Chadema Wasitumiwe na Wafadhili wa nje

asante michelle, lakini, kwa nini watusaidie? wao wananufaika na nini kutusaidia? halafu kwa nini tusaidiwe? rasilimali zetu hazitoshi kupiga hatua kidogo kidogo kwa uaminifu na dira ya pamoja?

Unajua sioni kama rasilimali za nchi zitagawanywa kwa ajili ya katiba na zaidi kuwapa nguvu CHADEMA ambao umesema wasitumiwe.So,kwa kujua mchakato wa Katiba ni mkubwa na pengine utachukua muda na kuhitaji hela nyingi ndo nikasema kama watajitokeza wenye nia njema na wasio tupa masharti yatakayofanya maslahi ya watanzania yasipewe kipaumbele then tunaweza pokea.....Mchakato uendelee vizuri japokuwa nina amini watanzania watachanga vizuri kama wakihamasika.
 
Unajua sioni kama rasilimali za nchi zitagawanywa kwa ajili ya katiba na zaidi kuwapa nguvu CHADEMA ambao umesema wasitumiwe.So,kwa kujua mchakato wa Katiba ni mkubwa na pengine utachukua muda na kuhitaji hela nyingi ndo nikasema kama watajitokeza wenye nia njema na wasio tupa masharti yatakayofanya maslahi ya watanzania yasipewe kipaumbele then tunaweza pokea.....Mchakato uendelee vizuri japokuwa nina amini watanzania watachanga vizuri kama wakihamasika.

michele, unajua hii nchi kila mtu anataka akifanya jambo lolote alipwe. ukimwita kwenye mkutano kujadili katiba umlipe usafiri, posho, malazi, n.k. na yule atakayetoa mada naye anataka kulipwa kama consultant. ndiyo maana nikasema kama chadema wakitumia utaratibu wa kukuwawezesha wananchi wamiliki ajenda, kwa mfano kama ilivyokuwa mazishi ya arusha, hatuhitaji pesa nyingi. sasasana tutahitaji pesa kidogo kwa ajili ya logistics tu. kisha wahamasishe wananchi wachangie, iliwezekana arusha.

kama ni watu binafsi kutoka nch za nje (phylanthropists) nakubaliana na wewe. mtu binafsi akituwapa chadema pesa halafu akija kuwageuka anataka fadhila fulani ni rahisi ku deal naye. lakini kama ni serikali za nje na mashirika yao ya maendeleo ya kimataifa, bado siamini kwamba watatoa to pesa hivi hivi bila kuwa na malengo fulani. kwa nini watoe pesa?
 
Fedha haramu ni kama za EPA, Sabodo na RA,etc

nafikri umeelewa.
Haramu ni pesa za ccm zilizokuwa zikitumiwa kununulia kofia, maji,nepi za watoto, vitambaa vya kichwani, tshirt, kanga, opener, na ushenzi wote ule, wakati wananchi hawawezi hata kulipa michango ya shule na wengine hawaendi tena hospital badala yake wanawatumia sangoma kufanya operation kwa kukata viungo vya albino.
 
Haramu ni pesa za ccm zilizokuwa zikitumiwa kununulia kofia, maji,nepi za watoto, vitambaa vya kichwani, tshirt, kanga, opener, na ushenzi wote ule, wakati wananchi hawawezi hata kulipa michango ya shule na wengine hawaendi tena hospital badala yake wanawatumia sangoma kufanya operation kwa kukata viungo vya albino.

asante mkuu, hebu tusaidie zaidi. inawezekana katika pesa zilizotumika na ccm kwenye uchaguzi zilikuwepo haramu. lakini unadhani maelezo yako yanatusaidia kujua pesa haramu au matumizi haramu? naomba msaada mkuu
 
Mawazo ya kitumwa yamejaa vichwani mwa jamii kwa kuwaza wafadhili kila mara wanapojadili maendeleo.
Msingi mkuu wa utumwa ni imani iliyojengeka kwa watumwa kwamba hawawezi kufanya chochote bila msaada wa mabwana au watawala wao.
Umasikini wa jamii utaondoka tu pale ambapo mawazo ya utegemezi yataondoka kuanzia kwa mtu mmoja mmoja hadi jamii yote ibadilike, hivyo siyo kutegemea chadema tu.
Jamii ikiwa na mawazo mazuri.then watapatikana viongozi wazuri kwa kuwa viongozi wanatokana na jamii yenyewe.
 
