CCJ yazidi kukomba... usajili wa kudumu wanukia!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Swahiba wa Makamba akimbilia CCJ




Na Lulu George





Aliyekuwa Kada na mpiga debe wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Yahya Gadaffi, ametangaza kukihama chama hicho kujiunga na Chama cha Jamii (CCJ) na kugombania ubunge Jimbo la Tanga.
Kada huyo ameahidi kutimkia CCJ akiambatana na wafuasi zaidi ya 1000 wa kutoka CCM na vyama vingine vya siasa vilivyopo mkoani Tanga.
Alisema hatua hiyo ni ya kumuunga mkono aliyekuwa Mbunge wa Kishapu, Fred Mpendazoe, kwa kile alichodai kuwa kuhamia kwake CCJ ni kuonyesha uzalendo wa hali ya juu na kujali maslahi ya Watanzania.
Alifafanua kuwa wanachama anaohama nao CCJ 600 ni kutoka CCM na 400 waliobaki ni kutoka vyama vingine vya siasa vilivyopo mkoani Tanga.
Alisema uamuzi wa kuihama CCM ni kutokana na kuchoshwa na ahadi hewa alizopewa na viongozi wa juu wa chama hicho wakati alipokuwa akijiunga nacho mwaka 2007 kwamba kingesaidia kuleta mabadiliko ya Mkoa wa Tanga, ahadi aliyosema kuwa haikutekelezwa mpaka sasa.





CHANZO: NIPASHE

Wakati huo huo, CCJ inaendelea taratibu kukamilisha taratibu za kupata usajili wa kudumu na kama mambo yataenda inavyotarajiwa hilo litafanyika ifikapo mwanzoni mwa mwezi Juni na hivyo kuweka CCJ katika ulingo wa kushiriki uchaguzi mkuu kikiwa na lengo la kusimamisha wagombea katika viti vyote vya Ubunge na Urais... MM
 
Aliyekuwa Kada na mpiga debe wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Yahya Gadaffi, ametangaza kukihama chama hicho kujiunga na Chama cha Jamii (CCJ) na kugombania ubunge Jimbo la Tanga.
Kada huyo ameahidi kutimkia CCJ akiambatana na wafuasi zaidi ya 1000 wa kutoka CCM na vyama vingine vya siasa vilivyopo mkoani Tanga.
Alisema hatua hiyo ni ya kumuunga mkono aliyekuwa Mbunge wa Kishapu, Fred Mpendazoe, kwa kile alichodai kuwa kuhamia kwake CCJ ni kuonyesha uzalendo wa hali ya juu na kujali maslahi ya Watanzania.
Alifafanua kuwa wanachama anaohama nao CCJ 600 ni kutoka CCM na 400 waliobaki ni kutoka vyama vingine vya siasa vilivyopo mkoani Tanga.
Alisema uamuzi wa kuihama CCM ni kutokana na kuchoshwa na ahadi hewa alizopewa na viongozi wa juu wa chama hicho wakati alipokuwa akijiunga nacho mwaka 2007 kwamba kingesaidia kuleta mabadiliko ya Mkoa wa Tanga, ahadi aliyosema kuwa haikutekelezwa mpaka sasa.



CHANZO: NIPASHE
 
Makamba naye..kwanini huyu asimpe kitengo kama Tambwe Hiza?
 
Ahadi hizo alihaidiwa yeye binafsi kama cheo vile au kwa maendeleo ya wana-Tanga na watanzania kwa ujumla? Nafikiri ahadi za kwake binafsi, kwanza kajiunga na CCM 2007 baada ya uchaguzi mkuu wa 2005. CCJ wawe waangalifu na watu hawa!
 
