CCM imekosea sana kubadili sera ya Ujamaa na kuhamia Ubepari

Desprospero

JF-Expert Member
Feb 1, 2023
887
2,201
LEO ni siku ambayo nchi mbili huru kwa maana ya Tanganyika na Zanzibar ziliungana na kuzaa nchi moja Tanzania lakini nchi hiyo ikiwa na muundo wa Serikali mbili. Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Ni jambo jema watu wamoja tena ndugu waliokuwa wametengwa na wakoloni wanapoamua kuwa kitu kimoja. Ukuta wa Berlin uliowatenganisha ndugu wamoja wa Ujerumani ulipobomolewa Wajerumani walitoa machozi ya furaha kama Zanzibar na Tanganyika walipoungana. Kongole kwa Hayati Julius Nyerere na Abeid Aman Karume.

Hata hivyo, tunapoadhimisha siku hii muhimu ni vizuri tukatafakari nia na shabaha ya waasisi hawa walitaka kujenga Jamii ya aina gani? Ukweli ni kwamba baada ya TANU na ASP kuungana na kuzaa CCM waasisi hawa walitamani kujenga jamii ya watu wenye usawa, jamii isiyo na wanyonyaji kwa maana ya makupe. Na hapa ndipo ilipojikita siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Ni siasa hii ya Ujamaa iliyozaa Azimio la Arusha.

Hata ndani ya Katiba yetu ya mwaka 1977 bado inaelezwa bayana kuwa Tanzania inafuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Swali ambalo wana-CCM wanatakiwa kujibu bila unafiki ni je, nchi hii bado ni ya kijamaa?

Ni uongo na unafiki kama jibu litakuwa ni NDIYO maana ngoma inayopigwa (Katiba) ni Ujamaa lakini uchezaji ni Ubepari. Ile dhima ya usawa katika jamii imetoweka na ndiyo madhara tuliyoanza kuona na yumkini kuna hatari kubwa ya nchi hii kuingia katika machafuko mabaya sana huko tuendako na ni CCM itabeba lawama na laana!

Pengo kati ya matajiri na masikini inapanuka kila uchao. Kikundi kidogo sana Cha mabepari wanahodhi ukwasi wa kutisha huku kundi kubwa wakiishi maisha dhalili mno. Hii ni hatari sana. Sasa tunashuhudia tabaka la watawala wanavyojitenga na watawaliwa wasiojua hata mlo wao wa kesho.

Dhana ya Kujitegemea imeondoka na tunadhani tuko salama tunaposifiwa na mabepari wa mtaa wa Brettonwood, New York WB na IMF eti uchumi wetu unakuwa kwa kasi. Haya mashirika mumiani wakikusifia jifikirie mara mbili. Mikopo yao inayoondoa Kujitegemea ni ndoano hatari sana hapo baadaye.

Mwalimu Nyerere aliwapinga wazi wazi na kanini yao ya GDP kwa hoja nzito kwamba eti kupata pato la kila mwananchi ni kuchukua pato lote na kisha kugawia idadi ya wananchi. Huu ni upumbavu maana mali imehodhiwa na watu 100 then unataka kuwagawia na kina Mama Lishe, bodaboda, vinyozi, mafundi mchundo nk. Ujinga uliovuka mawingu.

Kuendelea na mfumo huu wa Ubepari ni sawa na kumwagia nyumba yako petroli. Ninaambiwa mshauri wa masuala ya uchumi wa Rais Samia Suluhu Hassan ni mtaalamu wa fani hiyo tena mwanamke. Sijui ni kwa nini ameteua ushauri huu katili. Laiti kama angesikia vilio vya wananchi walio wengi wanateseka angeachana na ushauri huu kwa Samia na kama hashauriki angeachana naye na kurudi UDSM kufundisha

Kama kweli tunaenzi Muungano basi tuyaenzi na mawazo, maono na visheni kali ya waasisi wake. Tujenge Taifa la watu wenye usawa wanaofaidi keki ya nchi yao kwa pamoja. Kinyume na hapo ipo siku (haiko mbali) masikini watakuwa tayari kutafuta mbadala.
Kheri ya Muungano!
#BringBackOurMoney. CAG report.
 
