Sikua nimefatilia sana hilo sakata la Jose Chameleone wa Uganda na Eric Shigongo, leo baada ya kusikia kwenye habari kwamba hata DJ JD (wengi tunamfahamu) alikua dj maarufu sana hapa mjini na kwa kiasi kikubwa mtu mwenye heshima sana akilalamika kwamba alidhulumiwa na chameleone USD 3,000 miaka saba iliyopita nikaamua kufwatilia hili suala, na haya ndio niliyokutana nayo
- Kutoka facebook page ya chameleone utakutana lugha mbaya sana zikielekezwa kwa shigongo lakini sio tu kwa shingongo ila kwa watanzania wote, kila mganda anayeingia pale anatutukana, iliyoniuma zaidi ni post moja iliyosema watanzania ni wajinga na maskini, na hata wafanyaje hawawezi kufikia level ya waganda, imenikera, sipendi dharau.
- chameleone ameenda ku-protest ubalozi wa Tanzania UG, na haraka eric akaitwa na passport imeishatumwa UG baada ya wanadiplomasia kuingilia kati, lakini wakati eric kapata tabu ya kudhulumiwa, alienda ubalozi wa UG hapa, hakusikilizwa, ndio kwanza ubalozi wa UG hapa ukampa papers za kusafiria hivyo kumuwezesha kukwepa kulipa pesa anazodaiwa.
- Baada ya kupata passport yake jose kaendelea kujisifia kwenye mitandao kwamba yeye hawezekani, na amewaonyesha watanzania kwamba yeye ni nani (haelekezi hizo dhararu kwa eric, no anazielekeza kwa watanzania). . . Waganda, pamoja na kuwatandika 1978 lakini wanatudharau sana
c utupe bac hyo facebook page ya huyo kinyonga tuwanyooshe,sa wao wana nn,kiingereza cha kishamba?,ah ah ah ah,wagandaaaa,vilazaaaa
Shigongo alishindwaje kudai pesa yake kwa njia tofauti hadi akamate passport ambayo kimsingi ni nyaraka ya serikali ya Uganda? Kwa jinsi ilivyokua ilikua ni lazima airudishe hiyo passport..ajilaumu mwenyewe kwa kuingizwa king dolali zake na kutumia mbinu dhaifu kudai njuruku zake.
Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
Shigongo alishindwaje kudai pesa yake kwa njia tofauti hadi akamate passport ambayo kimsingi ni nyaraka ya serikali ya Uganda? Kwa jinsi ilivyokua ilikua ni lazima airudishe hiyo passport..ajilaumu mwenyewe kwa kuingizwa king dolali zake na kutumia mbinu dhaifu kudai njuruku zake.
Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
Mwana habari za shigongo huna haja ya kutafuta upande wa pili zichukue hivyo hivyo kishigongo!mhhhhhhhhhhh sasa ngoja tusubiri naupande wa pili washiringi ndipo tuanze kuchangia la! anaeujua upande wa pili wa hiyo coin basi atu dadavulie
Tatizo la Shigongo ni elimu ndogo aliyonayo, ndio maana hufanya mambo kwa kukurupuka kwa mtindo huo. Na ndio sababu alikurupuka kumtangaza Cheka kuwa atapigana bila kuangalia kiwango cha kidunia cha mpinzani wake. Mwisho akamuomba Cheka akubali kupima uzito tu ili watu wasiache kuja.
Na kwa taarifa nilizonazo alimlazimisha Wema Sepetu kupigana na Wolper, coz Wema alikataa katakata kupigana kutokana na kutumia mkorogo, akazima simu na kutoweka.
Shigongo akaenda kumpiga mkwara mama Wema, vinginevyo angewachafua yeye na mwanawe kwenye gazeti lake, ndo Wema akaibuliwa.