Aliyekuwa Kada na mpiga debe wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Yahya Gadaffi, ametangaza kukihama chama hicho kujiunga na Chama cha Jamii (CCJ) na kugombania ubunge Jimbo la Tanga. Kada huyo ameahidi kutimkia CCJ akiambatana na wafuasi zaidi ya 1000 wa kutoka CCM na vyama vingine vya siasa vilivyopo mkoani Tanga. Alisema hatua hiyo ni ya kumuunga mkono aliyekuwa Mbunge wa Kishapu, Fred Mpendazoe, kwa kile alichodai kuwa kuhamia kwake CCJ ni kuonyesha uzalendo wa hali ya juu na kujali maslahi ya Watanzania. Alifafanua kuwa wanachama anaohama nao CCJ 600 ni kutoka CCM na 400 waliobaki ni kutoka vyama vingine vya siasa vilivyopo mkoani Tanga. Alisema uamuzi wa kuihama CCM ni kutokana na kuchoshwa na ahadi hewa alizopewa na viongozi wa juu wa chama hicho wakati alipokuwa akijiunga nacho mwaka 2007 kwamba kingesaidia kuleta mabadiliko ya Mkoa wa Tanga, ahadi aliyosema kuwa haikutekelezwa mpaka sasa
CCJ Wanatakiwa kuwa macho sana na watu watakaojiunga hapo,tuko wengi ila tunasubiri kisajiliwe kwanza.
 
mbona hakipati usajili tu na siku zinaisha jamani au muda bado upo
 
Swahiba wa Makamba akimbilia CCJ

Wakati huo huo, CCJ inaendelea taratibu kukamilisha taratibu za kupata usajili wa kudumu na kama mambo yataenda inavyotarajiwa hilo litafanyika ifikapo mwanzoni mwa mwezi Juni na hivyo kuweka CCJ katika ulingo wa kushiriki uchaguzi mkuu kikiwa na lengo la kusimamisha wagombea katika viti vyote vya Ubunge na Urais... MM
Mzee Mwanakijiji, this is my thinking aloud, CCJ ni spare tairi tuu, baada ya kile kitisho cha kumuengua Sitta, ili akienguliwa tuu, yeye na makamanda wake wote na wabunge wengine zaidi ya 100 wangetimka CCM na kuleta upinzani wa kweli.

Taarifa zilifika kwa mkulu, akaamua kukinusuru chama, akamuweka chini Sitta, waka compromise, sasa hakuna tena kitisho cha kumuengua Sitta. Mkulu kakubali kumtosa sahiba wake RA, Sitta akakubali kutoendelea kuisulubu serikali bungeni, ndio maana issue zote hot, akazimaliza kiaina.

Masikini Mpendazoe, hakuijua hiyo compromise na hakuona mbali, akajitoa muhanga ili aonekane shujaa, akatimka mbio kutimkia CCJ, akijiaminisha ndio amefungua njia, kumbe ndio kwanza amekwenda kulitoboa hilo spare tairi na kulitia pancha!. Kama tayari spare tairi inapancha kabla hata ya kuanza kwa safari, hiyo safari itakuwaje?.
 
Mzee Mwanakijiji, this is my thinking aloud, CCJ ni spare tairi tuu, baada ya kile kitisho cha kumuengua Sitta, ili akienguliwa tuu, yeye na makamanda wake wote na wabunge wengine zaidi ya 100 wangetimka CCM na kuleta upinzani wa kweli.

Taarifa zilifika kwa mkulu, akaamua kukinusuru chama, akamuweka chini Sitta, waka compromise, sasa hakuna tena kitisho cha kumuengua Sitta. Mkulu kakubali kumtosa sahiba wake RA, Sitta akakubali kutoendelea kuisulubu serikali bungeni, ndio maana issue zote hot, akazimaliza kiaina.

Masikini Mpendazoe, hakuijua hiyo compromise na hakuona mbali, akajitoa muhanga ili aonekane shujaa, akatimka mbio kutimkia CCJ, akijiaminisha ndio amefungua njia, kumbe ndio kwanza amekwenda kulitoboa hilo spare tairi na kulitia pancha!. Kama tayari spare tairi inapancha kabla hata ya kuanza kwa safari, hiyo safari itakuwaje?.


