CCM na CHADEMA sasa turudi kujadili solutions za issues muhimu kwa taifa letu!

Hata ccm ipewe miaka hamsini tena kutawala hatutaona maendeleo yeyote sanasana tutajikuta na wananchi tumetaifishwa, broda mbona mgumu kuelewa?, hata picha huoni



@ facebook:by william malecela on monday, may 23, 2011 at 4:11am


- mjadala wa suala la ukabila na udini ni mjadala ambao umeshapittwa na wakati. Sioni sababu kwanini baadhi ya viongozi wa ccm bado wanatumia karata hiyo linapokuja suala la chadema. Hatari yake ni kuwa jambo hili litafanya chama chetu kionekane kinawagawa watanzania kwa misingi ya dini, kabila na hata rangi vitu ambavyo ni vigeni kabisa ndani ya ccm.
Ccm ni chama ambacho kinahitaji wakati huu kuliko wakati mwingine wowote ule kuonesha uongozi katika kujadili issue na siyo watu. Kwa kuanza kujadili watu ccm kimejiingiza kwenye mtego ambao ni vigumu sana kutoka na ni mtego ambao mwisho tutajikuta tunanasa sisi wenyewe. Sasa turudi kwenye issue muhimu za taifa.

- kuna masuala mengi ambayo watanzania tunataka kuona tofauti katika maisha yetu na yanayohitaji majibu kutoka chama tawala. Tulienda kwenye uchaguzi na kuomba kura za watanzania ili tuwaongoze kwa miaka mitano ijayo na hilo ndilo tunatakiwa kufanya siyo kujitetea kila kukicha au kulalamikia upinzani. Kama tutawapatia watanzania uongozi wakati huu basi hoja nyingi za upinzani zitakufa zenyewe. Lakini tukisikia tena mambo ya chadema chama cha wachagga au cha wakristu kutoka viongozi wa ccm tutakuwa tunakaribisha mgawanyiko mkubwa kati ya wananchi. Ccm iachane na hoja hizi za udini na ukabila na iwe mwepesi kujitenga nazo wala isizilee au kuhusishwa nazo kabisa. Siasa za udini na ukabila zimepitwa na wakati twende kwenye siasa za issue:


yapo masuala ya:

utawala bora
elimu
utawala wa sheria
nishati
katiba mpya
n.k

- viongozi wetu wa ccm na chadema, mtaanza lini kuzungumzia haya badala ya kuhangaika na mambo ya ccj na siasa za chama cha wachagga? Hebu turudi sasa kwenye issues muhimu kwa taifa letu, kama hamuwezi jivueni magamba tuanze upya!


mungu ibariki tanzania!


william malecela.
 
......... Kwa kuanza kujadili watu CCM kimejiingiza kwenye mtego ambao ni vigumu sana kutoka na ni mtego ambao mwisho tutajikuta tunanasa sisi wenyewe. Sasa turudi kwenye issue muhimu za taifa.

- Kuna masuala mengi ambayo Watanzania tunataka kuona tofauti katika maisha yetu na yanayohitaji majibu kutoka Chama Tawala. Tulienda kwenye uchaguzi na kuomba kura za Watanzania ili tuwaongoze kwa miaka mitano ijayo na hilo ndilo tunatakiwa kufanya siyo kujitetea kila kukicha au kulalamikia upinzani...............

WJM,

Unachokiongea hapo juu ni ukweli ptupu shida iliyopo hakuna atakaekusikia ndani ya chama chako.
CCM imetumia kete ya ukabila na udini toka 1995 wakiwaita NCCR wachagga sababu ya Mrema, tukaonyeshwa ITV mauaji ya Rwanda huku CUF wakiwa branded chama cha waislam na tukaonyeshwa visu vya kukatia nyanya (kitchen knives) na Bw. Mahita kwamba CUF wamejipanga kumwaga damu.
Wanasema mazoea hujenga tabia na ndio kusema hii imekuwa mbinu ya chama chako bila kujali kwamba imepitwa na wakati.

