Chadema mtoto habembelezwi kwa nyimbo mbaya!!

Mohammed Hamad

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
3,988
1,304
Great Thinkers,

Habari zenu na ni matumaini mu wazima wa afya na wale wanaumwa ni mategemeo yangu watajaaliwa afya na siha njema na Mwenyezimungu.

Tangu kukamatwa kwa viongozi wa chama kikuu cha "upinzani" kumetolewa kauli nyingi sana hapa jamvini na wapenda "chama" na nyingi ya kauli hizo ni za kuvuruga amani na utulivu zenye lengo la kuchochea machafuko na umwagaji damu! Bila kujielewa au kwa kuelewa wengi wamediriki hata kusema "watapindua" nchi na ndio uhuru wa kweli utapatikana! Nimejiuliza watu wenye kuweza kupindua nchi lazima watakuwa na majeshi yao sitaki kuamini kuna jeshi zaidi ya jeshi la ulinzi na usalama la Tanzania. Tumekuwa tukisikia watu wakipewa vyeo vya "kamanda" na "mpiganaji" nadhani hatuhitaji kupigana tunataka maendeleo yatakayo leta tija kwetu na kwa vizazi vijavyo.

Ndugu yangu Waberoya ameelezea nini kile wananchi wanacho kitaka katikama thread yake https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-maslahi-ya-taifa-they-are-just-another-tool japo wengi wenu mmeona kama ni kejeli kwa sababu hoja zake ni za kujenga na nyie sera yenu ni ya kubomoa na kuleta chuki na mifarakano wengi wenu hamkuipokea wala kuitafakari. Sisi tunahitaji utaifa kwanza! tunataka Tanzania iwe nchi yenye kutawalika! tunataka watoto wetu waje kuiridhi nchi ikiwa kwenye hali ya kutawalika!

Imefikia wakati napata wakati mgumu sana kutofautisha wanachama wa cdm na waumini wasabato masalia. Kuna fikra zenu na mawazo mnayoyatoa humu jamvini ni ya kufikirika zaidi kama yale ya kusafiri bila ya passport wala visa!

Nafasi mnayo ya kujenga Tanzania msije mkaandika historia ambayo itakuja kuwa chungu kwetu na kwa vizazi vijavyo. Tujifunze ustaarabu kidogooooo tujaribu kuipenda nchi na si kuwapenda "wapiganani" na vyama. Hii nchi itaendelea kuwepo lakini hawa "wapiganaji na makamanda" pamoja na vyama vyao vitakufa!

Ushauri wangu mdogo sana kwenu mlio na upofu wa kutoona uzuri wa maelewano/mshikamano/uhuru wa kwenda popote ni kuwa kuna nchi zina zilianza chokochoko kama zetu lakini mpaka leo hazitawaliki moja wapo ni Somalia.

Nimesikitishwa na ndugu jangu mmoja ambae ni memba nguli hapa JF kwenye FB status yake amewataadharisha Polisi na wanasiasa "watawala" wawe na busara na kuepusha maafa kwa kinachoweza kutokea kwenye issue ya Mhe Mbowe. Huyu ni mwandishi anatumia fani yake kama mwandishi kujaribu kujenga mazingira kuwa mamlaka ni za kionevu na busara zifanyike. Pengine ataandika makala ya kuelezea uonevu wa mamlaka zilizokuwa zinashughulikia hii issue naamini haitajenga ila kuongeza chuki! Natamani tupate waandishi wenye kujali maslahi ya nchi zaidi kama kuwaonya wawaonye wahusika wote. Mfano amwonye mtu ambae ana kesi aweze kuhudhuria kesi yake yeye au wakili wake kwani kwa kutokufanya hivyo kunaweza kukafanya akamatwe na kuleta machafu anayotaka yazuiwe kwa kukwepa kufata misngi ya sheria.

Mwandishi Nguli Ngugi wa Thiong'o amepata kusikiaka akisema pale Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kuwa, "Ukitaka kujua nchi itakuwaje kesho basi waangalie vijana wake wa leo" Vijana wa leo wa cdm ambayo kesho wanataka kuchukua nchi wanataka Arusha isikalike wanasema eti leo wataandamana na kuingia bungeni kuchukua viti! Kwahiyo mtaona kesho nchi yetu itakuwaje!


Najua hampendi kuambiwa ukweli lakini sioni tofauti yenu kifikra na wasabato masalia mnatofautiana kuwa nyie ni wanachama wa chama cha siasa wao ni waumini wa dini.
 
Tunayoipenda nchi tumeshukuru yale yote mabaya mliosema yatatokea hayakutokea na Mungu atatuepushi leo na siku za usoni Amin.
 