Kama chadema wanapata wafadhili wa nje kuishambulia seriaki sasa kwa nini william ngeleja anashirikiana na wafadhiri wa irani(rostam aziz) kututapeli kupitia richmond/dowans na kagoda
 
Nimefarijika sana ulipoongelea nchi maskini na Misaada!
Africa is making a huuge mistake to depend on external AID! Kuna wakati namkumbuka mkapa. Mkapa kafanya blunder nyingi lakini kwenye jambo moja ninamuunga mkono kwamba, alisisitiza watanzania wafanye kazi kwa bidii badala ya kufikiria misaada at the same time pressurizing big nation to help Afria. Ninamkumbuka alivyomhamasisha yule jamaa aliyeandika "mtaji wa maskini ni nguvu zake"
Misaada ina hasara na matatizo mengi kuliko faidi!!!! moja ambalo ni kubwa saaana misaada inajenga kifra kwa mpokeaji kuwa bila mtoa misaada kuchangia mpokeaji hawezi kufanikisha azma yake. fikiria mfano rahisi wa mafuriko ya kilosa tathmini ilionyesha kunahitajika shilingi bilioni tatu. Mkuu wa maafa akasema anaomba wafadhili wa ndani na nje watoe misaada ilhali kodi ya ndani kwa wakati huo ilikuwa ni shilingi billioni mia nne kwa mwezi. THINK ABOUT THIS IN WIDELY!
 
Mawazo ya kitumwa yamejaa vichwani mwa jamii kwa kuwaza wafadhili kila mara wanapojadili maendeleo.
Msingi mkuu wa utumwa ni imani iliyojengeka kwa watumwa kwamba hawawezi kufanya chochote bila msaada wa mabwana au watawala wao.
Umasikini wa jamii utaondoka tu pale ambapo mawazo ya utegemezi yataondoka kuanzia kwa mtu mmoja mmoja hadi jamii yote ibadilike, hivyo siyo kutegemea chadema tu.
Jamii ikiwa na mawazo mazuri.then watapatikana viongozi wazuri kwa kuwa viongozi wanatokana na jamii yenyewe.

Heshima mbele kabisa mkuu,

nakuunga mkono mkuu, ingawa hapo kwenye rangi nyekundu nitohowe kidogo. Hapa tulipofikia, kwamba kuanzia mkuu wa nchi hadi mfagiaji katika ofisi ya serikali anaabudu mzungu, bila kuja kama ni mfadhili au la, ni hatari kabisa. kwa wale ambao wanatembelea ofisi za serikali, unaweza kuwa unaongea na ofisa fulani wa ngazi ya juu, akiingia mzungu yule afisa anaruka kutoka kwenye kiti chake na kuanza kumtetemekea, anasaha kabisa kwamba kuna binadamu mwingine hapo yaani mwenye nchi. wafagizi watasafisha ofisi vizuri zaidi kama wanajua kuna ugeni, wazungu. wakikusikia unampinga mfadhili kila mtu anakaa kimya na kukukwepa asije akaonekana ana uhusiano na wewe, asijedhaniwa alikutuma.

katika hali kama hii, tunahitaji mfumo wa siasa utakaotukomboa fikra zetu. tunahitaji viongozi wa siasa ambao wataweza kukomboa fikra hizi na kutufanya tuwe na uhuru wa kweli. kama mkuu wa nchi anajipendekeza kwa wazungu/wafadhili kwa kiwango hiki, nidhamu ya uoga itawataka wote walio chini yake kufuata nyayo. ndiyo maana jamaa mmoja hapa kwenye thread hii alimtolea mfano Hugo Chavez.

