CHADEMA yasitisha oparesheni M4C na kuitisha kikao cha Kamati Kuu

Kila la heri CHADEMA.

Ila ni muhimu sana mje na mkakati-kazi na sio kauli kali na nzito tu.
 
Mungu ibariki chadema. Mungu ibariki Tanzania. Laana ya damu zilizomwagika kwa viongozi hawa walafi ziishukie ccm na wote waipendao.
 
Najua ushauri wangu amuupendi CDM,lakini kwa kuwa M4C imesitishwa basi zile change za michango ya wafadhili na wananchi zirejeshwe kwenye vitabu vya uhasibu,msiruhusu mtu kukopa wala kuja na visingizio.Au unaonaje kamanda Komu?.
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesitisha operesheni yake ya M4C mkoani Iringa na kuitisha kikao cha dharura cha Kamati Kuu.

Kikao hicho cha Kamati kuu kitafanyika siku ya Jumapili jijini Dar es Salaam chini ya viongozi wake wakuu Mkiti Freeman Mbowe na Katibu mkuu Dr Wilbroad Slaa.

Mkuu wa operesheni M4C Benson Kigaila amesema haiwezekani kuendelea na operesheni huku polisi wakiua watu kwenye mikutano ya CDM kwa maelekezo maalum. Amesema Kamati kuu itatoa mwelekeo rasmi wa chama kuhusu hali hii ambayo haiwezi kuvumiliwa.

Pia inatarajiwa kamati kuu kujadili vitisho vya msajili wa vyama John Tendwa dhidi ya chama hicho,msajili ambaye watanzania wengi wanaamini ni kada mwaminifu wa chama tawala.


Source: Tanzania Daima/Majira.

Mungu Mkuu wa israel ibariki CHADEMA.
 
Natambua kuwa hapa si FB ule ni mtandao wa ullimwengu mzima si kama hapa JF kwa CDM. Lakini ukweli lazima tuwe tunausema. Tunajua wazi wewe ni mmoja wa wanaofaidi fedha za harambee wanazochangishwa walipa kodi wetu. Mnazitumia kupiga propaganda ambazo hazina maana yoyote, hebu jaribu kutembelea TANURU LA FIKRA kule FB ujionee hoja zinavyowasilishwa na kuchangiwa kwa uwazi. Kule FB SLAA, MBOWE na wngine wanachambuliwa kwa undani na na madudu yao kuwekwa hadaharani wakati huku JF ukimgusa SLAA unakula burn ya nguvu na naamini kwa mchango huu lazima leo nile burn , fuatilia baada ya dk 10 hutaniona tena nitakuwa nimeshakula kitanzi toka kwa MODs ambao nao wanakula za walipa kodi. Ukiona mtu anang'ang'ania humu JF ujue huyo anafanyia CDM, na mfano mzuri ni wewe ambaye hutaki kupanua uelewa wako na unabaki kunyoosha vidole juu kama unaimba taarabu.

Acha viroja kama huna hoja. BTW, ni ban na sio burn. Lugha za watu hizo, usikurupuke!
 
Mimi napendekeza tuandamane dhidi ya huyu Msajili wa vyama vya siasa. Lakini maandamano yetu yawe ya ujumbe wa simu kwa siku 3 mfululizo, tukimtaka asimamie haki kwa vyama vyote. Ujumbe wetu usomeke "SOTE TUNA HAKI, KWANINI IWE YA CCM TU?". Kwa wingi wetu tukipeleka text msg kwa siku 3 mfululizo, kwanza tutaonyesha jinsi tunavyoguswa Watanzania kwa ujumla wetu, pili, tutazuia mawasiliano na yoyote kupitia namba zake za mkononi.
Tuwekewe namba zake zote za mkononi tuanze maandamano yetu. Nakumbuka hili lilifanyika kipindindi kilichopita baada ya kuanzishwa na Mwanakijiji na lilikuwa na mafanikio makubwa sana

Acha unafiki, hujawahi kushiriki maandamano hata mara moja. Wewe bingwa wa kuchochea tu. Upo Kigoma, wakija huko tutakupima, kwa sasa endelea kuvua samaki.
 
Chama makini huwa na mikakati makini wakati wote, cdm wamefanya jambo la Busara sana kusitisha M4C na kuamua kuita kamati kuu ili kujadili yaliyojiri kwenye M4C iliyo ambana na vifo vilivyo sababishwa na polisi kwa malengi maalumu ya kuchafua taswira ya chama.

Natagemea watakuja na tamko zito ambalo litakuwa muarobaini wa kumaliza mkakati wa ccm kuwatumia polisi ili kudhofisha harakati za chadema, mtu mwenye akili timamu hahitaji kuwa na 'phd' kama za Nchimbi kuona kuwa ccm inabebwa na polisi, tunahitaji kusikia kamati kuu inakuja na tamko la nguvu kukemea matendo maovu yanayoweza kuliingiza taifa letu kwenye machafuko au ccm kuondoka madarakani huku wakiwa wameiacha nchi ikiwa na makovu yasiyo tibika.

Tuwaombee kamati kuu mje na tamko zito lenye kuangalia maslahi mapana ya nchi yetu.
 
Ni vyema wakatathmini mwendeno wa chama chao kwani kimeanza kujenga taswira mbaya kwa watanzania.

Wewe Ni mwanachama wa hicho chama? I can see your not. Sasa kama taswira mbaya wewe usijali chama chako ndo kinajenga taswira nzuri na kupata uungwaji mkono zaidi. si chill down.
 
Wawe makini sana wakati wa kuendesha mkutano na waandae ulinzi wa kutosha kwani kwa sasa wanaweza hata kuwekewa zile silaha haramu zilizoingizwa na CCM wakaambiwa CDM sasa wanapanga kupindua nchi na silaha zimekamatwa kwenye mkutano wao. Tunatarajia tamko ambalo si la kuchecheka watu huku chini wanaumia/mioyo inavia
 
Chama chenye mipango,mikakati na malengo.
Ooh! naipenda CHADEMA.
Kila lakheri makamanda,
Mungu azidi kuwahekimisha.
 
Waje na kitu ambacho kitawaonesha kuwa hatimaye wanaelewa uzito wa kile kinachowakabili. Maana tangu 2010 bado wanaonekana walikuwa wanaamini kuwa wanaweza kuishawishi serikali ya CCM to be nice to them...

MM nakubaliana nawe kwa sehemu, lakini lazima tufahamu kuwa watanzania wako katika kipindi cha mpito. Tulizoea kuamini kuwa kauli za viongozi huwa za mwisho na hazipaswi kuhojiwa. Tukiwa too aggressive kuna wananchi wengi tunaweza kuwapoteza kwani hawajazoea mchakamchaka wa kimageuzi. Natumaini Chadema watakuja na mpango kazi thabiti katika kuelekea kuchukua dola.
 
CDM naamini wanajua kuwa kwenye msafara wa mamba na kenge wamo. Mungu awabariki.
 
Back
Top Bottom