Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Kilichonipa hamasa kuja na mjadala huu ni kauli ya hivi karibuni ya Katibu Mkuu wa Chadema Dr. W.P. Slaa aliyoitoa kama sehemu ya majibu yake kwa Mzee Samuel Sitta aliyetoa kauli kwamba ‘Chadema haipo tayari kuongoza nchi kwa sababu bado hakina hazina ya kutosha ya viongozi'. Katika majibu yake kwa Mzee Sitta, Dr. Slaa alitamka yafuatavyo (nanukuu):
Nia yangu leo SIO kujadili suala la Dr. Slaa na Mzee Sitta; nimenukuu tu sehemu ya maneno ya Dr. Slaa in order to set this discussion in its context. Kwa ujumla wake, mjadala wangu utalenga zaidi kwenye kujadili mwenendo wa kisiasa, hasa chaguzi katika nchi yetu kutokana na ukweli kwamba ushindani wa kisiasa pamoja na mikakati inayotumiwa na vyama vingi nchini wakati wa kampeni za uchaguzi ipo centred zaidi on PERSONALITIES rather than ISSUES; Nadhani sote tunaelewa madhara ya mwenendo huu katika demokrasia ni yepi, hivyo ni muhimu kumpa Dr. Slaa pongezi kwa kuchukua hatua za kuondokana na hilo, kama kiongozi wa kitaifa wa chamakikuu cha upinzani Tanzania. Moja ya mambo makubwa yanayo dhoofisha demokrasia nchini Tanzania ni pamoja na uwepo wa ‘OMBWE LA ITIKADI' miongoni mwa vyama vyote vyasiasa (pamoja na chama tawala - CCM), jambo ambalo linapelekea wananchi wengi kuchagua viongozi kwa vigezo vilivyo nje kabisa ya MASUALA yanayozunguka maisha yao (hasa kiuchumi na kijamii), na badala wanatumia vigezo vya UTASHI/HAIBA YA WAGOMBEA, Mazoea,Ukabila, Udini, Ubaguzi wa Jinsia n.k.
Specifically,nitajadili Siasa za ‘MASUALA' vis-à-vis Siasa 'WATU' kwa kutumia ‘reference' yamambo yaliyojiri' katika Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge (2010). Katika tazamatazama zangu, nimegundua uwepo wa ‘DISCREPANCIES' kubwa sana kwenye matokeo huko majimboni baina ya washindi ngazi ya Urais [kwenye kura za Rais majimboni] dhidi ya washindi katika ngazi za Ubunge kwenye majimbo mbalimbali. Nitalifafanua hili baadae kidogo. Ni matarajio yangu kwamba mwisho wa siku, sote tutaoshiriki katika mjadala huu tutafanikiwa kujifunza mambo mengi baada ya kubadilishana mawazo, experience, lakini kwa nia ya kujenga na sio kubomoa, kwani hivyo ndivyo tutaweza kuimarisha demokrasia nchini Tanzania.
Let me declare at the outset kwamba mimi ni Mwanachama wa CCM ninayeamini katika demokrasia ya kweli, lakini muhimu zaidi, ninayeamini kwamba: BILA CHADEMA MADHUBUTI, CCM MAKINI HAIWEZEKANI.
Katika mjadala wangu, nitafanya ‘reference'kwa kwenye majimbo kumi na tano ambayo Chadema ilishinda viti vya ubunge kwenye uchaguzi uliopita (2010):
Katika mjadala wangu, nitajaribu kuchambua matokeo mbalimbali katika majimbo haya kwangazi ya Urais na Ubunge baina ya CCM na Chadema; Ni matumaini yangu kwamba hii itatusaidia sote kwa pamoja kubaini MAPUNGUFU na CHANGAMOTO zinazotukabili kama nchi yenye Demokrasia changa, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea 2015.
Baada ya kusema haya, sasa niingine kwenye uchambuzi wa majimbo kumi na tano niliyoyataja awali.
a) Je, kushinda kwa Zitto Ubunge lakini kushindwa kwa Dr. Slaa Urais Kigoma Kaskazini ni ishara kwamba watanzania wengi huchagua wabungekwa vigezo vya LOCALISM na RAIS kwa vigezo vya NATIONALISM?
b) Kigomani moja ya mikoa ambayo ipo nyuma sana kimaendeleo katika nyanja nyingi; Je mwenendo huu wa wapiga kura unatupa taswira gani kuhusu wapiga kura wa mikoa kama Kigoma na mingineyo iliyopo nyuma kimaendeleo?
c) Kwa vile sasa ni wazi kwamba Zitto ana mikakati ya kugombea Urais 2015 kupitiaChadema; Je, kama hakuwa na uwezo wa kushawishi wapiga kura wake wamchague Dr.Slaa kiti cha urais, kama walivyomchagua yeye kiti cha ubunge, what's the justification and rationale juu ya uwezo wake kushinda Urais (ngazi ya taifa)2015? Inawezekana justification and rationale ipo, lakini tukija jadili hili, nimuhimu tuanze na dhana ya "CHARITY BEGINS AT HOME".