LEO ni siku ambayo nchi mbili huru kwa maana ya Tanganyika na Zanzibar ziliungana na kuzaa nchi moja Tanzania lakini nchi hiyo ikiwa na muundo wa Serikali mbili. Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Ni jambo jema watu wamoja tena ndugu waliokuwa wametengwa na wakoloni wanapoamua kuwa kitu kimoja. Ukuta wa Berlin uliowatenganisha ndugu wamoja wa Ujerumani ulipobomolewa Wajerumani walitoa machozi ya furaha kama Zanzibar na Tanganyika walipoungana. Kongole kwa Hayati Julius Nyerere na Abeid Aman Karume.

Hata hivyo, tunapoadhimisha siku hii muhimu ni vizuri tukatafakari nia na shabaha ya waasisi hawa walitaka kujenga Jamii ya aina gani? Ukweli ni kwamba baada ya TANU na ASP kuungana na kuzaa CCM waasisi hawa walitamani kujenga jamii ya watu wenye usawa, jamii isiyo na wanyonyaji kwa maana ya makupe. Na hapa ndipo ilipojikita siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Ni siasa hii ya Ujamaa iliyozaa Azimio la Arusha.

Hata ndani ya Katiba yetu ya mwaka 1977 bado inaelezwa bayana kuwa Tanzania inafuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Swali ambalo wana-CCM wanatakiwa kujibu bila unafiki ni je, nchi hii bado ni ya kijamaa?

Ni uongo na unafiki kama jibu litakuwa ni NDIYO maana ngoma inayopigwa (Katiba) ni Ujamaa lakini uchezaji ni Ubepari. Ile dhima ya usawa katika jamii imetoweka na ndiyo madhara tuliyoanza kuona na yumkini kuna hatari kubwa ya nchi hii kuingia katika machafuko mabaya sana huko tuendako na ni CCM itabeba lawama na laana!

Pengo kati ya matajiri na masikini inapanuka kila uchao. Kikundi kidogo sana Cha mabepari wanahodhi ukwasi wa kutisha huku kundi kubwa wakiishi maisha dhalili mno. Hii ni hatari sana. Sasa tunashuhudia tabaka la watawala wanavyojitenga na watawaliwa wasiojua hata mlo wao wa kesho.

Dhana ya Kujitegemea imeondoka na tunadhani tuko salama tunaposifiwa na mabepari wa mtaa wa Brettonwood, New York WB na IMF eti uchumi wetu unakuwa kwa kasi. Haya mashirika mumiani wakikusifia jifikirie mara mbili. Mikopo yao inayoondoa Kujitegemea ni ndoano hatari sana hapo baadaye.

Mwalimu Nyerere aliwapinga wazi wazi na kanini yao ya GDP kwa hoja nzito kwamba eti kupata pato la kila mwananchi ni kuchukua pato lote na kisha kugawia idadi ya wananchi. Huu ni upumbavu maana mali imehodhiwa na watu 100 then unataka kuwagawia na kina Mama Lishe, bodaboda, vinyozi, mafundi mchundo nk. Ujinga uliovuka mawingu.

Kuendelea na mfumo huu wa Ubepari ni sawa na kumwagia nyumba yako petroli. Ninaambiwa mshauri wa masuala ya uchumi wa Rais Samia Suluhu Hassan ni mtaalamu wa fani hiyo tena mwanamke. Sijui ni kwa nini ameteua ushauri huu katili. Laiti kama angesikia vilio vya wananchi walio wengi wanateseka angeachana na ushauri huu kwa Samia na kama hashauriki angeachana naye na kurudi UDSM kufundisha

Kama kweli tunaenzi Muungano basi tuyaenzi na mawazo, maono na visheni kali ya waasisi wake. Tujenge Taifa la watu wenye usawa wanaofaidi keki ya nchi yao kwa pamoja. Kinyume na hapo ipo siku (haiko mbali) masikini watakuwa tayari kutafuta mbadala.
Kheri ya Muungano!
#BringBackOurMoney. CAG report.
Ujamas ndio uliturudisha nyuma ya nchi nyingi za Africa.
 
