CHADEMA 2010: Kutoka "Hapa" mpaka "kule"

WAAAT? hapo pekundu inaelekea hujakaa chini na kufikiria. Kwanza kuna transitional period katika govt yeyote.

Katika Tanzania hakuna Transition period hiyo ndefu kama nchi nyingine - Marekani kwa mfano, Uchaguzi hufanyika wiki ya kwanza ya Novemba, lakini Rais anaapishwa Januari 20! karibu miezi mitatu baadaye. Rais wa Tanzania akichatangazwa kashinda anatakiwa aapishwe ndani ya siku 7 (kwani hakuna mahakama inayoweza kuchunguza kuchaguliwa kwake hata kama mnafikiria kuna kura zimeibwa!) na ndani ya siku 14 anatakiwa awe na Waziri Mkuu. Kwa CCM hili ni rahisi sana, kwa chama kipya ambacho hakijawahi kushika madaraka huko nyuma kikishika madaraka kwa mara ya kwanza yafuatayo yatatokea:

a. Rais wake atatakiwa awe na Waziri Mkuu ndani ya siku 14 na Baraza lake
b. Atatakiwa awe na Mawaziri na Manaibu (kama inahitajika)
c. Atatakiwa awe na Mwanasheria Mkuu

Hizi ni nafasi ambazo mtu yeyote anayetaka kuwa Rais anatakiwa awe anazo kichwani kabla ya kutaka kugombea Urais!

Rais mpya anapoapishwa tu, wateule wote wa Rais ambao hufanya kazi kwa ridhaa ya Rais hupoteza nafasi zao (hapa tunaonda wateule ambao wakishateuliwa na Rais, hawezi kuwaondoa kirahisi).

Hivyo Rais mpya atatakiwa aidha kuwaombea mabalozi, wakuu wa mikoa, n.k walioteuliwa na serikali ya CCM waendelee na nafasi zao au wote wajiuzulu ili aweke watu wake. Kama hatokuwa na watu hao tayari option anayobakiwa nayo ni ama awaombe waendelee na nyadhifa zao, au aache nafasi hizo bila kujaza huku akitafuta watu wa kuzijaza. Yote mawili siyo hekima.

Katika kipindi hicho, kuna negotiations kibao zinaendelea katika chama kilichoshinda kuweza kujipanga vizuri. Chadema haihitaji kuja na list ya viongozi wake. Kwani Obama alikuja na list ya viongozi? Si walichaguliwa katika hii transition period. Na kuna wengine waliobaki kutoka serikali ya Bush.
Ni kweli, lakini Obama alijua kabisa anapoingia madarakni nani atamwomba kushika nafasi gani. Wakati anajiandaa kuingia madarakani kulikuwa na negotiation na background checks n.k kwa watu mbalimbali ambao walikuwa washike nafasi mbalimbali za uongozi. Alipoingia madarakani alianza kujaza nafasi za msingi kwa urahisi kwa mfano Ulinzi, Mambo ya Nje, Fedha, Mnadhimu Mkuu n.k Hawa siyo watu aliowatafuta baada ya kuingia madarakani.

Kumbuka a civil servant hatakiwa kuwa na mshikamano wowote na chama chochote. Kwa mfano Mkuu wa Majeshi, IGP
, wakoo wa mikoa, wilaya, etc. Wao ni kufanyia kazi policies za the ruling party. Ama sivyo, uchaguzi ungekuwa ni kazi bure kama kila chama lazima kije na viongozi wote.hahahhaa
Wakuu wa mikoa siyo civil servants, ni political appointees, Rais mpya akiingia wote hupoteza nafasi zao.

This is exactly why naona bado unaumia na CCJ.hahahaha!
well if it suits you.
 
