Mabilioni ambayo NGOs zinapata kutoka kwa wafadhili yazua mjadala

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,116
49,840
Nimewahi kuhoji kwanini hizi pesa ambazo hawa wanaojiita asasi zisizo za kiserikali wasiwe wanazitumia ku compliment mipango ya Serikali badala yake nao wanakuwa na mambo yao ambayo hakuna tija yoyote inaonekana kwenye jamii.

Kama hawataki Serikali iwapige marufuku sio lazima wawepo maana kwa pesa zao kutoratibiwa zinaingia kwenye uchumi kinyemela na pia ndio hutumika kufadhili mambo ya ushoga, utakatishaji pesa, Madawa ya kulevya na kuingiza silaha kienyeji.

Ukisoma Takwimu zake ni pesa zaidi ya Trilioni 3 zinaingia Nchini kwa njia ya hawa NGOs lakini hakuna impacts inayoonekana kwenye jamii.

Laiti kama wao wangekuwa wana compliment mipango ya Serikali tungekuwa mbali ila hawataki jwa sababu wanazozijua wao.

Kwanini Mwendazake alishindwa kuwapiga marufuku Hawa? Wanajifanyaga kutoa Elimu, Elimu ipi ya maana wanatoa?

My Take
Serikali Wasajilini Upya na Kila NGOs ihakikishe Ina complements mipango ya Serikali Kwa Kila Moja na usajili wake vinginevyo wapigwe marufuku hakuna kitu Cha maana wanasaidia jamii.


======

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dk Seif Shekalaghe akizungumza. Picha na Mtandao

Dodoma. Wakati mashirikia yasiyo ya kiserikali yakizungumzia namna fedha za wafadhili zilivyowanufaisha Watanzania, wadau wameonyesha wasiwasi wao kama zote zinafika maeneo husika.

Akizungumza na Mwananchi kwa simu jana kuhusiana na fedha hizo, Mhadhiri wa Chuo cha Elimu ya Biashara, Dk Nasibu Mramba alisema huenda kuna fedha ambazo huishia kwenye mifuko ya watu binafsi kwa sababu wanaoweza kuwakagua ni wafadhili waliotoa fedha hizo pekee.

Chanzo: Ripoti ya Ufuatiliaji wa Kaya (NPS)

Mwenendo wa fedha za NGOS zinazoingia nchini

Ongezeko la fedha zinazopatikana nchini kupitia ufadhili wa NGOs
Imeandaliwa na: George Helahela
Mchanganuo wa fedha za NGOs

“Hizi NGO zinapaswa kuangalia thamani ya fedha kwa kuhakikisha zinakwenda kwa wale waliokusudiwa, tumeshashuhudia fedha hizi za ufadhili wa mradi zikiishia mifukoni mwa watu na Serikali haina nguvu ya kutia mkono huko,” alisema Dk Mramba.

Kwa mujibu wa Ripoti iliyotolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto inaonyesha Sh2.24 trilioni zilizopatikana nchini kupitia mashirika hayo zimewanufaisha watu milioni 119.69 katika kipindi cha Januari hadi Desemba mwaka 2022.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa fedha hizo ni ongezeko la Sh1.05 trilioni na asilimia 88.3 ya mapato ya mashirika ikilinganishwa na mwaka 2021.

Mapato hayo ni asilimia 5.3 ya bajeti ya Serikali kwa mwaka 2022/23, yanatokana na mashirika 1,257 yaliyowasilisha taarifa zao serikalini kati ya mashirika 6,635 yaliyopo.

Imeainisha kati ya fedha hizo Sh2.14 trilioni zilitokana na wafadhili kutoka nje ya nchi, ndani wametoa Sh18.77 bilioni huku michango kutoka sekta binafsi ikiwa ni Sh7.58 bilioni.

Michango ya jamii ni Sh4.20 bilioni, malipo ya huduma Sh5.64 bilioni, mapato ya vitega uchumi Sh3.40 bilioni, michango ya wanachama Sh29.23 bilioni, ruzuku Sh290.65 milioni, msamaha wa kodi Sh540.49 milioni, bakaa Sh37.18 bilioni.

Katika fedha hizo zilizopatikana kupitia mashirika yasiyo Serikali kiasi kikubwa kimeenda katika kutekeleza miradi ya sekta ya afya ambayo ilipata Sh72.82 bilioni ikifuatiwa na uwezeshwaji wa jamii ambayo ilikuwa na Sh57.51 bilioni.