Ujamaa umetuchelewesha sana. Naiomba serikali iongeze kasi kubwa kuelekea kwe ubepari. Tuondoe mashirika uchwara yanayo tumia kodi zetu kama ruzuku
 
Ujamaa ni USHETANI.

Jinasue huko ndugu! Kimbia mbali na vifungo na wavu wa propaganda za Kijamaa uliopofusha fikra zako, ili uweze kuona nuru na kutambua mambo kwa uhalisi na usahihi wake.

In brief, KILA KITU kitu cha Ujamaa ni UHARIBIFU wa maisha ya mwandamu - yaani ustawi na maendeleo yake kiuchumi, kiakili, kijamii, kiroho, kisiasa nk.

Ujamaa ni "tusi baya" sana kwa mwanadamu yeyote mwenye akili timamu na moyo wa utu.

Ujamaa sio "mfumo mbadala" wa ubepari, la hasha; kama ulivyoaminishwa na wengine kama wewe.

Tafuta utaona ya kuwa Ujamaa ni mfumo mbadala wa Mwanadamu na Mungu. To replace both with their devilish ideologies, assumptions and destructive practices.

It's satanic in form, contents and purpose to the core. Ni sahihi na haki nikitamka leo kwamba UJAMAA NI KINYUME KABISA CHA MAUMBILE NA MAKUSUDI YA MWANDAMU NA MUNGU!!

Sisi wenye kuujua Ujamaa vizuri tunauchukia na tutauchukia siku zote uovu wake kwa nguvu zetu zote, siku zetu zote na kwa vizazi vyetu vyote!
Ijulikane hivyo tangu sasa na kuendelea.

# Tutaupinga Ujamaa kwa aina zake na rangi zake zote popote...yes:-

# Tutaupinga mchana, tutaupinga usiku pia. Asubuhi na jioni tutaupinga.

# Tena, tutaupinga Ujamaa, mijini na vijijini; milimani na mabondeni; mashuleni na mitaani; maofisini na majumbani; nchi kavu na baharini; angani na ardhini; mbali na karibu;

# Tutapambana na Ujamaa kwa uhodari, weledi na furaha kubwa... siku zetu zote, vizazi vyetu vyote na kwa nguvu zetu zote!!!

# Hatutakubali tena Tanzania irudi kwenye lile giza nene. Magufuli was close to take us back there but thanks GOD, HE INTERVENED! So we now say "Never Again".

Keep this for your lasting information.
 
Ujamaa ni USHETANI.

Jinasue huko ndugu! Kimbia mbali na vifungo na wavu wa propaganda za Kijamaa uliopofusha fikra zako, ili uweze kuona nuru na kutambua mambo kwa uhalisi na usahihi wake.

In brief, KILA KITU kitu cha Ujamaa ni UHARIBIFU wa maisha ya mwandamu - yaani ustawi na maendeleo yake kiuchumi, kiakili, kijamii, kiroho, kisiasa nk.

Ujamaa ni "tusi baya" sana kwa mwanadamu yeyote mwenye akili timamu na moyo wa utu.

Ujamaa sio "mfumo mbadala" wa ubepari, la hasha; kama ulivyoaminishwa na wengine kama wewe.

Tafuta utaona ya kuwa Ujamaa ni mfumo mbadala wa Mwanadamu na Mungu. To replace both with their devilish ideologies, assumptions and destructive practices.

It's satanic in form, contents and purpose to the core. Ni sahihi na haki nikitamka leo kwamba UJAMAA NI KINYUME KABISA CHA MAUMBILE NA MAKUSUDI YA MWANDAMU NA MUNGU!!

Sisi wenye kuujua Ujamaa vizuri tunauchukia na tutauchukia siku zote uovu wake kwa nguvu zetu zote, siku zetu zote na kwa vizazi vyetu vyote!
Ijulikane hivyo tangu sasa na kuendelea.

# Tutaupinga Ujamaa kwa aina zake na rangi zake zote popote...yes:-

# Tutaupinga mchana, tutaupinga usiku pia. Asubuhi na jioni tutaupinga.

# Tena, tutaupinga Ujamaa, mijini na vijijini; milimani na mabondeni; mashuleni na mitaani; maofisini na majumbani; nchi kavu na baharini; angani na ardhini; mbali na karibu;

# Tutapambana na Ujamaa kwa uhodari, weledi na furaha kubwa... siku zetu zote, vizazi vyetu vyote na kwa nguvu zetu zote!!!

