Ndagullachrles
Member
- Jun 20, 2023
- 54
- 51
Kuna video inasambaa mitandaoni ikionyesha mama mmoja mkazi wa kata ya Mbokomu akilalamika kuwa Mbunge wao, Profesa Patrick Ndakidemi aliwaahidi kuwaboreshea mazingira ya barabara endapo wangechagua kuwa mbunge wa jimbo la moshi vijijini.
Tofauti na hivyo mama huyo anasema tangu achaguliwe hajawahi kufika katika eneo hilo la kwamba wanatumia gharama kubwa kusafrisha mazao yao kwenda sokoni kutokana na ubovu wa miundombinu ya barabara na kwamba kwa hali hiyo hawana hamu tena yakupiga kura.
Kwenye video hiyo pembeni zinasikika sauti za wanaume ni kama wanamwongoza cha kusema mama huyo na wanaishia kucheka.
aSsa Mbunge baada ya kuipata clip hiyo alifunga safari hadi eneo hilo na kuzungumza na mama huyo ambaye anakana kauli hiyo.
Huu ni mwendelezo wa siasa za kuchafuana ambazo zinaonekana kuchipukia kwenye majimbo ya moshi vijijini na Moshi mjini ambako wabunge hawa wa ccm, Priscus Tarimo (moshi Mjini) na Ndakidemi (moshi vijini) wanaonekana kuwa na maadui wengi ndani ya chama chao kuelekea uchaguzi mkuu hapo mwakani.
Tofauti na hivyo mama huyo anasema tangu achaguliwe hajawahi kufika katika eneo hilo la kwamba wanatumia gharama kubwa kusafrisha mazao yao kwenda sokoni kutokana na ubovu wa miundombinu ya barabara na kwamba kwa hali hiyo hawana hamu tena yakupiga kura.
Kwenye video hiyo pembeni zinasikika sauti za wanaume ni kama wanamwongoza cha kusema mama huyo na wanaishia kucheka.
aSsa Mbunge baada ya kuipata clip hiyo alifunga safari hadi eneo hilo na kuzungumza na mama huyo ambaye anakana kauli hiyo.
Huu ni mwendelezo wa siasa za kuchafuana ambazo zinaonekana kuchipukia kwenye majimbo ya moshi vijijini na Moshi mjini ambako wabunge hawa wa ccm, Priscus Tarimo (moshi Mjini) na Ndakidemi (moshi vijini) wanaonekana kuwa na maadui wengi ndani ya chama chao kuelekea uchaguzi mkuu hapo mwakani.