CHADEMA yaibwaga CCM Arumeru Mashariki; CCM Yakubali kushindwa (Zaidi ya kura 6,000)

Ushindi huu ni ishara ya kuchokwa kwa CCM na sera zisizotekelezeka.Wanataka kutuletea utawala wa kifalme..Tutakutana 2015 ili tuichukue nchi kabisa..Peoples power
 
Haleluya!
CDM JUUUU!!
Mtandao wa JamiiForums waweza kutangaza kwa uhakika kabisa kutokana na vyanzo makao makuu ya Jimbo huko Arumeru Mashariki kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeshinda uchaguzi mdogo ambapo mgombea wake Bw. Joshua Nassari ameibuka kidedea baada ya kumbwaga vibaya mgombea wa CCM Bw. Siyoi Sumari. Matokeo yanaonesha hadi hivi sasa baada ya zaidi ya asilimia 80 ya vituo vyote kuripoti CDM imeshinda kata 14 dhidi ya 3 za CCM.

Chama cha Mapinduzi tayari kimekuballi kushindwa na kutoa pongezi kwa mgombea wa CDM.

CDM imeshinda kwa zaidi ya kura 6000


MATOKEO SEMI-OFFICIAL:

CHADEMA 32,543
CCM 26,452


My Take:
Bila ya shaka Uongozi wa taifa wa CDM hauna sababu ya kujiuzulu kwa wakati huu! Upepo umevuma upande wao na mtumbwi unaelekea kwenye ushindi 2015!

Kutoka kwa Zitto (FB)

zitto-status.jpg
 
Mie sijaridhika na huo ushindi? Kwa nini ccm wana kura nyingi hivo? Mie nilitaka wapate angalau robo ya kura zote, anyway mwanzo mgumu
 
Mimi nimechelewa kula daku maana nipo kwenye Kwaresma.... Mungu atanisamehe maana anajua nafanya jambo la haki kufurahia huru dhidi siasa za mabavu zisizo na tija kwa Wana Arumeru Mashariki na Watanzania kwa ujumla! Mungu Ibariki Tanzania, Mungu bariki Mabadiliko!
 
Wakuu, mpaka sasa tumebakiza kukusanya matokeo ya vituo vinne tu, narudi vituo si kata, vituo vya kupigia kura katika kata nne tofauti. Matokeo mpaka sasa yanasomeka hivi;

CHADEMA 32, 535
CCM 26, 296
AFP 131
DP 72
NRA 32
SAU 22
TLP 16
UPDP 22

Tusiwe na wasiwasi hzo vitu hvyo vinne hata cdm wakipata zero na sisiemu kupata kura zote bado ushindi ni kwa cdm(vituo vinne havizidi kura 1200)
 
Wakuu, mpaka sasa tumebakiza kukusanya matokeo ya vituo vinne tu, narudi vituo si kata, vituo vya kupigia kura katika kata nne tofauti. Matokeo mpaka sasa yanasomeka hivi;

CHADEMA 32, 535
CCM 26, 296
AFP 131
DP 72
NRA 32
SAU 22
TLP 16
UPDP 22
 
Back
Top Bottom