Chenge ajiuzulu!

Ni kweli kuna watu wengine hatumjui huyu Dr.Mauwa Daftari, Je unaweza kutuelimisha zaidi kuhusu mtu huyu. najua muda ni mali ila kwa kitu kama hiki sidhani kama utakuwa unaupoteza bali utakuwa unautumia ipaswavyo. Kwanza nataka kujua kama ni Dr. wa watu au ni title? Unaweza kutufahamiasha ana sifa gani za kuweza kuongoza wizara nyeti kama hiyo? sio kwamba ninam-grill ila naogopa kurudia makosa. Haitakuwa the same kama la aliyetangulia lakini impact yake ni ile ile...kurudisha maendeleo nyuma au kuwanyima wananchi accessibility previlage. Kama mlivyosema watu wengi wanasoma michango yetu, basi tuwe waangalifu tusiwapotoshe kwenye maamuzi yao.


Kwa kukumegea kidogo tu

Waziri aomba Mahakama Kuu imfutie kesi

Na Grace Michael

NAIBU Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Maua Daftari ameiomba Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam kutupilia mbali kesi ya madai ya sh. milioni 500 iliyofunguliwa dhidi yake na mfanyabiashara, Bi. Fatma Salmin kwa kumkashifu.

Katika utetezi wake uliowasilishwa Mahakamani hapo mwishoni mwa wiki kupitia wakili wake, Bw. Peter Swai, Dkt. Daftari alieleza kuwa kesi hiyo namba 34/2008 haina msingi wowote kwa kuwa mdai hana kigezo cha kusimamia madai hayo.

Dkt. Daftari alidai kuwa madai ya mfanyabiashara huyo hayana msingi wowote kwa kuwa hakuna maneno yoyote yenye kashfa aliyoyatoa yenye lengo la kumkashifu kama ilivyodaiwa kwenye hati ya madai ya mlalamikaji....
http://www.majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=6401
 
According to the dataz, ni kwamba alikuwa na barua ya kujiuzulu tayari toka akiwa u-China, ndio maana hakwenda US, hizi filimbi za vijisenti alikuwa anazuga tu kwani alikuwa tayari amemfahamisha rais walipopata habari tu kule China kuwa anajiuzulu mara moja,

More dataz ni kwamba kuna wanasiasa wa hapa bongo wakishirikiana na wa UK hasa Blair, wanamshinikiza Brown, asimamishe uchunguzi wa Radar uliomponza Chenge..........!

tunaendelea kuzitafuta dataz on how it happened.....mpaka Chenge kujiuzulu!

so aliona a-make scene b4 hajaondoka? bad idea!!!!!!!!!
 
Andrew Chenge ajiuzulu

na Tamali Vullu

WAZIRI wa Miundombinu, Andrew Chenge, amejiuzulu wadhifa huo kuanzia jana kwa kile alichoeleza kuwa ni kulinda masilahi ya taifa.

Chenge, ambaye anakabiliwa na tuhuma za kumiliki zaidi ya dola milioni moja za Marekani katika akaunti yake iliyopo Kisiwa cha Jersey, nchini Uingereza, jana alimwandikia Rais Jakaya Kikwete barua ya kuomba kujiuzulu, ambayo rais aliiridhia.

Akizungumza kwa njia ya simu na Tanzania Daima jana usiku, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salvatory Rweyemamu, alithibitisha rais kupokea barua ya Chenge ya kuomba kujiuzulu wadhifa wake.

Alisema rais aliridhia barua hiyo, huku akimkariri akisema kuwa kwa mazingira ya wakati huu uamuzi huo unafaa kuchukuliwa.

Aidha, mkurugenzi huyo akikariri barua ya Chenge, alisema amefikia uamuzi huo ili kulinda masilahi ya nchi pamoja na kwamba uchunguzi wa suala hilo bado unaendelea.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa uamuzi huo wa Chenge umefikiwa baada ya mashauriano kati yake na Rais Kikwete.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa kufikiwa kwa uamuzi huo hakumaanishi kukiri tuhuma hizo, bali kutambua uzito wa tuhuma zinazomkabili.

Aidha, habari zinaeleza kuwa uamuzi huo wa Chenge umechangiwa na dhamira yake ya kuitisha mkutano na waandishi wa habari na kuzungumzia kwa kina tuhuma hizo.