# Hatutakubali tena Tanzania irudi kwenye lile giza nene. Magufuli was close to take us back there but thanks GOD, HE INTERVENED! So we now say "Never Again".

Keep this for your lasting information.
Hujaeleza sababu hata moja ya ushetani wa Ujamaa.
 
Nimegusia hapo juu "briefly". Maisha ya mwandamu, ustawi na maendeleo yake kimwili, kiakili, kiuchumi, kiroho nk
Hujaona?
Hujaeleza ni kwa vipi Ujamaa unaathiri ustawi na maendeleo yake kimwili, kiakili, kiuchumi na kiroho. Ungetoa walau mifano hai.
 
Hujaeleza ni kwa vipi Ujamaa unaathiri ustawi na maendeleo yake kimwili, kiakili, kiuchumi na kiroho. Ungetoa walau mifano hai.
Good, I'm glad to oblige.

Nianze na ulivyoanza wewe - "usawa". Jambo "dogo" lakini kubwa.

Hebu jiulize maswali rahisi tu - je ni kweli binadamu wote ni sawa? Je imewahi tokea au kuwa hivyo mahali popote ktk historia ya mwandamu tangu Adamu?
Wewe na ndugu zako mko sawa? Au kama una watoto, je wako sawa?
Vitu rahisi tu kama vidole vyako je viko sawa? So you can go on and on.

Na kama Mwenyezi Mungu alikusudia tuwe sawa, surely angetuumba sawa. That's simple. Kwa nini "akosee" then aje mjamaa kuturekebisha?
Yaani YEYE Mwenyezi atuumbe tofauti/different (kwa malengo na faida Zake na zetu pia) halafu eti iwe "kazi" ya Ujamaa na wajamaa kutusawazisha. No way!

Eti kutufanya sawa. Kutu shape kwa malengo yao! See now, that's blatant evil, satanic plan/program/system - however, thank God as it's always doomed to fail - as you can easily verify qualitatively.

Ndio maana nikasema mapema kuwa ujamaa ni USHETANI, na tena ni kinyume kabisa na maumbile, makusudi na mpango wa Mwenyezi. Mungu na mwanadamu.

Ujamaa sio mfumo mbadala wa ubepari au mfumo mwingine wowote kama mnavyodhani. Rather, it's a system/force bent for the destruction, substitution and replacement of both GOD and human civilization. By its core and nature, Ujamaa is against the CREATOR and the mankind. I can't emphasize this enough.

If you really are honest and want to learn more on just this littlething of ujamaa "equality", it's very possible. Just learn to read/see beyond or beneath their propaganda and literatures vs REALITY (actual/tangible results). It's not that subtle or difficult to locate; just seek and search the truth with open mindedness.

Socialism/Communism "Equality" is a deadly lie, a complete waste of your time, resources and valuable life. It was developed so to disract mankind from real essentials of life and well-being both individually and collectively; at the same time trap and plunging mankind into self and collective destructions.

It's a "good & sweet" lethal poison wrapped in seductive packages which you happily swallow since you deludely call it what they fansily name as "education", "knowledge" "ideology" etc - which you drink and die. Literally!
So don't be fooled with their conship game and "arts of deceptions".
There's no dot of truth, life or good in that lethal poison.

"Usawa" wa Ujamaa ni uzushi wenye malengo "ovu" mengi sana. Wengi mnadhani usawa umetoka Magharibi. No! Ulipelekwa Magharibi toka Moscow kisha ukasambazwa hadi Africa. Malengo yao yalipotimia, majira yakawadia wakasema sasa "usawa kwa mashoga". Baadhi yenu mka react na kushangaa kulikoni.?!

Narudia tena "usawa" wa Kijamaa si kitu halisi wala cha ukweli. Ni uzushi, ni fantasy, uwendawazimu, ulevi tu na huletwa kwa nia ya kudanganya, kushawishi, kupumbaza watu ili waangamie au wajiangamize - hasa walengwa ambao mnaitwa makabwela, wavuja jasho, wanyonge na majina mengine mengi yenye kutweza utu wa mwanadamu.

