Chenge ajiuzulu!

Mimi nitaungana na wewe baada ya Kikwete kukamata walioiba fedha BOT (EPA), Meremeta & Tangold, Twin Towers (BOT), Richmond na Import Support. Sioni kama ni ujasiri kwa haya yaliyotokea.

Bado Kikwete na Serikali yake wameshindwa kuwa wawazi, waseme basi Chenge aliandika hiyo akaunti kwenye fomu ya maadili?

Ila nitakuwa si mkweli nisipokubali kwamba Kikwete amefanya vizuri kuvipa uhuru vyombo vya habari, namwombea kwa Mungu ili aendelee kuwa mvumilivu na kuviacha vyombo vya habari vifanye kazi yake.

Well, Chenge hakuiandika hilo kwenye fomu ya kamati ya maadili.

JK hakua akijua hilo, alivyojua umeona kilichofanyika. Hawa watu wana hela nyingi sio vizuri kukurupuka na kuwa kamata, tutakosa hata kidogo walichobakisha, twendeni taratibu tuondoe nguvu ya kipesa wanachoringia then TUNAWAMALIZA.

JK kazi nzuri Muungwana tupo nyuma yako katika haya mambo!
 
Aidha, waandishi walipotaka kujua kama kiongozi huyo ameorodhesha mali zake kwenye fomu ya Tume ya Maadili kama ambavyo sheria inaelekeza, Pinda alisema fomu za kiongozi kuorodhesha mali ni suala binafsi, hivyo si rahisi yeye (Waziri Mkuu) kufahamu kiasi cha mali alizonazo ama alichoorodhesha.

http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/4/21/habari3.php

Naomba msaada ni kweli kuorodhesha mali ni la siri????
 
tunamtaka Rais JK aje hapa atuombe radhi watanzania wote kwa kutuchagulia viongozi mafisadi.
na tuombe radhi tena kwa kutuchagulia viongozi mafisadi mara mbili kwenye baraza lake.

na aje atuombe radhi KABISA kwa waziri mpya atakayetuchagulia kwa vile na huyu atakuwa bogust kama wale waliotangulia.

Rais hafanyi kazi hivyo, hata kama ni kweli sisi ndio tumemuajiri.

Kuchagua viongozi inabidi upewe information, vipi kama system haiko safi na anapewa uongo?. Msimlaumu sana tumpeni muda taratibu anasafisha.

Si unakumbuka Chenge alisema HAJIUZULU? nini unafikiri kimemfanya ajiuzulu?

BIG UP to Muungwana.
 
WT na tushukuru mungu kwamba ile list ya MAFISADI inapungua hongera JF uzi uwe huo huo lakini pia tuwe na mikakati ya nani afuatie baada ya Chenge. Mi nadhani wa kufuatia sasa ni huyu bosi wa PCB Mr Hosea, anahitaji na yeye kuachia ngazi vile vile
 
Tunasubiri kwa hamu MAGUFULI wetu arudishwe miundo mbinu ili akarekebishe mambo ambayo CHENGE alianza kuyaboronga boronga. Nimeamini na kujifunza kuwa: UFISADI + UJEURI= KUKOSA HESHIMA MBELE YA JAMII.

Yes i sadi na nimeshaanzisha Thread,Magufuli is the right person to solve our Infrastructure problems that we have.Chenge hajawahi kujenga barabara toka awe waziri
 
FD, habari za chenge hakuna asiye zijua.
na kunifanya niamini kuwa kikwete alikuwa anafikiri Chenge ni mtu mwema ni ngumu. tena si ngumu kidogo, ni ngumu sana.
ukinambia alimchagua kwa kuwa hakuwa na choice vile alikuwa anajibu fadhila, nitakuelewa kidogo. lakini sio kwa kusema alikuwa hamjui chenge.
 
Rais hafanyi kazi hivyo, hata kama ni kweli sisi ndio tumemuajiri.

Kuchagua viongozi inabidi upewe information, vipi kama system haiko safi na anapewa uongo?. Msimlaumu sana tumpeni muda taratibu anasafisha.

Si unakumbuka Chenge alisema HAJIUZULU? nini unafikiri kimemfanya ajiuzulu?

BIG UP to Muungwana.

amejiuzuru baada ya kugundua watu wanaujua utajiri wake ulivyomkubwa hasa baada ya ndugu yangu katika mapambano Saed kubenea kumwanika wazi wazi.
 
