CHADEMA Yajitoa mchakato wa Katiba; Yadai Rais kawauza!

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kuwa kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kusaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya mwaka 2011, kimekiuka makubaliano yao, hivyo kimeamua kususia mchakato mzima wa kuratibu maoni kwa ajili ya kupata Katiba Mpya kwa kutumia sheria hiyo. Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa hatua hiyo imefikiwa ili kuonyesha kutoridhishwa na namna kiongozi huyo wa nchi, alivyowachezea akili.

"Kitendo cha Rais Kikwete kuusaini muswada huo bila ya kuupitia ni kinyume na makubaliano, jambo ambalo linatufanya tususie mchakato mzima wa kuuratibu maoni ya kwa ajili ya Katiba Mpya kupitia sheria ailiyoisaini,"alisema Mnyika na kuendelea: "Tumeamua kujitoa kwenye mchakato mzima wa kuratibu Marekebisho ya Muswada wa Sheria ya Katiba kutokana na Rais kukiuka makubaliano yetu Ikulu yaliyomtaka aupitie kwanza kabla ya kuusaini."

Mnyika aliendelea kueleza kuwa Chadema iliwasilisha waraka wa mapendekezo sita kwa Rais ikiwa ni pamoja na kumtaka asiusaini muswada huo kutokana na wananchi kutoshirikishwa ipasavyo kwenye mchakato wa ukusanyaji wa maoni.


Zaidi: Chadema: Rais ametuuza




 
Last edited by a moderator:
Mnyika kwani ulitaka mapendekezo yote lazima Jk ayakubali? kama yalikuwa sita unajuaje labda matano yalibaki kayakubali?
 
Hawa CHADEMA nao kama hawaeleweki eleweki vile...
Yaani hata mimi siwaelewi, nilitegemea wangevuta subira ili kuona kama serikali itapeleka mapendekezo ya kurekebisha sheria hii katika bunge lijalo. Job true true
 
kukataa pendekezo moja tu kati ya sita sio kukiuka mapendekezo. chadema wakubali win win situation katika mazungumzo na Rais. kama walikwenda Ikulu ili matakwa yao yote yatekelezwe ni kumjaribu JK vibaya
 
Kwa makubaliano yale na JK ambayo yalisainiwa na Mnyika na Nchimbi hakuna hata moja lililosema kuwa Rais asisaini Muswada kabla ya marekebisho.

Ila nakumbuka la kwanza lilikuwa linasema "Pamoja na sheria hiyo kupitishwa na Bunge ipo haja ya kuendelea kuiboresha ili ikidhi mahitaji ya kujenga kuaminiana na muafaka wa kitaifa".

Sina hakika kama mlilielewa hili. Yawezekana mlinogewa chai ya Ikulu na kushindwa kulitafakari hili kabla ya kulisaini. Kwa maana hiyo kusema kwamba rais kawauza mmeniboa
.
 
kukataa pendekezo moja tu kati ya sita sio kukiuka mapendekezo. chadema wakubali win win situation katika mazungumzo na Rais. kama walikwenda Ikulu ili matakwa yao yote yatekelezwe ni kumjaribu JK vibaya
unataka kutuaminisha kwamba swala la hii sheria ni swla la hisani ya Kikwete?
kwamba anweza kuamua atakavyo kwasababu he is the president na sisi tunyamaze kwasababu ameamua hivyo?

the bigger issue here is, issue za msingi zizingatiwe..........binafsi najua kwamba hakuna jema linaloweza kutoka kwa CCM wala JK wa CCM.......sio katiba mpya wala tanzania tuitakayo.
 
Mnyika huko sio kujitoa mlishajitoa muda mrefu mlikwenda ku-mbeep Jk na yeye kawapigia hamtaki kupokea simu
 
Kwani ni nani anyeongoza nchi hii?
Haiwezekani kupata katiba kwa njia wanayoitaka mpaka waingie madarakani.
Mbona Lema kimya?....
 
Mnyika ndo katuuza. Katika makubaliano aliyotia saini pale Ikulu wakati anapiga ile 'tea', hakuna hata moja lilosema kuwa mmekubaliana rais asisaini muswada kuwa sheria kabla ya marekebisho.

Ni afadhali muheshimiwa Mnyika akae kimya na atuombe radhi kwa kutokutafakari makubalianao kabla ya kusaini. Ni sawa kabisa na wale wanaoingia mikataba mibovu.
 
Mnyika naona unaona maoni ya watu wengi hapo juu, hata kitaani ni hivyo hivyo

All I can say to you guys please STICKY to your decision, chadema ijulikane ina mlengo gani, mlengo wa kulia, kushoto au kati, amueni kuwa radicals na dunia ijue hivyo...au muwe kondoo na dunia itawajua hivyo. Mmekuwa mnabadilika badilika sana.....

Hata iwe vipi hamtakuwa na uwezo wa kumfurahisha kila mtu.....ila amueni muwe vipi na mtavuta wengine kwa vile mtakavyokuwa!!

Leo mtakasirika, kesho mtamchekea yule yule aliyewakasirisha jana, kitu gani huwa kinatokea??...hatujui

Lingine, jamani ikiwezekana hiyo ruzuku ichukue nafasi ya posho zenu za bungeni...susieni vikao vya bunge na DUNIA ijue hivyo CCM wanajua kuwa huwa mnatisha leo....mnakuja kesho! this aint good not neither for your supporters nor for your members.
 
Back
Top Bottom