Wiki iliyopita, gazeti la The Guardian la nchini Uingereza liliandika kuwa, katika uchunguzi wa SFO iligundulika akaunti moja inayohusishwa na Chenge ikiwa na zaidi ya dola za Marekani milioni moja iliyopo kwenye Kisiwa cha Jersey.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, SFO inamchukulia Chenge kuwa mtu anayeweza kuwa shahidi muhimu katika uchunguzi wa zabuni ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE System ya nchini Uingereza.

Gazeti hilo liliandika kwamba, SFO inatarajia kuanza upya kufanya uchunguzi kuhusu fedha hizo, ili kuangalia iwapo zina uhusiano na zile zinazoaminika kutolewa kwa njia ya rushwa wakati Tanzania iliponunua rada ya kijeshi kutoka nchini humo kwa paundi milioni 28 ambazo ni sawa na sh bilioni 70, mwaka 2002.

Hata hivyo, inaaminika kwamba uchunguzi wa SFO unatarajia kuanza katika kipindi cha wiki sita zijazo ingawa ule wa awali ulionyesha kuwa moja ya mambo yanayofuatiliwa ni kujua iwapo fedha zinazoaminika kuwa za Chenge zina uhusiano na zile zilizotoka katika Kampuni ya BAE inayotuhumiwa kuinyonya Tanzania kwa kuiuzia rada mbovu kwa bei kubwa kuliko ilivyotakiwa.

The Guardian katika habari yake hiyo iliyowekwa katika mtandao wa intaneti, linaripoti kuwa, taarifa hizo zinakuja ikiwa ni miaka mitatu sasa tangu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) kwa kushirikiana na SFO na taasisi za uchunguzi za Uswisi na Jersey zilipoanza kuchunguza kuhusu kashfa nzima ya ununuzi wa rada.

Gazeti hilo lilimkariri Waziri Chenge akikiri kwamba fedha hizo ni zake na akatumia fursa hiyo kukanusha kuwapo kwa uhusiano wowote kati ya fedha hizo na kashfa nzima ya ununuzi wa rada, uliofanywa wakati yeye akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Akizungumzia kwa mara ya kwanza tuhuma hizo Jumatano iliyopita, Chenge aliwataka Watanzania kusubiri uchunguzi dhidi yake unaofanywa na SFO.

"Tusubiri uchunguzi ukamilike... kama uthabiti ukithibitisha hata hivyo vijisenti, ijajulikana vilipatikanaje," alisema Chenge nje ya chumba cha wageni mashuhuri (VIP) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, akitokea nchini China.

Kutokana na kauli yake ya kuziita mabilioni ni vijisenti, wananchi walionyesha kukerwa na kauli hiyo kwa maelezo kuwa ni dharau, na kwamba huenda atakuwa akimiliki fedha zaidi ya hizo.

Pamoja na hayo, baadhi ya vijana wanaotoka katika vyama kadhaa vya upinzani mjini Dodoma walitangaza azima yao ya kuandamana, ili kumzuia asiingie bungeni wiki hii.

Kutokana na hali hiyo, Chenge alilazimika kuwaombva radhi Watanzania ambao walikwazika au kuumizwa na kauli hiyo.

Chenge alisema halikuwa lengo lake kuwakera wananchi kwa kauli hiyo iliyozua mjadala kiasi cha baadhi ya makundi ya watu wa kada tofauti kutoa maoni yao wakimtaka Rais Jakaya Kikwete amwajibishe.

"Mimi si Mzaramo. Hiki ni Kiswahili. Sisi wengine kule Usukumani kusema vijimambo, au vijisenti, vijitoto hivi ni kawaida kwa desturi zetu.

"Ndiyo maana napenda kusema wazi kwamba iwapo kuna Watanzania niliwaumiza kwa kauli ile niliyoitoa kwa nia njema kabisa na wala si kwa lengo la kuwakejeli, naomba radhi kwa hilo," alisema Chenge.

Chenge ni waziri wa nne kujiuzulu katika kipindi cha miezi miwili baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na aliyekuwa Waziri wa Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha kujiuzulu kutokana na kutajwa katika kashfa ya mkataba tata wa kuzalisha umeme wa dharura wa Kampuni ya Richmond.