You are right, Hiyo ndio Style ya Kikwete na wazaramo wote, kujikosha, hawapendi kuonekana wabaya kila upande


Chonde...KIKWETE siyo mzaramo japo anapenda sana kujiita mzaramo..huyu mtu ni mkwere. I am deeply offended kwa kugeneralize "WAZARAMO WOTE" huyo BANGUSILO kuvurunda haimaanishi wote tumevurunda...sasa ukianza kuwasema wazaramo, wachaga na wanyakyusa utasemaje?

kuhusu JK narudia: NGURUWE KUZALIWA KWENYE ZIZI LA NGOMBE HAKUMFANYI KUWA NI NGOMBE..ATABAKI NGOMBE TUUU

endelea kukata issues
 
Arudishe vijisenti vyetu; abaki na hela zake; BUngeni afukuzwe kwa kuzalilisha nchi nzima; nasikia ana Bil 15; hicho kisiwa nasikia huwa kinatumiks kutunzia hela chafu za wanasiasa; kweli hiyo; je kuna wengine wanazo huko; waangalieni akina Ben, Pesa2;Balala; nk je hawajaweka pia huko?
Zitto alishatoa Azimio la Kupambana na Kulinda rasilimali; kweli nchi iko ktk mapambano; mengine yaja zaidi!!
 
Chenge kafukuzwa hakujiuzulu.
  1. Majuzi akiongea na waandishi, Chenge alisema hatajiuzulu.
  2. Jana Kikwete akaingia DSM akitokea NYC, nafikiri hakusubiri hata hotuba ya Pope UN.
  3. Then, jana hiyo hiyo, Chenge anatangaza kuomba msamaha kwa kutumia neno vijisenti.
  4. Leo hii anatangazwa kuwa amejiuzulu.
Hivi hii ni trend ya kujiuzulu au amefukuzwa?

Kama amefukuzwa au kulazimishwa kujiuzulu (which is one and the same), kwa nini alidhani kuwa hatafukuzwa? Lipi lililokuwa linalazimisha yeye kuwapo madarakani hata baada ya kukataliwa na umma? Haya maswali yanahitaji majibu.




LOWASSA alijiuzulu au kufukuzwa..?

balali alijiuzulu au kufukuzwa..?

nadhani hoja hapa iwe ameondoka basi!!

njia aliyoondokea anaijua yeye..

kwani warren G ..WETU Hapendi kumuudhi mtu..au hawezi kumuambia mtu jambo usoni...sijapata kusikia tangazo kutoka ikulu likisema.."..rais ...ameamua kumfukuza kazi....kwa kosa la..." muda mrefu sasa....



Ndio maana inabidi ajiuzulu au aondolewe na Bunge. Kazi imemshida Vasco da Gama.
 
Ndio! Pesa zirudishwe! Ikiwezekana afilisiwe kabisa... haiwezekani kwa mshahara wake awe na pesa zote hizo, haiwezekani! Biashara gani mtu ufanye upate pesa zote hizo kama si rushwa alizojipatia kwa kusaini au kufanikisha kutuingiza kwenye mikataba ya kifisadi? Uchunguzi ukamilishwe na tupewe ripoti kamili. Ikiwezekana, iundwe Kamati Teule ya Bunge kuchunguza ufisadi huu... usanii sasa basi!
 
Aidha, waandishi walipotaka kujua kama kiongozi huyo ameorodhesha mali zake kwenye fomu ya Tume ya Maadili kama ambavyo sheria inaelekeza, Pinda alisema fomu za kiongozi kuorodhesha mali ni suala binafsi, hivyo si rahisi yeye (Waziri Mkuu) kufahamu kiasi cha mali alizonazo ama alichoorodhesha.

http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/4/21/habari3.php

Naomba msaada ni kweli kuorodhesha mali ni la siri????


Sidhani kama alichozema waziri mkuu ni sahihi, fomu hiyo sio suala binafsi bali ni public kama ingekuwa suala binafsi kwa nini serikali walirelease information kwenye magazeti ?

Mimi nadhani waziri mkuu ameonyesha dhahiri ya kuwa yeye pia ni mmoja wao kwa kujaribu kuwadefend hawa viongozi baada ya kudefend katiba ya nchi. Nilikuwa naomba wale wataalamu wa sheria watusaidie manake kuna mtu aliraise point nzuri sana kwamba sheria za nchi aziruhusu mtanzania kufungua account nje bila idhini ya benki kuu , jee habari hizi ni za kweli ? Kama ni kweli basi tutakuwa na kesi nzuri sana juu ya Chenge.