Majuzi pale Dodoma mpebadilisha timu lakini tofauti na wafanyavyo kina Barcelona ama Manchester, timu yenu imetoa wachezaji waliochoka mkaingiza waliochoka zaidi in the likes of Nnauye Jr. hii ni kuonyesha kuwa hapakuwa na substitution ya maana/kutosha kwenye benchi la ufundi.
Mwanzo nilidhani tatizo ni wazee wa CCM lakini inapofika hata kina Nape, January, Beno, L. Masha n.k hawajaweza kutoa japo matumaini kwamba CHANGE is coming ndipo naona kama unampigia mbuzi gitaa.

Ushauri uliotoa kwa Chadema nadhani utafanyiwa kazi maana mengi ya wanayoshauriwa wamekuwa wakifanyia kazi. Tuwawahi Chadema kabla hawajatumbukia kwenye uchafu ambao CCM iliufanyia mzaha na sasa kupona ni kwa kudra za Mungu tu. Wanasema "samaki mkunje angali mbichi", chama chako ni sawa na samaki aliyekauka tayari je utamkunja na asikatike??.

Kwenye ndondi kocha akiona bondia wake amezidiwa hutupa taulo uringoni ili kumwokoa na dhahama and would advise the same to CCM "throw in the towel" mkajipange upya inshallah Mungu atawajalia vijana kama wewe kukifanyia mageuzi chama. Huwezi ukafanya matengenezo makubwa huku gari ikitembea kama ambavyo CCM inajaribu kufanya, peleka gari gereji ili mfumo mzima uwe-overhauled.

Kiongozi WJM umesema kweli tatizo ni ukweli uliochelewa!
 
..........

Yapo masuala ya:

Utawala bora
Elimu
Utawala wa Sheria
Nishati
Katiba Mpya
n.k


Kama hutaji UFISADI basi unoajaribu kuwakumbusha na wewe hamna tofauti. wanajificha kwenye vivuli vyao. Hutakiwi kusahu neno UFISADI kama moja ya issue kuu
 
uuh hiki kijamaa wiliamu kinatafuta umaarufu kwa udi na uvumba......

 
Ndugu William, your beloved CCM is in big trouble. Kwanza wao wenyewe hawaelewani, kila siku ni vituko. Arusha hawamtaki katibu, Dar wamemkataza Azan(mwakilishi wa watu) asiongee na Media miezi 18, Hai wanatimuana, Katibu mkuu anazomewa, kuvua Gamba Sita na Lembeli wanadai kuchezewa rafu!! Everywhere you look at it's total chaos.

Unasema ni muda mwafaka wa CCM kuonyesha uongozi, brother wao wenyewe wanashindwa kujiongoza watamwongoza nani?

Personally I've lost hope with the government and their party. Unless something dramatic happens, not this fake "Skin Shedding", ninasubiri anothep party.
 
uuh hiki kijamaa wiliamu kinatafuta umaarufu kwa udi na uvumba......


ndo mana nikamuuliza nae anataka kuja kutuongoza kama watoto wa waliokuwa viongozi wengine? Maana naona juhudi zake utadhani Tz ina watu 20 tu, hv mtaacha lini huo ufalme wenu, mnadhani mnabusara kuliko watanzania wote! Tumechoka na majina yenu ala!
 
Kama hutaji UFISADI basi unoajaribu kuwakumbusha na wewe hamna tofauti. wanajificha kwenye vivuli vyao. Hutakiwi kusahu neno UFISADI kama moja ya issue kuu

Ufisadi tena? si utawagusa baba,mama, wa kambo na marafiki wote! no! huo tuuache ili tujadili mambo muhimu. Kweli @NYC unaleta utani kwenye kila jambo. Mwambie mzee malecela atubu kwa zambi yake ya kuhusika kwenye EPA na arudishe mchango wa harusi wa 200m kwa patel, hapo ingalau tutaanza kuelewa na U turn yako.

Yaani wewe unavinjari hapo NYC hujui ni kwa sababu wenzio waliokuwa na baba wezi wa mali za umaa waliamua kuweka maslahi ya taifa mbele na kuwakana na kuwawajibisha, leo USA ni nchi tajiri duniani. Lakini wewe ni kukumbatia wezi kisa ni baba na kuleta hizo porojo hapo juu. Unajua kwa nini Ghana ipo hapo ilipo we ngoja tu!
 
watanzania wamegeuzwa omba-omba. mzee mzima kaacha familia yake kwenda kuomba-omba khanga na vitenge kwa mgeni wa kijiji nape. na amewaagiza wanafamilia wamuombee kwa Mungu apate khanga, kitenge, kofia au fulana.

then William yupo NEWYORK huko anadai kuwa watanzania sio wajinga tena, wewe si mtoto wa mkubwa? watu huku tunataabika bana!! hata JF kuna watu hawajui ni kitu gani computer yenyewe hawajawahi kuiona , elimu hatuwapi tunasaini mikataba mibovu haiwanufaishi , na hawajui kuwa ni haki hao kuwa na maisha bora kama kina william wanaona kuwa lile life linavyowapiga kule kijijini ni haki yao.
 
laptop yangu inanipa alarm hapa kutoka kisutu kuwa maranda na farijala wamefungwa jela miaka 22......ngoja nifatilie nijue

back tio topic
 
- Mchungaji sisi Wa-Tanzania sio wajinga wala mabwege tena, tungekuwa Chadema wasingekuwepo the fact kwamba wapo kwa mujibu wa katiba ya jamhuri na tunawalipa kodi yetu kwa ajili ya ruzuku kila mwezi ni ukweli ulio wazi kwamba Wa-Tanzania sio wajinga tena!

William @ NYC, USA.

Na kweli watanzania siyo wajinga tena. Ndiyo sababu wale waliozoea kutumia mtaji wa ujinga wanapwaya. Hadithi za ukabila na udini zitachukua nafasi tu kwa CCM. Hawakujiandaa kuona watanzania wenye uelewa kama huu.
Mfano: miaka ya 2005-- huko Ukerewe Mwanza kijana wa kidato cha pili alimuuliza Lowassa kwanini serikali inalimbikiza madaraka kwa watu wachache kama vile mkuu wa mkoa/mbunge/mwenyekiti wa bodi mbalimbali hakujibu lakini baada ya ziara Afisa usalama wa Wilaya na wengine walibaki kumfuatilia na kumshughulikia huyu mtoto.

Yako mengi sana yanayoonyesha serikali haijajiandaa kutambua uelewa wa wananchi
Elimu ya uraia inayotolewa na CDM itawaamsha zaidi ili waweze kuchambua na kufanya uchaguzi sahihi kwa matakwa yao.
Jambo muhimu ni KUJIANDAA KUONA UELEWA WA WANANCHI UNAKUA. KUONA KUPEWA CHANGAMOTO SIO USALITI AU UHAINI NA KUKUBALI NA KUTEKELEZA AHADI WALIZOTOA WAKATI WA USANII UMEKWISHA.
 
hilo nipo na wewe bw wiliam lakini naomba ulijibu hili.
je viongozi walioiba hela za uma wakaenda kuficha ulaya na marekani na baba yako akiwa ni mtuhumiwa wewe unasemaje?
 
@ facebook:by william malecela on monday, may 23, 2011 at 4:11am

- mjadala wa suala la ukabila na udini ni mjadala ambao umeshapittwa na wakati. Sioni sababu kwanini baadhi ya viongozi wa ccm bado wanatumia karata hiyo linapokuja suala la chadema. Hatari yake ni kuwa jambo hili litafanya chama chetu kionekane kinawagawa watanzania kwa misingi ya dini, kabila na hata rangi vitu ambavyo ni vigeni kabisa ndani ya ccm.

Ccm ni chama ambacho kinahitaji wakati huu kuliko wakati mwingine wowote ule kuonesha uongozi katika kujadili issue na siyo watu. Kwa kuanza kujadili watu ccm kimejiingiza kwenye mtego ambao ni vigumu sana kutoka na ni mtego ambao mwisho tutajikuta tunanasa sisi wenyewe. Sasa turudi kwenye issue muhimu za taifa.

- kuna masuala mengi ambayo watanzania tunataka kuona tofauti katika maisha yetu na yanayohitaji majibu kutoka chama tawala. Tulienda kwenye uchaguzi na kuomba kura za watanzania ili tuwaongoze kwa miaka mitano ijayo na hilo ndilo tunatakiwa kufanya siyo kujitetea kila kukicha au kulalamikia upinzani. Kama tutawapatia watanzania uongozi wakati huu basi hoja nyingi za upinzani zitakufa zenyewe. Lakini tukisikia tena mambo ya chadema chama cha wachagga au cha wakristu kutoka viongozi wa ccm tutakuwa tunakaribisha mgawanyiko mkubwa kati ya wananchi. Ccm iachane na hoja hizi za udini na ukabila na iwe mwepesi kujitenga nazo wala isizilee au kuhusishwa nazo kabisa. Siasa za udini na ukabila zimepitwa na wakati twende kwenye siasa za issue:


yapo masuala ya:

utawala bora
elimu
utawala wa sheria
nishati
katiba mpya
n.k

- viongozi wetu wa ccm na chadema, mtaanza lini kuzungumzia haya badala ya kuhangaika na mambo ya ccj na siasa za chama cha wachagga? Hebu turudi sasa kwenye issues muhimu kwa taifa letu, kama hamuwezi jivueni magamba tuanze upya!


mungu ibariki tanzania!


william malecela.


kaka willy ,
kwanza nashukuru kwa ushauri wako, pili nauchukua na nitaufanyia kazi. Karibu tena wakati mwingine.
 
Mkuu WJM,

Agenda kubwa ni kuitoa CCM madarakani ambayo imeshindwa kuongoza na kuleta maendeleo. Miaka karibu ya 50 sasa tangia tumepata uhuru, ajabu hatuna cha kujivunia Kama taifa. CHADEMA wanafanya Kila kiwezekanacho wanainchi wajue uraia. Porojo za amani na utulivu wakati serikali haiweki miundo mbinu hazina nafasi tena. Ufisadi na wizi wa Mali ya umma ufikie mwisho. adui nambari moja wa Watanzania ni CCM ambacho mtaji wake ni ujinga wa Watanzania wenyewe.

Hoja hii inaweza kuwa na mantiki kama wale amabo wanapambana kuing'oa serikali wanasema watafanya nini katika matatizo yanayolikabili Taifa. Matatizo ya umasikini si nani alikuwa CCJ au siasa za maji taka. Yapo mengi ambayo yakizungumzwa wananchi wanaweza kujenga imani kuwa kuna nia ya dhati katika kulipeleka Taifa mbele. Kuna matatizo ndio kila mtu anakubali, mbona watu hawasemi mbadala? Elimu yetu ipo ICU, kilimo ndio kabisa, wafanyakazi wezi, wengine wavivu nk.

Sasa suluhu ni kukaa na kusema tunakung'oa bila kusema nini kitafuata. Hapa ndio lilipo tatizo, watu wanahitaji kusikia maisha baada ya CCM maana ya maisha ndani ya CCM yanafahamika tayari. CCM sasa hivi wanasema tutafanya hivi, CDM wao wanakazana na mabomu. Nadhani Watanzania yapo wanayohitaji zaidi ya mabomu.
 
Mawazo ni mazuri, sina shaka kwa CDM ila Je vp chama chako wako tayali kuchukua mawazo yako na kuyafanyia kazi.
Si unajua tena Chama Cha Mipasho wako tayali kumjadili mtu kwa gharama yoyote ile na si kujadili suala la maendeleo
 
kaka willy ,
kwanza nashukuru kwa ushauri wako, pili nauchukua na nitaufanyia kazi. Karibu tena wakati mwingine.
Nape kuna thread kule uliianzisha then ukatuacha kwenye mataa, tunajua una majukumu mengi ila ukipata muda usisite kutuibukia , tunafarijika kwa uwepo wako hapa kwani sisi adui yetu ni mmoja umaskini ujinga masifadi , haya mambo mengine matusi ya nguo, tuhuma na vikorombwezo vingine ni mbwembwe tu
 
kaka willy ,
kwanza nashukuru kwa ushauri wako, pili nauchukua na nitaufanyia kazi. Karibu tena wakati mwingine.

Pata washauri na kabla hujaongea fikiria kidogo wewe NAPE! Zile siku tisini za Magamba ni aje? Na ile Kauli ya Wachagga na CHADEMA hujasikika ukikanusha, kwa maana hiyo bado ina simama!
 
Back
Top Bottom