Mawaziri hao isipokuwa Dk. Msabaha ni miongoni mwa orodha ya mafisadi 11 iliyotajwa na kambi ya upinzani, Septemba 15 mwaka jana katika viwanja vya Mwembe Yanga.

Aidha, Chenge alikuwa ni miongoni mwa wanasiasa walioandamwa hasa baada ya kurejeshwa tena serikalini, wakati wa mabadiliko ya mawaziri yaliyotokana na kuvunjika kwa Baraza la Mawaziri, Februari mwaka huu.

http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/4/21/habari2.php
 
Next ni kurudisha senti zetu!
Alafu JK nae anaonekana msanii wee kila leo mawazili wako wanabwaga manyanga at the end of the day itabidi nae abwage manyanga pia atleast asiendelee na second term hii ya kwanza yamtosha kabisaa
 
Hivi lets be real kidogo here....Swali...Chenge has 25 million and all these funds magically appeared recently (EPA, BOT?) also Tangold Money from Deep greenfinance, if he was just the funds man....How much did the higher ups make (Mkapa, Rostam, Lowassa, Muungwana and others)...anyone can give us a ballpark figure. I am certain the "vijisenti"comment referred as to who got what.

CHENGE NA WALE WOTE WALIOJIUZULU SIKU ZILIZOTANGULIA WALIPATA NYAZIFA ZAO KUPITIA UBUNGE, JE HAWAONI KAMA ITAKUWA NA MAANA ZAIDI WAKIRUDISHA NA MAJIMBO YAO? AU KASHFA ZAO ZINA MIPAKA? KAMA HAWAWEZI KUJIUZULU WENYEWE CHAMA CHA MAPINDUZI KINA FIKRA GANI KUHUSU HILO? INABIDI MWENYEKITI WAO ATUAMBIE!!!!!!!!!
 
Well said. Mimi nampongeza JK kwa yote aliyofanya mpaka sasa. Anayepinga pongezi zangu anaweza kuuliza kwanini nami nitajieleza.

1. Kama binadamu wa kawaida lazima uwe na soni. JK lazima alipe fadhila za kusaidiwa kwenye kampeni. Tatizo ni kuwa waliotoa fadhila hawakuwa wasafi.

2. JK ana moyo mzuri tu, anaacha chips zi fall zipendapo (ES), ameshaanza kuziachia zianguke, sasa anasafisha uwanja tayari kwa kuijenga nchi.

3. Uhuru we press, JK amejitahidi sana kwenye hilo, jamaa ni simply muungwana. System alio nayo (aliyorithi) ilikuwa imeshachafuka, huwezi kupiga system yooote chini mara moja, it takes some days/years kui clean up. Muungwana ameanza. tumpeni support.

Ni yangu machache hayo.
 
Well said. Mimi nampongeza JK kwa yote aliyofanya mpaka sasa. Anayepinga pongezi zangu anaweza kuuliza kwanini nami nitajieleza.

1. Kama binadamu wa kawaida lazima uwe na soni. JK lazima alipe fadhila za kusaidiwa kwenye kampeni. Tatizo ni kuwa waliotoa fadhila hawakuwa wasafi.

2. JK ana moyo mzuri tu, anaacha chips zi fall zipendapo (ES), ameshaanza kuziachia zianguke, sasa anasafisha uwanja tayari kwa kuijenga nchi.

3. Uhuru we press, JK amejitahidi sana kwenye hilo, jamaa ni simply muungwana. System alio nayo (aliyorithi) ilikuwa imeshachafuka, huwezi kupiga system yooote chini mara moja, it takes some days/years kui clean up. Muungwana ameanza. tumpeni support.

Ni yangu machache hayo.

KHERI WEWE UNASABABU ZA KUMWAMINI MIMI SINA HATA MOJA. KWANI ALIVYOKABIDHIWA OFISI ALIKABIDHIWA NA MAWAZIRI AU MAKATIBU? SI ALIWACHAGUA MWENYEWE/ kwanini aliwarudia wachafu? ILE NCHI INA WATU ZAIDI YA 37M, YEYE KWA KUTAKA KUMALIZA KAZI HARAKA AKACHUKUA WENZAKE ANAOJUANA NAO. NAJUA KUNA WATU AMBAO WANA KALE KATABIA KAKUTOKUPENDA KU-STRUGGLE( PHYSICALLY OR MENTALLY) HIYO SIO EXCUSE KAMA WATU WAMEKUAMINI NA KUKUPA NCHI KUIONGOZI. SO UNATAKIWA KUJIREKEBISHA MAPEMA AU USIGOMBEE KABISA URAIS. HIYO SIO NAFASI YA KUTEULIWA SO MTU ANAPOOMBA KURA LAZIMA AWE TAYARI KUWAJIBIKA HATA INAPOBIDI KWENDA EXTRA MILES.
 