Mara nyingi wamefanikiwa kuwateka akili na hisia zenu. Kisha muwape maisha yenu, ndoto na mahitaji yenu halafu wawatumikishe sawasawa kuliko "wakoloni" wa Magharibi ambao wajamaa wanadai waliwakomboa toka kwao. Huwa mnaimba mapimbio yao ya "ukoloni mamboleo", ubeberu nk

Yaani ni hivi mmegeuzwa na kufanyika kuwa silaha za maangamizi dhidi yenu wenyewe - ninyi mnaoamini ujamaa.

Kwa mjamaa/Ujamaa binadamu ni kitu na SIO mtu kamili. Usitekwe na maneno na misamiati yao ambayo kwa haraka hulevya akili za watu. Ndio maana mjamaa haoni tabu kukulazimisha mtu mwenye talent, nidhamu, juhudi na maarifa ulingane (usawa) na mvivu, mpumbavu, mtu asiye na malengo ya kimaisha. Hiyo ni haki?

Meanwhile, mmejikita kutafuta "usawa" mkatunga na sheria na sera nk. Alipooana imekaa sawa, huyo Agent of Destruction, akasema sasa ili haki ziwe "sawa" mtamkabidhi yeye - sio hiari, (akijiita serikali, state nk) yeye eti ndiye atawagawia. Yaani wewe utakachochuma au kuzalisha na yule mwingine (kama amezalisha au la) eti sasa yeye (mjamaa) ndiye atakayewagawia nyote kulingana na "mfumo na mipango" yake na sio mipango au 'ndoto' zako. It kills individualism and differences which happened to the original intention of the CREATOR. Ninyi individualism mnaita ubinafsi. You then kill it. But what you havevent learnt here, it's there where the CREATOR have put a seed of life's productivity - we commonly call, rightly, as "gifts and talents ".
That's why the results of Socialist/Communist "equality" are consistently abject poverty, ignorance, corruption, tyranny, crisis, wars na yenye kufanana na hayo - World over!

Enough for now.
 
Hapo sijasemea hoja zako nyingine zinazobeba mada yako kama vile Muungano, Azimio la Arusha, Uchumi, Ubepari, Utajiri, Vipato na kubwa kuliko yote; KATIBA.

Nikipata wasaa nitachangia zaidi wakati mwingine.

Nimetumia hilo dogo ambalo ni "innocent" kwa mlio wengi - usawa.
Je tukichimba haya mengine makubwa itakuwaje?
 
LEO ni siku ambayo nchi mbili huru kwa maana ya Tanganyika na Zanzibar ziliungana na kuzaa nchi moja Tanzania lakini nchi hiyo ikiwa na muundo wa Serikali mbili. Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Ni jambo jema watu wamoja tena ndugu waliokuwa wametengwa na wakoloni wanapoamua kuwa kitu kimoja. Ukuta wa Berlin uliowatenganisha ndugu wamoja wa Ujerumani ulipobomolewa Wajerumani walitoa machozi ya furaha kama Zanzibar na Tanganyika walipoungana. Kongole kwa Hayati Julius Nyerere na Abeid Aman Karume.

Hata hivyo, tunapoadhimisha siku hii muhimu ni vizuri tukatafakari nia na shabaha ya waasisi hawa walitaka kujenga Jamii ya aina gani? Ukweli ni kwamba baada ya TANU na ASP kuungana na kuzaa CCM waasisi hawa walitamani kujenga jamii ya watu wenye usawa, jamii isiyo na wanyonyaji kwa maana ya makupe. Na hapa ndipo ilipojikita siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Ni siasa hii ya Ujamaa iliyozaa Azimio la Arusha.

Hata ndani ya Katiba yetu ya mwaka 1977 bado inaelezwa bayana kuwa Tanzania inafuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Swali ambalo wana-CCM wanatakiwa kujibu bila unafiki ni je, nchi hii bado ni ya kijamaa?

