CHADEMA msitishwe na RC Chalamila

DOMBWELA

JF-Expert Member
Jan 18, 2014
757
842
Baada ya CHADEMA kutangaza maandamano Jan 24, Mh RC Chalamila nae ametangaza kuwa siku ya tarehe 23 na 24 Januari kuwa siku za usafi utakaofanya na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama.

Mimi nasema hivyo ni vitisho tu, kanyagieni hapo hapo msinyanyue mguu tupo pamoja na ninyi, maana hata sisi tumechoka kuona yanayoendelea ndani ya Nchi yetu. Na sisi tunahitaji ujumbe uwafikie watawala.

Mkiona ngoma itakuwa ngumu badilisheni mbinu ya maandamano, ikiwezekana muagize kila Kata ifanye maandamano katika eneo lao, viongozi wa CHADEMA wa Kitaifa, kanda mbali mbali, na majibo kitaifa waje wagawanywe waongeze nguvu kwenye kila kata tuone kama hayo maandamano hayatafanyika na kufanikiwa kufikisha ujumbe uliokusudiwa.

Nasema tena msitishwe na hivyo vitisho vya MH RC Chalamila aliyelewa madaraka na kutaka kutumia vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vibaya, kwenye jambo la msingi kama hilo msihofu tupo pamoja.
 
Bila kufa watu kama milioni and so, CCM na unyama wao hawawezi kurekebisha/kuitikia matakwa ya wananchi.
 
Umeongea kwa uchungu sana, mimi 24 saa moja kamili nipo pale ofisi ya Chalamila na mfagio wangu na Dekio plus ndoo ya maji na sabuni ya Unga kufanya usafi, ndani ya ofisin kwake, analeta mchezo huyu haijui Dunia.
 
Back
Top Bottom