CHADEMA: Israel ituombe radhi

WE ACHA TUU MKUUU
TUNABANDARI INGETOSHA KULISHA RWANDA, BURUNDI, ZAMBIA, UGANDA NA DRC
TUNAMAZIWA NA BAHARI TUNGEWEZA KUUZA SAMAKI
TUNAMBUGA NZURI
TUNAMAENEO KIBAO YA KILIMO YENYE RUTUBA
MITO KIBAO HATA MAJI SAFI HATUNA
KWANINI TUSIDHARAULIKE EETI!:A S embarassed:

Kwanza Israel katusaidia kutuonyesha u-kondoo wetu.... UKWELI UTABAKI KUWA UKWELI.. hata tujitutumue vipi..!!! Mwingine anamuushisha Nyerere..!!! Enzi za Nyerere upuuzi wote uaotudharaurisha usingekuwepo!!! watu mnagawa dhahabu bure kwa majahili bado msidharaulike!!!! Hata wasiosema wanatudharau zaidi ila wanaona wanyamaze ili....... (people might not notice the difference).... Mtu mzima miaka 50 bado hata kutambaa hawezi!!! Kalaaniwa au ni zezeta.... SAMAHANI KAMA NIMEKUKWAZA
 
kwani unadhani israel wamekosea kwa hiyo kauli? hebu sema basi umuhimu wetu kwa israel ni ktk nini? watu huwa hawapendi kuambiwa ukweli sijui kwa nini
 
Ukiataka kufahamu kwamba Tanzania hatuna viongozi!!! Kwa mfano; Jaribu kufikiri Israeli tuwakabidhi Nchi yetu ya Tanzania alafu wao watukabidhi Nchi yao ya Israeli, baada ya miaka hamsini tuangalie nani kapiga hatua zipi katika maendeleo kwa ujumla?

Tatizo la Nchi yetu watu wanataka uongozi alafu hawajuhi wakishapata uongozi wawafanyie nini watanzania!!! Mfano mzuri na rahisi ni huyu ******, kazi yake kucheka cheka tu katika mambo serious.
 
Kwanza Israel katusaidia kutuonyesha u-kondoo wetu.... UKWELI UTABAKI KUWA UKWELI.. hata tujitutumue vipi..!!! Mwingine anamuushisha Nyerere..!!! Enzi za Nyerere upuuzi wote uaotudharaurisha usingekuwepo!!! watu mnagawa dhahabu bure kwa majahili bado msidharaulike!!!! Hata wasiosema wanatudharau zaidi ila wanaona wanyamaze ili....... (people might not notice the difference).... Mtu mzima miaka 50 bado hata kutambaa hawezi!!! Kalaaniwa au ni zezeta.... SAMAHANI KAMA NIMEKUKWAZA

hii imekaa vyema sana
 
kwanini watuombe radhi wakati ni ukweli mtupu, cha msingi ni kuangalia ni jinsi gani tutarudisha heshima yetu kwa kweli inauma sana kujiona upo kwenye nchi ambayo inashushwa kiasi hiki, wizara ya mambo ya nje ipo kinafki tu maana hamna wanachofanya !!!!
 
Israeli walichosema ni ukweli mtupui, Rais wetu kila siku anazunguka akiomba omba misaada (hadi chandarua JK anaomba), kwa misingi hii kwa nini tusitukanwe?
Assume wewe mwana JF kila siku jamaa wako anakuomba msaada (mara pesa ya kula, pesa ya mtoto shule, watoto wangu wanaumwa), mtu wa namna hii utahacha kumzarau?
Naungana na wachangiaji wengine inabidi C.C.M watuombe radha watanzania kwa sera zao mbovu, mikakati yao mibovu ndani ya miaka hamsini ya uhuru.
Alafu wananiuzi na msemo wao eti "TUMEDHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE" Mmeweza nini C.C.M ninyi? Hicho mlichoweza mbona hatukioni?
Huu ni muda watanzania wenzangu tuidai Tanganyika yetu.
a

Mkuu umsema vyema kabisa. Huwezi kupewa heshima ambayo hustahili hata kidogo. Kwa vitendo vinavyofanywa na rais wetu yafaa tulinganishwe na jimbo moja la libya. Kwa wanaolaani kauli ya waziri barak watoe mfano mmoja tu ambao Tanzania inaweza kupigiwa mfano. Kiuchumi sisi ni zero kabisa let alone kupata uwekezaji toka nje ambao kitakwimu unasimama kwa US$770m wa pili toka Uganda. Lakini hatuwezi kujisifu kuwa tumeweka mazingira mazuri ya Foreign Direct Investment(FDI) ila ni kwamba tunao bado vivutio kwa wawekezaji wa nje vilivyolindwa kama mboni ya jicho na Mwalimu Nyerere ambaye wakubwa wameamua kutumia vilaza kumkejeli lakini tumeamua kuwapa watu wa nje bila urari wa aina yoyote. Mfano ni madini ambayo tunayo mengi lakini yameishia kutajirisha wageni na watanzania wachahche wanaopkea mlungura kutokana na mikataba mibovu. Mikataba imebaki siri kwa sababu wahusika wanaogopa wasipigwe mawe. Wananchi tunaambulia ucahfuzi wa hali hewa, vyanzo vy a maji na udongo na mwisho maadaki wakishamaliza kuchimba madini. Kwa msingi huu kwa nini watu makini kama Waisrael wasikudarau. Kama hatujiheshimu basi tusitegemee mtu atuheshimu maana na ukubwa wa nchi yetu mtu ambaye hajawahi kufika atashangaa kama kweli wapo watu wanatumia ubongo au wapo katika zama za Robinson Crusoe.