Pia niseme kwamba – kuna dalili kubwa kwamba mwaka 2015, Lissu ataongeza margin ya ushindi wake jimboni kwake, lakini vile vile kuna uwezekano mkubwa ‘to deliver'kura kwa mgombea Urais Chadema 2015 pamoja na kwamba Singida kihistoria ningome kubwa sana ya CCM tofauti na Kigoma (kwa Zitto) au Kilimanjaro (kwaMbowe); Ni kwa maaana hii, Lissu anabakia kuwa hazina kubwa sana ya Chadema hata ngazi ya Urais kwa siku za usoni (hata 2015). Lissu ataipa CCM wakati mgumu sana kama atasimamishwa na Chadema 2015 pengine kuliko mgombea mwingine yoyote nje ya Dr. Slaa. Lakini huu ni mjadala tofauti na nisingependa kwenda huko kwa sasa.
So far, tumesha jadili majimbo matatu ambayo Dr. Slaa alianguka kwa margin kubwadhidi ya Kikwete. Kabla sijaendelea na majimbo yaliyobakia, ningependa kuorodhesha ‘TOP FIVE' ya majimbo ambayo wabunge wake hawakuweza kumsaidia Slaa kupata kura dhidi ya Jakaya Kikwete 2010:
a) Kigoma Kaskazini – Zitto: Dr. Slaa lost by 32% to Kikwete; [note – Zitto hakuwa mbunge mgeni na pia tayari alikuwa ni kiongozi wa Chadema Taifa, hivyo kuwa na nafasi ya kuvuta wapiga kura wengi zaidi kuliko wabuge wapya];
b) Singida Mashariki – Lissu: Dr. Slaa lost by 32% to Kikwete;[note – Lissu ni mbunge mpya na hakuwa na nafasi ya uongozi ya kisiasa ndani ta Chadema Taifa; Vile vile traditionally, Singida ni moja ya ngome nzito sana za CCM kama ilivyokuwa kwa Tanga ambapo wagombea wa CCM hata wakiwa wa ovyo hupita tu;
c) Hai– Mbowe – Dr. Slaa lost by 31% to Kikwete; [note – Mbowe alishawahi kuwa mbunge miaka ya nyuma, na pia amekuwa kiongozi wa kisiasa wa Chadema ngazi ya taifakwa muda mrefu];
d) Mbozi Magharibi – Silinde – Dr. Slaa lost by 27% to Kikwete; [note – Silinde ni mbunge mpya lakini aliweza kuwapiku Zitto na Mbowe kwenye delivery ya votes kwa Dr. Slaa dhidi ya Kikwete majimboni mwao];
e) Iringa Mjini – Rev. Msigwa – Dr. Slaa lost by about 10% to Kikwete; [note – Msigwa kama ilivyokuwa kwa Lissu na Silinde ni mbunge mgeni/mpya lakini bado na yeye delivered more votes kwa Dr. Slaa kuliko Mbowe na Zitto];
Yafuatayo ni majimbo mengine ambayo pamoja na kwamba Kikwete alishinda, lakini kwa margin ndogo sana ya percentage of votes:
Mwisho nimalizie na majimbo ambayo wabunge wa Chadema walifanikiwa kuwashawishi wapiga kura wao kumchagua Dr.Slaa dhidi ya Kikwete.
Ningependa kuhitimisha na maswali na nadharia tete kwa nia ya kuongezea mjadala huu uhai zaidi:
1. Je,wakati wa kupiga kura, Watanzania hutarajia mambo gani kutoka kwa yule wanae mchagua kuwa Mbunge wao?
2. Je,wapiga kura hutarajia mambo gani kutoka kwa yule wanaemchagua kuwa Rais wa nchi?
3. Je, PERSONALITY (MTU) & ISSUES (MASUALA) hutumiwa vipi na wanasiasa na pia je, hutumikaje na wananchi katika kuchagua viongozi wao (wabunge na rais)?
4. Je, Watanzania huchagua wabunge kwa vigezo vya LOCALISM? NATIONALISM? AU VYOTE VIWILI?
Katika hili la Localism na Nationalism, napendekeza NADHARIA TETE (Hypotheses) mbili. Naomba ieleweke kwamba nia yangu kuja na hizi nadharia tete ni kutengeneza mazingira bora ya mjadala huu na sio vinginevyo. Naomba haya yasichukuliwe kwamba ndio UKWELI ULIOSADIDIKA.