Acha porojo zako Pasco! Mkulu hawezi kumtosa RA kwani huyu Mdosi alifanikisha kuingia kwake Ikulu. 'Kumtosa' maana yake ni kwamba pia amemvua nguo na hivyo aweza kumpeleka kizimbani kujibu mashitaka ya wizi wa EPA (Kagoda). Hiyo RA hashituki kwani anavyo 'vimemo' alivyowasainisha vogogo wa CCM (Wabunge etc) alipokuwa anawapa fedha zile kule Mindu Street Upanga. RA ni mtu anayeogopwa saaana na Mkulu, in fact kawekwa mfukoni. Inasikitisha sana sana kuwa na Rais wetu kuishi katika hali hiyo ya 'blackmail'!
 
Zak:
Nakubaliana nawe, JK is a very weak President. And it is nauseating to think that we are set for another 5 years of him, of the outrage!
 
Mh! Nina wasiwasi hapa yatajirudia yaleyale ya NCCR na baadaye TLP. Au kama si hivyo hawa 'wahamaji' naona wanatafuta njia ya 'kujitafunia', nadhani CCM kumebana sana. Hii point ya kusema kitu kama 'tunahama kwa sababu tumechoshwa na ahadi hewa za CCM..' na vitu kama hivyo, sioni kama ina-sound! Hebu fikiria... Matatizo yamejitokeza ktk familia yako. Je, ni busara kuikimbia familia, au kukabiliana na matatizo ili uikoe hiyo familia? Hapa naona wa-TZ tunapigwa changa la macho. Still i believe that 'THE BEAUTYFUL ONES ARE NOT YET BORN'
 
Acha porojo zako Pasco! Mkulu hawezi kumtosa RA kwani huyu Mdosi alifanikisha kuingia kwake Ikulu. 'Kumtosa' maana yake ni kwamba pia amemvua nguo na hivyo aweza kumpeleka kizimbani kujibu mashitaka ya wizi wa EPA (Kagoda). Hiyo RA hashituki kwani anavyo 'vimemo' alivyowasainisha vogogo wa CCM (Wabunge etc) alipokuwa anawapa fedha zile kule Mindu Street Upanga. RA ni mtu anayeogopwa saaana na Mkulu, in fact kawekwa mfukoni. Inasikitisha sana sana kuwa na Rais wetu kuishi katika hali hiyo ya 'blackmail'!
Zak, kwa sasa ziite porojo, ukishathibitisha utarekebisha. Mkulu kamtosa RA asizidi kumshukia Sitta, in return, Sitta kalizui bunge lisizidi kuishukia serikali, unadhani kwa nini Six emecompromise?.

Suala la Kagoda, hakuna kesi kwa sababu huo ni uchafu wa Mr. Clean na ni fedha hizo ndizo zilizotumika kumuingiza mkulu, ikulu. Hivyo its a gone case. Kotoswa kwa RA kutathibitika hivi karibuni baada ya kuvunjwa bunge.
 
Na tusubiri basi, Pasco. Lakini atabakia bado katika CC na NEC ambako anaonekana ana nguvu zaidi kuliko Bungeni. Atakapotokomezwa kabisa kutoka kwenye vikao hivyo na kuhamia Nairobi ndipo hapo nchi inaweza kutulia!
 
Na tusubiri basi, Pasco. Lakini atabakia bado katika CC na NEC ambako anaonekana ana nguvu zaidi kuliko Bungeni. Atakapotokomezwa kabisa kutoka kwenye vikao hivyo na kuhamia Nairobi ndipo hapo nchi inaweza kutulia!
.
Kutokomezwa kabisa hawawezi kwa sababu wanamtegemea nguvu zake za kiuchumi na mtandao wake. Kwa taarifa tuu, huwezi amini ni RA ndie iliyempigia chapuo Six kupata uspika. Waliompigia kura kura Six ni waNEC kutoka Zanzibar chini ya payroll ya RA, wakati waNEC wa bara walimtaka Msekwa. Ni waNEC hao hao wa Zanzibar aliotaka kuwatumia kumsulubu Six kile kikao cha NEC na alifanikiwa sana, almanusura Six ang'oke ila JK ndio alimuokoa.

Jamaa is really powerfull and a true King Maker!.
 
Angalieni hiyo CCj inaweza ikajaa mamluki kibao na ikajaishia kuwa ccm -B ikiwa na mafisadi wale wale waliokosa ulaji ccm
 
Back
Top Bottom