Lakini pia angalia Vladimin Putin alipoikuta Urusi wakati Gobachevu alikwisha iuza na kuisaliti kwa wamarekani na mahali ilipo sasa. Putin alitumia gesi asilia tu kama fimbo yake. wamarekani na waulaya walipiga kelele sana na kumuita majina yote lakini alisimama imara. Leo hii urusi ambayo ilishafika hatua ya kupokea misaada ya mikate kutoka marekani, sasa inatoa misaada kwa nchi masikini ndani ya kipindi cha miaka takribani kumi tu. Urusi imerudi kwenye heshima yake ya kutingishana na Marekani kuhusu silaha za maangamizi!

Sasa sisi tuna gesi nyingi kuliko ya urusi lakini tunawachekea wawekezaji na wafadhili! tuna madini mengi na ya aina nyingi. tuna mazao ya misitu ambayo wachina karibu wanamaliza kuvuna. tuna miti mingi ambayo inatumika duniani kutengeneza dawa. tuna ardhi haipimiki. sidhani kama naweza kumaliza kuorodhesha rasilimali zetu zote.

Kwa hiyo point yangu mkuu ni kwamba, ili kila mtanzania aweze kubadili fikra na kujitegemea, tunahitaji mfumo wa siasa na viongozi wa siasa wanaotekeleza hilo kwa vitendo. na kuhamasisha wananchi wote kufanya hivyo, kama Chavez na Putin. Bila mfumo wa siasa na viongozi thabiti, ni rahisi wafadhili hao hao kutoa pesa kidogo kwa makundi kadhaa ya kijamii kusingizia demkrasia inakiukwa. ingawa ningependa tuendelee bila kukiuka demokrasia, wapigania demokrasia wengine ni kama kauli ya Kardinali Pengo na Frantz Fanon hapo juu. Na hiyo ndiyo mojawapo ya tahadhari yangu kwa Chadema!
 
Hapa tulipofikia, kwamba kuanzia mkuu wa nchi hadi mfagiaji katika ofisi ya serikali anaabudu mzungu, bila kuja kama ni mfadhili au la, ni hatari kabisa. kwa wale ambao wanatembelea ofisi za serikali, unaweza kuwa unaongea na ofisa fulani wa ngazi ya juu, akiingia mzungu yule afisa anaruka kutoka kwenye kiti chake na kuanza kumtetemekea, anasaha kabisa kwamba kuna binadamu mwingine hapo yaani mwenye nchi. wafagizi watasafisha ofisi vizuri zaidi kama wanajua kuna ugeni, wazungu. wakikusikia unampinga mfadhili kila mtu anakaa kimya na kukukwepa asije akaonekana ana uhusiano na wewe, asijedhaniwa alikutuma.
Dah, kweli tumefika pabaya sana. Inabidi watanzania wote walazimishwe kusoma kitabu cha Paulo Friere "Pedagogy of the Oppressed" ili kujikwamua kutoka kwenye mawazo ya kitumwa.
 
Gurudumu, salaam!

Kwanza nakushukuru kwa hoja yako. Mwanzoni nilishtuka nikidhani unaamini kwamba CDM inatumiwa na wafadhili katika mapambano yake ya kuleta mabadiliko. Baada ya kuisoma nimekuelewa. Umetoa tahadhari.

Najiuliza swali, tunahitaji misaada ili nini? Maendeleo ni nini kwa mtazamo wetu? Tumeshindwa kudefine maendeleo yetu badala yake tunatumia a comparative approach kudefine maendeleo. Tunaangalia maisha ya wazungu tunayatamani na kutaka kuwa kama wao! Tamaa zetu zinatufanya tuwasujudie na kuwaomba misaada ili tuwe kama wao!

Tamaa zetu zinatuponza na kutusabisha kujirahisisha kwao. Ujinga wetu ndio anguko letu!

Miaka 49 bado tunapigana na maradhi, umasikini na ujinga! Miaka 49 kata yangu kina mama wanajifungulia majumbani, watoto wanasomea nje, kipindupindu na kichocho, minyoo ni tatizo! Tunahitaji misaada kupambana na kipindupindu! Tunahitaji misaada kuondoa dampo la taka!