Halafu kama wachangiaji wengine walivyosema tukiwa katikati ya utajiri wote huu rais anatembeza bakuli la ombaomba kama kiwete na anajigamba kwamba Tanzania imkumbuke kwa kutembea nje kuombaomba. So disgusting. Watu wanalalamikia issue ya msingi wewe unawapa jibu jepesi eti nisipotembea mtakula mchicha. Sasa umetuletea vyungu vya nyama? Viko wapi? Mbona watu wanasema bora enzi za Mwalimu walitibiwa bure, shule bure na kujengewa nyumba. Operation ondoa makuti ya Magomeni ni mfano tosha. Mliofata mmejenga nini? Na Mungu anajua kuuonyesha ukwleli. Mbali na kumkejeli Mwalimu aliyekuwa na maono mafuriko ya juzi yamewaumbua maana hata emergency na rescue facilities hamna. Hata wale mliowapa mbuga zetu wakatangaza milki yao, mkawapa madini yetu na mabenki yetu mmeshindwa kuwaomba wawape hizo facilities ili mtambie kuwa mmeziweka nyie. Shame on you and you deserve Barak's description no language to sweeten it. My friend Mnyika next time try to view things on the wide spectrum. Maoni mengine mwachie Nape
 
  • Thanks
Reactions: Ame


Ukiataka kufahamu kwamba Tanzania hatuna viongozi!!! Kwa mfano; Jaribu kufikiri Israeli tuwakabidhi Nchi yetu ya Tanzania alafu wao watukabidhi Nchi yao ya Israeli, baada ya miaka hamsini tuangalie nani kapiga hatua zipi katika maendeleo kwa ujumla?

[h=2]Isaka na Abimeleki[/h] 1 Ikawa njaa katika nchi hiyo, mbali na njaa ile ya kwanza iliyokuwa siku za Ibrahimu. Isaka akamwendea Abimeleki, mfalme wa Wafilisti, huko Gerari. 2 BWANA akamtokea, akasema, Usishuke kwenda Misri, kaa katika nchi nitakayokuambia. 3 Kaa ugenini katika nchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe, na kukubariki, maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote. Nami nitakifanya imara kiapo nilichomwapia Ibrahimu baba yako. 4 Nitazidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, nami nitawapa uzao wako nchi hizi zote, na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia. 5 Kwa sababu Ibrahimu alisikia sauti yangu, akayahifadhi maagizo yangu, na amri zangu, na hukumu zangu, na sheria zangu. 6 Isaka akakaa katika Gerari.
Abimeleki akawaamuru watu wote, akisema, Amgusaye mtu huyu au mkewe lazima atauawa. 12 Isaka akapanda mbegu katika nchi ile, akapata mwaka ule vipimo mia kwa kimoja, BWANA akambariki. 13 Na mtu huyu akawa mkuu, akazidi kusitawi, hata akawa mkuu sana. 14 Akawa na mali ya kondoo, na mali ya ng'ombe, na watumwa wengi. Hao Wafilisti wakamhusudu. 15 Na vile visima vyote walivyochimba watumwa wa baba yake, siku za Ibrahimu babaye
HUYO NDO BABA YAKE NA ISRAEL; UKIPENDA MWITE YAKOBO........ nani amuombe msamaha mwenziye!!!!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Watanzaia kama sio wapumbavu au kama si wa tripolitania wangechaguaje chama ambacho viongozi wake wanongeza kodi kwenye mafuta ya taa an kupunguza au kufuta kodi kwenye madini? Big up waisraeli
 
