Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,262
- 9,714
Ndugu zangu Watanzania,
Huku mitaani kumechafuka na hali ni mbaya sana kwa CHADEMA,baada ya kuwa na mashambulizi makali na ukosoaji mkubwa sana kutoka kwa wananchi kwa hoja ya CHADEMA ya kutaka kwa kila jimbo kuwa na wabunge wawili.watu wana laani sana na kuipinga sana kauli hiyo iliyoonyesha ulafi mkubwa wa madaraka walionao CHADEMA.
Ni kauli ambayo imeidhalilisha sana CHADEMA mitaani na kuonekana ni chama cha kupigania maslahi yake tu. Ni kauli ambayo wananchi wanasema kuwa imeonyesha ni namna gani CHADEMA wasivyo na huruma wala uchungu wala kuguswa na maisha ya watanzania. Wanasema badala CHADEMA kubuni na kutoa hoja kwa serikali zinazoweza kupunguza gharama na mzigo kwa wananchi, wao wanakuja na hoja wanazoona zitawahakikishia shibe ya matumbo yao huku zikileta na kuwabebesha mzigo wa mateso watanzania wanyonge..
Kwa hakika CHADEMA inapaswa kuwaomba radhi watanzania na kufuta kabisa pendekezo hilo la kijinga lisilo na mashiko wala msaada wowote kwa maisha ya watanzania.yaani wao wanataka kodi zote na makusanyo yote zielekezwe katika kulipa mishahara na marupurupu ya wabunge badala ya huduma kwa wananchi.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Huku mitaani kumechafuka na hali ni mbaya sana kwa CHADEMA,baada ya kuwa na mashambulizi makali na ukosoaji mkubwa sana kutoka kwa wananchi kwa hoja ya CHADEMA ya kutaka kwa kila jimbo kuwa na wabunge wawili.watu wana laani sana na kuipinga sana kauli hiyo iliyoonyesha ulafi mkubwa wa madaraka walionao CHADEMA.
Ni kauli ambayo imeidhalilisha sana CHADEMA mitaani na kuonekana ni chama cha kupigania maslahi yake tu. Ni kauli ambayo wananchi wanasema kuwa imeonyesha ni namna gani CHADEMA wasivyo na huruma wala uchungu wala kuguswa na maisha ya watanzania. Wanasema badala CHADEMA kubuni na kutoa hoja kwa serikali zinazoweza kupunguza gharama na mzigo kwa wananchi, wao wanakuja na hoja wanazoona zitawahakikishia shibe ya matumbo yao huku zikileta na kuwabebesha mzigo wa mateso watanzania wanyonge..
Kwa hakika CHADEMA inapaswa kuwaomba radhi watanzania na kufuta kabisa pendekezo hilo la kijinga lisilo na mashiko wala msaada wowote kwa maisha ya watanzania.yaani wao wanataka kodi zote na makusanyo yote zielekezwe katika kulipa mishahara na marupurupu ya wabunge badala ya huduma kwa wananchi.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.