MTENDAHAKI
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 4,013
- 1,443
Pamoja na vuguvugu la nguvu mpya linaloonyeshwa na chadema, cuf na nccr mageuzi ni wazi kuwa chama tawala ccm kina nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi wa urais wa mwaka 2015.
Hata hivyo chadema ina nafasi kubwa sana ya kuwa na wabunge wengi kuliko ccm, hali hii inaifanya cdm kuwa chama cha pili ambacho kinaweza kushika dola!nafasi kubwa ya kushinda urais bado inabaki kwa ccm kwani chama hiki kina watu mahiri wengi wanaokubalika sana kwa wananchi kuliko chadema ambayo ina watu wachache mahiri wanaoweza kugombe kwa nafasi hiyo na kukubalika!
Yawezekana ccm ikaonekana kama imepoteza muelekeo lakini vipi ikiwa mh. Dr. John pombe magufuli akisimamishwa kugombea urais kwa tiketi ya ccm ni nani kutoka upinzani anaeweza kumzuia?kwa tathmini tuliyofanya inaonyesha magufuli ni mgombea wa kufikirika wa ccm anaeweza kukiokoa kisipoteze uongozi wa nchi.
Ndiye mtu pekee mwenye nguvu kwa wananchi ambaye anaonekana kutokuwa na kundi linaloeweka ndani ya ccm, lakini zaidi ni kuwa wananchi wanamuona kama mtu anaeweza kusimamia sheria bila upendeleo. Kama akigombea na kupitishwa ni wazi kuwa ccm itapata kura nyingi hata kwenye majimbo ambayo wapinzani watashinda ubunge!
Angalizo ni kuwa kama ccm itamsimamisha mamvi basi cdm itashinda kwa kishindo uchaguzi wa mwaka 2015 hata kama watamsimamisha aliyekuwa meya wa mwanza mh manyerere kugombea urais! Pamoja na huyo ccm haitaweza kupata ushindi kama wagombea kama sita, sumaye na membe watagombea, hali inaonyesha kuwa upinzania wa kwanza kwa wagombea hawa kama ilivyo kwa lowasa utatoka ndani ya ccm hivyo kuathiri juhudi zao kwa wananchi!hata hivyo tathmini ianonyesha watu kuvutiwa kwa kiasi fulani na dr. Mwakyembe ingawa pia wanasema ni mapema mno kwake kushika wadhifa wa urais kwani bado hana uzoefu wa kutosha wa uongozi katika ulingo wa kisiasa.
Vilevile tathmini ya uwezekano wa mh shamsi vuai nahodha kuwa rais unaonyesha kuwa mtarajiwa huyo kwa kiwango kikubwa hana ushawishi na mvuto kwa wananchi wengi kutokana na kuonekana ni mpole na hatoweza kuwakemea mapapa ndani ya ccm.
Wakati hali ikiwa hivyo kwa ccm, upande wa chadema unaonyesha kuwa na wagombea wote wenye nguvu ya kushinda urais kama ccm haitomsimamisha magufuli, ambao nwanongozwa na dr slaa, zito, mbowe na mnyika. Kwa hali ya kisiasa ilivyo sasa wilaya nyingi zinaonyesha kuchoshwa na wabunge wa ccm wanaosinzia bungeni na kuunga mkono hoja pindi wanapokurupushwa kutoka usingizini!
Upepo wa kisiasa unaonyesha zaidi ya wabunge kumi machachari wa sasa kutoka ccm hawatogombea tena ubunge kupitia ccm bali watahamia chadema na kushinda tena ubunge na wabunge zaidi ya ishirini wa ccm watapoteza majimbo yao!baada ya kumaliza utafiti huu nitauweka jamvini hapa mwanzoni mwa mwaka 2015!
karibuni kwa maoni
Hata hivyo chadema ina nafasi kubwa sana ya kuwa na wabunge wengi kuliko ccm, hali hii inaifanya cdm kuwa chama cha pili ambacho kinaweza kushika dola!nafasi kubwa ya kushinda urais bado inabaki kwa ccm kwani chama hiki kina watu mahiri wengi wanaokubalika sana kwa wananchi kuliko chadema ambayo ina watu wachache mahiri wanaoweza kugombe kwa nafasi hiyo na kukubalika!
Yawezekana ccm ikaonekana kama imepoteza muelekeo lakini vipi ikiwa mh. Dr. John pombe magufuli akisimamishwa kugombea urais kwa tiketi ya ccm ni nani kutoka upinzani anaeweza kumzuia?kwa tathmini tuliyofanya inaonyesha magufuli ni mgombea wa kufikirika wa ccm anaeweza kukiokoa kisipoteze uongozi wa nchi.
Ndiye mtu pekee mwenye nguvu kwa wananchi ambaye anaonekana kutokuwa na kundi linaloeweka ndani ya ccm, lakini zaidi ni kuwa wananchi wanamuona kama mtu anaeweza kusimamia sheria bila upendeleo. Kama akigombea na kupitishwa ni wazi kuwa ccm itapata kura nyingi hata kwenye majimbo ambayo wapinzani watashinda ubunge!
Angalizo ni kuwa kama ccm itamsimamisha mamvi basi cdm itashinda kwa kishindo uchaguzi wa mwaka 2015 hata kama watamsimamisha aliyekuwa meya wa mwanza mh manyerere kugombea urais! Pamoja na huyo ccm haitaweza kupata ushindi kama wagombea kama sita, sumaye na membe watagombea, hali inaonyesha kuwa upinzania wa kwanza kwa wagombea hawa kama ilivyo kwa lowasa utatoka ndani ya ccm hivyo kuathiri juhudi zao kwa wananchi!hata hivyo tathmini ianonyesha watu kuvutiwa kwa kiasi fulani na dr. Mwakyembe ingawa pia wanasema ni mapema mno kwake kushika wadhifa wa urais kwani bado hana uzoefu wa kutosha wa uongozi katika ulingo wa kisiasa.
Vilevile tathmini ya uwezekano wa mh shamsi vuai nahodha kuwa rais unaonyesha kuwa mtarajiwa huyo kwa kiwango kikubwa hana ushawishi na mvuto kwa wananchi wengi kutokana na kuonekana ni mpole na hatoweza kuwakemea mapapa ndani ya ccm.
Wakati hali ikiwa hivyo kwa ccm, upande wa chadema unaonyesha kuwa na wagombea wote wenye nguvu ya kushinda urais kama ccm haitomsimamisha magufuli, ambao nwanongozwa na dr slaa, zito, mbowe na mnyika. Kwa hali ya kisiasa ilivyo sasa wilaya nyingi zinaonyesha kuchoshwa na wabunge wa ccm wanaosinzia bungeni na kuunga mkono hoja pindi wanapokurupushwa kutoka usingizini!
Upepo wa kisiasa unaonyesha zaidi ya wabunge kumi machachari wa sasa kutoka ccm hawatogombea tena ubunge kupitia ccm bali watahamia chadema na kushinda tena ubunge na wabunge zaidi ya ishirini wa ccm watapoteza majimbo yao!baada ya kumaliza utafiti huu nitauweka jamvini hapa mwanzoni mwa mwaka 2015!
karibuni kwa maoni