Paul Makonda Mmoja ameisambaratisha na kuizima CHADEMA mitaani

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,305
9,734
Ndugu zangu Watanzania,

Mheshimiwa Paul Makonda ni Mwamba na chuma kwelikweli,ni field Marshall ,Ni jemedari hodari,ni mpambanaji mwenye moyo na damu ya kipambanaji. Mpaka inafika hatua unasema kwanini hakuingia mapema uwanjani? Lakini unajipa jibu kuwa kila jambo na wakati wake. Na wakati huu ndio ulikuwa umepangwa na Mungu ili Mheshimiwa Makonda aingie kuonyesha kipawa na Karama kubwa ya uongozi iliyopo ndani yake. Alichelewa kuja kwa kuwa Mungu alikuwa bado akimuandaa na kumuweka tayari kuwasemea wananchi wanyonge.ndio maana ujio wake uliitikisa nchi ,milima na mabonde.

Mheshimiwa Makonda tangia ameingia mitaani na kupiga mchaka mchaka wa kazi ya kusikiliza kero za wananchi na kuwapatia majibu, pamoja na kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM imeleta kilio kwa vyama vya upinzani kama CHADEMA ambavyo siku zote vimekuwa vikitegemea janja janja ya kudandia matukio na kuyafanya kama mtaji wake wa kisiasa.

CHADEMA imepotezwa na kusambaratishwa kabisa mitaani.imezimwa kama taa,imeyeyuka kama mshumaa,imefutika kama moshi,imetoweka kama ukungu na imepotea kama upepo. Husikii habari za CHADEMA wala matukio ya CHADEMA,haieleweki imekwenda kufungiwa katika kabati la wapi.nchi nzima imetekwa na kutawaliwa na ziara za Mheshimiwa Makonda ambazo zimekuwa kimbilio la watanzania wanyonge wenye shida na kero mbalimbali.

Hii ndio taabu na shida ya kutembelea na kutegemea matukio katika kuendesha siasa.siku zote CHADEMA ilikuwa inafanya usanii na ubabaishaji wa kusubiri matukio ndio ilipuke kama moto wa petrol .sasa Mwamba Paul Makonda kijana jasiri kusini mwa jangwa la sahara na aliyezaliwa kama kiongozi amekuja na siasa za kugusa maisha ya watu,kuzungumza kero na shida za watu,hisia za watu, changamoto za watu na lugha za watu mambo ambayo ndiyo watanzania wanayohitaji kuyasikia masikioni mwao siku zote.

Mheshimiwa Paul Makonda ameingia Mitaani kuwafuta machozi watu,kuwapa faraja, matumaini,furaha ,majibu ya maswali yao pamoja na kuwarejeshea tabasamu katika mioyo yao.hii ndio sababu Anaendelea kugusa mioyo ya watanzania,kukimbiliwa na wenye shida,kuliliwa na wenye kuhitaji msaada.kwa sababu watu wametambua kifua na moyo wa Mheshimiwa Makonda umebeba huruma na upendo mkubwa sana kwa watanzania wanyonge.wametambua ni mtu wa msaada.ni mtu mwenye moyo wa kusaidia na kugusa maisha ya watu.

Sasa ni nani mwenye akili Timamu na anayejitambua anayeweza kuanza kuwaunga mkono CHADEMA? Nani akiunge mkono CHADEMA kinachopendekeza uwepo wa wabunge wawili katika kila jimbo? Nani aunge mkono mawazo na mapendekezo hayo ya kilafi,kifisi na yenye kuonyesha uchu na tamaa ya madaraka ya CHADEMA iliyo jaa katika vifua vyao? Nani awaunge mkono CHADEMA ambao siku zote wao wanapigania mambo yatakayowarahisishia wao ukubwa wa mlango wa kuingia bungeni kwenda kula mishahara wasiyoitolea jasho?

Nani awaunge mkono CHADEMA ambao wanasema kazi ya uboda boda ,umama ntilie kuwa ni kazi za laana kama ambavyo alitamka lema? Nani awaunge mkono chama cha namna hii kilichokosa huruma na Upendo kwa watu?

Ndio maana watanzania kwa umoja wao wameamua kuwapuuza CHADEMA na kutofuatilia kabisa habari zao.ndio maana wameamua kuiunga mkono CCM na kuendelea kujiandaa kuipatia kura za ndio katika chaguzi zijazo. Sasa CHADEMA wamebakia wanachungulia ziara za Mheshimiwa Makonda huku mioyo yao ikitokwa machozi bila kukatika wanapoona Mheshimiwa Makonda na CCM wakipata mapokezi ya kishindo yaliyofurika maelefu ya watu wanaohudhuria kwa hiyari yao wenyewe.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
IMG-20240202-WA0004.jpg
IMG-20240114-WA0016.jpg
IMG-20240115-WA0040.jpg
IMG-20240115-WA0007.jpg
IMG-20240114-WA0037.jpg
IMG-20240202-WA0010.jpg
img_tmp_tag1705908502140.jpg
 
Nakusamehe bure kabisaa. Mungu aendelee kukujalia maisha marefu yeye heri na amani.uso wake uwe pamoja nawe. Akupiganie , kukutetea na kukulinda dhidi ya maadui zako. Isiwepo silaha yoyote itakayo inuka na kufanikiwa mbele yako.Mungu akufanye kuwa chombo chake kipya cha kueneza upendo na amani hapa Duniani.ukawe mpatanishi kwa watu na faraja kwa watu.
Sitaki Dua za MBUMBUMBU lenye Ugonjwa wa UZEZETA wewe ndio unaehitaji Maombi ili UZEZETA ukutoke.

Acha kutuhadaa Watanzania na kutumika kusambaza Propaganda za KIJINGA.
 
Sitaki Dua za MBUMBUMBU lenye Ugonjwa wa UZEZETA wewe ndio unaehitaji Maombi ili UZEZETA ukutoke.

Acha kutuhadaa Watanzania na kutumika kusambaza Propaganda za KIJINGA.
Naendelea kukusamehe bure kabisa maana nimeshatambua tatizo ulilonalo kichwani.kwa hiyo maombi yangu mema yatakusaidia kupona.
 
Back
Top Bottom