CHADEMA kuwashirikisha NCCR na TLP baraza jipya la Mawaziri Kivuli

Mimi sina ugomvi kabisa kwa vyama vya upinzani kushirikiana vyenyewe kwa vyenyewe -- na hata kuungana, iwapo sheria na kanuni zinaruhusu. Kinachonikera ni kwa chama cha upinzani kushirikiana au kuungana na chama kilichopo madarakani.

Bila shaka CUF wamelitambua hili na Prof Lipumba -- ambaye naamini kabisa ni kiongozi ambaye angefaa kabisa kuwa rais wa nchi hii -- amejikuta njia panda kutokana na yaliyojiri huko Visiwani kwa chama chake.

Na ndiyo maana juzi alionekana kumsapoti Mbowe alipokamatwa na polisi. CDM nawaomba wakutane pia na Profesa ili kuona taifa linaokolewa vipi kutoka kwa hao mafisadi, na ambao sasa pia wamekuwa wauaji wa raia.

Huwa nawaza: Jee sasa hivi Profesa akitangaza kuhamia CDM -- itakuwaje? nadhani watakaochanganyikiwa sana sana siyo CUF, wala CCM -- bali ni CDM! Just think about it!!!!!


Wacha kutufanya wapumbavu! Kauli hii unatamka sasa hivi ? Kwani kanuni sasa zimebadilika? Na pili jee huo muungano uliowakera nyinyi wa CCM na CUF kule Zanzibar umeondoshwa?
Unajuwa hii tabia yenu ya kimbelembele na kukimbilia sifa inawaponza kidogokidogo. Tunaomba mpeleke hoja ya kupunguza matumizi bungeni kwa kuondowa viti maalum ili mkomoke kama kweli mnawalenga wananchi na sio uroho wa kisiasa tu.
 
Tunapongeza hatua mlizoamua kuzichukua CDM lkn tahadhari ni muhimu hasa kwa vyama kama CUF na TLP. NCCR wameonyesha kuwa katika njia moja nanyi hata kihoja. Umakini na busara za hali ya juu ni lazima vitumike katika hili. Twende nalo taratibu tusikurupuke.

Kwani kilichoharibika nini? Endeleeni tu kuwa Wapinzani pekeyenu. Unatowa tahadhari lakini si unajuwa kuwa hivyo vyama ndio vilevile mlioviona kuwa si sawa nanyi. Nafikiri mgeanza kwa kuomba radhi.
 
Tahadhari ni muhimu saaana,ninapenda sana ushirika huu ingawaje tatizo langu bado liko palepale...kwamba CUF iliyokuwa inaikejeri CDM,leo wanaona CDM itawafaa?TLP kama chama sioni tatizo ila tatizo naliona kwa Mrema,huyu mzee katu sitakuja nimwelewe kamwe,ni zaidi ya kinyonga,ni zaidi ya popo,sidhani kama atakuwa na jema kwa CDM kwa 100%

Ushauri wangu,ni kweli tumeyasikia mengi,tumeyaona mengi,nawashauri CDM wawe waangalifu sana na waanzishe chombo maalumu cha kufatilia na kuripoti ushirika huu kwa ukaribu sana ili badala ya kujenga tusije kulia kilio cha kusaga meno

juzi kati tumetoka kuletewa thread humu ndani iliyokuwa ikisema- wakati sisi tunalala wenzetu wanakesha,amini usimini,tupende tusipende magamba yako kila mahali na nina uhakika hata kwenye ushirika huu wataingia ama phsically ama spiritually.... they are so opportunists!


Nafikiri mapenzi yako yalikupofuwa. Uliona mjadala wa kutaka kuundwa "Upinzani Rasmi". Ni CHADEMA waliojaa kejeli kwa wenzao lakini kwa vile ukweli siku zote ndio unaoshinda hapa mkubali kuwa hamko kama mnavyotaka kujisikia.
 
Mbowe ndio anaomba kuangana na TLP, NCCR, CUF, vipi mkuu utaama chama au utakubali na wewe ndoa

I think a good leader is the one who always unites rather than divides for the betterment of a country. On this CDM has shown leadership. Uwingi wa wabunge haina maana kwamba wachache hawana hoja za kujenga Taifa, kama tutafanya kazi pamoja as a team nchi itasonga mbele, tatizo lipo kwa wale wa CCM ambao kwao wao upinzani ni usaliti na ndiyo maana wanaona aibu hata kuchukua mazuri ya upinzani kwa faida ya nchi. They are know it all!
 
Ngekewa said:
Hamadi Rashid sie alieleta Serikali ya Mseto kule Zanzibar ambako mlitowa matusi ya nguoni, mlisahau msemo wa Waswahili " Msitukane wakunga na bado hamjazingoa.

Ngekewa,

..ni wapi yalitolewa hayo matusi ya nguoni?

..off course serikali ya mseto baina ya CCM na CUF inaleta complications ktk mahusiano baina ya CUF na vyama vingine vya upinzani.

..zaidi Hamad Rashid alikosea kujaribu kuwa-bulldoze CDM wakati wa mchakato wa kuundwa kwa kambi ya upinzani.

..there was no need kwa Hamad Rashid kutumika na CCM katika kubadilisha kanuni za uundaji wa kambi ya upinzani ili kuiumiza CDM kisiasa.

..suala hili lingezungumzwa kati ya Mbowe na Prof.Lipumba nadhani pangepatikana muafaka unaoeleweka na kuleta matumaini ktk duru za siasa za upinzani.