Mkuu nakupa hongera kwa makala yako. Safi sana. Siku zote tusiwe negative tu, wakati mwengine inatakiwa tuwe positive. Siasa za chuki na ugomvi zimepitwa na wakati. Mungu ibariki TANZANIA.
 
Great Thinkers,

Habari zenu na ni matumaini mu wazima wa afya na wale wanaumwa ni mategemeo yangu watajaaliwa afya na siha njema na Mwenyezimungu.

Tangu kukamatwa kwa viongozi wa chama kikuu cha "upinzani" kumetolewa kauli nyingi sana hapa jamvini na wapenda "chama" na nyingi ya kauli hizo ni za kuvuruga amani na utulivu zenye lengo la kuchochea machafuko na umwagaji damu! Bila kujielewa au kwa kuelewa wengi wamediriki hata kusema "watapindua" nchi na ndio uhuru wa kweli utapatikana! Nimejiuliza watu wenye kuweza kupindua nchi lazima watakuwa na majeshi yao sitaki kuamini kuna jeshi zaidi ya jeshi la ulinzi na usalama la Tanzania. Tumekuwa tukisikia watu wakipewa vyeo vya "kamanda" na "mpiganaji" nadhani hatuhitaji kupigana tunataka maendeleo yatakayo leta tija kwetu na kwa vizazi vijavyo.

Ndugu yangu Waberoya ameelezea nini kile wananchi wanacho kitaka katikama thread yake https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-maslahi-ya-taifa-they-are-just-another-tool japo wengi wenu mmeona kama ni kejeli kwa sababu hoja zake ni za kujenga na nyie sera yenu ni ya kubomoa na kuleta chuki na mifarakano wengi wenu hamkuipokea wala kuitafakari. Sisi tunahitaji utaifa kwanza! tunataka Tanzania iwe nchi yenye kutawalika! tunataka watoto wetu waje kuiridhi nchi ikiwa kwenye hali ya kutawalika!

Imefikia wakati napata wakati mgumu sana kutofautisha wanachama wa cdm na waumini wasabato masalia. Kuna fikra zenu na mawazo mnayoyatoa humu jamvini ni ya kufikirika zaidi kama yale ya kusafiri bila ya passport wala visa!

Nafasi mnayo ya kujenga Tanzania msije mkaandika historia ambayo itakuja kuwa chungu kwetu na kwa vizazi vijavyo. Tujifunze ustaarabu kidogooooo tujaribu kuipenda nchi na si kuwapenda "wapiganani" na vyama. Hii nchi itaendelea kuwepo lakini hawa "wapiganaji na makamanda" pamoja na vyama vyao vitakufa!

Ushauri wangu mdogo sana kwenu mlio na upofu wa kutoona uzuri wa maelewano/mshikamano/uhuru wa kwenda popote ni kuwa kuna nchi zina zilianza chokochoko kama zetu lakini mpaka leo hazitawaliki moja wapo ni Somalia.

Nimesikitishwa na ndugu jangu mmoja ambae ni memba nguli hapa JF kwenye FB status yake amewataadharisha Polisi na wanasiasa "watawala" wawe na busara na kuepusha maafa kwa kinachoweza kutokea kwenye issue ya Mhe Mbowe. Huyu ni mwandishi anatumia fani yake kama mwandishi kujaribu kujenga mazingira kuwa mamlaka ni za kionevu na busara zifanyike. Pengine ataandika makala ya kuelezea uonevu wa mamlaka zilizokuwa zinashughulikia hii issue naamini haitajenga ila kuongeza chuki! Natamani tupate waandishi wenye kujali maslahi ya nchi zaidi kama kuwaonya wawaonye wahusika wote. Mfano amwonye mtu ambae ana kesi aweze kuhudhuria kesi yake yeye au wakili wake kwani kwa kutokufanya hivyo kunaweza kukafanya akamatwe na kuleta machafu anayotaka yazuiwe kwa kukwepa kufata misngi ya sheria.

Najua hampendi kuambiwa ukweli lakini sioni tofauti yenu kifikra na wasabato masalia mnatofautiana kuwa nyie ni wanachama wa chama cha siasa wao ni waumini wa dini.

Unaturudisha nyuma magamba mkubwa wewe!!!!crap crap crap crap this!!!!
 
We ni gamba lisilovulika wala kukwangulika huna la maana.