Well said. Mimi nampongeza JK kwa yote aliyofanya mpaka sasa. Anayepinga pongezi zangu anaweza kuuliza kwanini nami nitajieleza.

1. Kama binadamu wa kawaida lazima uwe na soni. JK lazima alipe fadhila za kusaidiwa kwenye kampeni. Tatizo ni kuwa waliotoa fadhila hawakuwa wasafi.

2. JK ana moyo mzuri tu, anaacha chips zi fall zipendapo (ES), ameshaanza kuziachia zianguke, sasa anasafisha uwanja tayari kwa kuijenga nchi.

3. Uhuru we press, JK amejitahidi sana kwenye hilo, jamaa ni simply muungwana. System alio nayo (aliyorithi) ilikuwa imeshachafuka, huwezi kupiga system yooote chini mara moja, it takes some days/years kui clean up. Muungwana ameanza. tumpeni support.

Ni yangu machache hayo.

Mimi nitaungana na wewe baada ya Kikwete kukamata walioiba fedha BOT (EPA), Meremeta & Tangold, Twin Towers (BOT), Richmond na Import Support. Sioni kama ni ujasiri kwa haya yaliyotokea.

Bado Kikwete na Serikali yake wameshindwa kuwa wawazi, waseme basi Chenge aliandika hiyo akaunti kwenye fomu ya maadili?

Ila nitakuwa si mkweli nisipokubali kwamba Kikwete amefanya vizuri kuvipa uhuru vyombo vya habari, namwombea kwa Mungu ili aendelee kuwa mvumilivu na kuviacha vyombo vya habari vifanye kazi yake.
 
Wengi walisema hapa hapa Tanzania bila Mafisadi inawezekana. MAFISADI wanaweza kuondoka si kwa kutumia viongozi wetu bali kutumia nguvu ya UMMA. Kuondoka kwa Andrew Centis, ni kigezo kimojawapo tosha kuwa nguvu ya UMMA imemfukuza kazi.

Nategemea na wengine ambao si wasafi wakae mkao wa kula sasa hivi Lazima tushikane mashati hakuna haja ya kusubili 2010. Lazima watanzania wote popote tulipo tuunganishe nguvu kuondoa mzizi wa fitina uliopo nchini mwetu.

Suala linalotukabili siyo itikadi ya vyama ni utaifa. Pamoja na Mweshimiwa Andrew Centis kujiudhuru ana kesi za kujibu nyingi sana, Pesa amepata wapi, uchunguzi usio na upendeleo inatakiwa utumie mkondo wake. Haiwezekani tanzania kama taifa tukasubiri eti waingereza watoe majibu, kwani UK kwetu ni akina nani. Kwa nini basi brown asije kututawala? TUnatakiwa tufanye uchunguzi wetu wenyewe na mheshimiwa afikishwe panapostahili.

Pili wanasheria inabidi waangalie taratibu za Bunge hivi kwa nini huyu Mtu aendelee kukalia mahala pale patakatifu pa kutungia sheria wakati yeye si Msafi?
Je ataweza kuruhusu kupitishwa sheria ambayo itakwenda kinyume na UFISADI wake? Nafikiri CCM kwa hili itabidi wabebe mzigo ama kumfukuza chama au wasubiri kwenye Uchaguzi hili wananchi tuwajumuishe na mafisadi.

Tanzania imekuwa kawaida yetu mtu akijiudhuru anaendelea kufaidi matunda ya wizi wake tunaona leo EL, Karamagi, Msabaha na wengine wakiendelea kusherekea kwa mavuno waliopata wakati wakiwa viongozi. sasa Andrew ataendelea kuvuna mapato aliyoyapata.

