Chadema na Mwenendo Wa Wapiga Kura Tanzania

Tanzania hakichaguliwi chama anachaguliwa kiongozi. Mifano ni mingi tu, haina haja ya kuirudia.

Chadema haitoweza kushinda uchaguzi wa Urais nchi hii ikimsimamisha Slaa au Mbowe.

Au umchukuwe Slaa akagombee ubunge Uzini si itakuwa kiroja.
 
Tanzania hakichaguliwi chama anachaguliwa kiongozi. Mifano ni mingi tu, haina haja ya kuirudia.

Nadhani maana yako ni kwamba hakichaguliwi chama bali MGOMBEA, kwani ni wanasiasa wachache sana ndani ya CCM kwa mfano wenye sifa za kuitwa viongozi, ndio maana hata vijiweni tunaitana 'vipi kiongozi', kwani dhana ya uongozi ndani ya CCM baada ya kuondoka Mwalimu and to an extent Mkapa ni vituko kuliko mantiki. Vile vile hoja yako hii inatoa ishara kwamba nguvu ya CCM sio itikadi au sera bali viongozi waliopo na jinsi gani wanatumia mamlaka ya uongozi na taasisi zake kukifanya CCM kiwe na nguvu;

Chadema haitoweza kushinda uchaguzi wa Urais nchi hii ikimsimamisha Slaa au Mbowe

Kauli hii kidogo ina utata kwani haujaifafanua kama una maanisha ushindi wa kwenye sanduku la kura au ushindi wa mezani, au iwapo Slaa na Mbowe hawana mvuto kwa wananchi au iwapo Chama tawala hakipo tayari kuona hawa wawili wakishika madaraka ya nchi; yote haya yanajadilika, ila ukiwa wazi zaidi;

Au umchukuwe Slaa akagombee ubunge Uzini si itakuwa kiroja

Hii hoja sijaelewa maintiki yake ni nini hasa, je inahusiana na mjadala wetu kuhusu LOCALISM? Vinginevyo hata Lowassa, Pinda, Membe, Mwandosya, Migiro, wote hawa hawezi kushinda ubunge jimbo la Uzini;
 
Nadhani maana yako ni kwamba hakichaguliwi chama bali MGOMBEA, kwani ni wanasiasa wachache sana ndani ya CCM kwa mfano wenye sifa za kuitwa viongozi, ndio maana hata vijiweni tunaitana 'vipi kiongozi', kwani dhana ya uongozi ndani ya CCM baada ya kuondoka Mwalimu and to an extent Mkapa ni vituko kuliko mantiki. Vile vile hoja yako hii inatoa ishara kwamba nguvu ya CCM sio itikadi au sera bali viongozi waliopo na jinsi gani wanatumia mamlaka ya uongozi na taasisi zake kukifanya CCM kiwe na nguvu;



Kauli hii kidogo ina utata kwani haujaifafanua kama una maanisha ushindi wa kwenye sanduku la kura au ushindi wa mezani, au iwapo Slaa na Mbowe hawana mvuto kwa wananchi au iwapo Chama tawala hakipo tayari kuona hawa wawili wakishika madaraka ya nchi; yote haya yanajadilika, ila ukiwa wazi zaidi;



Hii hoja sijaelewa maintiki yake ni nini hasa, je inahusiana na mjadala wetu kuhusu LOCALISM? Vinginevyo hata Lowassa, Pinda, Membe, Mwandosya, Migiro, wote hawa hawezi kushinda ubunge jimbo la Uzini;

Tanzania hachaguliwi mgombea kwa kuwa ni mgombea tu, watu huchakuwa kiongozi wao. Kama unachaguliwa mgombea kama unavyotaka iwe, kwanini asichaguliwe Slaa kuwa Rais? si na yeye alikuwa Mgombea? au kwanini asichaguliwe Mbowe uchaguzi wa 2005? nae si alikuwa mgombea? Naam, Watanzania wengi hawakusita kumchaguwa kingozi wao waliyejuwa atawaletea mabadiliko ya ukweli nae anafanya kweli. Jakaya Mrisho Kikwete, kiongozi wa kutukuka.

Ushindi wa Kwenye sanduku la kura na ushindi wa mezani ndio nini? Mimi naelewa watu wanapiga kura zinahesabiwa anatangazwa mshindi. Sanduku la plastic linatumika kubebea kura, meza zinatumika kura zinapohesabiwa.


Hapana, siongolei "localism" naongelea kiongozi ambae wataona anafaa wapiga kura wa Uzini hususan kwa maadili. Ndiyo maana nikasema ukimpeleka Slaa kugombea "Uzini" kitakuwa ni "kiroja". Kitongoji cha "Uzini" nimekichaguwa kwa maana yake na ndio maana sikusema Micheweni au Kwa Mtipura, na hakihusiani na hayo majina mengine yote uliyoyaweka.
 
Hoja zako ni nzuri sana Mchambuzi. Kama ulivyoainisha kuwa iwe mahali pa CDM kujipanga wakati wa kuelekea 2015, ni vyema pia tukatafakari kwa kina yaliyotokea kwenye uchaguzi uliopita.

Hivi leo tukijiuliza, ilikuwa je, Maalim Seif S Hamadi ashindwe kura za Urais Visiwani, na wakati huo huo Prof Lipumba amshinde JK kwenye kura za Urais za Visiwani?

Kila ninapo tafakari hili, linaniondolea uwanja tambarare wa kusema kweli hizi margins za ushindi wa JK dhidi ya Slaa zilikuwa sahihi. Je, Kweli Lipumba alikuwa Maarufu kuliko JK visiwani na wakati huo huo Shein akawa Maarufu kuliko Hamadi visiwani?
Lkn kama ulivyosema, kwa kuwa hakuna data inakuwa vigumu kuyafanyia kazi. Hii inanikumbusha pale Mzee wa Mapesa alipokosa hata kura za familia yake ya karibu sana (mkewe na wanawe) katika kituo chao cha nyumbani!

