Elections 2010 CHADEMA yatoa tamko: Hatumtambui Kikwete kama rais

Kama CHADEMA hawamtambui Rais:
1. Watashiriki kupiga kura za kumpitisha/kutompitisha waziri mkuu? Waziri mkuu hupendekezwa na Rais, kushiriki katika kumpigia kura ni kutambua huyo aliyemleta ni Rais halali.

2. Baada ya waziri mkuu kupitishwa, wataweza kumuuliza mwaswali yeye pamoja na mawaziri wengine, ambao wote wameteuliwa na Rais wasiyemtambua?

Ndugu zangu wana JF, tamko hili la CHADEMA ni la kisiasa tu na halitekelezeki. Sababu kubwa ni kwamba wabunge wa CHADEMA hawawezi kugive-up ubunge wao - kwa katiba ya Tanzania kama humtambui Rais huwezi kuwa mbunge.

Mkuu hapa kweli tunahitaji kupata elimu kuhusu katiba yetu. Nina hakika Rais anachaguliwa na wananchi kama vile wabunge kwa kupigiwa kura. Sasa iweje upoteze ubunge kisa humtambui Rais kwa sababu ya wizi wa kura uliompeleka ikulu?? Mimi ni mbumbumbu wa katiba but vitu vingine havihitaji kwenda darasani, wote tumepigiwa kura.

Katika mfumo wa chama kimoja mtu uliweza kufukuzwa uanachama na ukapoteza ubunge. Sasa nitoke chama kingine ni vipi chama kingine kije kinivue uanachama!! Kama kweli katiba yasema hivyo, basi ndiyo utaona umuhimu wa kurekebisha katiba yetu.

Ni kifungu gani kwenye katiba kinasema hivyo, eti husimbomtambua Rais basi nawe si mbunge tena? Sorry, napendwa kuelimishwa tafadhali.
 
Sikubaliani na uamuzi wa kutokwenda mahakamani. Katika mabandiko yangu ya nyuma nilieleza suala hili kwa urefu sana na kuonyesha kuwa Mahakama ya Rufaa ilikwisha tamka kuwa kitendo chochote kile cha Tume ambacho kimefanywa kinyume cha sheria kinapingwa. Nilijitahidi kuwasilisha maoni yangu kwa mwanasheria wao lakini inaelekea wamekataa. Inasikitisha.

Bado ninasisitiza kuwa Mahakama Kuu inabanwa na uamuzi ule wa Mahakama ya Rufaa na hapo ndio ungekuwa uwanja mzuri wa Chadema kuanika ushahidi hadharani. Lakini Wanasheria hutofautiana mbinu za kupambana.


Mtikila alishinda Kesi kutaka serikali ifuate katiba ya nchi na kuruhusu Mgombea binafsi. Serikali ya CCM imekula jiwe na kujikausha kama vile haipo. Kifupi imeingiza ubabe na kuvalia miwani ya mbao katiba ya nchi.
Huu si kwamba ni uchuro tu ,hapana . Ni hatari kwa CCM yenyewe na nchi kwa ujumla.
Serikali ikikiuka Hukumu ya Mahakama maana yake inahalalisha Uhalifu kila mahali nchini Tanzania.

Tunahitaji kusema zaidi?

Fahamu kwamba wana mageuzi tunapambana na Jidude lisilofuata taratibu wala sheria. Jidude hili linajiendeshea mambo yake kwa taratibu ambazo hata lenyewe halijaziridhia.
Kimsingi Chadema kwenda mahakamani ni upuuzi, ni kupoteza muda na ni kurudi nyuma hatua zaidi ya elfu.

Kesi hii imefunguliwa mbele ya Wananchi.
Wao wananchi ndiyo Majudge watasikiliza malalamiko ya upinzania,watapitia vielelezo na ushahidi wote, wataenda chemba na kunong'ona kisha watatoa Hukumu ya HAKI.

Sidhani ushauri wa kwenda Mahakamani una nafasi hapa.

Nchi zote Duniani zenye misukosuko isababishwayo na Vyama Dola kama CCM malalamiko na kesi zote huwekwa mbele ya wananchi ili watoa uamuzi wao. Ni wananchi pekee ndiyo wenye uwezo wa kutoa hukumu ya Haki.

CCM ni chama cha Siasa chenye wafuasi waliosehemu ya watu wa tanzania,CCM siyo wananchi wote wa Tanzania na CCM siyo serikali ya Tanzania.

Wananchi watatoa Hukumu baada ya kupitia Ushahidi wote.

Pengine wengi hapa Jamvini wanaweza dhani maneno matupu hayavunji mfupa, mkono mtupu haulambwi nk Lakini pia wanasahau kwamba kuna msemo usemao Shughuli yeyote ile ni watu.
Ukiacha methali nyingi na misemo ya kiswahili ambayo mingine huleta maswali mengi kuliko majibu, kuna misemo mingi ya kisayansi itokanayo na uchunguzi wa muda mrefu inayothibisha kwamba Maneno na kitendo cha kuvunja mfupa ni kitu kimoja.
Kuna ukweli ulifanyiwa uchunguzi wa Kisayansi kwamba kuna Uhusiano Wa Moja kwa Moja kati ya Wazo na Kitu Halisi.
Vitu vyote ikiwa ni pamoja na vile tudhanivyo ni vitu asilia kama hewa maji na ardhi viliwahi kuwa wazo.
Hakuna kitu kianzacho tu bila kutungwa mimba ya wazo.
Wazo ndiyo asili,
wazo ndiyo chanzo,
wazo ndiyo mbegu na msingi wa kila kitu.
Hakuna kilichoko leo hapa ulimwenguni ambacho kwanza hakikuwa wazo.
Kwa hiyo ni ukweli usiopingika kwamba vingi visivyo kuwepo sasa,vitakavyokuwako baadaye sasa hivi ni mawazo tu.
Mtu yeyote mwenye hekima iliyopevuka kamwe hadharau wazo hata liwe la kiendawazimu kiasi gani kwa sababu anajua ukuu wa nguvu ya wazo.
Ndiyo maana Serikali zote Duniani hutumia mabilioni mengi sana sana na wakati wake mwingi kujaza mawazo ya aina fulani ndani ya vichwa vya watu wake ili hatimaye vitu fulani vipatikane kutoka kwa wananchi wake.Serikali zote zinafanya hivyo kwa sababu zinajua wazi kabisa kwamba hakuna tofauti kati ya wazo na kitu.
Upandapo mbegu ya wazomavuno ni kitu halisi.