Maeneo mengine ni ulinzi wa jamii Sh39.92 bilioni, Kilimo (Sh29.28 bilioni), Elimu (Sh26.83 bilioni), mazingira (Sh26.11 bilioni), Utawala Bora (Sh13.18 bilioni), nishati (Sh3.50 bilioni), maji (Sh3.06 bilioni) na haki za binadamu (Sh1.47 bilioni).

Ajira na wanufaika

Ripoti hiyo inaonyesha ajira 15,479 zilitolewa na mashirika yasiyo ya kiserikali 1,257 kwa mwaka huo huku 9,974 wakiwa ni Watanzania na wageni walikuwa 156.

Kati ya ajira hizo 8,627 zilikuwa ni za wanawake na 6,852 zilikuwa ni za wanaume.

Pia katika ripoti hiyo inaonyesha waliojitolea kwenye mashirika hayo walikuwa 5,505, kati yao Watanzania ni 5,255 na wageni 250.

Kwa upande wa wanufaika, jumla ya watu milioni 119.69 walinufaika na miradi iliyotekelezwa kupitia fedha hizo huku sekta ya afya ikichukua zaidi ya theluthi mbili ya wanufaika.

Sekta ya afya ilikuwa na wanufaika milioni 83.03 huku waliobakia wakiwa kwenye sekta nyingine tisa ambazo ni uwezeshaji wa jamii, ulinzi wa jamii, mazingira, kilimo, elimu, utawala bora, maji, haki za binadamu na jinsia.

Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dk Seif Shekalaghe alisema kuna mashirika ambayo hayajawasilisha taarifa zake katika mwaka huo, idadi ambayo ni robo tu ya mashirika yaliyopo.

Kwa mujibu wa Dk Shekalaghe, kuna jumla ya mashirika 6,635, lakini 1,257 tu ndiyo yaliyotoa taarifa zake.

“Kutokuwasilisha kwa taarifa kunapunguza utambuzi wa mchango wa mashirika yasiyo ya kiserikali katika maendeleo ya Taifa,” alisema.

Wadau wazungumzia

Akizungumzia hilo, Dk Mramba alisema ni jambo zuri la kuchangia katika maendeleo ya Taifa lakini fedha hizo nyingi zinatoka kwa wafadhili wanaopanga ni wapi ziende kutumika.

Alisema mara nyingi fedha hizo zinatolewa kama makubaliano kati ya mtoaji na mpokeaji na Serikali haihusiki, hivyo anayezikagua mara nyingi anakuwa ni aliyezitoa.

Naye Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Dk Paul Loisulie alisema wafadhili wamejenga minyororo yao kwa nchi walizozitawala na hata ufadhili wanaoufanya ni njia ya kuendelea kuboresha uwepo wao.


“Kuonyesha kwamba wao ni muhimu kwa nchi za Afrika kwa kuhakikisha kuwa minyororo yao haikatiki nchini. Na pia misaada hiyo ni njia ya kuendelea kuweka utegemezi,”alisema.


Alisema kutegemea kwa kiasi kikubwa ufadhili ili kujiendesha inamaanisha hata kimawazo na kisaikolojia hakuna wakati NGOs zitawaza kuja kufanya kazi kwa kujitegemea.
 
Mkuu hizo pesa wewe zinakuuma nin wenzako kuzila? ni mali ya walipakodi watanzania? je serikali itaweza kuwapa mkate wao wa kila siku watanzania ambao wanapata chochote kupitia hizi NGOs kama ikizifuta? what the hell are you talking dude? taarifa ya mwezi March unaileta leo
 
Mkuu hizo pesa wewe zinakuuma nin wenzako kuzila? ni mali ya walipakodi watanzania? je serikali itaweza kuwapa mkate wao wa kila siku watanzania ambao wanapata chochote kupitia hizi NGOs kama ikizifuta? what the hell are you talking dude?
Umesoma mada? Kwa hiyo Jamii iharibike Kwa sababu hizo pesa sitoi Mimi si ndio? Usiwe mpumbavu kutunza na kuhifadhi Maadili ya jamii ni muhimu kuliko pesa.
 