Unajua kebehi hata mie nazijua tena zinye kuumiza na kufurahisha kwa wakati huo huo hivi nikuulize wewe unashabikia chuki mwenyekiti wako anapeana mkono na Rais akienda jukwaani anakupika uwe na chuki na aliekuwa akisalimiana nae kwa bashasha unatakiwa hata kama una akili za kushikiza ujitambue. Nadhani kati yangu mimi na wewe ni wewe mwenye magamba tena unagamba ya Mamba!
 
kuongea umeongea lakini huna point, kumbuka historia tulipokuwa tunadai uhuru toka kwa wakoloni, kwanza walikuwapo wachache wenye kuwa na ujasiri wa kufuatilia, waliwashawishi wtz wengine, jaribu kuuliza ni magumu ganii walikutana nayo kabla hujaropoka non sense! na pia wakati huu kumbuka now tunafight against wale wanaotumia migongo ya wanyonge kunufaika, tunaposema nchi isitawalike haina maana vita, nah! we mean mbinu za unyonyaji wanazotumia tuzipinge! upo? fikiri kabla hujaongea!
 
kuongea umeongea lakini huna point, kumbuka historia tulipokuwa tunadai uhuru toka kwa wakoloni, kwanza walikuwapo wachache wenye kuwa na ujasiri wa kufuatilia, waliwashawishi wtz wengine, jaribu kuuliza ni magumu ganii walikutana nayo kabla hujaropoka non sense! na pia wakati huu kumbuka now tunafight against wale wanaotumia migongo ya wanyonge kunufaika, tunaposema nchi isitawalike haina maana vita, nah! we mean mbinu za unyonyaji wanazotumia tuzipinge! upo? fikiri kabla hujaongea!

Nakubaliana na wewe ni kweli walipata misukosuko nakumbuka hata Bibi Titi Mohamed alipata msukomsuko wa maana baada ya uhuru! Lakini kuwashawishi watu kuendane na hoja na sio maneno ya chuki na uchochezi. Kuwashawishi watu kwa njia ya kistaarabu ni vizuri kuliko kwa njia zenye kuleta mifarakano. Ahsante kwa kucomment na kuona kuwa sina hoja.
 
Great Thinkers,

Habari zenu na ni matumaini mu wazima wa afya na wale wanaumwa ni mategemeo yangu watajaaliwa afya na siha njema na Mwenyezimungu.

Tangu kukamatwa kwa viongozi wa chama kikuu cha "upinzani" kumetolewa kauli nyingi sana hapa jamvini na wapenda "chama" na nyingi ya kauli hizo ni za kuvuruga amani na utulivu zenye lengo la kuchochea machafuko na umwagaji damu! Bila kujielewa au kwa kuelewa wengi wamediriki hata kusema "watapindua" nchi na ndio uhuru wa kweli utapatikana! Nimejiuliza watu wenye kuweza kupindua nchi lazima watakuwa na majeshi yao sitaki kuamini kuna jeshi zaidi ya jeshi la ulinzi na usalama la Tanzania. Tumekuwa tukisikia watu wakipewa vyeo vya "kamanda" na "mpiganaji" nadhani hatuhitaji kupigana tunataka maendeleo yatakayo leta tija kwetu na kwa vizazi vijavyo.

Ndugu yangu Waberoya ameelezea nini kile wananchi wanacho kitaka katikama thread yake https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-maslahi-ya-taifa-they-are-just-another-tool japo wengi wenu mmeona kama ni kejeli kwa sababu hoja zake ni za kujenga na nyie sera yenu ni ya kubomoa na kuleta chuki na mifarakano wengi wenu hamkuipokea wala kuitafakari. Sisi tunahitaji utaifa kwanza! tunataka Tanzania iwe nchi yenye kutawalika! tunataka watoto wetu waje kuiridhi nchi ikiwa kwenye hali ya kutawalika!

Imefikia wakati napata wakati mgumu sana kutofautisha wanachama wa cdm na waumini wasabato masalia. Kuna fikra zenu na mawazo mnayoyatoa humu jamvini ni ya kufikirika zaidi kama yale ya kusafiri bila ya passport wala visa!

Nafasi mnayo ya kujenga Tanzania msije mkaandika historia ambayo itakuja kuwa chungu kwetu na kwa vizazi vijavyo. Tujifunze ustaarabu kidogooooo tujaribu kuipenda nchi na si kuwapenda "wapiganani" na vyama. Hii nchi itaendelea kuwepo lakini hawa "wapiganaji na makamanda" pamoja na vyama vyao vitakufa!

Ushauri wangu mdogo sana kwenu mlio na upofu wa kutoona uzuri wa maelewano/mshikamano/uhuru wa kwenda popote ni kuwa kuna nchi zina zilianza chokochoko kama zetu lakini mpaka leo hazitawaliki moja wapo ni Somalia.

