CHADEMA jengeni ofisi

Very good, hili ni wazo la mwaka !!! Nitachangia mifuko miwili ya cement,target iwe kukamilisha jengo kabla ya 2014.
 
mimi nawaomba mjenge ofisi na muanzishe kituo redio na tv humo humo
watu wapo tayari kuchangaa

sabodo tupo kibao tu humu nchini
 
Viongozi wa CMD wanachama wanataka jengo zuri la ofisi. Na wapotayari kuchingia msipuuze anzisheni kampeni ya ujenzi. Lazima tuende na mambo yote kutetea wananchi na kujenga ofisi.
 
Hilo jengo la dodoma limejengwa na wananchi, sio wana ccm. linapaswa kurudi serikalini haraka. cha kwanza ninacho waomba CDM wakishika madaraka ni kurudisha mali zote zilizoprwa na magamba.



CCM ilijimilikisha mali yaliyochumwa na watanzania enzi za mfumo wa chama dola.Kinachotakiwa ni mali zote kurudishwa serikalini na hiii inathibitisha kwamba mfumo wa vyama vingi ulianzishwa kukiwa hakuna uwanja sawa wa kisiasa,hili ni pigo mojwapo kwa upinzani na ukuaji wa demokrasiasa ya kweli

Chadema ni chama ambacho kimekua kwa kutegemea michango ya viongozi wake na baadhi ya watanzania wenye mapenzi mema na chama.Huko tulikotoka ilionekana kuichangia CCM ndiyo mambo yako yatakunyookea,wafanyabiashara wakubwa wakubwa (wenye kesi nyingi za ufisadi na wakwepa kodi wengi) ndiyo walioongoza kuichangia CCM kwa gharama ya watanzania na raslimali za taifa hili.

Suala la jengo lenye hadhi ni jambo muhimu.Pia tusisahau kwamba chama kinafanya kazi kwa kuzingatia mtiririko wa vipaumbele.Chadema haijatoa vipaumbele kwenye majengo ya kifahari kama chama tawala kilichoshindwa.Kama ofisi zilizopo zinaweza kukisaidia chama kupanga mipango yake (maanake mafanikio yote ambayo chama kimepata yamepangwa katika ofisi hizo) basi ni jambo la kuvuta subira.Mgombea urais mwaka 2010 Dr. Wilbroad Slaa alisema yupo tayari kula mihogo ikulu lakini awatumikie watanzania kwa dhati.Ishara ya uongozi uliotukuka,uongozi ambao watanzania wanaukumbuka sana kutoka kwa Mwl. J.K Nyerere.Hii inaashiri kwamba kama Chadema ingechukua dola mwaka jana tusingefuja mali ya umma kukarabati ikulu huku mita chache kutoka ikulu watu wanalala njaa,watoto wa mitaani wanaishi na kula majalalani.Wenye mapenzi mema na chadema watachangia kwa dhati ili kukiwezesha chama kuwa na vitendea kazi bora na vya kisasa zaidi ili kurahisisha miundombinu itakayotupelekea kuchukua dola kwa ajili ya watanzania wote

Kwa hiyo itakuwa jambo bora zaidi kama chama kitafanya fundraising kwa ajili ya kujenga ofisi,naamini kila mtanzania mwenye nia njema na chadema,msafi kimaadili atachangia kadiri yaa uwezo wake.Harakati hizi za ukombozi wa pili wa Taifa letu zitawezeshwa kama walivyofanya wazee waliopigania uhuru wetu mfano akina Dosa Aziz,Abdul Sykes n.k kwa kujitolea mali zao katika kuchangia harakati za uhuru.Naamini kwa kuanzia,WanaJF wenye mapenzi mema na chadema tuweke utaratibu wa kuchangisha kwa kufungua account maalum tukisaidiwa na administrators wa JAMII FORUMS.Tufanye hivi kama hamasisho kwa uongozi wa juu na pia kutoa mwamko kwa watanzania wengine.Nakiri muda ni mchache lakini Inawezekana kabisa,tuwe sehemu ya harakati hizi kwa vitendo.
 
Wana JF nawashikuru kwa kuchangia. Nimefurahi kuona kuwa wengi humu mna wazo linalofanana na langu. Ikumbukwe kuwa posti hii imekuja kwa nia njema ili kuhamasisha jambo hili.
Ni ukweli usiopingika kuwa kuaminika kwako kunatokana pia na wewe ulivyojiweka. Huwezi kutoka katika kajumba ka nyasi tukakupa kazi ya kusimamia maghorofa. Kwa mliobahatika kufika pale makao makuu mtakubaliana nami kuwa sura ya kitaifa inayoonyeshwa na CHADEMA utaihitaji kuiminya sana ili iingie kwenye kajumba kale.
Naileta kwenu ninyi viongozi muanze mara moja kuhamasisha uchangiaji ili jengo linunuliwe au kujengwa mara moja. Hii haimaanishi mambo mengine yasiendelee. Yote kwa pamoja yanawezekana. Niiteni hata mimi nitachangia!!
 
Wana JF nawashikuru kwa kuchangia. Nimefurahi kuona kuwa wengi humu mna wazo linalofanana na langu. Ikumbukwe kuwa posti hii imekuja kwa nia njema ili kuhamasisha jambo hili.
Ni ukweli usiopingika kuwa kuaminika kwako kunatokana pia na wewe ulivyojiweka. Huwezi kutoka katika kajumba ka nyasi tukakupa kazi ya kusimamia maghorofa. Kwa mliobahatika kufika pale makao makuu mtakubaliana nami kuwa sura ya kitaifa inayoonyeshwa na CHADEMA utaihitaji kuiminya sana ili iingie kwenye kajumba kale.
Naileta kwenu ninyi viongozi muanze mara moja kuhamasisha uchangiaji ili jengo linunuliwe au kujengwa mara moja. Hii haimaanishi mambo mengine yasiendelee. Yote kwa pamoja yanawezekana. Niiteni hata mimi nitachangia!!
Ubarikiwe mkuu,
Kwa kuanzia nawashauri baadhi wanaJF hasa baadhi ya viongozi ingawa najua JF ni jukwaa huru lisilofungamana na upande wowote basi watusaidie kwa kutumia mbinu na uzoefu wao wa fundraising kwa matukio yaliyopita ili kufanikisha hili
 
Kwanza ..Chadema hivi hicho kiwanja tayari kweli?? maana tusijali Ofisi kwanza..Tujue pia kaka kuna mahatua wamenunua kwa maendeleo ya Chama...Peoples Power
 
Ofisi za cdm zipo kwenye brain siyo majengo ya kifahari wakati nchi ni masikini. Kujenga gorofa siyo kip
 
Back
Top Bottom