Hizo NGOs acheni kuzionea nyinyi ndio wezi wakubwa wa fefha za KODI misaada na Mikopo.

Mwisho wenu waja.
Usiwe unaongea Kwa sababu za mihemko Yako.Kuingiza pesa ambazo hazina uratibu kwenye mfumo wa uchumi ni hatari kwa Ustawi wa jamii.

Wao wapange wanachotaka kufanya ila kiwe ni ku complements pale Serikali au jamii inapokwama sio kuleta blaa blaa zisizo na msingi.
 
Usiwe unaongea Kwa sababu za mihemko Yako.Khingiza pesa ambazo hazina uratibu kwenye mfumo wa uchumi ni hatari kwa Ustawi wa jamii.

Wao wapange wanachotaka kufanya ila kiwe ni ku complements pale Serikali au jamii inapokwama sio kuleta blaa blaa zisizo na msingi.
Acheni NGOs zifanye kazi ambazo Serikali ya CCM imeshindwa imebaki kupora tu Kodi na Tozo zetu.
 
Wanataka wapewe walipane posho nono na kununua V8 hawa wajinga
Nani kasema Wapewe? Wao wafanye miradi yenye Tija Kwa ku complements ya serikali na pia lazima wataje Bajeti zao Ili Serikali izijue wanazo.kiasi gani na wanafanya nini na wapi.

Vingine Hawa ndio huleta ugaini Nchini.
 
Acheni ujinga kama mmeshindwa kuongoza kaaeni pembeni
Fala nini,Takataka kama nyie machadomo Toka mumeanza kutafuna ruzuku za chama amabzo ni Kodi za Wananchi mumewahi wachimbia hata choo Cha Umma?

Mlikuwa mnaongoza Halmashauri kipi Cha maana mlifanya?

Mara nyingi Huwa nasema watu wapumbavu ndio wanaweza waamini nyie mbumbumbu.
 
Nimewahi kuhoji Kwa nini hizi pesa ambazo Hawa wanaojiita asasi zisizo za kiserikali wasiwe wanazitumia ku compliment mipango ya Serikali badala yake nao wanakuwa na mambo Yao ambayo hakuna Tija yeyote inaonekana kwenye jamii.

Kama Hawataki Serikali iwapige marufuku sio lazima wawepo maana Kwa pesa zao kutoratibiwa zinaingia kwenye uchumi kinyemela na pia ndio hutumika kufadhili mambo ya ushoga,utakatishaji pesa,Madawa ya kulevya na kuingiza silaha kienyeji.

Ukisoma Takwimu zake ni pesa zaidi ya Trilioni 3 zinaingia Nchini Kwa njia ya Hawa NGOs lakini hakuna impacts inayoonekana kwenye jamii.

Laiti kama wao wangekuwa Wana compliment mipango ya Serikali tungekuwa mbali ila Hawataki Kwa sababu wanazozijua wao.

Kwa nini Mwendazake alishindwa kuwapiga marufuku Hawa? Wanajifanyaga kutoa Elimu,Elimu ipi ya maana wanatoa?

View: https://twitter.com/MwananchiNews/status/1711266728737456195?t=ACrCggBVl37h6B9Xjv9GTQ&s=19

My Take
Serikali Wasajilini Upya na Kila NGOs ihakikishe Ina complements mipango ya Serikali Kwa Kila Moja na usajili wake vinginevyo wapigwe marufuku hakuna kitu Cha maana wanasaidia jamii.

Asimilimia 18 had 30 za hizo pesa zinalipwa selikalini kama kodi.
 
Mtoa mada ungekua na taarifa sahihi usingeleta 'upuuzi' huu hapa jukwaani.

Nenda katembelee hospitali iliyo karibu na wewe ujionee ni majengo mangapi yamejengwa kwa ufadhili wa hizo NGO.
Leo hii hatugharimii vipimo na matibabu ya kifua kikuu, gharama zote zinabebwa na hao unaowabeza leo.
Kuna mengi yanafanyika kwenye afya na elimu lakini kupitia hizo NGO
 
Mtoa mada ungekua na taarifa sahihi usingeleta 'upuuzi' huu hapa jukwaani.