Misaada ikifika tunaitumia vibaya. Tunanua magari ya bei kubwa, tunajenga nyumba za gharama, tunabadili fashion ya kila kitu! Kila toleo jipya la kitu tunataka! Gharama za uendeshaji tunazikuza wenyewe bila sababu za msingi. Mahitaji yetu yanaongezeka wakati uwezo wetu uko palepale!
 
Nimefarijika sana ulipoongelea nchi maskini na Misaada!
Africa is making a huuge mistake to depend on external AID! Kuna wakati namkumbuka mkapa. Mkapa kafanya blunder nyingi lakini kwenye jambo moja ninamuunga mkono kwamba, alisisitiza watanzania wafanye kazi kwa bidii badala ya kufikiria misaada at the same time pressurizing big nation to help Afria. Ninamkumbuka alivyomhamasisha yule jamaa aliyeandika "mtaji wa maskini ni nguvu zake"
Misaada ina hasara na matatizo mengi kuliko faidi!!!! moja ambalo ni kubwa saaana misaada inajenga kifra kwa mpokeaji kuwa bila mtoa misaada kuchangia mpokeaji hawezi kufanikisha azma yake. fikiria mfano rahisi wa mafuriko ya kilosa tathmini ilionyesha kunahitajika shilingi bilioni tatu. Mkuu wa maafa akasema anaomba wafadhili wa ndani na nje watoe misaada ilhali kodi ya ndani kwa wakati huo ilikuwa ni shilingi billioni mia nne kwa mwezi. THINK ABOUT THIS IN WIDELY!

mkuu, katika vichwa vya watz wengi, hakuna maendeleo bila wafadhili na hatuwezi kutatua tatizo lolote bila wafadhili. mfano mmoja ni huo ulioutoa, majanga. lakini angalia fikra zilivyokosa uhuru na kujitegemea. Kuanzia rais had afisa yeyote serikali akiulizwa kwa nini jambo fulani halijafanyika jibu ambalo limerekodiwa vichwani mwao na halibadiliki ni hivi;

serikali haina pesa kutokana na umaskini wetu. serikali yenu ya ccm imejitahidi sana na kufanya mazungumzo na wafadhili kadhaa kuomba watusaidie. raundi ya kwanza ya mazungumzo ilikwenda vizuri na ya pili sasa tuko kwenye raundi ya tatu. tulianza mazungumzo mwaka juzi, kulikuwepo na mambo ambayo hatukuweza kukubaliana mara moja lakini baada ya kuyafanyia kazi sasa tunaelekea kukubaliana. upembuzi yakinifu umekweshafanyika, mchakato wa kumpata mkandarasi umekwisha anza. kabla ya mwisho wa mwaka huu huo mradi unaweza kuanza.

mara ngapi umesikia hadithi kama hii?
 
Gurudumu, salaam!

Kwanza nakushukuru kwa hoja yako. Mwanzoni nilishtuka nikidhani unaamini kwamba CDM inatumiwa na wafadhili katika mapambano yake ya kuleta mabadiliko. Baada ya kuisoma nimekuelewa. Umetoa tahadhari.

Najiuliza swali, tunahitaji misaada ili nini? Maendeleo ni nini kwa mtazamo wetu? Tumeshindwa kudefine maendeleo yetu badala yake tunatumia a comparative approach kudefine maendeleo. Tunaangalia maisha ya wazungu tunayatamani na kutaka kuwa kama wao! Tamaa zetu zinatufanya tuwasujudie na kuwaomba misaada ili tuwe kama wao!

Tamaa zetu zinatuponza na kutusabisha kujirahisisha kwao. Ujinga wetu ndio anguko letu!

Miaka 49 bado tunapigana na maradhi, umasikini na ujinga! Miaka 49 kata yangu kina mama wanajifungulia majumbani, watoto wanasomea nje, kipindupindu na kichocho, minyoo ni tatizo! Tunahitaji misaada kupambana na kipindupindu! Tunahitaji misaada kuondoa dampo la taka!