Observation yako inapingana na matokeo sana, tofauti na conclusion yako.Yaani zinaonyesha zaidi jinsi matokeo hayana uhalisia katika fikra za watu wengi.

Hayo maswali yako yanonyesha jinsi ndoa ya CUF na CCM ilivyokuwa na madhara makubwa Zanzibar, na bara isngewezekana kwani CDM waliweka mashinikizo na hapakuwa na nafasi ya kusort out things in a hurry.Na kama CDM wangekuwa vyema kule basi hata sura ingebadilika na tungekuwa tunaangalia factor nyingine kuangalia data.



Alichoweka Mchambuzi na analysis yake yenye weledi mkubwa kinathibitisha kuwa dat hazina usahihi.bahati mbaya sana nadharia mbili zipo tofauti sana na statistics alizoweka.
 
Tanzania hachaguliwi mgombea kwa kuwa ni mgombea tu, watu huchakuwa kiongozi wao. Kama unachaguliwa mgombea kama unavyotaka iwe, kwanini asichaguliwe Slaa kuwa Rais? si na yeye alikuwa Mgombea? au kwanini asichaguliwe Mbowe uchaguzi wa 2005? nae si alikuwa mgombea? Naam, Watanzania wengi hawakusita kumchaguwa kingozi wao waliyejuwa atawaletea mabadiliko ya ukweli nae anafanya kweli. Jakaya Mrisho Kikwete, kiongozi wa kutukuka.
Kutukuka synonym yake ni tukufu; sio sahihi kusema Kikwete ni mtukufu, kwanini unaenda mbali hivyo, au kwa sababu ni rais wa sasa? na atakaekuja 2015 akiwa wa CCM atakuwa mtukufu pia au sio? Na Kikwete ataendelea kuwa mtukufu au utukufu wake utaisha na urais wake? nielewavyo mimi utukufu hauna kikomo, kwahiyo ni vyema ukatafuta namna nyingine ya kumuelezea Rais kikwete, kwani nina uhakika hata yeye neno mtukufu asingelipenda;

Kuhusu Kikwete kuwa kiongozi wa kweli kwa mtazamo wa wananchi, hilo kwa kweli sifahamu; nachofahamu ni kwamba nikiwa kama mwana CCM 2005 tuliweza kupata 80% ya kura, lakini five years later tukapata about 61% ya kura; kama tuna nia ya dhati ya kujenga chama chetu cha CCM ni muhimu tuache ushabiki wa kutukuka na kufanyia kazi takwimu hizi ili tujue tulikosea wapi, na turekebishe maeneo gani katika kipindi hiki kilichosalia cha miaka mitatu;

Ushindi wa Kwenye sanduku la kura na ushindi wa mezani ndio nini? Mimi naelewa watu wanapiga kura zinahesabiwa anatangazwa mshindi. Sanduku la plastic linatumika kubebea kura, meza zinatumika kura zinapohesabiwa.

I raised hizi issues kutokana na hoja yako kuwa ya kuchanganya kidogo i.e. kuhusu Dr. Slaa na Mbowe hawawezi kushinda; haikuwa na ufafanuzi na bado haina ufafanuzi; vinginevyo kushiriki katika GAME kwa attitude kwamba fulani hawezi kushinda ni strategy mbaya sana; the right strategy ni kuchukulia kwamba hapa ushindi ni 50/50, hii itakusaidia kujipanga badala ya kuhamaki na pengine kuleta madhara pale utakaposhindwa.

Hapana, siongolei "localism" naongelea kiongozi ambae wataona anafaa wapiga kura wa Uzini hususan kwa maadili. Ndiyo maana nikasema ukimpeleka Slaa kugombea "Uzini" kitakuwa ni "kiroja". Kitongoji cha "Uzini" nimekichaguwa kwa maana yake na ndio maana sikusema Micheweni au Kwa Mtipura, na hakihusiani na hayo majina mengine yote uliyoyaweka.
Maana ya neno kiroja ni kitu kinachozaa hisia za mshangao; sasa cha kushangaza Slaa akishinda huko ni nini, kwamba yeye ni mkristo? Mbara? hoja yako hii inaelekea kwenye mjadala usiokuwa na tija;
 
Kutukuka synonym yake ni tukufu; sio sahihi kusema Kikwete ni mtukufu, kwanini unaenda mbali hivyo, au kwa sababu ni rais wa sasa? na atakaekuja 2015 akiwa wa CCM atakuwa mtukufu pia au sio? Na Kikwete ataendelea kuwa mtukufu au utukufu wake utaisha na urais wake? nielewavyo mimi utukufu hauna kikomo, kwahiyo ni vyema ukatafuta namna nyingine ya kumuelezea Rais kikwete, kwani nina uhakika hata yeye neno mtukufu asingelipenda;

Kuhusu Kikwete kuwa kiongozi wa kweli kwa mtazamo wa wananchi, hilo kwa kweli sifahamu; nachofahamu ni kwamba nikiwa kama mwana CCM 2005 tuliweza kupata 80% ya kura, lakini five years later tukapata about 61% ya kura; kama tuna nia ya dhati ya kujenga chama chetu cha CCM ni muhimu tuache ushabiki wa kutukuka na kufanyia kazi takwimu hizi ili tujue tulikosea wapi, na turekebishe maeneo gani katika kipindi hiki kilichosalia cha miaka mitatu;



I raised hizi issues kutokana na hoja yako kuwa ya kuchanganya kidogo i.e. kuhusu Dr. Slaa na Mbowe hawawezi kushinda; haikuwa na ufafanuzi na bado haina ufafanuzi; vinginevyo kushiriki katika GAME kwa attitude kwamba fulani hawezi kushinda ni strategy mbaya sana; the right strategy ni kuchukulia kwamba hapa ushindi ni 50/50, hii itakusaidia kujipanga badala ya kuhamaki na pengine kuleta madhara pale utakaposhindwa.