Pia mimi naami ya kuwa Rais wetu pia ana makosa makubwa sana . Aliambiwa ya kuwa huyu mtu afukuzwe baada ya ripoti ya Richmond lakini akufanya hivyo , halafu watu wengi awalizungumzii nadhani tuna tatizo kubwa sana. Haiwezekani katika kipindi cha miaka mitatu mawaziri watano wa baraza lako wajiuzulu kutokana na rushwa je hii inatuambia nini ? Mimi naona hapa kuna vitu vitatu either Rais akufanya homework zake vizuri au na yeye pia ana belong katika hilo group au BOTH !
 
Hili sio tatizo la JK!!! Ni tatizo la kitafa...

  1. Nani alimchagua Chenge kuwa Mbunge ambayo ndiyo sifa no.1 ya kuchaguliwa kuwa waziri?
  2. Nani alimchagua Chenge kuwa mjumbe wa NEC ya CCM? JK au wanaCCM?
Kuwa makini kidogo, Sio kila kitu ni cha Rais vingine ni vya jamii nzima tuliyonanyo!!! sasa imebadilika... lazima tuelewe hivyo... Na JK anatuongoza vyema kwenye mabadiliko haya kwa kukubali wanaojiuzulu wajiuzulu...

Umesahau swali la tatu.
3. Ni nani ambaye alimteua Chenge kuwa Waziri, hata baada ya kupewa ushauri kuwa asimteue?

Kuchaguliwa kwa Chenge kuwa mbunge na mjumbe wa vitu gani sijui hakukumlazimisha JK kumteua kuwa Waziri.
 
Nimesoma thread hii ndefu sana na ninayo machache ya kuchangia
(1) Tangia siku ya kwanza alipoleta baraza kuuuuuuubwa, JK alionekana ni mlipa fadhila na hatakuja na jipya
(2) Alipopewa angalizo la kutopandisha kodi za mafuta kwa kuwa ataathiri uchumi mzima, akakataa yeye na Meghji kwa madai kuwa hapo ndo tutapata hela maana kila mtu atumia mafuta, aliashiria kuwa Rais asiyetumia walau elimu yake ya uchumi aliyopata UDSM
(3) Shutuma za ufisadi zilipotolewa na yeye hakuona ni vema kuzishughulikia, saaaaana akiwa kanisani alitoa mwito wa watu wa kutokuwa mahakimu, aliendelea kujaza kikombe chake cha kuwa Rais asiye msikivu wa kilio cha wananchi wake
(4) Hata baada ya Lowassa kuanguka, anakuja na maneno ya kuwa alikuwa mchapakazi na kumlilia, alielekea kutoona haja ya kuwa Rais makini mwenye kulinda maslahi ya walio wengi
(5)Chenge alisemwa na wengi kutoingia baraza jipya ambalo nalo liko hoi tu kama la mwanzo...JK kwangu mimi nilimwona ana mkono katika ufuska huu wa VIJISENTI

Mimi nakubaliana na wote wanaosema amevipa vyombo vya habari uhuru..lakini utendaji wake ni wa mashaka, woga, kulipa fadhila, na ni sifa zisizofaa kwa kiongozi mkubwa wa nchi.

Ninaomba wana JF, tuchangie nini kifanyike ili Chenge, Mkapa na mkewe, Yona, Abdala Kigoda, Mramba, Rutabazimbwa, Mgonja, Lowassa, Rostam, Karamagi (orodha ni ndefu) wafanyiwe ili tuondokane na jinamizi hili la ufisadi...

Huwa naona suluhisho moja ambalo haliwezekani kwa wengi
ASSASSINATION (one after another) huenda wataogopa? huenda CCM watafunguka macho waone hee kumbe hivi viti vya moto eeh??
 
Sitaki ieleweke kwamba Wabunge na Madiwani wa CCM hawana haki ya kuikosoa Serikali. Wanayo haki hiyo. Lakini, kuna tofauti ya kukosoa utekelezaji wa sera, ambao ni wajibu wa Wabunge na Madiwani wa Chama Tawala; na kukosoa sera yenyewe, ambao ni wajibu wa Wabunge na Madiwani wa Upinzani. Katiba na busara zinataka tupambanue wapi na lini tukosoe sera na utekelezaji wake. Mbunge na Diwani lazima aamue yuko upande gani

haya ni maneno ya mzee mkapa.