Misaada ikifika tunaitumia vibaya. Tunanua magari ya bei kubwa, tunajenga nyumba za gharama, tunabadili fashion ya kila kitu! Kila toleo jipya la kitu tunataka! Gharama za uendeshaji tunazikuza wenyewe bila sababu za msingi. Mahitaji yetu yanaongezeka wakati uwezo wetu uko palepale!

mkuu wangu alberto, nimekupat kabisa. una ufahamu wa hii hoja kuliko hata mimi, na mifano yako ni kama umenichoma visu mwili mzima. ndiyo maana nikazungumzia mfumo wa siasa na viongozi wa siasa ambao wanakusudia kutuondoa hapa kwenye hizi fikra. kwangu mimi fikra hizi ndiyo msingi wa kile ambacho watu wanakiita uhuru. kwamba ujiamini, upange mipango yako kutokana na uwezo wako, utumie vile unavyozalisha wewe, usijifananishe na jamii nyingine katika matumizi (wazungu), na tuwe na mipango realistic.

je, kodi tunakusanya? je, kuna mtu alikwisha piga hesabu kwa mwaka tz inapokea msaada kiasi gani na ni kiasi gani cha fedha na rasilimali kinatoka nje ya nchi? je, nini imekuwa mchango wa wasomi wetu kututoa katika utumwa wa mawazo?

mkuu, najaribu kukuunga mkono kwamba umasikini wetu ni wa mawazo tu.
 
Naunga hoja mkono! Oops naunga mkono hoja. Suala la kutegemea wafadhili kwakweli nalipinga,na nitalipinga pale kaburini.

Ivi hao wafadhili wakati walipoanza kuendelea walifadhiliwa na nani? Walikua wanatembeza bakuli kwa nani?

Ukisoma historia ya industrial revolution kwa Amerika na Ulaya,utaona kwamba jamaa walitumia rasilimali zao na zile walizoiba toka Afrika na Amerika ya Kusini kwa maendeleo yao. Walitumia wataalamu wao katika kukabiliana na changamoto ambazo ziliwafanya wawe wadadisi na wagunduzi. Pia walitumia pesa zao kutoka kwenye kilimo kuwekeza katika mabenki na kuweza kupata nafasi ya kukopeshana na kuendesha vyema shughuli za viwanda.

Tanzania yetu tuna rasilimali zote,ila bado tunawaza kupeleka bakuli kuomba. Tunapokabiliwa na changamoto,tunawaza mfadhili gani wa kumtafuta ili atusaidie kutatua changamoto hiyo. Tunakopa benki na kununua magari ya kutembelea!

Kwa namna hii hakika maendeleo kwetu yatakua ndoto!

Nini tufanye: tunahitaji viongozi jasiri wanaoweza kusimama bila ya kua na mawazo ya omba omba. Viongozi wanaoweza kumkoromea na kumpinga Obama,Cameroon,Sarkozy,IMF,WB na mashirika yote ya nje yanayoleta na kushinikiza utekelezaji wa sera zenye mlengo wa kutimiza matakwa yao. Pili tunahitaji raia walio na mitazamo chanya ya kupata maendeleo ya taifa kwanza,jamii na kisha binafsi. Pia raia wajue njia bora za kutumia mikopo ya benki,na si kununua gari ya kutembelea ambayo inakua haizalishi chochote,bali inakula tu. La msingi zaidi ni KATIBA MPYA ambayo itaweka misingi imara ya uongozi bora (na si utawala bora),ushirikishwaji wa wananchi wa kada zote na demokrasia halisi.

Huu ni mtazamo wangu. Kukosolewa kunakaribishwa.
 
Naunga hoja mkono! Oops naunga mkono hoja. Suala la kutegemea wafadhili kwakweli nalipinga,na nitalipinga pale kaburini.

Ivi hao wafadhili wakati walipoanza kuendelea walifadhiliwa na nani? Walikua wanatembeza bakuli kwa nani?

Ukisoma historia ya industrial revolution kwa Amerika na Ulaya,utaona kwamba jamaa walitumia rasilimali zao na zile walizoiba toka Afrika na Amerika ya Kusini kwa maendeleo yao. Walitumia wataalamu wao katika kukabiliana na changamoto ambazo ziliwafanya wawe wadadisi na wagunduzi. Pia walitumia pesa zao kutoka kwenye kilimo kuwekeza katika mabenki na kuweza kupata nafasi ya kukopeshana na kuendesha vyema shughuli za viwanda.

