Chaguzi za CCM zimegubikwa na rushwa. Ni aibu kwa chama tawala

Idugunde

JF-Expert Member
May 21, 2020
6,273
6,637
Sasa chaguzi zinafutwa hovyo

=====

Chama cha Mapinduzi (CCM), kimefuta chaguzi tano za Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) kutokana na kukiuka Katiba, Kanuni na taratibu za uchaguzi.

Hayo yamesemwa leo Jumanne Septemba 27, 2022 na Katibu wa Halimashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Hamdu Shaka baada ya kumalizika kwa kikao cha NEC kilichofanyika leo jijini Dodoma.

Amesema changamoto ziko katika jumuiya zote za chama hicho na kwamba idadi kamili ya malalamiko waliyoyapokea haijajulikana kwasababu bado wanaendelea kupokea malalamiko na kuyafanyia kazi.

“Mfano hadi kufikia juzi, kwa upande wa vijana (UVCCM) kuna chaguzi zaidi ya tano zimefutwa na lakini kwa upande wa wanawake kuna chaguzi zaidi ya tatu zimesimamishwa,”amesema bila kutaja maeneo ambako chaguzi hizo zimefutwa.

Amesema Jumuiya ya wazazi haina malalamiko mengi lakini kwa upande wa jumuiya nyingine bado wanaendelea kufanyia kazi malalamiko yao na wanafuatilia kwa karibu.

“Chama kinafuatilia sana mwenendo wa chaguzi hizi na pale itakapobainika kuwa haki haijatendeka pale itakapobainika kanuni na taratibu zimekiukwa basi hatua za kufuta ama kutengua matokeo hayo hazitasita kuchukuliwa,”amesema.

Ametoa wito kwa wana CCM kuheshimu Katiba ya chama hicho na kuheshimu kanuni za chama ili kupata viongozi walio bora wakuongoza nafasi mbalimbali.

Amesema hapo ndipo wanajenga msingi ambao utakuja kuwavusha kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na 2025.

Amesema chama kitahakikisha kinasimamia kuhakikisha kuwa haki inapatikana mahali ilipopindishwa.

Shaka amesema wanafuatilia sana masuala ya rushwa katika chaguzi zinazoendelea ndani ya chama na kwamba hilo ni eneo ambalo watasimamia kwa nguvu kubwa

Kuhusu kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa, Shaka amesema wamefanya uteuzi wa mwisho wa wagombea wenyeviti wa ngazi za wilaya katika wilaya 168 za chama.

Amesema uchaguzi wa wenyeviti wa wilaya wa CCM utafanyika Oktoba Mosi hadi 2 mwaka huu.

Aidha, Nec imeongeza muda wa kuchukua na kurejesha fomu za kuomba kuteuliwa kugombea wajumbe wa NEC.

Chanzo: Mwananchi
 
Sikio la kufa halisikii dawa. Rushwa ni nyenzo muhimu ya kulainisha wajumbe wa uchaguzi toka viongozi wa shina hadi wale wa taifa.
 
Kwasababu CCM inategemea vyombo vya dola kukaa madarakani, ni wazi rushwa lazima zifanyike ndani ya CCM, maana mtu anajua akishinda tu ndani ya ccm, basi atapata mbeleko ya vyombo vya dola kuingia kwenye ulaji. Na rushwa ndani vya CCM inaanzia toka kwa mwenyekiti wao taifa.

Namna pekee ya kuifanya CCM iondokane na rushwa ni kutokea machafuko ambayo yaiondoa madarakani. CCM ikitoka madarakani, ndio itakuwa mwisho wa rushwa ndani ya CCM, na si ajabu ikafa kabisa maana msingi wa uwepo wake ambao ni rushwa utakuwa umekatwa.
 
Chama chakavu hakina dira kipo kipo tu uko ndani kumejaa watu wenye tabia ya Tumbocracy hivyo lazima njia zote haramu zitumike ile kupata ulaji
 
Sasa chaguzi zinafutwa hovyo

=====

Chama cha Mapinduzi (CCM), kimefuta chaguzi tano za Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) kutokana na kukiuka Katiba, Kanuni na taratibu za uchaguzi.