Maana ya neno kiroja ni kitu kinachozaa hisia za mshangao; sasa cha kushangaza Slaa akishinda huko ni nini, kwamba yeye ni mkristo? Mbara? hoja yako hii inaelekea kwenye mjadala usiokuwa na tija;

Kikwete ni kiongozi aliyetukuka, ukipenda meza hukupenda tema. Jee, kuna tatizo Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ni Mtukufu? Huujuwi Utukufu wa kuwa Rais ndiyo maana unapata shida na hilo neno.

Slaa na Mbowe wameshabwagwa vibaya sana na Kikwete, kila mmoja kwa wakati wake, na hao si "Chaguo la Mungu". Watakuwa na ubavu wa kupambana na Lowassa? Maaweee!

Slaa na Uzini ni kiroja, la hasha si kwa dini zao, hukusoma neno "maadili" katika post ile? usitake niseme kuwa una macho lakini hayaoni.
 
Kikwete ni kiongozi aliyetukuka, ukipenda meza hukupenda tema. Jee, kuna tatizo Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ni Mtukufu? Huujuwi Utukufu wa kuwa Rais ndiyo maana unapata shida na hilo neno.

Slaa na Mbowe wameshabwagwa vibaya sana na Kikwete, kila mmoja kwa wakati wake, na hao si "Chaguo la Mungu".

Slaa na Uzini ni kiroja, la hasha si kwa dini zao, hukusoma neno "maadili" katika post ile? usitake niseme kuwa una macho lakini hayaoni.

Mna nafasi nzuri huko CCM za kuleta mabadiliko ili na sisi tuwe na ushindani thabiti dhidi ya upinzani lakini mnadhania mnayoyafanya ni mnakijenga chama kumbe mnakibomoa. Mkija shtuka, hasa uhalisia wa mambo utakapo kick in, tayari itakuwa ni too too late; Sisi vijiweni huku tunaendelea kukipigania chama kwa mwendo mdogo mdogo na tunafanikiwa kujijengea heshima, huku pia tukikilinda chama katika vicinity zetu, na for some reasons, hao hao mnaowatukana wanatuheshimu, wapo tayari kujenga taifa kwenye maeneo yaliyo over and above siasa za vyama kwa kushirikiana na sisi ingawa tupo vyama tofauti kwani wanatutofautisha sana na wengi ya waliopo jikoni;

Ingekuwa busara sana kama mngeweka sura zenu na majina yenu mjulikane kuliko kujificha na majina na picha za uongo; vinginevyo kila la kheri huko jikoni mkuu;
 
Mchambuzi,
Mkuu wangu samahani kidogo sikupata kukuelewa vizuri... Ulipotoa mifano ya jimbo la Zitto, Mbowe na Dr.Slaa (as the big three) Kisha kuonyesha ushindi wa wabunge hao lakini sio Dr. Slaa ktk kiti Urais inanipa taabu kidogo zinapokutana.. Je, una maana kwamba Chadema hawana mtu zaidi ya Dr.Slaa (kama madai ya Sitta) aliyeshindwa na JK ,au Dr.Slaa hakufaa angekuwa mtu mwingine pengine Chadema wangeshinda ktk majimbo hayo kutokana na kwamba wabunge wake walishinda au JK ni zaidi ya Dr.Slaa...

Mimi binafsi napata shida sana kuamini Popular vote vinavyotumika hasa pale wananchi walipoichagua Chadema kutokana na msukumo wao ktk mageuzi ilihali wakijua kwamba kwa kuichagua Chadema serikali ya CCM itakwaza maendeleo yao kama walivyokuwa wakijitangaza ktk ilani zao za Uchaguzi.. CCM walisema wazi mkiwachagua Chadema mtakosa maendeleo na bado watu hawa wakamchagua mbunge mgombea wa Chadema, sasa nashindwa kabisa kuunganisha wala kuelewa mtu alomchagua Mbunge wa Chadema lakini akamchagua rais kutoka CCM akijua hatapata maendeleo au labda walidhani JK na CCM ni vitu viwili tofauti?...hii kidogo inanipa shida kuelewa japokuwa sipo vichwani mwa hawa wananchi ambao ndio tunataka kuwalaumu na sio chombo kinachohusika na uchaguzi..

Nafikiri yaliyotokea mwaka 2010 hayawezi kuwa na majibu sahihi hasa baada ya kulazimishwa kukubali matokeo. Kama tulivyolazimishwa kuamini mkataba wa Richmond na Dowans haukuwa na matatizo au swala la rada..Na binafsi yangu nisingependa hata kuwazia kilitokea nini maana NDIVYO TULIVYO...
 
Kuhusu swali lako la kwanza, uchaguzi huru ukija leo, bado CCM itashinda kwa sababu, again and again huwa nasisitiza umuhimu wa Chadema kulitazama upya suala la kanuni ya uchaguzi kwamba mshindi ni mshindi; kwani kwa jinsi hali ilivyo leo, CCM (Kikwete) akishinda tena leo kwa 50.9% na Chadema (Dr. Slaa) kwa 49.1%, kwa kanuni ya mshindi ni mshindi, CCM itaibuka kidedea tena; ushindi wa Chadema sana sana utakuwa uundwaji wa serikali ya pamoja kwama ile ya CUF na CCM Zanzibar; ;
Kabla sijaendelea na mchango wangu mdogo kuhusu hii mada, nimekutana na hii na nimeona bora niiseme kwa mujibu wa ufahamu wangu au nielezwe kaam sivyo ilivyo.

Katika mfumo wa sasa wa ushindi katika chaguzi zetu (jambo ambalo ni hatari na nimeshalitolea maoni kwenye mchakato wa Katiba Mpya) ni kuwa mshindi hahitajiki kupata asilimia 50+1 ili awe mshindi, bali awe amewashinda wapinzani wake kwa asilimia yoyote.

Hii ni kusema kuwa ikiwa vyama vinne tu vimeshindana, yule anayepata asilimia 26 ndiye anakuwa mshindi na nadhani hakuna ruhusu ya hivi vyama vitatu au viwili kuungana baada ya uchaguzi ili kupata asilimia 27 za kunyang'anya ushindi yule aliyepata asilimia 26. Hatari ya mfumo huu, na kutokana na utitiri wa vyama uliopo sasa, kuna uwezekano wa siku moja kuja kuongozwa na raisi na pengine mbunge, aliyepata asilimia 11 kwa kuwa tu kavishinda vyama tisa.

