya Uingereza iliyoiuzia Tanzania rada kwa bei ya juu.

Licha ya kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati mkataba wa mauzo hayo unafikiwa, makachero wa SFO walimkuta Chenge akiwa na akiba ya takriban dola za Marekani milioni moja kwenye akaunti iliyo katika benki moja katika visiwa vya Jersey.

Tangu ajiuzulu nafasi hiyo, Chenge hajawahi kuhudhuria vikao vya Bunge, na ni kweli hivi sasa anawajibika kutafuta nafasi ya kukaa kwa kuwa hataweza tena kukaa katika nafasi ya mawaziri aliyokuwa akikaa zamani.

Tukio hilo limewaweka wabunge roho juu, hasa baada ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, kuugua ghafla katikati ya wiki iliyopita na kulazimika kukimbizwa katika kliniki ya Bunge ili kupata huduma za kiafya.

Wabunge kadhaa sasa wanaonekana kuogopa kuusogelea ukumbi wa Bunge, kutokana na taarifa hizo za kuwepo kwa vitendo vya kishirikina.

"Hili tukio limetutia hofu, tunadhani kuna kila sababu ya kukamilisha uchunguzi wa tukio hili mapema. Spika ameeleza kuwa tukio hili linachunguzwa, tunaomba lichunguzwe kweli, tena kwa haraka, ili kutuondolea hofu tuliyonayo sasa," alisema mmoja wa wabunge kutoka Mkoa wa Mwanza.

Mbunge mwingine ambaye pia hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alilieleza gazeti hili kuwa Spika anapaswa kutoa taarifa ya tukio hili bungeni na kulitolea ufafanuzi badala ya kuendelea kulizungumza kwenye vyombo vya habari.

"Hizi taarifa zipo, wabunge wengi wanazijua, lakini Spika analizungumzia kwenye vyombo vya habari. Mimi nadhani suala hili linagusa maisha yetu, ni bora akalieleza Bunge nini kilitokea," alisema mbunge huyo.

Akizungumza na waandishi juzi, Sitta alisema kuwa, ofisi yake imekabidhi picha za video zilizomnasa mbunge huyo akiwa ameambatana na Ofisa Mwandamizi wa Bunge kwa siri, waliokuwa wakiweka vitu vinavyoaminika kuwa vya kishirikina au aina fulani ya sumu kwenye kila kiti cha mbunge.

Kwa mujibu wa Sitta, picha za mkanda huo zilizonaswa na kamera za usalama zilizomo ndani ya jengo hilo la kisasa, zimefifia kiasi cha kushindwa kubaini kwa haraka watu wanaoonekana ndani ya mkanda huo.

Kutokana na hali hiyo, Sitta alisema ofisi yake imeamua kuukabidhi mkanda wa picha hizo kwa maofisa usalama wa taifa na kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, kwa ajili ya kuzifanyia uchunguzi zaidi.

Source: Tanzania Daima

Chiligati tunakuheshimu sana kama huna kazi kaa kimya kuliko kuleta propaganda katika maisha ya watu. Ina maana huyo "Mwanga" hajui kiti cha spika?
 
No! Chenge the wizard ooops sorry .... the night dancer ... maybe he mistook the bunge for a night club!!!
 
Back
Top Bottom