Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Bwana harusi, Mahankali Anill mwenye umri wa miaka 22 alichinjwa na kuvunjwa kichwa kwa jiwe kubwa na familia ya msichana mwenye umri wa miaka 18 aliyekuwa akimuoa.
Mashirika ya habari yalisema familia ya msichana huyo, walivamia mahali ambapo wawili hao walikuwa wakifunga ndoa wakamkamata kwa nguvu mwanamume huyo na kwenye nae nje.
Bibi harusi aliyetambuliwa kama Hastapuram Mounika alisemekana kutazama kwa mshtuko mkubwa wakati mume wake mtarajiwa alipokatwa shingo na Kuuawa kikatili mbele yake.
Ilisemekana wawili hao walikuwa wametoroka pamoja lakini familia ya msichana iliwatafuta hadi ikawapata katika hekalu la Thimmapur, India ambako walikuwa wakifunga ndoa.
Walikuwa wamechumbiana kwa mwaka mmoja lakini familia ya msichana haikuwa imependezwa na uhusiano huo wakajaribu kuwatenganisha.
Kulingana na ripoti za habari, walijaribu kuoana awali lakini famili ya msichana ikafanikiwa kushawishi polisi kuwa umri wake ulikuwa chini ya miaka 18 wakazuiliwa kuoana.
Mkuu wa polisi wa eneo hilo Kamalasan Reddy alinukuliwa akisema washukiwa kadhaa wamekamatwa, huku ripoti zikisema watu 10 walikuwa kizuizini.