Mbona hii ni kauli ya kawaida kabisa katika medani za diplomasia. Inategemeana huyu bwana alikuwa anaongelea suala gani na kuhusu nini. Umuhimu wa nchi unategemeana na ushiriano uliopo katika nyanja mbali mbali aidha kiuchumi, kisiana au kiutamaduni. Hivyo hivyo na uhusiano unaweza kuwa imara au legelege kutegemeana na hii.
Kwa mfano, uteuzi wa mabalozi huwa unategemeana sana umuhimu wa nchi balozi atakapokwenda. Israel kwa mfano, ina Ubalozi mmoja tu mjini Nairobi unaohudumia nchi 9 zilizoko kati na mashariki mwa Africa wakati Africa kusini licha ya ubalozi wa Jorbug pia wana ofisi kibao karibu kila state kule SA. Hii ni kutokana na umuhimu wa nchi husika. Africa kati na mashariki hakuna lolote la maana linaloweza kuipata nguvu Israel iwe na mahusiano nayo ya karibu na vivyo hivyo sisi huku tunahitaji Israel kwa kipi hasa?!
Usisahau kuwa nchi chache sana zina balozi kila nchi (mfano USA) lakini nyingi zina balozi katika nchi ambazo ni za karibu sana kimahusiano.
Chukulia hiyo kauli ya Barak kiuchanya (positively) na usibebe tu kama vile uko mtaani.
 
Israel wako sahihi. Si wao waliotudhalilisha bali ni kukosa kwetu akili ndiko kunakotufanya tudhalilike duniani.
 
Tatizo letu mkuu hatujijui how irrelevant we are as a country.
Hy Waziri yupo sawa kabisa, Mi mwenyewe sioni umuhimu wa Tanzania kama nchi kwenye anga la kimataifa.Ila serikali ikanushe tu maanake tumeshazoea kukanusha ukweli ka ule wa mapanki
 
kauli ya Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo, Ehud Barak, kudai kuwa "Tanzania si nchi ya muhimu wala ya maana" imekolezwa kisiasa aliongea maneno hayo nane tu kuhusu Tanzania mengine ni ya John mnyika.
 
John Mnyika unataka kusema na lile suala la sera ya nje ya nchi hizo kuhusu ushoga ni mapungufu ya sera yetu ya nje? tumeambiwa Tanzania haina haki za binadamu kwa sababu nchi yetu haiwapi mashoga haki yao ya kuwa huru. Mbona hii ukuifuatilia sana? au kwa sababu chama cha conservative cha Uingereza ni mfadhili na rafiki wa chadema?
 
Sidhani kama wamekosea waizrael ingekuwa enzi za Mwalimu wasingethubutu kuongea hayo!Ni matokea ya uongozi legelege wa JK
 
Mambo mengine mnyika ni lazima kuzama ndani kuna taarifa kwamba Waziri huyo wa Ulinzi alitaka kutanua himaya ya jeshi lake na kuiomba Tanzania kuwa mshiriki wake wa Afrika akisaidiana na Marekani kuanzisha vituo vya kijeshi lakini sisi tukakataa. sasa inawezekana hii ni njia ya kulipiza kisasi au kutukomoa. katika mazingira ya tamko lake si lazima tuwe na sera mbovu.
 
John Mnyika kwa nini hushangai Waziri wa ulinzi wa Israel ndiye anazungumzia sera za nje badala ya waziri husika wa mambo ya nje wa Israel ambaye tuna uhakika anajua vema zaidi mambo hayo? hapa kuna namna!!!!
 
Walianza kwa kututaka tuukubali ushoga kama haki za binadamu na sasa wamekuja na hili la kusema we are nothing. Hizi zote ni signs za dharau iliyosababishwa na kutembeza bakuli ilhali upande mwingine tunawalegezea wanachukua rasilimali zetu kadiri wanavyotaka na kutushurutisha kusaini mikataba in their favour. I think its time to change turudishe heshima yetu waweze kujua umuhimu wetu kwao especially kwenye resources tulizo nazo. Hivi mbona rahisi tu jamani??? Kwa mfano, hivi tunahitaji rocket science kuamua kuwa kwenye madini tugawane mali tujue pa kuuzia badala ya percent za ajabu tunazopewa sijui kwenye mrabaha/mrahaba?? Fine hata kama wao watatuzidi kidogo sababu ya kuleta facilities ambazo hatuna lakini atleast tugawane mali tujue tuuze wapi. Kuvutia utalii ndio hadi tuiname kuwalamba miguu? Ona sasa tumeinama kuwalamba miguu wanaanza kutushika makalio na hizo statement zao, kinachofuata sasa ni kututia vidole walahi! Duh! kweli viongozi legelege ndio wanatupa serikali legelege!!

tutake tusitake... hata washikaji (type ya akina Musafiri Diof) huwa wanadharaulika!!!

what we hear from this one minister may be a common word from europe na north america.... ukishakuwa ombaomba, kubali kudhalilika
 
Israel wanataka kufungua tena ubalozi hapa Tanzania lakini kama alivyosema Nyerere kwamba Tanzania inatambua taifa la Palestina na ndio msimamo wetu hadi sasa. Mwalimu ndiye alifunga ubalozi wa Israel kwa hivi sasa tunatumia uliopo Nairobi kenya kwa mambo ya kibalozi na Israel.
 
Back
Top Bottom