Communist
JF-Expert Member
- Jun 1, 2012
- 5,400
- 1,181
Tarehe 27 August, Jumatatu, umekuwepo na mkutano mkubwa sana ambao haujawahi kutokea hapo K ndege (Fire) kwa ajili ya wakazi wa morogoro mjini.
Maandamano yaliingiliwa na polisi lakini yalifanyika
Muuza magazeti maeneo ya msamvu amefariki baada ya kupigwa kichwani na Polisi
CDM hawakufanya vurugu.
Mkutano ulianza saa nane mchana hadi saa kumi na mbili jioni.
Baadaye uchaguzi wa viongozi ulifanyika katika hoteli
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi CHADEMA na Mbunge wa jimbo la Ubungo Jijini Dar es Salaam John Mnyika akipanda jukwaani wakati akiwasili katika uwanja huo (Photo by Molemo the great)
Angalia mambo yanavyoendelea vijijini, nafikiri njini itatisha.
"Hali inaonyesha kuwa vijana wengi na wazeee hasa wale waliokuwa vyama vya CCM na CUF wamehama vyama hivyo na kukiunga mkono CDM. Mfano mmoja wapo ni pale Tawi moja wapo lililokuwa na washabiki wa chama cha CUF karibu na BUSH BAR...SUA ROAD limebadilika na kuwa CDM.kama upo morogoro pita hapo utaona mwenyewe. Pia kwa mjibu wa kijana mmoja hivi yeye anakaa chamwino anadai kuwa nyumbani kwao kulikuwa na shina la CCM..hivo shina hilo nalo limebadilika na kuwa CDM. Jamani haya ni maneno ya kweli...Ngome ya CCM sasa inakwenda alijojo.....nawakilisha". (Matata 2011)
Tarehe 27 August 2012, fungueni masikio na macho, hukuna kuogopa.
====================================
MATUKIO KATIKA PICHA WAKATI WA MKUTANO HUO
====================================
Kiongozi mkuu wa upinzani nchini na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibrod Slaa, akiwahutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Morogoro na vitongoji vyake, katika mkutano wa hadhara wa operesheni sangara, kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Uwanja wa Ndege
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lisu akizungumza na wananchi wa Manispaa ya Morogoro waliojitokeza katika mkutano huo.
Makamu Mwenyekiti CHADEMA Zanzibar Said Issa Mohamed akifafanua jambo kwa wananchi hao.
Aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Igunda kupitia CHADEMA, Joseph Kashinde akizungumza na wananchi waliohudhuria katika mkutano huo
Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Morogoro na Mbunge wa viti Maalum CHADEMA Suzan Kiwanga akimwaga sera za chama hicho.
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi CHADEMA na Mbunge wa jimbo la Ubungo Jijini Dar es Salaam John Mnyika akipanda jukwaani wakati akiwasili katika uwanja huo