Kwa mfano,Hakuna tofauti kati ya wazo la kumiliki gari na Gari lako lililopaki nje ya nyumba yako.Kuna Time Delay kati ya Wazo la kuwa na Gari na Gari unalolimiliki lililopaki mbele ya nyumba yako.

Wazo la gari---> Time Delay ---> Gari.

Mtu akitaka Usinunue gari pengine hadi kufa kwako anacheza na Time tu, kwa sababu anajua wazi hakuna namna ya kukuzuia kuendelea kuwaza juu ya gari.

Sasa utajiuliza time inazewa vipi?

Time na Space vimeshikamana na kuchangamana. ukitikisa Space time nayo inatikisika, ukiikunja space time nayo inakunjika, ukirefusha space time nayo inarefuka.Ukiondoa Space yote ukabakiwa na utupu pekee Time nayo inatoweka jumla au tuseme inakuwa infinite kwa maana kwamba sekunde moja inakuwa sawa na miaka billion kadhaa.

Hakuna awezaye kufupisha wala kurefusha Muda.Lakini inawezekana kucheza na Space kwa sana hivyo indirect kucheza na time.

Watu tukiwa kwenye raha na furaha relativelyTime inakatika kwa sana na akili zetu zinajaa mawazo Positive kibao.
Watu tukiwa katika majonzi Time inaslow Down na wengi tunakata tamaa na kuuwa mawazo yetu mengi mazuri, tunabakiza mawazo yale tudhaniyo ni ya msingi. Kula kuvaa na mahali pa kurara tu.

Kimsingi Inawezekana kurefusha muda kati ya Wazo la gari na gari unalolimiliki.

Kwa sababu space ni yote tuyafanyayo kila siku,ni yote tuonayo, ni yote tuwezayo kushika , ni yote tutambuayo kwa akili zetu, ni rahisi sana kwa Serikali dharimu kutengeneza aina fulani ya utaratibu na kuujaza vichwani mwa watu kwa namna moja au nyingine ili watu waendelee ku mark time wenyewe bila kuguswa na mtu na kuamini kabisa kwamba uwezo nia na hamu yao imefikia ukomo.

Watu wanakuwa matajiri wakubwa kwa kutumia mbinu hii.
Serikali zinaweza kuwcontrol watu wake kwa kutumia mbinu hii hii.

Wazo ni hatua muhimu, hatua nyingine muhimu ni, tamko. Tamko ni hatua ya kuliweka wazo katika maandishi au usemi. Tamko ni sawa kabisa na kuvuna wazo kutoka vichwani mwa watu kadhaa na kulipanda katika vichwa vya watu wengi katika safari ya wazo kuwa kitu.

Watu wengi hudhani tamko ni hatua ya kwanza la hasha,Tamko ni hatu ya pili hatua ya kwanza ni wazo.

watu walioko kwenye majonzi time kwao iko streached kwa maana hiyo wakipewa wao sahihi wanamuda mrefu sana wakutafakari.
Watu wlaio katika majonzi wakiachwa bila wazo la maana wanatumia muda wao mwingi kukata tamaa na kujilaumu bila kisa.
Wakati huohuo watu walioko katika furaha hawana muda wa kutafakari kwani kwao muda ni mfupi unakatika upesi,muda kwao ni mali na mambo ya kufanya mazuri na yenye kufurahisha moyo ni mengi.
Hawana muda wa kulitafakari wazo na kutambua matokeo yake.umuhimu mkubwa kwao ni juu ya vile vilivyopo mbele yao tu.

Kuna kitu Wazungu wanaita Manifestation.
Tangu wakati wazo linapandwa ndani ya vichwa vya watu wengi mpaka kitu halisi kuzaliwa kuna kitu wenzetu wanaita Manifestation. Katika ubinafsi wa kila mtu kuna wakati utambuzi na ufahamu hukaa pamoja na kuzaa msukumo wa kutenda. Hali hiyo ikifikiwa hakuna kurudi nyuma tena, wazo ni lazima liwe kitu kwa sababu time =0.

Hapo ndipo waswahili walikuja na methali isemayo kimya kingi kina mshindo. Kimya halafu Mshindo??

Hatuna ubavu wa kubeza wazo yakinifu kwa sababu ukuu wa hekima zetu hauruhusu hata kidogo.
 
Baada ya Chadema kutoa tamko lao la kutomtambua JK...............inabidi sasa waandae hoja ya vote of no confidence.................safi kabisa....