Nimesikitishwa na ndugu jangu mmoja ambae ni memba nguli hapa JF kwenye FB status yake amewataadharisha Polisi na wanasiasa "watawala" wawe na busara na kuepusha maafa kwa kinachoweza kutokea kwenye issue ya Mhe Mbowe. Huyu ni mwandishi anatumia fani yake kama mwandishi kujaribu kujenga mazingira kuwa mamlaka ni za kionevu na busara zifanyike. Pengine ataandika makala ya kuelezea uonevu wa mamlaka zilizokuwa zinashughulikia hii issue naamini haitajenga ila kuongeza chuki! Natamani tupate waandishi wenye kujali maslahi ya nchi zaidi kama kuwaonya wawaonye wahusika wote. Mfano amwonye mtu ambae ana kesi aweze kuhudhuria kesi yake yeye au wakili wake kwani kwa kutokufanya hivyo kunaweza kukafanya akamatwe na kuleta machafu anayotaka yazuiwe kwa kukwepa kufata misngi ya sheria.

Najua hampendi kuambiwa ukweli lakini sioni tofauti yenu kifikra na wasabato masalia mnatofautiana kuwa nyie ni wanachama wa chama cha siasa wao ni waumini wa dini.
Hivi unaelewa vizuri ni kitu gani kinafanya nchi ziwe na amani? Kwa mtizamo wako Tanzania kuna amani? Haki ndio msingi mkuu wa amani haki inapotoweka hiyo amani haipo tena
 
Shossi anagekamatwa wa CCM wangemfanyia hivi kwanini ikiwa ni CCM kuna kinga lakini kwa CHADEMA inakuwa tofauti??? Why??? Kwa maana hiyo kwenye Sheria pia haina haki
 
Kwa mtu makini yeyote aliyehuru katika mtazamo na maoni hatokubaliana na Kiongozi asiyetii mamlaka na sheria zinaongoza jamii. Hivyo kwangu mie Shosi yuko sahihi kimantiki na kikanuni. Lakini hoja yake ukiipima ktk mizania ya uhalisia, jinsi sheria hizohizo zinavyotumika kidhalimu unakubali kumsamehe Mkosaji Mbowe tena kwa aibu. Tukio kama hili ilikuwa muhimu litokee ili wananchi watambue sheria ilivyo msumeno kwa wapinzani, dagaa na wanyonge na si kwa watawala, mapapa/nyangumi wala wakwasi.
 
Mohamed Shosti tatizo la mifumo yetu ya sheria ni kuwa haiko fair kwa nini mbunge wa ccm awe na kinga lakini wa chadema au cuf au updp asiwe na kinga hiyo na wote ni wabunge wa bunge moja?

Najua huna maana ya kunidhalilisha nadhani jina langu linasomeka vizuri tu unless uwe unasababu zako binafsi za kuandika unavyotaka wewe.

Well maneno yako ni kweli na ndio maana utaona G Lema na girlfired wa Slaa hawakukamatwa na kupelekwa mahakamani japo kuwa na wao hawakuhudhuria mahakani lakini walifuata taratibu za kuwasilisha sababu za kutofika mahakani nasisitiza kwa hili nadhani CDM wameteleza kidogo lakini kuteleza huko haina maana tuhubiri machafuko. Napenda mageuzi lakini sio kwa machafuko ya kijinga kama yanayohubiriwa hapa JF na wapenzi vindakindaki wa CDM. Naomba mnisameh kwa kutokuwa mnafiki kwenu.
 
MS ... hakuna hata chembe moja ya point to discuss .... its sometimes better to remain silence
 
Tanzania bado ina kaaazi saana, tena saaana!,

Asante kwa Maada Bwana Shosi,

Asanteni kwa michango yenu wana JF, inatosha!
 
Shossi anagekamatwa wa CCM wangemfanyia hivi kwanini ikiwa ni CCM kuna kinga lakini kwa CHADEMA inakuwa tofauti??? Why??? Kwa maana hiyo kwenye Sheria pia haina haki

Tupinge njia zilizo sahihi kama ile waliyotumia LHCR kuhusu mgombea binafsi sio kwa kutumia uchochezi na vitisho hapo ndio mnapoharibu kuna kundi kubwa sana halishabikii vyama wanaanza kupata wasiwasi na mienendo yenu wanaowaambia wanawatakia mema.
 
Naomba kuuliza hivi Freeman yuko nje kwa Dhamana Mpya au anaendelea na dhamana ile ile ya kesi ya zamani? waliohudhuria mahakamani nijuzeni kuhusu hili
 
Back
Top Bottom