Hayo yamesemwa leo Jumanne Septemba 27, 2022 na Katibu wa Halimashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Hamdu Shaka baada ya kumalizika kwa kikao cha NEC kilichofanyika leo jijini Dodoma.

Amesema changamoto ziko katika jumuiya zote za chama hicho na kwamba idadi kamili ya malalamiko waliyoyapokea haijajulikana kwasababu bado wanaendelea kupokea malalamiko na kuyafanyia kazi.

“Mfano hadi kufikia juzi, kwa upande wa vijana (UVCCM) kuna chaguzi zaidi ya tano zimefutwa na lakini kwa upande wa wanawake kuna chaguzi zaidi ya tatu zimesimamishwa,”amesema bila kutaja maeneo ambako chaguzi hizo zimefutwa.

Amesema Jumuiya ya wazazi haina malalamiko mengi lakini kwa upande wa jumuiya nyingine bado wanaendelea kufanyia kazi malalamiko yao na wanafuatilia kwa karibu.

“Chama kinafuatilia sana mwenendo wa chaguzi hizi na pale itakapobainika kuwa haki haijatendeka pale itakapobainika kanuni na taratibu zimekiukwa basi hatua za kufuta ama kutengua matokeo hayo hazitasita kuchukuliwa,”amesema.

Ametoa wito kwa wana CCM kuheshimu Katiba ya chama hicho na kuheshimu kanuni za chama ili kupata viongozi walio bora wakuongoza nafasi mbalimbali.

Amesema hapo ndipo wanajenga msingi ambao utakuja kuwavusha kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na 2025.

Amesema chama kitahakikisha kinasimamia kuhakikisha kuwa haki inapatikana mahali ilipopindishwa.

Shaka amesema wanafuatilia sana masuala ya rushwa katika chaguzi zinazoendelea ndani ya chama na kwamba hilo ni eneo ambalo watasimamia kwa nguvu kubwa

Kuhusu kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa, Shaka amesema wamefanya uteuzi wa mwisho wa wagombea wenyeviti wa ngazi za wilaya katika wilaya 168 za chama.

Amesema uchaguzi wa wenyeviti wa wilaya wa CCM utafanyika Oktoba Mosi hadi 2 mwaka huu.

Aidha, Nec imeongeza muda wa kuchukua na kurejesha fomu za kuomba kuteuliwa kugombea wajumbe wa NEC.

Chanzo: Mwananchi
Hata kwenye uchaguzi wa wabunge wa EALA , inasemekana Msimamizi wao Mizengo Pinda alinyamazia Rushwa nzito sana
 
Tangu Nyerere ang'atuke kwenye chama, rushwa imebakia kuwa msingi pekee wa kupata wagombea wa nafasi mbalimbali ndani ya chama. Hivyo hakuna jipya.

Hata wakati wa Magufuli mnaye msifia, bado rushwa ilitolewa katika mazingira yote ya uteuzi wa wagombea. Hivyo mwenye kisu kikali atakata nyama.


Kamwe huwezi kuitenganisha ccm na vitendo vya rushwa. Na bila ya kutumia rushwa, huwezi kushinda nafasi yoyote ile ya maana ndani ya chama! Labda utashinda ile ya ubalozi wa nyumba 10!
 
Kwasababu CCM inategemea vyombo vya dola kukaa madarakani, ni wazi rushwa lazima zifanyike ndani ya CCM, maana mtu anajua akishinda tu ndani ya ccm, basi atapata mbeleko ya vyombo vya dola kuingia kwenye ulaji. Na rushwa ndani vya CCM inaanzia toka kwa mwenyekiti wao taifa.

Namna pekee ya kuifanya CCM iondokane na rushwa ni kutokea machafuko ambayo yaiondoa madarakani. CCM ikitoka madarakani, ndio itakuwa mwisho wa rushwa ndani ya CCM, na si ajabu ikafa kabisa maana msingi wa uwepo wake ambao ni rushwa utakuwa umekatwa.
Huu ni uchochezi.
 
Back
Top Bottom