Naomba nisisitize tena kwamba hizi ni nadharia tete tu ambazo zinaweza kuwa TRUE au FALSE, hivyo mjadala wetu ukielekea huko, kutakuwa na tija zaidi. Vinginevyo, huu sio UKWELI ULIOSADIKIKA.
Nawasilisha.
["Leo nalazimika kumzungumzia MTU, Watanzania wanajua mara chache sana CHADEMA huwa tunalazimika kuzungumzia WATU badala ya MASUALA…"].
Dr. W.P Slaa, August 2012
Dr. W.P Slaa, August 2012
Specifically,nitajadili Siasa za ‘MASUALA' vis-à-vis Siasa 'WATU' kwa kutumia ‘reference' yamambo yaliyojiri' katika Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge (2010). Katika tazamatazama zangu, nimegundua uwepo wa ‘DISCREPANCIES' kubwa sana kwenye matokeo huko majimboni baina ya washindi ngazi ya Urais [kwenye kura za Rais majimboni] dhidi ya washindi katika ngazi za Ubunge kwenye majimbo mbalimbali. Nitalifafanua hili baadae kidogo. Ni matarajio yangu kwamba mwisho wa siku, sote tutaoshiriki katika mjadala huu tutafanikiwa kujifunza mambo mengi baada ya kubadilishana mawazo, experience, lakini kwa nia ya kujenga na sio kubomoa, kwani hivyo ndivyo tutaweza kuimarisha demokrasia nchini Tanzania.
Let me declare at the outset kwamba mimi ni Mwanachama wa CCM ninayeamini katika demokrasia ya kweli, lakini muhimu zaidi, ninayeamini kwamba: BILA CHADEMA MADHUBUTI, CCM MAKINI HAIWEZEKANI.
Katika mjadala wangu, nitafanya ‘reference'kwa kwenye majimbo kumi na tano ambayo Chadema ilishinda viti vya ubunge kwenye uchaguzi uliopita (2010):
- Ilemela;
- Ubungo;
- Singida Mashariki;
- Nyamagana;
- Arusha Mjini;
- Ukerewe;
- Moshi Mjini;
- Kawe;
- Hai;
- Mbeya Mjini;
- Karatu;
- Rombo;
- Mbozi Magharibi;
- Iringi Mjini;
- Kigoma Kaskazini;
Katika mjadala wangu, nitajaribu kuchambua matokeo mbalimbali katika majimbo haya kwangazi ya Urais na Ubunge baina ya CCM na Chadema; Ni matumaini yangu kwamba hii itatusaidia sote kwa pamoja kubaini MAPUNGUFU na CHANGAMOTO zinazotukabili kama nchi yenye Demokrasia changa, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea 2015.
Baada ya kusema haya, sasa niingine kwenye uchambuzi wa majimbo kumi na tano niliyoyataja awali.
- JIMBO LA KIGOMA KASKAZINI
a) Je, kushinda kwa Zitto Ubunge lakini kushindwa kwa Dr. Slaa Urais Kigoma Kaskazini ni ishara kwamba watanzania wengi huchagua wabungekwa vigezo vya LOCALISM na RAIS kwa vigezo vya NATIONALISM?
b) Kigomani moja ya mikoa ambayo ipo nyuma sana kimaendeleo katika nyanja nyingi; Je mwenendo huu wa wapiga kura unatupa taswira gani kuhusu wapiga kura wa mikoa kama Kigoma na mingineyo iliyopo nyuma kimaendeleo?
c) Kwa vile sasa ni wazi kwamba Zitto ana mikakati ya kugombea Urais 2015 kupitiaChadema; Je, kama hakuwa na uwezo wa kushawishi wapiga kura wake wamchague Dr.Slaa kiti cha urais, kama walivyomchagua yeye kiti cha ubunge, what's the justification and rationale juu ya uwezo wake kushinda Urais (ngazi ya taifa)2015? Inawezekana justification and rationale ipo, lakini tukija jadili hili, nimuhimu tuanze na dhana ya "CHARITY BEGINS AT HOME".
- JIMBO LA HAI
- JIMBO LA SINGIDA MASHARIKI
Pia niseme kwamba – kuna dalili kubwa kwamba mwaka 2015, Lissu ataongeza margin ya ushindi wake jimboni kwake, lakini vile vile kuna uwezekano mkubwa ‘to deliver'kura kwa mgombea Urais Chadema 2015 pamoja na kwamba Singida kihistoria ningome kubwa sana ya CCM tofauti na Kigoma (kwa Zitto) au Kilimanjaro (kwaMbowe); Ni kwa maaana hii, Lissu anabakia kuwa hazina kubwa sana ya Chadema hata ngazi ya Urais kwa siku za usoni (hata 2015). Lissu ataipa CCM wakati mgumu sana kama atasimamishwa na Chadema 2015 pengine kuliko mgombea mwingine yoyote nje ya Dr. Slaa. Lakini huu ni mjadala tofauti na nisingependa kwenda huko kwa sasa.