Ushindi wa Kwenye sanduku la kura na ushindi wa mezani ndio nini? Mimi naelewa watu wanapiga kura zinahesabiwa anatangazwa mshindi. Sanduku la plastic linatumika kubebea kura, meza zinatumika kura zinapohesabiwa.

Hapa nikusaidie jawabu kutoka kwa zomba ambapo alishakata maamuzi hapo kwenye red chini, anagalia hoaja yake asilia hapa: #121. Maneno, mawazo na nia hii ya zomba ni kama mwangi tu wa hisia zilizojengeka ndani ya CCM, bara na visiwani kuwa katu wapinzani hawatawala nchi hii, kwa kura.
Hu mfumo unaendeshwa na katiba na sasa hivi kuna mchakato wa kubadili katiba. Usijidanganye kuwa kubadili chama ndio mwisho wa matatizo. Vyama vipya na hususan chama chenye mfumo kama wa chadema havifai kabisa, unaona wazi kabisa kuwa viongozi wa chadema hata maadili hawana, halafu unategemea lipi jema kutoka kwao?

Unaona kabisa jinsi wanavyoongea, wanavyosambaza chuki mpaka wanafikia kusema wazi kabisa kuwa hii nchi "haitatawalika" halafu bado unafikiri kuwa wao watakuwa bora? huo ni ufinyu wa mawazo. Nyota njema huonekana alfajiri. Chadema hawana madaraka ya nchi tunaona damu zikimwagika kila wanapopita wakishika madaraka jee?

Kwanza wasahau kupewa madaraka kwa kura, za nani? msidanganyike.


Tukija kwenye mada, siku ya mwanzo ya mjadala huu nilianza kwa kugusia suala la uchakachuaji wa matokeo, lakini ukashauri hilo tuliwache tujadili data zilizopo kwani ndizo zilizopo rasmi na sio suala kujadili uhalali wa data zenyewe.

Tunaweza kujadili masuala uliyotaja na yakasaidia kwenye nadharia kuvitafakarisha vyama vya siasa, na kwa ajili ya mjadala huu, vyama vya upinzani na hasa Chadema, lakini bado ikiwa siku ya siku ikifika, huku ikiwa CDM imejisahihisha makosa na kuchukua mikakati mipya, lakini ikiwa bado uchakachuaji umefanyika, itabidi mwaka 2016, 2021, 2026... turejee mada hii bila ya kupata suluhisho kwa vile bado hatuna demokrasia ya kweli.

Nikiachana na hilo, nikiri kama ulivyogusia kuwa Watanzania huwa tunachagua vyama na watu na wala sio masuala na sera. Na hili haliko CCM tu ambako tayari limekuwa sugu, lakini pia limeanza kupandikizwa CDM kiasi kwamba kuna kauli kuwa kwenye eneo fulani, kwa sababu ni ngome imara ya CDM, hata wakiweka jiwe litashinda. Kwa hivyo akitokea mwengine na sera, hata kama ni madhubuti na zinatekelezeka kiasi gani, litakaloshinda ni jiwe la CDM na kwengine litashinda kumbi la CCM. Hii inasikitisha, lakini ndio hali halisi.

Jengine ambalo ni adui wa demokrasia na maendeleo ya nchi hii (kama ulivyosema hapo juu) ni kuwa watu wanatumia vigezo vya UTASHI/HAIBA YA WAGOMBEA, Mazoea,Ukabila, Udini, Ubaguzi wa Jinsia n.k. Haya ni mambo yapo, tutake tusitake, ukiachia exceptions chache. Hata kama sheria ya uchaguzi inalikemea hilo na wanaobainika kuyatumia huadhibiwa wakigundulika, lakini wengine husalimika huku ikiwa ni wazi walifanya kampeni chafu za udini, ukabila, ukanda na jinsia.

Mimi kwa mawazo yangu, tunapaswa kufanya mambo mawili ili kuepukana na matatizo yote haya: a) kutoa elimu ya uraia kwa Watanzani na b) kuwa na tume huru ya uchaguzi.

Hilo la mwanzo nilishalitoa kama ushauri kwa CDM na upinzani kwa jumla, liwe kipaumbele chao cha kwanza. Vyama visikae kusubiri ruzuku ya wafadhili na serikali kufanyakazi hiyo kwani huwa haifanyiki zaidi ya "mchanganuo wa maandishi kuwa fedha fulani imetumika kwa elimu ya uraia" wakati ukweli imetumika kwa kujengea nyumba, hoteli, kusomesha watoto wa vigogo. Kwa serikali au CCM, kadiri wananchi wanavyokosa elimu ya uraia, ndio maslahi kwake.

Kukosekana kwa elimu ya uraia ndiko kunakowafanya wapiga kura wetu tuliowategemea kwa kuona wanajaza viwanja vya mikutano wakati wa kampeni na uhamasishji, lakini siku ya siku hughilibiwa na "kitu kidogo" a.k.a takrima".

Pamoja na elimu ya uraia, ni tume huru ya uchaguzi. Bila ya hii, tutaendelea kupigizana kelele, lakini ikifika wakati wa uchaguzi kunaibuka utata katika kila kitu na kufikia hatua ya kukimbilia sheria huku tukijua kuwa mara nyengine, sheria inakuwa adui wa haki.
 
Hongera sana kaka umechambua vizuri sana juu ya hilo na pia ingefaa kutoa ushauri juu gani ya kuona mambo ya msingi sana kama haya yanakuwa kwenye platform moja kipindi cha uchaguzi hivyo ukija kutazama vizuri utaona kuwa Chadema watashinda kwa kiasi kikubwa sana mwaka 2015
 
Mchambuzi,

..JK tayari alikuwa Raisi, kwa hiyo ni vigumu mgombea kama Slaa, out of nowhere, kuweza kumpiku.