Nenda katembelee hospitali iliyo karibu na wewe ujionee ni majengo mangapi yamejengwa kwa ufadhili wa hizo NGO.
Leo hii hatugharimii vipimo na matibabu ya kifua kikuu, gharama zote zinabebwa na hao unaowabeza leo.
Kuna mengi yanafanyika kwenye afya na elimu lakini kupitia hizo NGO
Sijawahi ona jengo hata Moja kutoka NGO ndio maana naandika ,Huwa wanajifanya sijui kutoa Elimu eti ya Afya mara ukatili na upuuzi kama huo lakini hakuna vitu tangible vya kuonesha.

Kama wewe unavijua onesha maana nakumbuka hata Mwigulu aliwahi hoji Hilo.Nyie mnaoongea hapa mngejua matrilioni wanayotumia Hawa Jamaa msingeongea utumbo wenu.
 
Nimewahi kuhoji Kwa nini hizi pesa ambazo Hawa wanaojiita asasi zisizo za kiserikali wasiwe wanazitumia ku compliment mipango ya Serikali badala yake nao wanakuwa na mambo Yao ambayo hakuna Tija yeyote inaonekana kwenye jamii.

Kama Hawataki Serikali iwapige marufuku sio lazima wawepo maana Kwa pesa zao kutoratibiwa zinaingia kwenye uchumi kinyemela na pia ndio hutumika kufadhili mambo ya ushoga,utakatishaji pesa,Madawa ya kulevya na kuingiza silaha kienyeji.

Ukisoma Takwimu zake ni pesa zaidi ya Trilioni 3 zinaingia Nchini Kwa njia ya Hawa NGOs lakini hakuna impacts inayoonekana kwenye jamii.

Laiti kama wao wangekuwa Wana compliment mipango ya Serikali tungekuwa mbali ila Hawataki Kwa sababu wanazozijua wao.

Kwa nini Mwendazake alishindwa kuwapiga marufuku Hawa? Wanajifanyaga kutoa Elimu,Elimu ipi ya maana wanatoa?

View: https://twitter.com/MwananchiNews/status/1711266728737456195?t=ACrCggBVl37h6B9Xjv9GTQ&s=19

My Take
Serikali Wasajilini Upya na Kila NGOs ihakikishe Ina complements mipango ya Serikali Kwa Kila Moja na usajili wake vinginevyo wapigwe marufuku hakuna kitu Cha maana wanasaidia jamii.

Nimewahi kuhoji Kwa nini hizi pesa ambazo Hawa wanaojiita asasi zisizo za kiserikali wasiwe wanazitumia ku compliment mipango ya Serikali badala yake nao wanakuwa na mambo Yao ambayo hakuna Tija yeyote inaonekana kwenye jamii.

Kama Hawataki Serikali iwapige marufuku sio lazima wawepo maana Kwa pesa zao kutoratibiwa zinaingia kwenye uchumi kinyemela na pia ndio hutumika kufadhili mambo ya ushoga,utakatishaji pesa,Madawa ya kulevya na kuingiza silaha kienyeji.

Ukisoma Takwimu zake ni pesa zaidi ya Trilioni 3 zinaingia Nchini Kwa njia ya Hawa NGOs lakini hakuna impacts inayoonekana kwenye jamii.

Laiti kama wao wangekuwa Wana compliment mipango ya Serikali tungekuwa mbali ila Hawataki Kwa sababu wanazozijua wao.

Kwa nini Mwendazake alishindwa kuwapiga marufuku Hawa? Wanajifanyaga kutoa Elimu,Elimu ipi ya maana wanatoa?

View: https://twitter.com/MwananchiNews/status/1711266728737456195?t=ACrCggBVl37h6B9Xjv9GTQ&s=19

My Take
Serikali Wasajilini Upya na Kila NGOs ihakikishe Ina complements mipango ya Serikali Kwa Kila Moja na usajili wake vinginevyo wapigwe marufuku hakuna kitu Cha maana wanasaidia jamii.

Tuanzie hapa kwanza:

1. Tuambie kirefu na maana neno NGO.

2. Tuambie majukumu ya hizo NGO kwenye jamii.

3. Je, ni nani anayezisajili hizo NGO.

4. Je, watendaji na wasimamizi wa hizo NGO ni raia au wageni?

5. Je, hela zinazoingia chini kwa ajili ya NGO hizo hupitia benki gani?

6. Je wanufaika na walengwa wa hizo NGO ni watanzania au wageni?
 
Back
Top Bottom