Si sahihi kusema ukikubali kuwa mbunge..................then umemkubali Rais..............na ndio maana kuna nafasi kama ya vote of no confidence.............

ni sahihi kusema......itakuwa difficult ku-operate kama mbunge usipomtambua Rais.............

Actually ili upige vote of no confidence ni lazima umtambue rais, kama humtambui unapiga vote of no confidence kutokuwa na confidence kwa nani ?
 
Mkuu hapa kweli tunahitaji kupata elimu kuhusu katiba yetu. Nina hakika Rais anachaguliwa na wananchi kama vile wabunge kwa kupigiwa kura. Sasa iweje upoteze ubunge kisa humtambui Rais kwa sababu ya wizi wa kura uliompeleka ikulu?? Mimi ni mbumbumbu wa katiba but vitu vingine havihitaji kwenda darasani, wote tumepigiwa kura.

Katika mfumo wa chama kimoja mtu uliweza kufukuzwa uanachama na ukapoteza ubunge. Sasa nitoke chama kingine ni vipi chama kingine kije kinivue uanachama!! Kama kweli katiba yasema hivyo, basi ndiyo utaona umuhimu wa kurekebisha katiba yetu.

Ni kifungu gani kwenye katiba kinasema hivyo, eti husimbomtambua Rais basi nawe si mbunge tena? Sorry, napendwa kuelimishwa tafadhali.

http://www.tanzania.go.tz/images/katibamuungano.pdf

SURA YA TATU, BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO, SEHEMU YA KWANZA
BUNGE

Bunge
Sheria ya 1984 Na.15 ib.12
62.-(1) Kutakuwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano ambalo litakuwa na sehemu mbili, yaani Rais na Wabunge.

Kama humtambui rais, hulitambui bunge ambalo sehemu yake ni rais, kama hulitambui bunge, huwezi kukubali ubunge. Simple as that.
 
Kuwe na time frame ktk kuanika uovu huo wa uchakachuaji wa wa matokeo kwani uchelewashaji wake unaresult mbaya kwa chama na taifa
 
Baada ya Chadema kutoa tamko lao la kutomtambua JK...............inabidi sasa waandae hoja ya vote of no confidence.................safi kabisa....

Si sahihi kusema ukikubali kuwa mbunge..................then umemkubali Rais..............na ndio maana kuna nafasi kama ya vote of no confidence.............

ni sahihi kusema......itakuwa difficult ku-operate kama mbunge usipomtambua Rais.............

leh! Sasa kama rais humtambui utapiga vote of no confidece kwa nani utapigia hewa?
 
http://www.tanzania.go.tz/images/katibamuungano.pdf

SURA YA TATU, BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO, SEHEMU YA KWANZA
BUNGE

Bunge
Sheria ya 1984 Na.15 ib.12
62.-(1) Kutakuwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano ambalo litakuwa na sehemu mbili, yaani Rais na Wabunge.

Kama humtambui rais, hulitambui bunge ambalo sehemu yake ni rais, kama hulitambui bunge, huwezi kukubali ubunge. Simple as that.
Unaweza kutambua urais lakini usikubali process iliyomwingiza rais mamlakani.
 
Siku zote tusiache kukumbuka kwamba sauti ya wengi wanaolia kwa kudhulumiwa demokrasia ni sauti ya Mungu; wewe subiri tu si muda mrefu mwenye watu hawa walioporwa demokrasia atashuka na panga; itakuwa ni kilio na kusaga meno kwa JK na Kiravu na Makame wake ambao wamediriki hata bila aibu kupelekeka, kuhalalisha na hata kuapisha wabunge batili licha ya onyo lililotolewa mapema sana na mwanamapinduzi M. M. Mwanakijiji katiaka makala yake katika gazeti la Mwanahalisi Jumatano , Sepetemba,2010 Ukuras wa 6 kwa kichwa "Wabunge Waliobebwa ni Batili". Kijapo kiburi ndipo huja aibu!!!!!!!!!!!!!!!!!! Hiyo aibu haiko mbali, serekali iliyojengwa juu ya msingi wa ushirikina hauwezi kusimama mbele ya nguvu kubwa ya Mungu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!Pipooooooooooos Pawasssssssssssssssssss!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Machozi ya watu wa Mungu hayataenda bure!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Unaweza kutambua urais lakini usikubali process iliyomwingiza rais mamlakani.

Issue hapa si kutambua urais, usitambue urais utatambua nini sasa, ufalme? Uchifu? Usultani?

Of course tunaongelea process iliyomchagua Kikwete, lakini usipoikubali process iliyomchagua Kikwete, then una choice ya kufanya gradual changes kuibadilisha hiyo process au kufanya immediate changes kama hizi za kutomtambua rais.

Hapa cha kutambuliwa au kutotambuliwa ni rais, si urais. Ukitaka kukataa urais ina maana nyingine kabisa, una sound kama monarchist unayetaka kuleta ufalme or something like that.
 
Siku zote tusiache kukumbuka kwamba sauti ya wengi wanaolia kwa kudhulumiwa demokrasia ni sauti ya Mungu; wewe subiri tu si muda mrefu mwenye watu hawa walioporwa demokrasia atashuka na panga; itakuwa ni kilio na kusaga meno kwa JK na Kiravu na Makame wake ambao wamediriki hata bila aibu kupelekeka, kuhalalisha na hata kuapisha wabunge batili licha ya onyo lililotolewa mapema sana na mwanamapinduzi M. M. Mwanakijiji katiaka makala yake katika gazeti la Mwanahalisi Jumatano , Sepetemba,2010 Ukuras wa 6 kwa kichwa "Wabunge Waliobebwa ni Batili". Kijapo kiburi ndipo huja aibu!!!!!!!!!!!!!!!!!! Hiyo aibu haiko mbali, serekali iliyojengwa juu ya msingi wa ushirikina hauwezi kusimama mbele ya nguvu kubwa ya Mungu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!Pipooooooooooos Pawasssssssssssssssssss!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Machozi ya watu wa Mungu hayataenda bure!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Habari za kumtegemea mungu ndiyo iliyoweka CCM kwenye power miaka yote hiyo, wenye nguvu wanaombea wananchi mumtegemee mungu.