Nimevutiwa sana na hili pendekezo - ni la aina yake:


Kuwatangazia mapema wananchi kuwa endapo watachagua wabunge wengi zaidi wa Chadema (siyo wa upinzani tu!) wananchi watalazimisha serikali ijayo iwe na Waziri Mkuu kutoka Chadema kwani Katiba inasema kuwa Waziri Mkuu atatoka kwenye chama chenye "wabunge wengi" au atakayeonekana "kuungwa mkono na wabunge wengi". Ili kuondoa utata wa nani atakuwa Waziri Mkuu endapo wabunge wengi watatoka Chadema, basi Chadema inapaswa kumtangaza mmoja wa wagombea wake Ubunge kuwa atakuwa ni Waziri Mkuu endapo wananchi watawapigia na kuwachagua wabunge wa Chadema. Kwa maneno mengine, kwa kumtangaza kwa mfano Freeman Mbowe kuwa atakuwa ni Waziri Mkuu na wananchi wakajua mapema kuwa endapo watamchagua Mbunge wa Chadema kwenye jimbo lao basi kura yao ya kumpigia mgombea wa Chadema jimboni itakuwa vile vile ni kura ya kumpigia Mbowe kuwa Waziri Mkuu.



Sheria yetu haikatazi na Katiba haikatazi mahali popote kwa chama kutangaza mapema mgombea wake wa Ubunge ambaye anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu endapo chama chake kitakuwa na wabunge wengi. Chadema isipoteza nafasi hii. Fikiria kuwa wananchi wanajua tayari wana mgombea wa Urais na wanajua nani atakuwa Waziri Mkuu.
  1. Pamoja na hilo la Uwaziri Mkuu, Chadema inaweza kutangaza pasipo woga wowote mtu ambaye endapo watapata wabunge wengi atashika nafasi ya Uspika. Kwa mfano, wakimtangaza kijana Zitto Kabwe kuwa atakuwa ni Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania basi wananchi watajua kuwa kwa kumchagua mgombea wa Chadema jimboni kwao watakuwa wanapiga kura ya kumchagua Waziri Mkuu Mbowe, na Spika Kabwe. Kama kwenye hilo la hapo juu sheria na Katiba yetu havikatazi chama kutangaza wagombea wa nafasi hizo mapema na inaruhusiwa kutumika katika kampeni.
 
Da, sio siri, Chadema ikifanya haya lazima CCM ichanganyikiwe:

Kwa vile sasa wanataka kutawala Uongozi wa Chadema ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa na si zaidi ya miezi miwili iwe imeandaa orodha ya nafasi zote ambazo Rais anatakiwa kuzijaza . Hii ina maana Dr. Slaa anatakiwa ifikapo mwisho wa muda huo mkononi mwake awe na orodha ya nafasi zote za Uwaziri na Unaibu, Ukuu wa Mikoa na Wilaya, Jeshi la Polisi, JWTZ, Usalama wa Taifa, Mashirika ya Serikali, Balozi zote, n.k.