Tanzania yetu tuna rasilimali zote,ila bado tunawaza kupeleka bakuli kuomba. Tunapokabiliwa na changamoto,tunawaza mfadhili gani wa kumtafuta ili atusaidie kutatua changamoto hiyo. Tunakopa benki na kununua magari ya kutembelea!

Kwa namna hii hakika maendeleo kwetu yatakua ndoto!

Nini tufanye: tunahitaji viongozi jasiri wanaoweza kusimama bila ya kua na mawazo ya omba omba. Viongozi wanaoweza kumkoromea na kumpinga Obama,Cameroon,Sarkozy,IMF,WB na mashirika yote ya nje yanayoleta na kushinikiza utekelezaji wa sera zenye mlengo wa kutimiza matakwa yao. Pili tunahitaji raia walio na mitazamo chanya ya kupata maendeleo ya taifa kwanza,jamii na kisha binafsi. Pia raia wajue njia bora za kutumia mikopo ya benki,na si kununua gari ya kutembelea ambayo inakua haizalishi chochote,bali inakula tu. La msingi zaidi ni KATIBA MPYA ambayo itaweka misingi imara ya uongozi bora (na si utawala bora),ushirikishwaji wa wananchi wa kada zote na demokrasia halisi.

Huu ni mtazamo wangu. Kukosolewa kunakaribishwa.

Siamini kama utakosolewa ila sitashangaa kama atatokea mtu akukosoe. Nimefika mahali sishangai matendo ya baadhi ya watu nchini kwetu!

Umeongea vizuri sana. Tuungane tupiganie haki na kweli
 
Naunga hoja mkono! Oops naunga mkono hoja.


Nini tufanye: Pia raia wajue njia bora za kutumia mikopo ya benki,na si kununua gari ya kutembelea ambayo inakua haizalishi chochote,bali inakula tu.
Huu ni mtazamo wangu. Kukosolewa kunakaribishwa.

mkuu naunga mkono yote uliyoyasema. hata hivyo niruhusu nikokotoe hiyo red hapo juu. nimekua najirudia sana kwenye hii thread kwamba tunahitaji mfumo wa siasa na viongozi wa siasa watakaoweza kututoa katika huu utumwa wa fikra tulimo. nimetoa mifano ya Putin, Chavez, Kagame, na Botswana.

Binafsi siwezi kwa sasa kuwalaumu wananchi wanaochukua mikopo benki kujinunulia magari ambayo hayazalishi. tatizo liko kwenye mfumo wa siasa na viongozi wa siasa. sera za ccm zimezungumzia kuboresha miundombinu ya DSM ili kupunguza foleni, lakini hazijawahi kutekelezwa na pale zikitekelezwa kidogo ni kwa sababu kuna ufisadi. magari mengi yaliyoko barabarani hapa DSM ni ya mkopo.

kwa nini? kwa sababu public transport has failed them. kama kila raia DSM angetoka nyumbani kwake akafika kituo cha basi au treni na kukuta usafiri wa uhakika na wa heshima hakuna mtu angenunua gari binafsi. ni kutokana na ugumu wa public transport ndipo kila mtu anataka awe na gari. na kwa kuwa mishahara ni midogo (na kodi kubwa) watu wanalazimika kukopa.

wale watu binafsi wanaonunua magari ya kifahari ya bei mbaya pia wanatekeleza utashi wa serikali. unakumbuka mwaka jana ikulu iliamua kwamba siyo heshima rais kutembelea Benz hivyo wakanunua utitiri wa BMW? umemsoma MsandoAlberto hapo juu kwamba serikali inaomba msaada kununua magari ya kifahari? Pia ameuliza maendeleo ni nini?

Kwa hiyo mfumo wetu wa siasa na serikali yetu vimetufanya tudhani kwamba kufanya matumizi ya kifahari ni kuendelea. na wakati tunafanya hivyo, hakuna dawa hospitali, hakuna walimu na vifaa mashuleni, na wanafunzi wa vyuo vikuu wanagoma kwa kukosa huduma.