Ni uongo na unafiki kama jibu litakuwa ni NDIYO maana ngoma inayopigwa (Katiba) ni Ujamaa lakini uchezaji ni Ubepari. Ile dhima ya usawa katika jamii imetoweka na ndiyo madhara tuliyoanza kuona na yumkini kuna hatari kubwa ya nchi hii kuingia katika machafuko mabaya sana huko tuendako na ni CCM itabeba lawama na laana!

Pengo kati ya matajiri na masikini inapanuka kila uchao. Kikundi kidogo sana Cha mabepari wanahodhi ukwasi wa kutisha huku kundi kubwa wakiishi maisha dhalili mno. Hii ni hatari sana. Sasa tunashuhudia tabaka la watawala wanavyojitenga na watawaliwa wasiojua hata mlo wao wa kesho.

Dhana ya Kujitegemea imeondoka na tunadhani tuko salama tunaposifiwa na mabepari wa mtaa wa Brettonwood, New York WB na IMF eti uchumi wetu unakuwa kwa kasi. Haya mashirika mumiani wakikusifia jifikirie mara mbili. Mikopo yao inayoondoa Kujitegemea ni ndoano hatari sana hapo baadaye.

Mwalimu Nyerere aliwapinga wazi wazi na kanini yao ya GDP kwa hoja nzito kwamba eti kupata pato la kila mwananchi ni kuchukua pato lote na kisha kugawia idadi ya wananchi. Huu ni upumbavu maana mali imehodhiwa na watu 100 then unataka kuwagawia na kina Mama Lishe, bodaboda, vinyozi, mafundi mchundo nk. Ujinga uliovuka mawingu.

Kuendelea na mfumo huu wa Ubepari ni sawa na kumwagia nyumba yako petroli. Ninaambiwa mshauri wa masuala ya uchumi wa Rais Samia Suluhu Hassan ni mtaalamu wa fani hiyo tena mwanamke. Sijui ni kwa nini ameteua ushauri huu katili. Laiti kama angesikia vilio vya wananchi walio wengi wanateseka angeachana na ushauri huu kwa Samia na kama hashauriki angeachana naye na kurudi UDSM kufundisha

Kama kweli tunaenzi Muungano basi tuyaenzi na mawazo, maono na visheni kali ya waasisi wake. Tujenge Taifa la watu wenye usawa wanaofaidi keki ya nchi yao kwa pamoja. Kinyume na hapo ipo siku (haiko mbali) masikini watakuwa tayari kutafuta mbadala.
Kheri ya Muungano!
#BringBackOurMoney. CAG report.
DUNIA NZIMA IMEACHANA NA UJAMAA
 
Kama kuna kitu kilitupumbaza watanzania basi ni siasa za ujamaa, siasa zile ndio zimetugeuza kuwa mazombie.
 
Hujaeleza ni kwa vipi Ujamaa unaathiri ustawi na maendeleo yake kimwili, kiakili, kiuchumi na kiroho. Ungetoa walau mifano hai.
Wewe mwenyewe hujaeleza nini serikali ifanye ili kurejea kwenye ujamaa, maana mojawapo ya nguzo kuu za ujamaa ni kuwa na State Economy, je unataka serikali ianze kujenga viwanda? Ianze kumiliki njia zote za uchumi?

Sent from my SM-A035F using JamiiForums mobile app
 
Nyerere alianza vizuri akamaliza vibaya siasa ya ujamaa na kujitegemea na anguko lake ni ishara ya kufeli kwa Nyerere na utawala wake.
 
Kwa taarifa tu, muda huu kuna kitu kinaitwa BRICS (Brazil, Russia, India, China, India). Wajamaa wamejiunga dhidi ya G7. Pia wanataka kuwa na sarafu yao na kuitoa U$. (Ifahamike sitetei G7 wala U$ hapa)

Hivyo siku zijazo mtasikia "news" propganda kuhusu, ukuu, ufanisi, kukubalika, kupanuka nk kwa hicho kitu chao. Watafanya drama na fujo nyingi sana tu. Just be ready to meet, fight and defeat the communists.

Hivyo ni lazima sisi wapenda haki, uhuru, maendeleo na ustawi wa nchi yetu na mwanadamu kwa ujumla tuwe tayari kupambana nao - kwa rangi yoyote, umbo lolote , mahali popote na siku zote.
Uovu hupata nguvu au nafasi kwa sababu watu wema huwa hatuchukui hatua kukabiliana nao.

