Imenishangaza sana hii. Kuna mama mmoja anamiliki mini-supermarket moja hapa A town alitupatia tenda ya kumwekea CCTV kwenye biashara yake. Watu wa installation walifanya kwenye angles walizochagua, sisi tulimwekea software kwenye computer yake ofisini ya kumwezesha kufanya monitoring, surveillance na reviews muda wowote anaotaka. Actually anaweza aka-copy footage za siku hiyo kwenye laptop na kwenda kuzi-review nyumbani kwa muda wake. Mama kaipenda sana, akatuita pembeni akasema anataka tukamfanyie huduma kama hiyo nyumbani kwake. Cha kushangaza, mojawapo ya sehemu alikotaka ifungwe CCTV camera ni chumba cha housegirl wake. Bedrooms zingine zote hajaweka, ni hiyo ya house girl tu. Hii imekaaje wadau.