Katika kufanya hivyo, Chadema itajijua kama iko katika nafasi ya kuweza kutawala. Hii ina maana kuwa katika ya majukumu ya kwanza kabisa ambayo Dr. Slaa anatakiwa kuyafanya sasa hivi ni kuteua timu ya watu anaowaamini (wasiwe wagombea wa nafasi nyingine ya uongozi) ili waweze kufanya usaili wa watu mbalimbali ambao watakuwa tayari kufanya kazi chini ya Rais wa Chadema. Endapo kwa namna yoyote timu hiyo
inajikuta inashindwa kujaza nafasi hizo basi ijue kabisa kuwa Chadema bado haijawa katika nafasi ya uwezo wa kutawala.
  1. Dr. Slaa kama mbeba bendera ya Chadema na "Rais Mtarajiwa" ni lazima aanze kuonesha kuwa ni kweli yuko tayari kushika usukani wa uongozi wa taifa letu. Ni tofauti na kuwa Mbunge na msemaji Bungeni na ni jambo jingine kabisa kuwa kiongozi wa watu milioni 40 huku ukiwa na nafasi ya viongozi wa dunia. Kuomba na hatimaye kukubali kufanya yote mawili kunahitaji Dr. Slaa ainue kiwango chake cha kisiasa kwenye ngazi nyingine kabisa. Umakini na usikivu, lugha na mwenendo wa kiongozi tunayemtaka ni lazima iwe ya juu kiasi cha kufanya wengine wote kuona tofauti. Baadhi ya vitu ambavyo ningependa kuviona Dr. Slaa anavifanya mapema ni hivi vifuatavyo:
- Kukutana na watendaji wakuu wa vyombo vya usalama ili kubadilishana mawazo juu ya masuala mbalimbali ya usalama. Si vizuri angojee hadi atakapokuwa Rais aanze kukutana nao. Chadema ihitaji mara moja serikali itoe ulinzi kwa wagombea wote wa Urais hadi pale Rais mpya atakapochaguliwa. Ni wazi kuwa ulinzi huo hauwezi kuwa sawa na ule wa Rais aliyeko madarakani lakini ni muhimu vyombo vya usalama kuhakikisha kuwa wagombea wengine wa Urais wanapatiwa ulinzi mara moja kwa mujibu wa sheria.
  1. Kupanga na kukutana na mabalozi wa nchi za nje wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania. Hii ni katika kujiweka katika mazingira ya kufahamiana na kubadilishana mawazo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu siasa za Tanzania na zile za Kimataifa na mahusiano baina ya Tanzania na nchi hizo. Haitaji kibali cha serikali au baraka zake kufanya hivyo.
  1. Kufanya ziara mahsusi za kutembelea sehemu mbalimbali kuweza kuona na kukutana na watendaji mbalimbali wa serikali na taasisi binafsi. Ziara hizi ni tofauti na mikutano ya kampeni. Kwa mfano, Dr.
  1. Slaa na ujumbe wake waende kukutana na uongogi wa Tanesco au kutembelea taasisi kama hizo. Yote ni katika kumpa mwanga tofauti wa kuelewa masuala mbalimbali ya kitaifa kutoka katika macho ya "mtawala" na siyo "mpinzani". Mwanzoni walipokuwa wanatembelea na kukutana na watu mbalimbali ilikuwa kwa ajili ya kuihoji serikali "Bungeni" sasa hivi kama Rais Mtarajiwa, lengo ni kuweza kuona nini cha kufanya akiindia madarakani.
  2. Kwa ufupi ni kuwa hatutaki kuwa na Rais mwingine atakayetumia miaka miwili "kujifunza" na miaka mitatu kuandaa utaratibu wa utekelezaji na miaka mingine mitano ya kuanza "mchakato". Tunataka kiongozi ambaye "yuko tayari kuongoza" siku ya kwanza akiingia madarakani siyo akiingia ndio aanze kujiuliza "nitaongoza vipi".
 
Companero,
Mkuu nakubaliana sana na mchango wako lakini kuna kitu hapa sisi tunashindwa kukielewa. Tusiwa underestimate sana Chadema na uwezo wa Dr. Slaa kwani hadi kufikia hapa haikuwa furuku..

Chadema kama chama tayari wamekwisha yatazama maeneo mengi sana tofauti na dhana zetu. Mimi nafikiri maswali mengi yanakuja kutokana na kwanza Dr.Slaa amechaguliwa muda mfupi kufikia Uchaguzi pasipo sisi kuelewa kwamba pengine ilikuwa ni janja ya Chadema all the time kusubiri wakati Muafaka. Hivyo, sii kwa kubahatisha Dr.Slaa amechaguliwa isipokuwa kwa kuzingatia mbinu za CCM na hali halisi ya siasa za Tanzania.

Ikumbukwe tu kwamba Tanzania ina watu millioni 40 na sii swala la ugumu wa Dr.Slaa kuongoza watu hawa ila tufikirie urahisi wa Dr.Slaa kupata viongozi makini toka hesabu hiyo hiyo. Wakuu zangu, kikubwa zaidi tuzungumzie watu millioni 40 kuwa nyuma ya Dr, hivyo kujaribu kukana uwezo wa Chadema ni sawa na kukubali kwamba hatuna watu wenye uwezo wa kuongoza toka hesabu ya watu milioni 40 isipokuwa wale waliopo ndani ya chama CCM.

Tukumbuke tu kwamba tupo ktk wakati wa mageuzi na ktk hali hii tusifikirie uongozi kwa mfumo wa CCM chama tawala hivyo kudhania hakuna mfumo au njia nyingine bora ya kiutawala. Nina hakika wapo watu wengi sana wanaoweza kabisa kuziendesha wizara, idara na taasisi zote za serikali pasipo kufikiria tena CCM na tukasonga mbele.

Ujio wa Dr.Slaa ni tumaini jipya na hakika kampeni zake lazima ziwe zenye mvuto mkubwa sana na zijengwe kulingana na mategemeo ya wananchi kama JK alivyoweza kuitumia nafasi hiyo mwaka 2005. Dr. anajua fika wapi panawagusa wananchi, anajua fika wapi macho ya walalahoi yameelekea na wanategemea picha nzima itakuwa na actions zipi..Tuzidi kumpa moyo, nguvu na matumaini kwamba hata yeye anaweza kututegemea ktk kulisukuma hili gurudumu la mageuzi.
 
nataka kujua watacompromise vipi ratiba ya wagombea nafasi za ubunge kama Zitto na Mbowe ili waweze kushiriki kwenye mikutano ya kampein ya Dr. Slaa?
 
mkjj
huwezi kushinda urais au ubunge kwa kutumia speeches za kwenye majukwaa tu, lazima uwe na management ya kumobilize watu, kukusaidia kwenye policy nk (kwa kifupi good campaign team). Inahitaji organisation ya hali ya juu ili kushinda uchaguzi. Baada ya ushindi hii campaign team inageuka kuwa viongozi na sio kuendelea kuwa campaign team.
kwa hiyo sasa hivi wakati wa campaign ni nafasi ya mwisho ya dr slaa kujua tabia/sifa za watu(campaign team) ambao atafanya nao kazi baada ya uchaguzi, na hii itamsaidia kujua nani awe mshauri wake ikulu nani waziri nk.

kama chadema inaweza ku-organise management ya ushindi basi chadema inaweza ku-organise management ya nchi.

do not underestmate the strength and depth of chadema....

dr slaa usifanye kosa la kutaja uongozi wako kwa sasa, kwa ajili ukitaja uongozi wako watu wengine wataona wao hawawezi kupata chochote na wata punguza ushirikiano au msaada watakao kupa. Pili utatengeneza matabaka ya wale ambao wanajiona wao watakuwa mawaziri against wale ambao hawata pata kitu.
 
mkjj
huwezi kushinda urais au ubunge kwa kutumia speeches za kwenye majukwaa tu, lazima uwe na management ya kumobilize watu, kukusaidia kwenye policy nk (kwa kifupi good campaign team). Inahitaji organisation ya hali ya juu ili kushinda uchaguzi. Baada ya ushindi hii campaign team inageuka kuwa viongozi na sio kuendelea kuwa campaign team.
kwa hiyo sasa hivi wakati wa campaign ni nafasi ya mwisho ya dr slaa kujua tabia/sifa za watu(campaign team) ambao atafanya nao kazi baada ya uchaguzi, na hii itamsaidia kujua nani awe mshauri wake ikulu nani waziri nk.

kama chadema inaweza ku-organise management ya ushindi basi chadema inaweza ku-organise management ya nchi.

do not underestmate the strength and depth of chadema....

dr slaa usifanye kosa la kutaja uongozi wako kwa sasa, kwa ajili ukitaja uongozi wako watu wengine wataona wao hawawezi kupata chochote na wata punguza ushirikiano au msaada watakao kupa. Pili utatengeneza matabaka ya wale ambao wanajiona wao watakuwa mawaziri against wale ambao hawata pata kitu.
Ni makosa makubwa kwa Dr.Slaa kutangaza jina au majina ya viongozi wake kwa sababu nyingi za kisiasa na kimsingi. Na kibaya zaidi inaonyesha wazi itkadi,sera na ilani hazitoshi kuwashawishi wananchi, jambo ambalo mzee Mwanakijiji narudi kuamini maneno yetu kwamba Itikadi haziwezi kuleta ushindi isipokuwa SABABU, NIA na UMOJA wetu kujenga uwezo. Nina hakika kabisa kwa hesabu kubwa ya population yetu Chadema wana kila uwezo wa kuiongoza nchi kwa urahisi zaidi kuliko Mwalimu Nyerere aliyekuwa na wasomi wasiozidi 10....
 
Kutaja au kuto taja yote yana faida na hasara zake. Ingekuwa ni vizuri kama tungeweza kuchambua kabla ya kufika conclusion kuwa haifai kabisa. Kwa mfano cioncern ya voters ikiwa kuwa wanaona Chadema hawawezi kuunda serikali strong basi kutaja itakuwa ni ku taka ku win hao voters. Muda wa kuleta visasi umekwisha hapa ni kupereka gurudumu mbele
 
simaanishi Slaa ataje watumishi wote atakaokuwa nao.. nimesema awe na orodha binafsi ya uongozi atakoujaza, siyo autaje! Sidhani kama nimetumia neno kuwa 'ataje'.. naomba msome vizuri. Nafasi pekee ambazo nimesema zinatakiwa zitaje ni ya Uwaziri Mkuu na Uspika. It is very strategically revolutionary.
 
sasa itapendeza kabla ya uchaguzi uje na uchambuzi mwingine wenye Title ya CCM. " Kutoka 1961 mpaka 2010."

kwa kweli ni uchambuzi mzuri lakini kwa faida ya wananchi wote wanaotaka mabadiliko watafurahi kama ukitoa uchambuzi kama huu unaohusu CCM.
 
MMKJ unatugawa? Kwa nini unataka watu waanze kuwaza sana sasa ni vyeo gani watapata?

Kibaki na wenzake walipoing'oa KANU walitumia mbinu unazotaka hapa?

Kama alivyosema Semilong, ni kwenye kampeni ndiko kutatoa sehemu muhimu ya viongozi wa kisiasa.

Dr Slaa hatakuwa na shida yoyote kupata Wakuu wa Mikoa na Makatibu Wakuu. Watanzania wenye uwezo wa kazi hizo ni wengi (ni pamoja na wewe) na washauri wa kupendekeza majina kwa Slaa wako wengi pia.

Mie nadhani kwa sasa tuzungumzie zaidi namna ya kuing'oa CCM. Kutawala haitakuwa shida. TANU ilianza kutawala bila hata kuwa na wananchi waliosoma.

Naona unasema ungeingia kwenye viongozi wa CHADEMA ungewaumiza sana. Una lengo gani? Ni la kujenga kweli?

Inawezekana, timiza wajibu wako. Tuko tayari.
 
Kitu kingine ambacho Dr. Slaa na timu yake wanaweza ku-release kwa wananchi kw ajaili ya Campaign ni idadi ya Wizara na Mawaziri.......zisizidi 20...............na ninapendekeza kama ifuatavyo

Ministry of Finance and Public Service
Ministry of Foreign Affairs (includes EA portfolio)
Ministry of Education, Science and Technology
Ministry of Health
Ministry of Legal Affairs
Ministry of Housing, Lands and Surveys
Ministry of Agriculture, Livestock and Marine Resources
Ministry of Labour and Social Development
Ministry of National Security and Immigration (Polisi, Jeshi, TAKUKURU, UwT, Magereza na Uhamiaji)
Ministry of Public Works and Transport
Ministry of the Environment, Minerals and Water Resources
Ministry of Tourism
Ministry of Information,Youths, Sports and Culture
Ministry of Trade and Industry
Ministry of Local Governments
Ministry of Aviation and Telecommunication
 
simaanishi Slaa ataje watumishi wote atakaokuwa nao.. nimesema awe na orodha binafsi ya uongozi atakoujaza, siyo autaje! Sidhani kama nimetumia neno kuwa 'ataje'.. naomba msome vizuri. Nafasi pekee ambazo nimesema zinatakiwa zitaje ni ya Uwaziri Mkuu na Uspika. It is very strategically revolutionary.

waziri mkuu si mpaka uwe mmbunge

pili spika si anapigiwa kura bungeni, hii itatokana na idadi ya wabunge waliokuwa nao kama itawawezesha kushinda nafasi ya uspika bila kushirikiana na chama chochote au la. kama itabidi washirikiane na chama kingine ili washinde then itabidi wakubaliane jina la mgombea. hizi position zote zinategemeana na event za uchaguzi. Dr slaa atakuwa na majina kichwani mwake lakini sasa concentration ni kushinda uchaguzi first.
kwa urais , kutaja mgombea mwenza inatosha......

sasa hivi dr slaa tunataka kusikia slogan logo mbiu ya uchaguzi wa 2010.

SLOGAN yangu: "CHAGUA SLAA YA MAENDELEO, CHAGUA CHADEMA. 2010"

ATTACK: "MIAKA 49 YA CCM BILA MAENDELEO INATOSHA, CHAGUA MAENDELEO
CHAGUA CHADEMA"
 
Kuna point MWanakijiji kaiweka nadhani inahitaji kufikiriwa kwa makini, Japokuwa CHADEMA watakuwa na sera za kichama, lakini ni kitu cha muhimu sana Mgombea say Dr Slaa awe na sera zake binafsi ambazo zitauzika kirahisi kwa wananchi, ukiangalia hotuba ya JK pale bungeni alielezea maendeleo ya Taifa hili ambayo hayamgusi mwananchi kabisa, CHADEMA INAPOSIMAMA NA KUSEMA INAPAMBANA NA UFISADI kwa mwananchi wa kawaida hiyo anaiona ni high level na haimuhusu kwa sababu anajiringanisha yeye na mtu kama Chenge au Rostam, mtu anayepata chini ya dola moja kwa siku unamwelezea kuwa chenge ana billions ambazo kwakwe ni visenti tu, kwa mtu wa kawaida inakuwa ni vigumu kujua link kati ya fedha za ufisadi na maendeleo yake

maana ya kusema mgombea angalau awe na sera zake binafsi hiyo itakuwa na faida pale mgombea anapotoka eneo moja kwenda lingine, matatizo ya Tanzania hayafanani, kama sera ya Chadema ni kuzungumzia elimu kwa wote, hiyo sera inaweza kuuzika kwenye baadhi ya mikoa lakini kwa mikoa kama Kilimanjaro hiyo sio sera, hiyo habari ya elimu na mambo ya shule za kata kwao ilikuwa ni kampeni ya 80's,

JK alishinda kwa kishindo kwa mambo machache sana lakini kubwa lilikuwa "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA", HIYO SLOGAN iliuzika kwa kila raia, ilienda deep mpaka kwa mlalahoi wa kawaida kabisa na hiyo kauli ilikuwa na hope ndani yake na watu walijiridhisha kwamba sasa wamepata mkombozi wa kweli,

SIJAJUA HASA SERA ZA CHADEMA KATIKA KAMPENI HII ZIKOJE LAKINI KWA WANANCHI WENYE UELEWA MKUBWA HASA WAMIJINI NADHANI PIA MNATAKIWA KUJA NA CLITICAL POINTS AMBAZO ZITAKUWA NA MATUMAINI MAKUU, NA KUBWA KABISA LAZIMA MUWE WAZI CHANGES ZENU ZITAANZIA WAPI KAMA MKICHUKUA NCHI,

Dr Slaa na Wenzio mlio kwenye kamati ya kampeni kwa ushauri wangu hebu jaribuni sana kukazania mabadiliko makubwa kwenye wizara Mama, AMBAYO KWA MIMI NI WIZARA YA SHERIA NA MAMBO YA KATIBA, JARIBUNI KUTENGEZA HOJA AMBAZO ZITAUZIKA, KWA MIMI SIWEZI KUONA MABADILIKO YA HII NCHI KAMA HII WIZARA HAITAFANYA KAZI YAKE SAWSAWA, WATU WANA KESI ZA KUJIBU LAKINI KWA SABABU HII WIZARA HAIFANYI KAZI HAKUNA KINACHOENDELEA, RUSHWA,MAUHAJI, KUTOKUJITUMA, MIKATABA MIBOVU, DEMOKRASIA NA MENGINE MENGI HAYAENDI KWA SABABU YA HII WIZARA, HEBU JARIBUNI KUTAFUTA WATAALALUMU NA KUITENGENEZEA SERA ZITAKAZO KUBALIKA
 
SLOGAN yangu: "CHAGUA SLAA YA MAENDELEO, CHAGUA CHADEMA. 2010"

...............

Ina-sound kinyume to me.................it may well sound as "Silaha ya maendeleo".........unajua tena kuna wengine badala ya kusema "silaha" hutamka "slaa"...............
 
waziri mkuu si mpaka uwe mmbunge

pili spika si anapigiwa kura bungeni, hii itatokana na idadi ya wabunge waliokuwa nao kama itawawezesha kushinda nafasi ya uspika bila kushirikiana na chama chochote au la. kama itabidi washirikiane na chama kingine ili washinde then itabidi wakubaliane jina la mgombea. hizi position zote zinategemeana na event za uchaguzi. Dr slaa atakuwa na majina kichwani mwake lakini sasa concentration ni kushinda uchaguzi first.

Semilong.. umepata point lakini umeimiss wakati huo huo. Huoni kuwa kama wananchi wakijua kwa kuchagua mbunge wa Chadema jimboni kwao wataiongozea Chadema wabunge wengi ili iweze kutoka Spika na Waziri Mkuu? Huoni kama wananchi wakijua kuwa x na y ndio watakuwa waziri mkuu na Spika kutoka chadema watapata motisha zaidi wa kumchagua mbunge wa chadema ili hilo litimie. Kumbe kampeni ya kitaifa tunaibadilisha kabisa kutoka the traditional ya Rais tu kitaifa na kuwa kura ya Rais, Waziri Mkuu na Spika? This is a strategic maneuver.
kwa urais , kutaja mgombea mwenza inatosha......

sasa hivi dr slaa tunataka kusikia slogan logo mbiu ya uchaguzi wa 2010.

Haitoshi.. siyo logo tu inayoshinda uchaguzi na mikakati vile vile. you have to think outside the box.

SLOGAN yangu: "CHAGUA SLAA YA MAENDELEO, CHAGUA CHADEMA. 2010"

ATTACK: "MIAKA 49 YA CCM BILA MAENDELEO INATOSHA, CHAGUA MAENDELEO
CHAGUA CHADEMA"

Uchaguzi huu ni zaidi ya kuchagua slogan inayosikika vizuri. Kama kweli tunataka kubadilisha uongozi wa taifa, basi uchaguzi ni utawala wa taifa.
 
Nimesoma mengi humu.

Moderators: Kwa kuwa kuna kifufe cha kubofya cha THANKS nashauri kiwepo pia kitufe cha SHAME ili tupate sehemu ya kuonyesha kusikitishwa kwetu na hoja legelege.
 
kusema ukweli kazi ya kushawishi inahitajika kwa sana kwani wengi hawaelewei......umuhimu wa haya mabadiliko..................nimeanza kazi ya kuelimisha........kuanza na closest people.........nina hakika kila mmoja wetu akifanya hii kazi mabadiliko.....ni ya kwetu..............

............binafsi nimeshaanza kampeni.................tayari nina uhakika wa watu makini (toka CCM) wanne kuwa watampigia kura Dr. Slaa na watashawishi wengine kutumia influence yao ili kumpigia kura Dr. Slaa................na kazi iendelee
 
Kuhusu ushauri wa magwanda, kwa kawaida Rais Mtarajiwa, Dakta Slaa, huwa hayavai. Ila kwenye ile picha ya kikao kilichomchagua agombee nimeona kama ameyavaa vile. Nakubaliana na Mwanakijiji kuwa inabidi sasa aanze kuvaa kama Rais, kuongea kama Rais, kutembea kama Rais, na kuongoza kama Rais. Akiweza kutumia mbinu hii hakika ataishangaza Tanzania kama Obama alivyoishangaza Marekani. Je, atafanya hivyo?
 
Kuhusu ushauri wa magwanda, kwa kawaida Rais Mtarajiwa, Dakta Slaa, huwa hayavai. Ila kwenye ile picha ya kikao kilichomchagua agombee nimeona kama ameyavaa vile. Nakubaliana na Mwanakijiji kuwa inabidi sasa aanze kuvaa kama Rais, kuongea kama Rais, kutembea kama Rais, na kuongoza kama Rais. Akiweza kutumia mbinu hii hakika ataishangaza Tanzania kama Obama alivyoishangaza Marekani. Je, atafanya hivyo?

.........mwaka huu ni muhimu kuamua mustakabali w aTaifa letu..............this is an opportunity........kila mmoja wetu afanye atakalo weza kusaidia kuleta mabadiliko...............Dr. Slaa peke yake hatoweza...................
 
Back
Top Bottom