Hivi unakumbuka ni lini CDM au vyama vya upinzani walianza kuwapigia kelele watanzania kuhusu wizi/ujambazi unaofanywa na viongozi wa chama tawala lakini watanzania hawakutaka kuelewa au kwa namna moja au nyingine walibezwa na kupanindikiziwa chuki za uongo? Lakini leo hii watanzania wameweza kujionea wenyewe na kukubali japo si saaana lakini angalau wamezinduka. Taratibu, saizi safari ndiyo imekolea na siraha hazijaanikwa zote kwani zinazotumika bado zinawakimbiza CCM vibaya sana. Tusubiri muda utafika utasikia mengi mbadala!!
mkubwa!....@Nakapaya wewe ni Gamba, na naweza kukuita mnafiki kwakua unamapenzi na CCM lakini unaogopa umma usikujue kama wewe ni mpenzi wa CCM.Wapo wapenzi wa magamba tumewaona na wapo wazi kihoja,hata wanatamka ka kabisa nazadhani unawafahamu sina sababu ya kuwataja.Toka jana unatapatapa na post kibao za CHADEMA,umebaki kuhaha tu huna hoja
Awali ya yote naomba niseme namshukuru mungu muweza wa yote kwa kutuwezesha kuwepo tena kwa siku ya leo,poleni wagonjwa na poleni wote mliopoteza watu wenu wa karibu,amani iwe kwenu wote wenye shida mbalimbali,mtegemee mungu na mtayashinda yote,Amen.
Nirudi kwenye mada yangu;kwanza niseme mimi si mshabiki,mnazi,mkereketwa,mwanachama,au kada wa chama chochote kile cha siasa.Ndugu zangu wa CHADEMA naomba niwaambie kitu;hakuna mtu au kundi la watu lisilo na makosa au kasoro,unapokuwa na makosa au kasoro jiua wazi kuwa utakosolewa na kukosolewa ndio mwanzo wa kujirekebisha na kujijenga upya kwa ufanisi zaidi,cha ajabu ndugu zetu nyie hampendi kukosolewa kama vile nyie ni malaika na hamfanyi makosa,mnakosea sana.Ikitokea mtu akaikosoa CHADEMA ujue atashambuliwa kwa kila aina ya kejeli,matusi na lugha zote mbovu.
Wao wanaona kauli zote na mabo yafanywayo na viongozi wao na wanchama ni sahihi na hayahitaji kukosolewa ila akisema wa CCM yote huwa ni mabaya na ni pumba tupu,tunakosea hatuendi hvyo kubalini kukosolewa ndipo mtafika mbali.Au mnataka kuwa kama mfalme Juha?ni hayo tuu.GOD'S GREAT ALL THE TIME.
kama sina hoja nipe basi ya kwako.
mkubwa!.....usiwahadae watu kuwa huna chama,wewe ni mwana-CCM,jiweke wazi ili upambane na hoja zinazo ikabili chama chako.unaogopa nini?au huamini kile unachokisimamia/kukitumikia?content za post zako zote zipo wazi