FairPlayer
JF-Expert Member
- Feb 27, 2006
- 4,145
- 716
Mimi nitaungana na wewe baada ya Kikwete kukamata walioiba fedha BOT (EPA), Meremeta & Tangold, Twin Towers (BOT), Richmond na Import Support. Sioni kama ni ujasiri kwa haya yaliyotokea.
Bado Kikwete na Serikali yake wameshindwa kuwa wawazi, waseme basi Chenge aliandika hiyo akaunti kwenye fomu ya maadili?
Ila nitakuwa si mkweli nisipokubali kwamba Kikwete amefanya vizuri kuvipa uhuru vyombo vya habari, namwombea kwa Mungu ili aendelee kuwa mvumilivu na kuviacha vyombo vya habari vifanye kazi yake.
Well, Chenge hakuiandika hilo kwenye fomu ya kamati ya maadili.
JK hakua akijua hilo, alivyojua umeona kilichofanyika. Hawa watu wana hela nyingi sio vizuri kukurupuka na kuwa kamata, tutakosa hata kidogo walichobakisha, twendeni taratibu tuondoe nguvu ya kipesa wanachoringia then TUNAWAMALIZA.
JK kazi nzuri Muungwana tupo nyuma yako katika haya mambo!