Chama Cha Mapinduzi ndicho hasa kiongozi wa nchi hii. Au tuseme hivyo ndivyo inavyopasa kuwa. Chama kwanza, mtu baadaye. Ndiyo maana huko nyuma tukasema, "Chama legelege huzaa Serikali legelege". Nami leo naongeza: Chama shupavu, huzaa viongozi shupavu.

na haya hapa tena.

Mtaalamu mmoja wa menejimenti alisema: "Wajibu wa kwanza wa kiongozi ni kuwafafanulia anaowaongoza hali halisi." Kama Chama Cha Mapinduzi kinataka kuendeleza sifa zake za uongozi, na nguvu yake katika siku za usoni, lazima kiwe chama shupavu, chama kisichoogopa kusimamia maadili yake, chama kisichoogopa kusema ukweli, chama cha kuwafafanulia wananchi hali halisi ya tulipo, na mahitaji na masharti ya mafanikio ya huko tuendako.

ukifuatilia kwa makini hotuba hii ya Courage of Leadership utaamini Mkapa alijua ni nini kitatokea pindi Jk atakapokuwa Rais.na hapa ndio alimaliza kabisa

Tunahitaji ushupavu wa uongozi. Nikiwaulizeni hapa mmojammoja, nina uhakika wengi watasema kuwa zimeanza kampeni za chinichini huko mikoani na wilayani. Wengine wameniambia wapo wenye mkakati wa kununua wajumbe wa Mikutano Mikuu ya Wilaya, Mikoa na hata Taifa. Kama ni kweli, ujasiri wa viongozi huko mliko wa kusimamia maadili uko wapi? Kwa nini sisikii viongozi wa CCM wanaokerwa na hali hiyo wakiikemea katika vikao vya ndani? Kwa nini taarifa za namna hiyo haziji rasmi, kwa taratibu zetu, lakini zinakuja kwa njia ya tuhuma, minong'ono na kupakana matope? Waasisi wetu wasingekuwa jasiri na shupavu tusingepata uhuru, wala kufanikisha Mapinduzi matukufu ya Zanzibar. Ujasiri na ushupavu wetu sisi, tunaodai haki ya urithi wa waasisi wetu, uko wapi?
 
Nimesoma thread hii ndefu sana na ninayo machache ya kuchangia
(1) Tangia siku ya kwanza alipoleta baraza kuuuuuuubwa, JK alionekana ni mlipa fadhila na hatakuja na jipya
(2) Alipopewa angalizo la kutopandisha kodi za mafuta kwa kuwa ataathiri uchumi mzima, akakataa yeye na Meghji kwa madai kuwa hapo ndo tutapata hela maana kila mtu atumia mafuta, aliashiria kuwa Rais asiyetumia walau elimu yake ya uchumi aliyopata UDSM
(3) Shutuma za ufisadi zilipotolewa na yeye hakuona ni vema kuzishughulikia, saaaaana akiwa kanisani alitoa mwito wa watu wa kutokuwa mahakimu, aliendelea kujaza kikombe chake cha kuwa Rais asiye msikivu wa kilio cha wananchi wake
(4) Hata baada ya Lowassa kuanguka, anakuja na maneno ya kuwa alikuwa mchapakazi na kumlilia, alielekea kutoona haja ya kuwa Rais makini mwenye kulinda maslahi ya walio wengi
(5)Chenge alisemwa na wengi kutoingia baraza jipya ambalo nalo liko hoi tu kama la mwanzo...JK kwangu mimi nilimwona ana mkono katika ufuska huu wa VIJISENTI

Mimi nakubaliana na wote wanaosema amevipa vyombo vya habari uhuru..lakini utendaji wake ni wa mashaka, woga, kulipa fadhila, na ni sifa zisizofaa kwa kiongozi mkubwa wa nchi.

Ninaomba wana JF, tuchangie nini kifanyike ili Chenge, Mkapa na mkewe, Yona, Abdala Kigoda, Mramba, Rutabazimbwa, Mgonja, Lowassa, Rostam, Karamagi (orodha ni ndefu) wafanyiwe ili tuondokane na jinamizi hili la ufisadi...

Huwa naona suluhisho moja ambalo haliwezekani kwa wengi
ASSASSINATION (one after another) huenda wataogopa? huenda CCM watafunguka macho waone hee kumbe hivi viti vya moto eeh??

You mean political assasination or not.... ?. otherwise huu ni ushauri wa hatari sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom