Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Miaka ya sitini Mwalimu Nyerere aliwahi kusema "Let the people make their own decisions, including their own mistakes". Sijachambua kama kweli alitekeleza maneno yake mwenyewe katika utawala wake.
Mwaka jana Paul Kagame wa Rwanda alisema, "While more than US$ 300 billion in aid has apparently been disbursed to our continent since 1970, there is little to show for it in terms of economic growth and human development". What is the case for Tanzania, is aid working?
Frantz Fanon, miaka ya sitini aliwahi kusema katika kitabu chake Wretched of the Earth kwamba viongozi wanaopigania uhuru Africa (wakati huo) hawana malengo sawa na ya umma. Kwamba umma unataka mabadiliko na maendeleo wakati viongozi wao wanataka waingie madarakani ili wapate fursa ya kula kama wazungu, kuendesha magari ya kizungu,kuongea kizungu, kulala nyumba za kizungu na ikiwezekana kulala na wanawake (wanaume) wa kizungu.
Mwaka 2008 Kardinali Pengo aliwahi kuhoji kama makamanda wanaopiga vita ufisadi wanafanya hivyo kwa sababu wanachukia ufisadi au kwa sababu wanawachukia mafisadi.
Najua sasa hivi unajiuliza mbona huyu gurudumu anakwenda zigzag?
Tumefikia kiwango hiki cha umasikini, kiasi kikubwa, kwa sababu ya kutegemea wafadhili. Wanatuambia nini tufanye, lini tusifanye na tufanye vipi. Hufanya hivi kwa kuweka mifumo ya kufanya maamuzi ambayo sisi huikubali na kutekeleza.
Kuna dude linaitwa MKUKUTA na linguine JAST. Wengi wenu hapa janvini mnajua zaidi kuliko mimi. Lakini kuna kamati ambazo hukutana karibu kila mwezi kuratibu shuhuli katika kila wizara. Zaidi ya nusu ya wajumbe wa mikutano hii huwa ni wazungu, wako makini na kila kinachoandikwa (huandika wao) na kupitishwa. Hufadhili safari za nje, semina na magari ya kifahari kwa maafisa wetu wa serikali kama incentive ya kuwatawala.
Kikwete alitangaza kwenye kampeni zake za uchaguzi kwamba serikali yetu inapendwa na wafadhili kwa sababu ya sera nzuri, amani na utulivu. Wiki iliyopita aliwaita mabalozi akawaomba radhi kutokana na mauaji ya raia Arusha. Wananchi?
Kisha nikaona jinsi wananchi walivyojitolea katika tukio la kuwazika mashujaa wetu wapigania uhuru waliouawa na polisi kule arusha. Kwa hali na mali, kwa moyo wote kabisa. Nikaamini kwamba kumbe inawezekana kupanga mambo yetu wenyewe, kuyagaramia na kuyatekeleza.
Kwa hiyo nikaamini kwamba viongozi wa chadema wasipotiwa najisi na wafadhili, watatekeleza matakwa ya umma, siyo ya wafadhili. Kwamba tutapata maendeleo ya kweli badala ya maendeleo ya takwimu kwenye makaratasi.
Hivyo, Chadema please, changisheni wananchi badala ya kutembeza bakuli kwa wafadhili. Hata wafadhili wakiwabemb eleza vipi, please kataeni. Kwani ukimuona ngiri anakukimbilia meno nje usidhani anakuchekea, ndivyo meno yake yalivyo, kwamba anafuata huo mguu wako! Mguu wetu ni rasilimali zetu.
Mwaka jana Paul Kagame wa Rwanda alisema, "While more than US$ 300 billion in aid has apparently been disbursed to our continent since 1970, there is little to show for it in terms of economic growth and human development". What is the case for Tanzania, is aid working?
Frantz Fanon, miaka ya sitini aliwahi kusema katika kitabu chake Wretched of the Earth kwamba viongozi wanaopigania uhuru Africa (wakati huo) hawana malengo sawa na ya umma. Kwamba umma unataka mabadiliko na maendeleo wakati viongozi wao wanataka waingie madarakani ili wapate fursa ya kula kama wazungu, kuendesha magari ya kizungu,kuongea kizungu, kulala nyumba za kizungu na ikiwezekana kulala na wanawake (wanaume) wa kizungu.
Mwaka 2008 Kardinali Pengo aliwahi kuhoji kama makamanda wanaopiga vita ufisadi wanafanya hivyo kwa sababu wanachukia ufisadi au kwa sababu wanawachukia mafisadi.
Najua sasa hivi unajiuliza mbona huyu gurudumu anakwenda zigzag?
Tumefikia kiwango hiki cha umasikini, kiasi kikubwa, kwa sababu ya kutegemea wafadhili. Wanatuambia nini tufanye, lini tusifanye na tufanye vipi. Hufanya hivi kwa kuweka mifumo ya kufanya maamuzi ambayo sisi huikubali na kutekeleza.
Kuna dude linaitwa MKUKUTA na linguine JAST. Wengi wenu hapa janvini mnajua zaidi kuliko mimi. Lakini kuna kamati ambazo hukutana karibu kila mwezi kuratibu shuhuli katika kila wizara. Zaidi ya nusu ya wajumbe wa mikutano hii huwa ni wazungu, wako makini na kila kinachoandikwa (huandika wao) na kupitishwa. Hufadhili safari za nje, semina na magari ya kifahari kwa maafisa wetu wa serikali kama incentive ya kuwatawala.
Kikwete alitangaza kwenye kampeni zake za uchaguzi kwamba serikali yetu inapendwa na wafadhili kwa sababu ya sera nzuri, amani na utulivu. Wiki iliyopita aliwaita mabalozi akawaomba radhi kutokana na mauaji ya raia Arusha. Wananchi?
Kisha nikaona jinsi wananchi walivyojitolea katika tukio la kuwazika mashujaa wetu wapigania uhuru waliouawa na polisi kule arusha. Kwa hali na mali, kwa moyo wote kabisa. Nikaamini kwamba kumbe inawezekana kupanga mambo yetu wenyewe, kuyagaramia na kuyatekeleza.
Kwa hiyo nikaamini kwamba viongozi wa chadema wasipotiwa najisi na wafadhili, watatekeleza matakwa ya umma, siyo ya wafadhili. Kwamba tutapata maendeleo ya kweli badala ya maendeleo ya takwimu kwenye makaratasi.
Hivyo, Chadema please, changisheni wananchi badala ya kutembeza bakuli kwa wafadhili. Hata wafadhili wakiwabemb eleza vipi, please kataeni. Kwani ukimuona ngiri anakukimbilia meno nje usidhani anakuchekea, ndivyo meno yake yalivyo, kwamba anafuata huo mguu wako! Mguu wetu ni rasilimali zetu.