..HAMAD RASHID ALIKUWA KIKWAZO. CUF WAMETUMIA BUSARA KUMPUMZISHA.
 
Anything done by CHADEMA is good, Chadema itaendelea kutesa tu na itakuwa inawatumia hawa wengine pale tu itakapoona kuwajumlisha watachangia kuleta mabadiliko kwa wananchi na kuwaweka pembeni pale tu itakapoonekana wanatetea masilahi yao na ya CCM.
 
Sasa mtu kama Sugu, Lema au Wenje, wanaweza kweli kuchambua bajeti ya wizara yoyote zaidi ya maandamano
 
Chadema naona wamekubali yale maneno ya Waberoya kuwa bila kushirikiana na vyama vingine hamna kitu, nasubiri wale wote walikuwa wanapinga sijui wataama Chadema
 
Chadema si mlisema chama cha upinzani Tanzania ni kimoja tu, sasa imekuaje tena mnaanza mchakato wa kushirikisha vyama vingine vya siasa, miezi sita tu taingia kuundwa kwa Baraza la Mawaziri Kivuli mpo hoi, Chadema-JF, sijui mtaama Chadema wakiungana na CUF,NCCR Mageuzi, UDP, TLP
hivi upo nchi gani? kwanini haufuatilii mambo ya nchi yako ? aliye kudanganya hivyo ni nani? pole sana be updated IQ ikutume kujadili hoja za msingi toa mpendekezo ya kujenga kulingana na upeo wako CDM wataungana na yeyeote maadamu ni kwa kulinda na kukuza demokrasia ya nchi kama unaelewa fuatilia UCHAGUZI wa mwaka jana
 
JF Great thinkers wafuata mkumbo. Ikitokea Mbowe na CDM wanakuja na Mtizamo fulani! Huwa wengi huunga mkono. Ikitokea wakaamua kwenda kinyume na mawazo yao ya mwanzo bila hata kutoa sababu, kuna watu humu watawaunga mkono na kuanza hata kuwasifia wale waliokuwa wanawaponda. Hivi ile Serikali ya Mseto Zenji umekufa hadi wawe wapinzani leo? Tanzania zaidi ya uijuavyo.
 
Kafulila huyu si yule aliyewahi kuwa Chadema na baadae wanamfukuza ndio akaingia NCCR.

Sasa vipi wanakaa nae meza moja?

Nashangaa!!!!!!!!!!!!???
 
Kafulila huyu si yule aliyewahi kuwa Chadema na baadae wanamfukuza ndio akaingia NCCR.

Sasa vipi wanakaa nae meza moja?

Nashangaa!!!!!!!!!!!!???

hamad rashid na maalim seif walikuwa ccm wakatoka wakaenda cuf na sasa hivi wameungana na kukaa pamoja na ccm

mbona haushangai hii!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!???????
 
That is a good move! Kwa sasa wabunge wa upinzani wote kwa ujumla isipokuwa wachache walio kwenye mkumbo wa CCM wameanza kuelewa kuwa maslahi ya Watanzania ni muhimu kuliko maslahi yao binafsi!!!
 
Kafulila huyu si yule aliyewahi kuwa Chadema na baadae wanamfukuza ndio akaingia NCCR.

Sasa vipi wanakaa nae meza moja?

Nashangaa!!!!!!!!!!!!???

Kafulila ni kichwa kile, na wanajilaumu kwa nini walitumia jazba ile kumfukuza, walim-understate kwa kusema eti Kafulila ni mtu mdogo tu kama sisimizi ndani ya CDM lakini leo wanamwona ni mkubwa zaidi ya tembo ndani ya siasa za Tanzania.
 
CDM wanataka kula matapishi yao! Inabidi kwanza wawaombe radhi wenzao kabla ya kuendelea na mchakato! HR aliwaambia ni utoto tuu unawasumbua.............sasa nadhani wameanza kupata akili!
Hoja zao za mwanzao..........CUF kushirikiana na CCM Zanzibar, NCCR hawaaminiki.......

Sasa nini kimebadilika?
 
Sasa mtu kama Sugu, Lema au Wenje, wanaweza kweli kuchambua bajeti ya wizara yoyote zaidi ya maandamano
Acha ujinga wako wewe!
sisi tuliowachagua ndo tunajua kazi wanaiweza mbona hatusemi ccm 85% ni vichwa maji kabisa!
HV mtu kama KOMBA unamfananisha na SUGU? au ROSTITAMU unamfananisha na Wenje?
 
Kafulila ni kichwa kile, na wanajilaumu kwa nini walitumia jazba ile kumfukuza, walim-understate kwa kusema eti Kafulila ni mtu mdogo tu kama sisimizi ndani ya CDM lakini leo wanamwona ni mkubwa zaidi ya tembo ndani ya siasa za Tanzania.
Kwenye siasa hakuna adui wala rafiki wa kudumu. Ingawa binafsi nawaona jamaa zangu wengi wa Kigoma ni wabishi tu wasio na msimamo hata kwa maamuzi ya pamoja.
 
Sasa mtu kama Sugu, Lema au Wenje, wanaweza kweli kuchambua bajeti ya wizara yoyote zaidi ya maandamano
Kuna gazeti moja limeandika likiwakariri wasomi wa Nchi hii wakipendekeza mishahara ya WABUNGE itofautiane kulingana viwango vya elimu, uzoefu. Nadhani si haki Sugu kulingana mshahara na Zitto!
 
Back
Top Bottom