Fredrick Sanga
JF-Expert Member
- Jan 27, 2011
- 3,153
- 697
Hata Mandela alikata tamaa kwa makaburu, ni suala la tafsiri tu. Lakini kwa maana yangu mapambano dhidi ya ufisadi yamekolea. Hata mbwa ukamfukuza, akafika ukingoni asione pa kutokea, hakika atakujeruhi. Kukata tamaa sio kujikunja na kulia yowe. Kwa mimi nikikata tamaa napigangumi za macho.Dr. Slaa akikusikia atasikitika. Ameshaandika humu (kunionya mimi hapo nyuma)kwamba kukata tamaa ni kosa kubwa kuliko makosa yote.
Najua tunaudhiwa sana na CCM, lakini tusikate tamaa. Tufuate mfano wa makamanda wetu wa kuwakaba CCM kotekote. Tukumbuke Regia Mtema alivyoasa kwamba watakaba ndani na nje ya Bunge.