Tusiwape waovu nafasi tena
 
LEO ni siku ambayo nchi mbili huru kwa maana ya Tanganyika na Zanzibar ziliungana na kuzaa nchi moja Tanzania lakini nchi hiyo ikiwa na muundo wa Serikali mbili. Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Ni jambo jema watu wamoja tena ndugu waliokuwa wametengwa na wakoloni wanapoamua kuwa kitu kimoja. Ukuta wa Berlin uliowatenganisha ndugu wamoja wa Ujerumani ulipobomolewa Wajerumani walitoa machozi ya furaha kama Zanzibar na Tanganyika walipoungana. Kongole kwa Hayati Julius Nyerere na Abeid Aman Karume.

Hata hivyo, tunapoadhimisha siku hii muhimu ni vizuri tukatafakari nia na shabaha ya waasisi hawa walitaka kujenga Jamii ya aina gani? Ukweli ni kwamba baada ya TANU na ASP kuungana na kuzaa CCM waasisi hawa walitamani kujenga jamii ya watu wenye usawa, jamii isiyo na wanyonyaji kwa maana ya makupe. Na hapa ndipo ilipojikita siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Ni siasa hii ya Ujamaa iliyozaa Azimio la Arusha.

Hata ndani ya Katiba yetu ya mwaka 1977 bado inaelezwa bayana kuwa Tanzania inafuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Swali ambalo wana-CCM wanatakiwa kujibu bila unafiki ni je, nchi hii bado ni ya kijamaa?

Ni uongo na unafiki kama jibu litakuwa ni NDIYO maana ngoma inayopigwa (Katiba) ni Ujamaa lakini uchezaji ni Ubepari. Ile dhima ya usawa katika jamii imetoweka na ndiyo madhara tuliyoanza kuona na yumkini kuna hatari kubwa ya nchi hii kuingia katika machafuko mabaya sana huko tuendako na ni CCM itabeba lawama na laana!

Pengo kati ya matajiri na masikini inapanuka kila uchao. Kikundi kidogo sana Cha mabepari wanahodhi ukwasi wa kutisha huku kundi kubwa wakiishi maisha dhalili mno. Hii ni hatari sana. Sasa tunashuhudia tabaka la watawala wanavyojitenga na watawaliwa wasiojua hata mlo wao wa kesho.

Dhana ya Kujitegemea imeondoka na tunadhani tuko salama tunaposifiwa na mabepari wa mtaa wa Brettonwood, New York WB na IMF eti uchumi wetu unakuwa kwa kasi. Haya mashirika mumiani wakikusifia jifikirie mara mbili. Mikopo yao inayoondoa Kujitegemea ni ndoano hatari sana hapo baadaye.

Mwalimu Nyerere aliwapinga wazi wazi na kanini yao ya GDP kwa hoja nzito kwamba eti kupata pato la kila mwananchi ni kuchukua pato lote na kisha kugawia idadi ya wananchi. Huu ni upumbavu maana mali imehodhiwa na watu 100 then unataka kuwagawia na kina Mama Lishe, bodaboda, vinyozi, mafundi mchundo nk. Ujinga uliovuka mawingu.

Kuendelea na mfumo huu wa Ubepari ni sawa na kumwagia nyumba yako petroli. Ninaambiwa mshauri wa masuala ya uchumi wa Rais Samia Suluhu Hassan ni mtaalamu wa fani hiyo tena mwanamke. Sijui ni kwa nini ameteua ushauri huu katili. Laiti kama angesikia vilio vya wananchi walio wengi wanateseka angeachana na ushauri huu kwa Samia na kama hashauriki angeachana naye na kurudi UDSM kufundisha

Kama kweli tunaenzi Muungano basi tuyaenzi na mawazo, maono na visheni kali ya waasisi wake. Tujenge Taifa la watu wenye usawa wanaofaidi keki ya nchi yao kwa pamoja. Kinyume na hapo ipo siku (haiko mbali) masikini watakuwa tayari kutafuta mbadala.
Kheri ya Muungano!
#BringBackOurMoney. CAG report.
Ujamaa ni neema kwa viongozi na mzigo kwa wananchi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom