dudus
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 22,141
- 49,410
Basi jirani akiita tokomile kwenye harusi ya mwanaye nasisi tuite vanga tucheze wakati hatuna harusi? CCM sio vichaa Siku tukipata sababu ya kufanya maandamo tutaandamana bila wasiwasi wowote, maandamo pekee hayatatua matatizo ya nchi yetu, tunatafakari njia sahihi.
Tafakuri gani ya miaka 50! Tena hata baada ya muda wote huo Mkuu anasema hajui chanzo cha umaskini wetu! Tatizo kuu la CCM, hasa ya miaka hii, ni UONGO, GHILIBA, na PROPAGANDA ZA KIZUSHI; silaha ambazo kwa kweli hazitakifikisha chama mahali popote tena kwa hasara ya taifa.
Laiti CCM ingeukubali ukweli kama ulivyo na kuchukua hatua lakini hili ndani ya chama hiki, kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ni vigumu kufikiwa angalau kwa kizazi hiki. Hata hivyo, uzuri ni kwamba kushindana na UKWELI ni kama kupiga ngumi ukutani.