..kitu kingine kilichomsaidia JK ni MTANDAO mkubwa wa CCM uliopo vijijini, rasilimali watu[watumishi wa serikali, polisi, wasanii, jumuiya za chama, waandishi wa habari] pamoja na FEDHA nyingi zilizotumika wakati wa kampeni.

..pia sina uhakika kama timu ya kampeni ya CDM ilikuwa inaielewa vizuri saikolojia ya wapiga kura. kwa mtizamo wangu, wapiga kura wa Tanzania, kutokana na umasikini wao, wana-respond vizuri zaidi kwa mgombe mwenye kutoa ahadi lukuki aliyokuwa akifanya JK. naamini kulikuwa na kiasi fulani cha mapungufu ktk campaign message ya CDM as it relates to uelewa na matamanio ya wa-Tanzania.

..mwisho, naomba nieleze kwamba CDM had a better candidate compared to CCM. Hata CUF walikuwa na mgombe mweledi zaidi kulinganisha na yule wa CCM. Hicho ndicho kilichopelekea CCM kukwepa kushiriki kwenye mdahalo wa wagombea Uraisi. In the future, CDM waangalie their campaign message, pia wahakikishe wana mtandao mkubwa, na zaidi wawe na fedha na vitendea kazi kwa ajili ya kampeni.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi,
Mkuu wangu samahani kidogo sikupata kukuelewa vizuri... Ulipotoa mifano ya jimbo la Zitto, Mbowe na Dr.Slaa (as the big three) Kisha kuonyesha ushindi wa wabunge hao lakini sio Dr. Slaa ktk kiti Urais inanipa taabu kidogo zinapokutana.. Je, una maana kwamba Chadema hawana mtu zaidi ya Dr.Slaa (kama madai ya Sitta) aliyeshindwa na JK ,au Dr.Slaa hakufaa angekuwa mtu mwingine pengine Chadema wangeshinda ktk majimbo hayo kutokana na kwamba wabunge wake walishinda au JK ni zaidi ya Dr.Slaa...

Mimi binafsi napata shida sana kuamini Popular vote vinavyotumika hasa pale wananchi walipoichagua Chadema kutokana na msukumo wao ktk mageuzi ilihali wakijua kwamba kwa kuichagua Chadema serikali ya CCM itakwaza maendeleo yao kama walivyokuwa wakijitangaza ktk ilani zao za Uchaguzi.. CCM walisema wazi mkiwachagua Chadema mtakosa maendeleo na bado watu hawa wakamchagua mbunge mgombea wa Chadema, sasa nashindwa kabisa kuunganisha wala kuelewa mtu alomchagua Mbunge wa Chadema lakini akamchagua rais kutoka CCM akijua hatapata maendeleo au labda walidhani JK na CCM ni vitu viwili tofauti?...hii kidogo inanipa shida kuelewa japokuwa sipo vichwani mwa hawa wananchi ambao ndio tunataka kuwalaumu na sio chombo kinachohusika na uchaguzi..

Nafikiri yaliyotokea mwaka 2010 hayawezi kuwa na majibu sahihi hasa baada ya kulazimishwa kukubali matokeo. Kama tulivyolazimishwa kuamini mkataba wa Richmond na Dowans haukuwa na matatizo au swala la rada..Na binafsi yangu nisingependa hata kuwazia kilitokea nini maana NDIVYO TULIVYO...

Mkuu Mkandara,

Asante kwa mchango wako. Kuhusu suala la wabunge wa Chadema kushinda kura za ubunge majimboni kwao lakini kushindwa kumsaidia mgombea wao wa urais humo humo jimboni kwao kwa kweli hata mimi limeshindwa kuingia akilini, na ni moja ya sababu moja kubwa kwanini nimekuja na mada hii; nashukuru umeliona hili suala kwamba halijakaa vizuri tofauti na wengine ambao mtazamo wao ni tofauti sana, hasa wakijaribu kulitolea ufananuzi kuliko kujikita katika kuangalia kama mapungufu yapo ili kulitafutia ufumbuzi wa kwa siku za huko mbeleni;

Nilipendekeza nadharia tete mbili katika original post yangu (rejea post hiyo sehemu za mwishoni) kama njia ya kuchokoza mjadala ili pengine tuweze kubaini mwenendo wa wapiga kura tanzania katika hili upo vipi; Vinginevyo nia yangu nyingine ya kuja na mada hii ni kujaribu kutafuta majibu juu ya hoja hizi hizi za wengi wetu humu kwamba matokeo ya 2010 hayakuwa halali kwahiyo uchambuzi wake nao ni batili; kwa mtazamo wangu, tukifany akazi backwards katika takwimu hizi, tutaweza kugundua mapungufu mengi sana ambayo yatasaidia kubaini pengine ni wapi ndio kura zilichakachuliwa; bila ya kuchambua mwenendo wa wapiga kura na matokeo katika majimbo mbalimbali, hatutaweza kufanikisha lengo hili, vinginevyo ni imani yangu kubwa kwamba ni dhahiri hatutapata majibu ya mia kwa mia lakini angalau tutapata mwanga juu ya suala husika;

Ukipata muda naomba uangalie nadharia tete zangu mbili ambazo sana sana ni za uchokozi lakini nina imani zitatusaidia kuchambua na kubaini mengi;
 
Mkuu Mkandara,

Asante kwa mchango wako. Kuhusu suala la wabunge wa Chadema kushinda kura za ubunge majimboni kwao lakini kushindwa kumsaidia mgombea wao wa urais humo humo jimboni kwao kwa kweli hata mimi limeshindwa kuingia akilini, na ni moja ya sababu moja kubwa kwanini nimekuja na mada hii; nashukuru umeliona hili suala kwamba halijakaa vizuri tofauti na wengine ambao mtazamo wao ni tofauti sana, hasa wakijaribu kulitolea ufananuzi kuliko kujikita katika kuangalia kama mapungufu yapo ili kulitafutia ufumbuzi wa kwa siku za huko mbeleni;