Mkuu naunga hoja yako yote mkono ila ninajaribu kusema msingi wa uhuru wa fikra ni katika mifumo ya siasa zetu na uongozi wa nchi yetu. tukianza hapo kila mtu ataingia kwenye mstari tu, na maendeleo tutayapata kufumba na kufumbua!
 
Gurudumu, fikra! Ukombozi wa fikra. Jaribu kujiuliza mtanzania wa kawaida anafikiria nini kuanzia anapoamka mpaka anapolala? Fikra hizo zinamsaidiaje kimaendeleo? Anajua maendeleo yake binafsi ni nini? Kwa mfano, wengi wa graduates ukiwauliza wanataka nini jibu ni 'gari zuri, nyumba na kazi nzuri'. Kabla sijaendelea, ni nini mawazo yako kwa jibu hilo la msomi?
 
Gurudumu, fikra! Ukombozi wa fikra. Jaribu kujiuliza mtanzania wa kawaida anafikiria nini kuanzia anapoamka mpaka anapolala? Fikra hizo zinamsaidiaje kimaendeleo? Anajua maendeleo yake binafsi ni nini? Kwa mfano, wengi wa graduates ukiwauliza wanataka nini jibu ni 'gari zuri, nyumba na kazi nzuri'. Kabla sijaendelea, ni nini mawazo yako kwa jibu hilo la msomi?

of course ni hatari, lakini hebu nisaidie mawazo yako mkuu. pia uwahusishe na wahadhiri katika mawazo yako please. nakumbuka nilipokuwa undergraduate mhadhiri mmoja siku moja aliingia lecture room na mkoba umejaa fedha akatuonesha kisha akasema yeye siyo masikini kama hao wahadhiri wengine uchwara!!!!!!!!!!

shusha mawazo mkuu
 
Ni hatari kweli kweli. Hatufikirii mbali zaidi ya hayo. Badala yake tunatafuta njia za mkato kupata hayo tunayoyataka....rushwa, ujambazi, wizi, kujiuza (kwa baadhi ya kina dada) n.k. Kwa wanaofanikiwa kupata wanataka zaidi na zaidi. Tunakusanya mali kwa ajili ya watoto wetu. Badala ya kubuni biashara ambazo watoto wetu wataziendeleza na zitatoa ajira kwa wenzetu tunafikiria kununua majumba ya kifahari ili tuwarithishe watoto wetu. The circle remains!! Wasomi wetu wanajisifia kusoma na kuelezea waliyoandika wenzao! Hawana jipya! Ni lini umesikia msomi wa Tanzania anayefundisha UDSM sociology ameongeza kitu kwenye hiyo course? Ni wachache sana kama wapo!

Haturidhiki na maisha yetu, kama ni nyumba tunataka iwe na swimming pool na marumaru wakati wazazi wetu wanaishi kwenye mbavu za mbwa! Kama ni usafiri raisi awe na ndege yake ya kisasa. Kama ni radar tununue hata kama hakuna tishio lolote la usalama wetu! Kama ni magari tununue VX V8 hata kama ya zamani bado yanafaa kutumika!

Hatuna priority. Nini kianze katika maisha yetu ni kitendawili kisichoweza kuteguliwa na viongozi wetu. Tunataka kufanya kila kitu!! Elimu, Afya, Kilimo, Maji, Barabara, Umeme nk. Ndio maana tunabaki kuahidi kila kitu! Hatuna tunachofanikiwa! Hatuwezi kufanikiwa! Kutokana na kutaka kila kitu basi tunajiuza kwa wafadhili sijui wahisani! Wanatumia tamaa zetu na fikra zetu mbovu na mgando kutunyonya!! Sasa kama hatujui uwezo wetu na kuishi ndani ya uwezo wetu wataachaje kutulala? Nisamehe kwa matumizi ya neno hilo imenibidi kutumia kwa sababu ndicho wanachotufanya!!

Tufike mahali tuamue, nini tunachotaka? Kipi kianze? Tusipoamua hatutafanikiwa kamwe! Hatuwezi kutaka kila kitu, hatuwezi kuanza na kila kitu!
 
Back
Top Bottom