nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Monday, 20 June 2011 19:22 newsroom
NA SHAABAN MDOE, ARUSHA
SAKATA la Meya wa Jiji la Arusha, limefikia tamati baada ya CHADEMA kutangaza kumtambua rasmi Meya wa Jiji hilo, Gaudance Lyimo (CCM). Awali, CHADEMA wakiongozwa na mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), waligoma kumtambua Lyimo licha ya kuchaguliwa na kikao halali. Katika kuhalalisha kutomtambua huko, CHADEMA walifanya maandamano makubwa kinyume cha sheria, ambayo yalisababisha mauaji ya watu kadhaa na wengine kujeruhiwa. Akizungumza mara baada ya kikao cha Baraza Maalumu lililofanyika jana kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji, Mwenyekiti wa kikao, Michael Kivuyo, alisema mwafaka juu ya suala hilo umepatikana. Kivuyo, ambaye ni Diwani wa Kata ya Sokoni One (TLP), imeridhiwa Lyimo kuwa Meya wa Jiji kwa kipindi cha miaka mitano, huku nafasi ya Naibu Meya ikishikwa na CHADEMA kwa miaka mitatu na mwaka mmoja utakuwa chini ya TLP.
Alisema kuwa katika kikao hicho, ilikubaliwa kufanyika kwa uchaguzi wa Naibu Meya, ambapo Diwani wa Kimandolu Estomii Mallah (CHADEMA), alichaguliwa kwa kura 21 kati ya 25, huku tatu zikiharibika na moja kumkataa.
Katika makubaliano, Mallah ataanza kushika madaraka hayo kwa miaka mitatu na baadaye Kivuyo atahitimisha kwa kumalizia muda uliobaki. Kivuyo ndiye diwani pekee wa TLP.
Unajua hali ilikuwa mbaya na wananchi walikuwa wakitushangaa, huku wakihoji walituchagua kuwa madiwani si meya, sasa tumeelewana ili kuweka mambo sawa, alisema.
Alisema hatua inayofuata sasa ni kwa madiwani na watendaji wote kufanya kazi, kwani ndani ya halmashauri hiyo kuna ubadhirifu mkubwa unaofanywa na watendaji wasio waaminifu.
Pia, alisema madiwani walifanya uchaguzi wa nafasi za kamati tatu zikiwemo za Elimu, Afya na Uchumi, ambayo itaongozwa na Diwani wa Kata ya Elerai John Bayo (CHADEMA).
Kamati ya Mipango Miji ya Ujenzi na Mazingira, itaongozwa na Diwani wa Olasiti, Ismail Katamboi (CCM).
Nyingine ni Fedha ambayo inakuwa chini ya Meya wa Jiji, Lyimo na Katibu wake anakuwa Naibu Meya, Mallah, huku wajumbe wake wakiwa ni Bayo, Katamboi, Alphonce Mawazo, Mary Kisaka, Reuben Ngowi na Michael Kivuyo.
NA SHAABAN MDOE, ARUSHA
SAKATA la Meya wa Jiji la Arusha, limefikia tamati baada ya CHADEMA kutangaza kumtambua rasmi Meya wa Jiji hilo, Gaudance Lyimo (CCM). Awali, CHADEMA wakiongozwa na mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), waligoma kumtambua Lyimo licha ya kuchaguliwa na kikao halali. Katika kuhalalisha kutomtambua huko, CHADEMA walifanya maandamano makubwa kinyume cha sheria, ambayo yalisababisha mauaji ya watu kadhaa na wengine kujeruhiwa. Akizungumza mara baada ya kikao cha Baraza Maalumu lililofanyika jana kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji, Mwenyekiti wa kikao, Michael Kivuyo, alisema mwafaka juu ya suala hilo umepatikana. Kivuyo, ambaye ni Diwani wa Kata ya Sokoni One (TLP), imeridhiwa Lyimo kuwa Meya wa Jiji kwa kipindi cha miaka mitano, huku nafasi ya Naibu Meya ikishikwa na CHADEMA kwa miaka mitatu na mwaka mmoja utakuwa chini ya TLP.
Alisema kuwa katika kikao hicho, ilikubaliwa kufanyika kwa uchaguzi wa Naibu Meya, ambapo Diwani wa Kimandolu Estomii Mallah (CHADEMA), alichaguliwa kwa kura 21 kati ya 25, huku tatu zikiharibika na moja kumkataa.
Katika makubaliano, Mallah ataanza kushika madaraka hayo kwa miaka mitatu na baadaye Kivuyo atahitimisha kwa kumalizia muda uliobaki. Kivuyo ndiye diwani pekee wa TLP.
Unajua hali ilikuwa mbaya na wananchi walikuwa wakitushangaa, huku wakihoji walituchagua kuwa madiwani si meya, sasa tumeelewana ili kuweka mambo sawa, alisema.
Alisema hatua inayofuata sasa ni kwa madiwani na watendaji wote kufanya kazi, kwani ndani ya halmashauri hiyo kuna ubadhirifu mkubwa unaofanywa na watendaji wasio waaminifu.
Pia, alisema madiwani walifanya uchaguzi wa nafasi za kamati tatu zikiwemo za Elimu, Afya na Uchumi, ambayo itaongozwa na Diwani wa Kata ya Elerai John Bayo (CHADEMA).
Kamati ya Mipango Miji ya Ujenzi na Mazingira, itaongozwa na Diwani wa Olasiti, Ismail Katamboi (CCM).
Nyingine ni Fedha ambayo inakuwa chini ya Meya wa Jiji, Lyimo na Katibu wake anakuwa Naibu Meya, Mallah, huku wajumbe wake wakiwa ni Bayo, Katamboi, Alphonce Mawazo, Mary Kisaka, Reuben Ngowi na Michael Kivuyo.