Nilipendekeza nadharia tete mbili katika original post yangu (rejea post hiyo sehemu za mwishoni) kama njia ya kuchokoza mjadala ili pengine tuweze kubaini mwenendo wa wapiga kura tanzania katika hili upo vipi; Vinginevyo nia yangu nyingine ya kuja na mada hii ni kujaribu kutafuta majibu juu ya hoja hizi hizi za wengi wetu humu kwamba matokeo ya 2010 hayakuwa halali kwahiyo uchambuzi wake nao ni batili; kwa mtazamo wangu, tukifany akazi backwards katika takwimu hizi, tutaweza kugundua mapungufu mengi sana ambayo yatasaidia kubaini pengine ni wapi ndio kura zilichakachuliwa; bila ya kuchambua mwenendo wa wapiga kura na matokeo katika majimbo mbalimbali, hatutaweza kufanikisha lengo hili, vinginevyo ni imani yangu kubwa kwamba ni dhahiri hatutapata majibu ya mia kwa mia lakini angalau tutapata mwanga juu ya suala husika;

Ukipata muda naomba uangalie nadharia tete zangu mbili ambazo sana sana ni za uchokozi lakini nina imani zitatusaidia kuchambua na kubaini mengi;
Nakumbuka tuliwahi kufanya hivyo baada ya uchaguzi wa mwaka 2005 na nilipigwa vita wala sii mchezo lakini mwisho wa siku Chadema ilimsimamisha Dr.Slaa kama nilivyokuwa nikisema japokuwa nilichukiwa sana mwanzoni na wapambe halafu Mbowe mwenyewe ndiye aliyependekeza kwanza kumsimamisha Dr.Slaa..
 
Mkuu Kobello,

Nashukuru kwa mchango wako; unaposema kwamba wapiga kura tanzania hutazama personalities kwa sababu vyama havina itikadi zinazoeleweka wazi, lakini hasa zinazouzika kwa wananchi walio wengi, nakubaliana na wewe kwa hili mia kwa mia; lakini pale Dr. Slaa anaposema kwamba kwa kawaida Chadema inajadili masuala na sio watu, kwa mtazamo wako, Chadema ifanye nini kuboresha kile anacholenga kukijenga Dr. Slaa, hasa katika mazingira ya itikadi bora na sio bora itikadi? Kwani ni dhahiri kwamba kwa Sasa Chadema hawana itikadi bora, bali bora itikadi; same applies to CCM;

Nimependa pia hoja yako kuhusu mwamko wa wapiga kura uchaguzi wa 2005, kwani unazidi kushindilia hoja yako kwamba mwenendo wa wapiga kura wengi Tanzania ni kuchagua WATU, na sio chama wala masuala yanayosimamiwa na Chama; Kuna ukweli katika hili, lakini je, nini mtazamo wako kuhusu upigaji kura kwa wabunge kwa vigezo nilivyojadili vya LOCALISM vis-a-vis vigezo vya NATIONALISM kwa nafasi ya Urais?
Mchambuzi sijui kwanini mimi napata shida sana kuwalewa watuw anaosema "itikadi bora na sio bora itikadi? Kwani ni dhahiri kwamba kwa Sasa Chadema hawana itikadi bora, bali bora itikadi; ". Hii dhana imesambaa sana humu ndani.Ila naamini ukitoka na kumuuliza mwanaCCM wa kweli kuhusu CDM halfu umwambie hicho hapo juu atakuambia ukweli...Wengi wao wanajaribu kwepesha ukweli kwa kusema "...ni wazuri sana ila Vurugu..." au kingine kinachofanana na hicho amabye yeye ndio kamezeshwa.

Si kweli watu wanavyoamini kuwa Tanzania watu wanachagua Mtu na si chama .Ukweli ni kwamba CDM iliplay role kama brand by itself na hivyo kuwabeba wabunge wake wengi sana.Tofauti na JK kama JK kipindi cha kwanza aliwabeba sana wabunge wa CCM kwa ule upepo wa umaarufu alioanza nao.

Mchambuzi huwezi amini hizo sababu nilizokupa mapema kabisa ni very real zaidi ya unavyoweza dhani.Hizo factors ukiziweka kama equalizer ,halafu kila parameter ipande na kushuka kama ilivyochangia kuongeza kura kwa mshindi kwa kila jimbo ,utashngaa sana.Kwani ni sehemu chache sana zitakuwa na additional parameters.Ni vitu niliobserve mikoa karibu nane niliykuwepo kabla ,kipindi cha kura na baadaye.Niliongea na watu wengi sana kila nilipokuwepo.Si habari ya kufikirika.

Pia nimesikia watu wakilalamikia CDM kuchelewa mtangaza mgeombea,kwa CDM ilikuwa ni strategy ya kuwasurprise CCM, na ilifanya Kazi vizuri sana.Waliwashangaza kuwa alikuja mtu mpya na hawakuwa na options nzuri sana kwani wamefanya nae kazi kwa karibu na kumkubali.Na after shocks bado zinawatafuna sana CCM.CCM walikuwa wameandaa rundo la scandles za kuzusha wakidhani atakuwa Mbowe kwa vile walikuwa na taswira ya CUF,TLP,NCCR.Mbowe kawa Free kutanya kazi nyingine muhimu kwa chama.
 
Mimi hapa nitazungumzia dhana tu lakini kwa mujibu wa uzoefu wangu.

Katika hali ya kawaida ya kibinadamu na kisaikolojia, pia kwa kuzingatia unazi wa Watanzania kwa vyama vyao; na ingawa mwananchi ana uhuru wa kuchagua kile anachokipenda, si rahisi kwa mtu wa jimbo hilo hilo, akapewa karatasi za wagombea wa uraisi, ubunge na udiwani, akatia kura kwa mgombea wa chama tafauti katika kila karatasi.

Ninachotaka kusema hapa, na hii narudia tena kuwa ni dhana yangu tu kwa sababu niliyoeleza hapo juu, hatuoni kama kulikuwa na uwezekano mkubwa wa Dr. Slaa kushinda kwenye majimbo ya Kigoma Mjini, Hai na Singida, lakini Kikwete akaibuliwa mshindi kwa uchachakuaji wa matokeo?

Just thinking aloud.

Nitarejea baadaye kwa mchango wa kina ambao hautakuwa umeathiriwa na wasiwasi wangu wa hapo juu.

Mimi ni mpiga kura jimbo la Ubungo nilichagua rais chama kingine na Mbunge chama kingine, hilo linawezekana kabisa kwa walio wengi.
 
Mna nafasi nzuri huko CCM za kuleta mabadiliko ili na sisi tuwe na ushindani thabiti dhidi ya upinzani lakini mnadhania mnayoyafanya ni mnakijenga chama kumbe mnakibomoa. Mkija shtuka, hasa uhalisia wa mambo utakapo kick in, tayari itakuwa ni too too late; Sisi vijiweni huku tunaendelea kukipigania chama kwa mwendo mdogo mdogo na tunafanikiwa kujijengea heshima, huku pia tukikilinda chama katika vicinity zetu, na for some reasons, hao hao mnaowatukana wanatuheshimu, wapo tayari kujenga taifa kwenye maeneo yaliyo over and above siasa za vyama kwa kushirikiana na sisi ingawa tupo vyama tofauti kwani wanatutofautisha sana na wengi ya waliopo jikoni;

Ingekuwa busara sana kama mngeweka sura zenu na majina yenu mjulikane kuliko kujificha na majina na picha za uongo; vinginevyo kila la kheri huko jikoni mkuu;

Wanaposhindwa hoja wanaanza viroja.
 
Mchambuzi sijui kwanini mimi napata shida sana kuwalewa watuw anaosema "itikadi bora na sio bora itikadi? Kwani ni dhahiri kwamba kwa Sasa Chadema hawana itikadi bora, bali bora itikadi; ". Hii dhana imesambaa sana humu ndani.Ila naamini ukitoka na kumuuliza mwanaCCM wa kweli kuhusu CDM halfu umwambie hicho hapo juu atakuambia ukweli...Wengi wao wanajaribu kwepesha ukweli kwa kusema "...ni wazuri sana ila Vurugu..." au kingine kinachofanana na hicho amabye yeye ndio kamezeshwa.

Si kweli watu wanavyoamini kuwa Tanzania watu wanachagua Mtu na si chama .Ukweli ni kwamba CDM iliplay role kama brand by itself na hivyo kuwabeba wabunge wake wengi sana.Tofauti na JK kama JK kipindi cha kwanza aliwabeba sana wabunge wa CCM kwa ule upepo wa umaarufu alioanza nao.

Mchambuzi huwezi amini hizo sababu nilizokupa mapema kabisa ni very real zaidi ya unavyoweza dhani.Hizo factors ukiziweka kama equalizer ,halafu kila parameter ipande na kushuka kama ilivyochangia kuongeza kura kwa mshindi kwa kila jimbo ,utashngaa sana.Kwani ni sehemu chache sana zitakuwa na additional parameters.Ni vitu niliobserve mikoa karibu nane niliykuwepo kabla ,kipindi cha kura na baadaye.Niliongea na watu wengi sana kila nilipokuwepo.Si habari ya kufikirika.

Pia nimesikia watu wakilalamikia CDM kuchelewa mtangaza mgeombea,kwa CDM ilikuwa ni strategy ya kuwasurprise CCM, na ilifanya Kazi vizuri sana.Waliwashangaza kuwa alikuja mtu mpya na hawakuwa na options nzuri sana kwani wamefanya nae kazi kwa karibu na kumkubali.Na after shocks bado zinawatafuna sana CCM.CCM walikuwa wameandaa rundo la scandles za kuzusha wakidhani atakuwa Mbowe kwa vile walikuwa na taswira ya CUF,TLP,NCCR.Mbowe kawa Free kutanya kazi nyingine muhimu kwa chama.

Nimekusoma na kukuelewa mkuu kuhusu jinsi gani uchaguzi mkuu 2010 uli play out, hasa kwa comparative analysis ya jinsi gani 2005 JK aliwabeba wabunge vis-a-vis 2010 (which i assume u meant Dr. Slaa aliwabeba wabunge wake); Pia naomba niseme kwamba sipo hapa kukuamini Mkuu Nicholas bali kujitaidi kuelewa hoja zako, hivyo kuzidi kuelimika kwani kuna mengi pia najaribu kujifunza pamoja na kwamba mimi ndiye mleta mada; kuleta mada sio lazima kwamba mtu unajaribu kulazimisha agenda fulani iaminike kama ndio ukweli wa kusadidika, na nilisema ili from the outset; ndio maana nikaja na nadharia tete kuchokonoa hoja mbalimbali kwani in the process mimi na wengine wengi tutaweza kupick up brain za wachangiaji mbalimbali, esp wale wenye nia ya kujenga badala ya kubomoa.

Hoja yake kuhusu mgombea Urais kubeba wabunge kwa kiasi fulani bado inanipa utata pamoja na kukuelewa kimsingi, hasakuhusu jinsi gani wapiga kura wanavyochagua wagombea wa Urais na Ubunge; Kwa mfano mimi bado sielewi kwanini Zitto na Mbowe wapiga kura wao hawakumpa ushindi Dr. Slaa majimboni kwao na badala yake wakampa Kikwete (hapa i am holding the kuchakachua factor constant); Je, was it a coincidence Dr. Slaa to loose Hai & Kigoma Kaskazini au kulikuwa na other factors at play? Hili bado sijalisikia kwa kifefu kutoka kwako;
 
MAMMAMIA,

Nashukuru sana kwa mchango wako mkuu; Naomba nifafanue awali kabisa kwamba sikukataa mjadala wa uchakachuaji wa kura 2010 ila nilishauri tusiupe kiupa umbele kwanza kwani itatufanye hata hizi takwimu zinazodaiwa kuchakachuliwa tusiweze kupata mwanga zaidi juu ya nini kilitokea; katika majibu yangu kwa mchangiaji mmoja nikasema kwamba tukiwa makini katika uchambuzi, hasa ukizingatia utata mwingi uliojaa kwenye matokeo ya kura huko majimboni kwenye ngazi ya urais, pengine tutaweza pata mwanga (sio lazima majibu) juu ya nini kilitokea; kwa mfano mimi bado hainiingii akilini Dr, Slaa kushindwa kura za Urais jimbo la Zitto na jimbo la Mbowe; nia yangu ilikuwa ni kuja na mjadala ambao unaweza kutusaidia kufanya kazi backwards na pengine kufanikiwa kupata angalau mwanga (sio lazima jibu) juu ya nini kilijiri katika suala zima la uchakachuaji. Lakini tukianza mjadala kwa kudharau takwimu zilizopo, tutapoteza nafasi muhimu kujaribu kutafuta mwanga huo towards ukweli;

Kuhusu Zomba na kauli zake dhidi ya Chadema, mimi ni mwana CCM lakini sipo katika kundi la wana CCM wenye mwono alionao yeye; mimi naweka utaifa kwanza mbele kwa kuangalia mambo ambayo yapo above and beyond partisan politics, baada ya hapo naipa heshima dhana ya demokrasia na RULE OF LAW (hasa itakayokuja kwenye katiba mpya), sio RULE BY LAW (iliyopo kwenye katiba ya sasa), lakini muhimu zaidi najali zaidi siasa za kujenga taifa letu, sio za kubomoa kwani in the future itakuwa ni watoto wetu na wajukuu wetu, atakachofaidika mchambuzi au zomba na siasa za maslahi ya chama na watawala haina maana kwamba wajukuu wa mchambuzi na zomba watakuja pata faida hizo, sana sana watakuja angamia; ndio maana mijadala ya aina ya kina zomba mimi sioni kama ina tija kwa taifa, kwangu, na nina uhakika hata kwa vitukuu vya zomba miaka 50 ijayo; pengine ina tija kwake yeye kwa miaka ya sasa, ndio maana nikamwambia kila la kheri katika hilo;
 
Mchambuzi,

..JK tayari alikuwa Raisi, kwa hiyo ni vigumu mgombea kama Slaa, out of nowhere, kuweza kumpiku.

Nilipata opportunity kushiriki katika kampeni za Urais CCM 2010 lakini nikiri kwamba pamoja kwamba mgombea wetu alikuwa ana seek to be re-elected, hiyo haikuwa sababu kubwa kwanini lazima tushinde; hili lilijitokeza pia uchaguzi wa1995 lakini ni nyerere aliyeokoa jahazi kwa kiasi fulani; Uchaguzi wa 2010 CCM iliingia kwenye uchaguzi sio kama Chama chenye mgombea mmoja ambae anaungwa mkono mia kwa mia na wanachama wote bali chama chenye mgombea mwenye wanachama (w CCM) wachache waliojitolea kumpigania kufa na kupona licha ya changamoto kubwa zilizokuwepo; katika maeneo mengi tuliyokuwa tunapita kwa ajili ya kampeni, kuna baadhi ya majimbo tulikuwa tunatukanwa na kukejeliwa na wana CCM wenzetu ambao walikuwa wanampigia kampeni mgombea wao wa ubunge lakini hawakuwa na mapenzi ya dhati na mgombea wao ngazi ya urais (JK); hoja yangu ya msingi hapa ni kwamba mgombea urais ambae anatafuta kuwa re-elected for another term sio kigezo tosha cha kumshinda mgombea wa upinzani, hasa katika mazingira ya siasa za Tanzania ya leo ambayo wananchi wengi ni maskini na wanazidi kuelimika juu ya mapungufu kadhaa ya Chama tawala cha CCM;

..kitu kingine kilichomsaidia JK ni MTANDAO mkubwa wa CCM uliopo vijijini, rasilimali watu[watumishi wa serikali, polisi, wasanii, jumuiya za chama, waandishi wa habari] pamoja na FEDHA nyingi zilizotumika wakati wa kampeni.

Ni kweli hili lilichangia sana tushinde kwa asilimia 62%

..pia sina uhakika kama timu ya kampeni ya CDM ilikuwa inaielewa vizuri saikolojia ya wapiga kura. kwa mtizamo wangu, wapiga kura wa Tanzania, kutokana na umasikini wao, wana-respond vizuri zaidi kwa mgombea mwenye kutoa ahadi lukuki aliyokuwa akifanya JK. naamini kulikuwa na kiasi fulani cha mapungufu ktk campaign message ya CDM as it relates to uelewa na matamanio ya wa-Tanzania.

Nakubaliana na wewe katika hili na ni hili ni moja ya maeneo muhimu kwa Chadema kuyafanyia kazi iwapo wana dhamira ya kweli kuingia ikulu 2015; lakini pia tusisahau kwamba wapiga kura wameshajifunza kuhusu siasa za ahadi; Mwalimu alipaya kusema haya in the 1970s na nadhani taratibu yana trickle down kwa wapiga kura wetu leo:

"I hope that both candidates in each election will be intelligent enough to recognize that not everything can be done at once, and that nothing is this world is free. For the fact is that if a person is urging more communal services or better communal services, he or she is probably also urging that you, as the voter, should be willing to pay more local rates or more taxes. For if they are promising lots of new activities if they are elected, and if they are promising that these will be done without any cost to you, or effort on your part, they are either deliberately misleading you - thinking you are fools - or they themselves are fools."

Mind you, Mwalimu alizungumza haya wakati wa utawala wa chama kimoja cha TANU (uchaguzi mkuu 1970);

..mwisho, naomba nieleze kwamba CDM had a better candidate compared to CCM. Hata CUF walikuwa na mgombe mweledi zaidi kulinganisha na yule wa CCM. Hicho ndicho kilichopelekea CCM kukwepa kushiriki kwenye mdahalo wa wagombea Uraisi. In the future, CDM waangalie their campaign message, pia wahakikishe wana mtandao mkubwa, na zaidi wawe na fedha na vitendea kazi kwa ajili ya kampeni.

Hili linajadilika na mwisho wa mjadala, wengi watakuwa upande wako wa hoja.
 
Back
Top Bottom