So far, tumesha jadili majimbo matatu ambayo Dr. Slaa alianguka kwa margin kubwadhidi ya Kikwete. Kabla sijaendelea na majimbo yaliyobakia, ningependa kuorodhesha ‘TOP FIVE' ya majimbo ambayo wabunge wake hawakuweza kumsaidia Slaa kupata kura dhidi ya Jakaya Kikwete 2010:
a) Kigoma Kaskazini – Zitto: Dr. Slaa lost by 32% to Kikwete; [note – Zitto hakuwa mbunge mgeni na pia tayari alikuwa ni kiongozi wa Chadema Taifa, hivyo kuwa na nafasi ya kuvuta wapiga kura wengi zaidi kuliko wabuge wapya];
b) Singida Mashariki – Lissu: Dr. Slaa lost by 32% to Kikwete;[note – Lissu ni mbunge mpya na hakuwa na nafasi ya uongozi ya kisiasa ndani ta Chadema Taifa; Vile vile traditionally, Singida ni moja ya ngome nzito sana za CCM kama ilivyokuwa kwa Tanga ambapo wagombea wa CCM hata wakiwa wa ovyo hupita tu;
c) Hai– Mbowe – Dr. Slaa lost by 31% to Kikwete; [note – Mbowe alishawahi kuwa mbunge miaka ya nyuma, na pia amekuwa kiongozi wa kisiasa wa Chadema ngazi ya taifakwa muda mrefu];
d) Mbozi Magharibi – Silinde – Dr. Slaa lost by 27% to Kikwete; [note – Silinde ni mbunge mpya lakini aliweza kuwapiku Zitto na Mbowe kwenye delivery ya votes kwa Dr. Slaa dhidi ya Kikwete majimboni mwao];
e) Iringa Mjini – Rev. Msigwa – Dr. Slaa lost by about 10% to Kikwete; [note – Msigwa kama ilivyokuwa kwa Lissu na Silinde ni mbunge mgeni/mpya lakini bado na yeye delivered more votes kwa Dr. Slaa kuliko Mbowe na Zitto];
Yafuatayo ni majimbo mengine ambayo pamoja na kwamba Kikwete alishinda, lakini kwa margin ndogo sana ya percentage of votes:
- JIMBO LA UBUNGO
- JIMBO LA ROMBO
- JIMBO LA KAWE
Mwisho nimalizie na majimbo ambayo wabunge wa Chadema walifanikiwa kuwashawishi wapiga kura wao kumchagua Dr.Slaa dhidi ya Kikwete.
- JIMBO LA ILEMELA
- JIMBO LA UKEREWE
- JIMBO LA ARUSHA MJINI
- JIMBO LA KARATU
- JIMBO LA MOSHI MJINI
- JIMBO LA MBEYA MJINI
Ningependa kuhitimisha na maswali na nadharia tete kwa nia ya kuongezea mjadala huu uhai zaidi:
MASWALI YA KUJADILI NI MANNE
2. Je,wapiga kura hutarajia mambo gani kutoka kwa yule wanaemchagua kuwa Rais wa nchi?
3. Je, PERSONALITY (MTU) & ISSUES (MASUALA) hutumiwa vipi na wanasiasa na pia je, hutumikaje na wananchi katika kuchagua viongozi wao (wabunge na rais)?
4. Je, Watanzania huchagua wabunge kwa vigezo vya LOCALISM? NATIONALISM? AU VYOTE VIWILI?
Katika hili la Localism na Nationalism, napendekeza NADHARIA TETE (Hypotheses) mbili. Naomba ieleweke kwamba nia yangu kuja na hizi nadharia tete ni kutengeneza mazingira bora ya mjadala huu na sio vinginevyo. Naomba haya yasichukuliwe kwamba ndio UKWELI ULIOSADIDIKA.
NADHARIA TETE ZA KUJADILI NI HIZI ZIFUATAZO:
- NADHARIA TETE YA KWANZA:
- NADHARIA TETE YA PILI:
Naomba nisisitize tena kwamba hizi ni nadharia tete tu ambazo zinaweza kuwa TRUE au FALSE, hivyo mjadala wetu ukielekea huko, kutakuwa na tija zaidi. Vinginevyo, huu sio UKWELI ULIOSADIKIKA.
Nawasilisha.