Watawala miaka yote, kuanzia Wababeli, Wachina, Wamisri, Wagiriki, Warumi, ufalme wa Uingereza mpaka George W. Bush wamemtumia mungu ili kuwpumbaza wananchi wa kawaida.

Hata Mkapa ambaye hakujishughulisha na kanisa alipopata kuwa rais alionekana St. Immaculate pale U.N Road, Upanga, alivyoondoka Ikulu haonekani tena, anajua ili kuwapumbaza wananchi ni muhimu kujifanya uko karibu na mungu. Kutoka Wababeli, Wamisri mpaka Selassie, wote wamejiita "elect of god".

Hata wakoloni walitupa biblia ili tuamini "pie in the sky". Tushachoka hii habari ya mungu, hii ni habari ya wakandamizaji.

Hakuna mungu wala mwanaye, kama kungekuwa na mungu muweza yote anayejua haki wezi wasingeiba bwana.

Tuambie habari nyingine, lakini si hii ya kuamini mungu. Ukimuamini mungu unaweka fate yako nje ya mikono yako, kinyume kabisa na ideas za mapinduzi na "people's power". People' power maana yake watu wenyewe wanaamua mambo yao, iyo kumuachia mungu. Ukimuachia mungu utajuaje kwamba rais hatachakachua maaskofu, vitabu na experience yako yote ya dini ?
 
Makame na Makungu ninyi ni Majaji, kwa kofia ya Tume ya Uchaguzi, yaani Ret. Justice Makame na Justice Makungu mliyofanya kwa umma wa Tanzania mbele za Mungu yamewavua kabisa sifa hiyo ya u-; hivyo mnastahili kuanza kuitwa Ret. INJUSTICE Makame na INJUSTCE Makungu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!.
 
Wabunge
Sheria ya
1984 Na.15
Ibara 13
sheria ya 1992
Na.4 Sheria
1992 Na.4
Ibara 18
Sheria ya
1995 Na.12
Ibara 9
Sheria ya
2000
Na.3 ib.11​
66​
.-(1) Bila ya kuathiri masharti mengine ya ibara hii, kutakuwa
na aina zifuatazo za Wabunge, yaani-
(a) Wabunge waliochaguliwa kuwakilisha majimbo ya
uchaguzi;
(b) Wabunge wanawake wa idadi inayoongezeka, kuanzia
asilimia ishirini ya Wabunge waliotajwa katika aya ya
(a), (c ) na (d), itakayotajwa mara kwa mara na Tume
ya Uchaguzi kwa taarifa iliyochapishwa katika Gazeti
la Serikali baada ya kupata kibali cha Rais,
watakaochaguliwa na vyama vya siasa
vinavyowakilishwa Bungeni, kwa mujibu wa ibara ya
78, na kwa kuzingatia masharti ya uwiano wa
uwakilishi baina ya vyama hivyo;
(c) Wabunge watano waliochaguliwa na Baraza la
Wawakilishi kutoka miongoni mwa wajumbe wake;
(d) Mwanasheria Mkuu;
(e) Wabunge wasiozidi kumi walioteuliwa na Rais kutoka
miongoni mwa watu wenye sifa kwa mujibu wa ibara
ya 67, isipokuwa sifa iliyotajwa katika ibara ya
67(1)(b).
(2) Rais na Makamu wa Rais kila mmojawao hatakuwa
Mbunge.

Bunge
Sheria ya
1984 Na.15
ib.12
62
.-(1) Kutakuwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano ambalo

litakuwa na sehemu mbili, yaani Rais na Wabunge.

Bunge lina sehemu mbili.

Rais na Wabunge.
Kwa sababu Bunge haliundwi na watu wasio wa Bunge kwa mujibu wa katiba. rais hawezi kuwa sehemu ya Bunge kwa sababu kifungu 66(2) kinasema Rais si mbunge.

Katiba inajichanganya yenyewe haina tofauti na Mkataba wa Buzwagi.

Upuuzi upuuzi!
 
Wabunge
Sheria ya
1984 Na.15
Ibara 13
sheria ya 1992
Na.4 Sheria
1992 Na.4
Ibara 18
Sheria ya
1995 Na.12
Ibara 9
Sheria ya
2000
Na.3 ib.11​
66​
.-(1) Bila ya kuathiri masharti mengine ya ibara hii, kutakuwa
na aina zifuatazo za Wabunge, yaani-
(a) Wabunge waliochaguliwa kuwakilisha majimbo ya
uchaguzi;
(b) Wabunge wanawake wa idadi inayoongezeka, kuanzia
asilimia ishirini ya Wabunge waliotajwa katika aya ya
(a), (c ) na (d), itakayotajwa mara kwa mara na Tume
ya Uchaguzi kwa taarifa iliyochapishwa katika Gazeti
la Serikali baada ya kupata kibali cha Rais,
watakaochaguliwa na vyama vya siasa
vinavyowakilishwa Bungeni, kwa mujibu wa ibara ya
78, na kwa kuzingatia masharti ya uwiano wa
uwakilishi baina ya vyama hivyo;
(c) Wabunge watano waliochaguliwa na Baraza la
Wawakilishi kutoka miongoni mwa wajumbe wake;
(d) Mwanasheria Mkuu;
(e) Wabunge wasiozidi kumi walioteuliwa na Rais kutoka
miongoni mwa watu wenye sifa kwa mujibu wa ibara
ya 67, isipokuwa sifa iliyotajwa katika ibara ya
67(1)(b).
(2) Rais na Makamu wa Rais kila mmojawao hatakuwa
Mbunge.

Bunge
Sheria ya
1984 Na.15
ib.12
62
.-(1) Kutakuwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano ambalo

litakuwa na sehemu mbili, yaani Rais na Wabunge.

Bunge lina sehemu mbili.

Rais na Wabunge.
Kwa sababu Bunge haliundwi na watu wasio wa Bunge kwa mujibu wa katiba. rais hawezi kuwa sehemu ya Bunge kwa sababu kifungu 66(2) kinasema Rais si mbunge.

Katiba inajichanganya yenyewe haina tofauti na Mkataba wa Buzwagi.

Upuuzi upuuzi!

Hakuna kujichanganya hapo, wapi katiba imesema bunge haliundwi na watu wasio wabunge?

Achana na kuundwa, bunge linaweza hata kuongozwa na mtu asiye mbunge, na hata siongelei rais.

Spika wa bunge anaweza kuwa mtu asiye mbunge. Dr. Che Mponda katoka kugombea uspika juzi, na wala si mbunge sasa hiyo sehemu inayosema "bunge haliundwi na watu wasio wabunge" umeipata wapi, wakati shemu moja nzima ya bunge ni rais.
 
This is the so called "inconvenient truth" - katiba imetufunga mikono!

Kwa kuongezea...41 (7)

"Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi
kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi
hakuna Mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya
kuchunguza kuchaguliwa kwake."


KWA HIYO SUALA LA KWENDA MAHAKAMANI ITAKUWA NI KUPOTEZA MUDA!

Ni kweli kuwa licha ya hiyo Ibara ipo Ibara ya 41(7) nayo inasema:

(7) Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna Mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake.

Hoja yangu ni kuwa uamuzi wa Mahakama ya Rufaa kuhusu matangazo ya Tume ya Uchaguzi ni kuwa Uchaguzi ambao hauwezi kuchunguzwa ni ule ambao ni huru na wa haki na uliofanywa kwa mujibu wa sheria na katiba. Kama sheria na katiba vimekiukwa Mahakama ya Rufaa ilisema wazi kuwa hiyo na mpa mtu haki ya kwenda Mahakamani kupinga uchaguzi huo. Kwa wale wasio Wanasheria ni kuwa Uamuzi wa Mahakama ya Rufaa unaifunga Mahakama Kuu na hivyo basi kama Chadema wakifungua kesi dhidi ya Tume basi Mahakama Kuu itabidi ipokee kesi hiyo na kuangalia kwa undani madai yao. Nilitegemea watanielewa lakini nadhani wameamua vinginevyo na siwezi kuwalazimisha.

Kwa yule ambaye si Mwanasheria anaweza kubabaika na kuamini kuwa ni kweli kabisa kuwa Katiba inazuia lakini Wanasheria tuna kanuni za kutofautisha maamuzi na kuvuka kile ambacho kinaonekana kuwa ni kipingamizi au kizuizi kwa lugha ya kawaida kabisa. Uwezo na mbinu hizi ndizo zilimfanya Shakespeare aandike kuwa Mfalme Henry alipotaka kutunga sheria ambayo itaondoa kila aina ya upinzani kwa utawala wake alisema kuwa jambo la kwanza la kufanya ni kuua wanasheria wote "The first thing we do, we kill all lawyers". Hii ilitokana na yeye kuelewa kuwa hata kama angetunga sheria ambayo inaonekana kuwa inabana kila kitu bado Wanasheria wangeweza kupata upenyo na kuweza kumpinga. Inaelekea Chadema na Wanasheria wao wanaamini kuwa hakuna upenyo lakini mimi ninauona. Kwa hiyo naomba nitofautiane nao.
 
http://www.tanzania.go.tz/images/katibamuungano.pdf

SURA YA TATU, BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO, SEHEMU YA KWANZA
BUNGE

Bunge
Sheria ya 1984 Na.15 ib.12
62.-(1) Kutakuwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano ambalo litakuwa na sehemu mbili, yaani Rais na Wabunge.

Kama humtambui rais, hulitambui bunge ambalo sehemu yake ni rais, kama hulitambui bunge, huwezi kukubali ubunge. Simple as that.
Mbona hilo liko wazi Kiranga usichanganye watu rais ni sehemu ya bunge means president is a subset of bunge as universal bunge lina uwezo wa kumuondoa rais bungeni.
 
Ni kweli kuwa licha ya hiyo Ibara ipo Ibara ya 41(7) nayo inasema:

(7) Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna Mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake.

Hoja yangu ni kuwa uamuzi wa Mahakama ya Rufaa kuhusu matangazo ya Tume ya Uchaguzi ni kuwa Uchaguzi ambao hauwezi kuchunguzwa ni ule ambao ni huru na wa haki na uliofanywa kwa mujibu wa sheria na katiba. Kama sheria na katiba vimekiukwa Mahakama ya Rufaa ilisema wazi kuwa hiyo na mpa mtu haki ya kwenda Mahakamani kupinga uchaguzi huo. Kwa wale wasio Wanasheria ni kuwa Uamuzi wa Mahakama ya Rufaa unaifunga Mahakama Kuu na hivyo basi kama Chadema wakifungua kesi dhidi ya Tume basi Mahakama Kuu itabidi ipokee kesi hiyo na kuangalia kwa undani madai yao. Nilitegemea watanielewa lakini nadhani wameamua vinginevyo na siwezi kuwalazimisha.

Kwa yule ambaye si Mwanasheria anaweza kubabaika na kuamini kuwa ni kweli kabisa kuwa Katiba inazuia lakini Wanasheria tuna kanuni za kutofautisha maamuzi na kuvuka kile ambacho kinaonekana kuwa ni kipingamizi au kizuizi kwa lugha ya kawaida kabisa. Uwezo na mbinu hizi ndizo zilimfanya Shakespeare aandike kuwa Mfalme Henry alipotaka kutunga sheria ambayo itaondoa kila aina ya upinzani kwa utawala wake alisema kuwa jambo la kwanza la kufanya ni kuua wanasheria wote "The first thing we do, we kill all lawyers". Hii ilitokana na yeye kuelewa kuwa hata kama angetunga sheria ambayo inaonekana kuwa inabana kila kitu bado Wanasheria wangeweza kupata upenyo na kuweza kumpinga. Inaelekea Chadema na Wanasheria wao wanaamini kuwa hakuna upenyo lakini mimi ninauona. Kwa hiyo naomba nitofautiane nao.

Kimsingi, concept hii ndiyo aliyoitumia Dr. Slaa pale alipotishiwa baada ya kutoa listi ya mafisadi, kwa kusema kwamba hata kama katumia nyaraka za serikali ambazo zinatakiwa kuwa siri, lakini ukweli kwamba kazitumia kuonyesha uovu wa serikali zinaondoa uharamu wa kutumia nyaraka hizo.

Kwa hiyo unachosema ni kwamba kama ni kweli rais kapata urais isivyo halali, basi hana uhalali wa kulindwa na katiba kama rais halali.

It is an interesting legal argument, with a shaky foundation.To top it off CCM has too much clout, especially with a bordeline acceptable argument like this, with neither precedent nor concrete merit in the letter of the law as practised in Tanzania.

Let's see if Dr. Slaa can be as inventive this time. I have to say, the stakes are rather high this time around and hi prospects are almost nonexistent. Not even slim.

Ili kuonyesha kwamba rais si halali, inabidi uonyeshe kwamba mfumo uliomuweka -pamoja na majaji wa NEC- kwamba si halali. Majaji wenyewe utakaowapelekea hii kesi chances are wameteuliwa na rais, kwa hiyo kusema huyu rais si halali maana yake ni ku cast doubt hata kwenye uhalali wao, kwa sababu kama una cast doubt na appointer wao, una cast doubt kwao.

Ndiyo maana wengine wanasema hapa ni maandamano tu, ukitaka mahakama ifanyie kazi haya mambo hupati kitu.
 
Kumbe ni tamko lililotolewa kwenye hafla ya kujipongeza kwa uchaguzi ulopita hasa kuongeza idadi ya wabunge

Dada/Kaka (Whichever is correct)

Kwani neno 'TAMKO' lina maana gani? It doesn't matter kama umetamka shereheni, nyumbani, msikitini, n.k. Shina la neno TAMKO ni TAMKA; kwa hiyo sioni ubaya kutamka wakati wa kuwapongeza wabunge walioushinda udhalimu wa CCM. It was a right audience.:tape:
 
Nadhani tatizo kubwa ambalo litawakuta Chadema hapa ni suala la lugha; kutomtambua Rais katika siasa zetu hakuwezi kumfanya asiwe halali. Lakini zaidi ni kuwa kutomtambua Rais kunaashiria kuwa yeye mwenyewe alihusika katika kuvuruga uchaguzi. Hadi hivi sasa sijasikia mtu akimtuhumu Kikwete moja kwa moja kuwa alishiriki kujipa ushindi.

Lakini upande mwingine ni kuwa kwa vile matokeo ya uchaguzi ya Ubunge yanatangazwa Jimboni na kuwa Rasmi lakini matokeo ya Urais yanakusanywa Jimboni lakini yakawa rasmi kijimbo tu lakini kitaifa yanakuwa rasmi baada ya kujumlishwa na kutangazwa na tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Sasa, tuchukulie mfano wa majimbo kumi tu: Katika majimbo hayo kumi matokeo ya Urais (ambayo yanapatikana majimboni humo na ni rasmi (final) yanaonesha (katika fomu zilizosainiwa na vyama) mgombea wa CHADEMA amepata kura 25,000 na mgombea wa CCM amepata kura 19,000. Katika majimbo hayo hayo yanapotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi yanaonesha mgombea wa CCM kapata kura 27,000 na wa CHADEMA kapata kura 8000. CHADEMA WANA OPTION GANI HAPA?

Well, option ya kwanza na ya kimantiki ni kutaka Tume isitishe mara moja kuendelea kutangaza matokeo ya uchaguzi wa Rais kwani kuna discrepancy kubwa inaonekana kati ya kura zinazotangazwa na Tume na zile zilizoko majimboni? Hili halikatazwi kwani kisheria inaruhusiwa (niliandika thread yenye kunukuu sheria ya uchaguzi). Tume inakataa kusikiliza na inaendelea kutangaza matokeo kutoka "majimboni".

Option ya pili ni kwa vyombo vya habari na taasisi huru kuanza kutangaza matokeo jinsi wanavyoyapata kutoka majimboni ili kuona kama yanaoana na yale yanayotangazwa Tume. Serikali inakataza vyombo vyote vya habari kutangaza matokeo ya Urais hadi "yahakikiwe" na Tume ya Uchaguzi na kutangazwa na Tume; vyombo vya habari vinakubali na kuwa kimya. Waliokuwa wanaangalia ITV wanakumbuka jinsi mtangazaji wao alivyokuwa anawazuia maripota kutoka mikoani kutangaza matokeo ya Urais wakati yalikuwa tayari yanapatikana na badala yake kusubiri 'rasmi' yanatolewa na tume!

Option ya tatu ni kuanza kulazimisha kulinda kura kwa nguvu na kumiminika Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwazuia kutangaza matokeo "yaliyochakachuliwa" hadi credibility ya mchakato mzima ioneshwe. Hili hata hivyo lingesababisha vurugu na hata uwezekano wa kumwaga damu. Kama kura za Masha na Mrema na zile za Mbilinyi na Mnyika zilikuwa zinatishia vurugu kubwa kwenye kura za Rais ingekuwaje?

Hivyo, tume inaendelea kutangaza matokeo bila ya kujali malalamiko au matatio yaliyotokea kwa sababu wanajua hicho kipengele cha Katiba kuwa wakifika mwisho na kumtangaza mshindi then ITS OVER. Na hicho ndicho kinatokea.

Sasa CHADEMA tunaambiwa wanatakiwa wakubali sasa kuwa kwa vile "mshindi" keshatangazwa waende kukumbatiana naye na kupiga picha za pongezi. Tunaambiwa kuwa kwa vile sasa keshaapishwa na Katiba inasema huwezi kuhoji mahali popote basi Chadema wakubali kutuma pongezi za "ushindi" wakati dhamira zao zinawakatalia.


Sasa CHADEMA wafanye nini? Tunaambiwa lazima wakubali tu yaishe. Wakubali kwa sababu wameridhika na matokeo au kwa sababu kutangazwa kumekidhi the minimum requirement ya katiba?

Lakini kitu kingine ambacho hatujakigusa sana (nimekigusa kwenye makala yangu mojawapo Jumatano) nikuwa watu karibu milioni 12 hawakujitokeza kupiga kura siku ile japo watu waliamka kuanzia saa kumi alfajiri kupanga foleni na zilijaa! Watu hawa tumetafutiwa sababu za kusema kwanini hawakujitokeza. Yaani, tangu Muungano wetu 1964 kwenye chama kimoja na vyama vingi Watanzania hawajahi kupiga kura chini ya asilimia 70 ya waliojiandikisha, NEVER HAPPENED. Mwaka huu ni asilimia 42!!! Katika chaguzi kumi mfululizo hatujawahi kuwa chini ya asilimia 70 na tumewahi kufikia asilimia 84 awamu ya pili ya Mkapa lakini leo tumeambiwa ati ni asilimia 42, HAKUNA MTU anayeshangaa nini kimetokea? Tena tukumbuke kuwa mfumo mzuri wa kujiandikisha na kupiga kura. Watu milioni 12 hawajapiga kura, asilimia 42 ndio inaonekana.. tena siku ya Jumapili! THERE HAS TO BE A RATIONAL AND LOGICAL EXPLANATION.

Sasa binafsi naamini kabisa kuwa Kikwete angeweza kushinda katika mazingira safi kabisa japo siamini kama aliweza kufikia asilimia 61. Ushindi wake kama ungeachwa uje kama ulivyokuja wa Shein ungekuwa karibu asilimia 55 hivi. Ninaamini tume ya uchaguzi ina maswali ya kujibu lakini kulazimisha Taifa zima tuanze kupiga saluti za "kumtambua" ni kutoamini haki ya dhamira ya mwanadamu kukataa dhulma. Sasa, sijui kama ni suala la Kikwete mwenyewe au ni suala la Tume. Kama ni Tume (na mimi naamini ndivyo) basi ni maslahi ya Kikwete kulizungumzia hilo ili apate credibility ya uchaguzi wake. Kwamba Kikwete ni Rais hilo hakuna mtu anayeweza kupinga kwa sababu ametangazwa; lakini Kikwete ameshinda kiti cha urais free and squarely.. history nadhani itatusaidia kujibu.

Sasa, CHADEMA waseme wanamtambua Kikwete kuwa Rais ni kwa sababu imeoneshwa kashindwa au kwa sababu katangazwa kuwa ni Rais bila ya kujali matokeo? Wengi naona wanapenda atambuliwe kuwa ni Rais kwa sababu katangazwa kuwa Rais. Well.. wengi tutamtambua wengine hatutamtambua... lakini bora zaidi kutambuliwa na wananchi wote na siyo sehemu tu ya wananchi hao.
CHADEMA SASA NDIO wamesema kuwa wanatambua ushindi wa wabunge wao kwa sababu ni rahisi kuutubitisha lakini wanashindwa kukubali ushindi wa Rais kwa sababu well.. u guessed it..
 
Slaa apasua jipu kuwa hamtambui JK b'se ni result ya uchakachuaji; Mbowe akakazia kuwa ni msimamo wa CHADEMA

Source: STAR TV news 20hrs

Na Nation wameandika hivi:

By FLORENCE MUGARULA, Daily Nation
Monday, November 15 2010


In Summary: Chadema says it will not recognise the president elected at what it says were fraudulent elections

Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo on Monday announced that it would not to recognise President Jakaya Kikwete as a President because of several weaknesses that were recorded during the past general election.

The former Chadema Presidential candidate, Dr Wilbrod Slaa told the Press that President Kikwete was the product of fabricated election results, which Chadema does not recognise.


Dr Slaa added that the Presidential results were not allowed to be questioned anywhere after being released by the National Electoral Commission and that his party has no grounds to say anything in the line of the law.


“I said this before NEC announced the results and we wrote to them trying to explain our complaints but they did not even respond, therefore the only way was to reject the results and not to recognise the President,” said Dr Slaa.


According to Dr Slaa, Chadema has decided not to recognise President Kikwete because the results were fabricated and thus there was no reason to accept him as a President.


The former Karatu MP added that it was difficult to accept election results which were recorded without adhering to the principles of democracy.


Another reason behind rejecting the results and not recognising President Kikwete is that the general election was not free and fair.


“The whole election process was not conducted under conducive environments, we have been warning NEC on this matter but no important measures have been taken on the matter,” said Dr Slaa.


According to Dr Slaa, the matter has been officially handed over to the party (Chadema) so that important measures can be taken for future betterment of wananchi.


“I am using this opportunity to tell all Tanzanians that I was not satisfied by the results and therefore I do not recognize Mr Jakaya Kikwete as a President, I want Tanzanians to understand this,” said Dr Slaa.


But, when reached for the comments, the Attorney General, Judge Fredrick Werema said the new election Act demands that all complaints be filed in court.


1. “I think the law is open on all complaints about election issues, everything is supposed to be filed in court,” said the AG.


2. On the Chadema’s stand over President Kikwete’s win, Judge Werema said Chadema’s decision was ‘nonsense’. (Ni mawazo na msimamo wa kijinga na kipumbavu kutomkubali Rais)[/COLOR]


Commenting to the matter, the Chadema national chairman, Mr Freeman Mbowe said the party will pressurise for the independence committee to probe the violation of elections principles all over the country.


Source: Daily Nation


1. (kwenye red) Kama ni kweli sheria ya uchaguzi inasema malalamiko yote ya uchaguzi kwa ngazi zote yanaweza kupelekwa mahakamani mbona katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema HAPANA (ibara 41(7)? Na Katiba ni sheria mama, sasa iweje sheria mtoto inatengua sheria mama? Ni wapi kwenye sheria mpya za uchaguzi inasema matokeo ya Urais yanaweza kupingwa mahakamani? Legal power ya NEC ni hii "CONSTITUTIONAL PRIVILEGES OF THE NEC

1. In discharging its functions in accordance with the provisions of the Constitution, the National Electoral Commission shall not be obliged to comply with orders or directions of any person or any Government department or the views of any political party.
2. No Court shall have power to inquire into anything done by the National Electoral Commission in the discharge of its functions in accordance with the provisions of the Constitution.
3. For the better carrying out of its functions, the Electoral Commission is an autonomous department."

Werema ameyaona yote haya? Ni vizuri kwanza aka-harmonise hizi sheria halafu akaongea tena

2. (kwenye red) Ni inakuwaje mwanasheria mkuu anawatukana Chadema kuwa ni 'wajinga' na 'wapumbafu'? Si angesema tu sheria inasemaje kuliko kutoa lugha chafu? Hivi kuwa wa kwanza kuteuliwa na kuapishwa na JK ndio kujiona mungu mtu?

Hivi ni mambo gani ufanyika kuonyesha kutomtambua Rais? CUF kule Z'bar walikuwa wanafanyaje?
 
Mbona hilo liko wazi Kiranga usichanganye watu rais ni sehemu ya bunge means president is a subset of bunge as universal bunge lina uwezo wa kumuondoa rais bungeni.

1. Huwezi kuwa na universal set bila ya kuwa na subsets zote, kwa mujibu wa ulichosema hapo juu ni kama vile unaweza kuwa na bunge kamili bila ya rais, halafu bunge kamili hili likamuondoa rais. Ushasema rais ni subset ya bunge, kwa hiyo huwezi kuwa na universal set ya bunge bila subset ya rais.

2. To be sure kuna namna ya kumuondoa rais kwa kupitia bunge, hata hiyo vote of no confidence ni kwa waziri mkuu. Kwenye katiba wameweka an open ended clause.

http://www.tanzania.go.tz/images/katibamuungano.pdf

Ibara ya 38

(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Katiba hii, kiti cha Rais kitakuwa ki wazi, na uchaguzi wa Rais utafanyika au nafasi hiyo itajazwa vinginevyo kwa mujibu wa Katiba hii, kadri itakavyokuwa, kila mara litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo:-
(a) baada ya Bunge kuvunjwa;
(b) baada ya Rais kujiuzulu bila ya kulivunja Bunge kwanza:
(c) baada ya Rais kupoteza sifa za kushika nafasi madaraka ya kuchaguliwa;
(d) baada ya Rais kushtakiwa Bungeni kwa mujibu wa Katiba hii, na kuondolewa katika madaraka;
(e) baada ya kuthibitishwa kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 37 ya Katiba hii kwamba Rais hawezi kumudu kazi na shughuli zake;
(f) baada ya Rais kufariki.

Hata bunge likitaka kumuondoa rais tunaambiwa kiti cha urais kitakuwa wazi (d) baada ya Rais kushtakiwa Bungeni kwa mujibu wa Katiba hii, na kuondolewa katika madaraka;

A can of worms !
 
Back
Top Bottom