Hapa kuna haja ya kukusanya data za kuweza kuwafikisha watu hawa mahakamani hata kama itakuwa baada ya watu wanaowakingia vifua kutoka maofisini.

Mwisho kuna haja ya JK kuwa makini asilimia 80% ya kura alizozipata sijaona kama kweli ameonyesha kuwa alistahili kuzipata. Huwezi kutawala na viongozi wabovu. Kuna wengi bado wapo kwenye Serikali, makatibu wakuu, mawaziri nk.

Kama kweli JK ni Msafi tunategemea katika kujaza nafasi ya Andrew Centis, kuondoa wabovu wote asisubiri nguvu ya UMMA iwafikie
 
Ila nitakuwa si mkweli nisipokubali kwamba Kikwete amefanya vizuri kuvipa uhuru vyombo vya habari, namwombea kwa Mungu ili aendelee kuwa mvumilivu na kuviacha vyombo vya habari vifanye kazi yake.

Nani anayo ile List of Shame,Nadhani tungeanza na watu wote waliopo pale bila kuangalkia nani abaki..ila haya yote Mzee Mkapa aliyasema katika hotuba yake ya Courage of Leadership.

Alimjua Jk na ndio maana liyasema haya,Mie sidhani kama hii inamsaidia Jk ila inambomoa Muungwana.nadhani anahitaji msaada mkubwa na kuongeza washauri zaidi ili mambo yasizidi kwenda mrama.
 
Next ni kurudisha senti zetu!
Alafu JK nae anaonekana msanii wee kila leo mawazili wako wanabwaga manyanga at the end of the day itabidi nae abwage manyanga pia atleast asiendelee na second term hii ya kwanza yamtosha kabisaa

Similarly..pia anaweza kuonekana kuwa ni non-nonsense president..uki boronga tu anakupa read card. After all hatujui what triggered resignation ya Chenge..huenda JK ali mkalia kooni na kumtaka kujiuzulu, na yes he did it.
 
Hivi ina maana Tanzania (Watanzania) au in short wana JF mnaogopa kumwambia Rais ajiuzulu atakapohisiwa kushirikiana katika kupanua mianya ya rushwa na kubariki azma za mafisadi watarajiwa na mafisadi waliobobea?
 
Wanachuma then kila mtu anajiuzulu sasa tunafanya nini,inawezekana hawa jamaa wana mikakati yao na Muungwana kwamba wachume mpaka wahakikishe imebaki mifupa,kwani naona kama mbio za kijiti vile au mstari kati.wanapokezana tu.
 

Attachments

  • kpleo.jpg
    kpleo.jpg
    14.5 KB · Views: 33
Hivi ina maana Tanzania (Watanzania) au in short wana JF mnaogopa kumwambia Rais ajiuzulu atakapohisiwa kushirikiana katika kupanua mianya ya rushwa na kubariki azma za mafisadi watarajiwa na mafisadi waliobobea?

Haika,
Kwanza karibu mtandaoni. Hili nimepiga kelele kila siku hapa mtandaoni kuwa hivi sasa ili kutatua haya yote, ni tu kwa kumuondoa JK ili tuanze upya na kufanyia uchunguzi wale wote waliokwishatajwa kuwa mafisadi lakini JK akakataa kuwafanyia uchunguzi. Sijui kwa nini kelele za ufisadi hazielekezwi kwa JK aliye kiongozi wa huo mtandao wa mafisadi.

Bunge halina budi kumng'oa Kikwete na kufanya uchunguzi dhidi ya washukiwa wote, bila hivyo, tutaendelea kuchezea makaratasi wakati nchi inaenda mrama.
 
Tunasubiri kwa hamu MAGUFULI wetu arudishwe miundo mbinu ili akarekebishe mambo ambayo CHENGE alianza kuyaboronga boronga. Nimeamini na kujifunza kuwa: UFISADI + UJEURI= KUKOSA HESHIMA MBELE YA JAMII.
 
tunamtaka Rais JK aje hapa atuombe radhi watanzania wote kwa kutuchagulia viongozi mafisadi.
na tuombe radhi tena kwa kutuchagulia viongozi mafisadi mara mbili kwenye baraza lake.

na aje atuombe radhi KABISA kwa waziri mpya atakayetuchagulia kwa vile na huyu atakuwa bogust kama wale waliotangulia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom