benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
‘Hivi ni vijimambo’ unaweza ukaita hivyo, baada ya sintofahamu kutanda katikati ya sherehe ya harusi kutokana na vurugu iliyosababishwa na taarifa iliyomfikia bi harusi kuwa anayefunga nae ndoa ana familia yenye watoto saba.
Sherehe hiyo iliyokuwa ikifanyika siku ya Jumapili katika jimbo la Edo kusini mwa Nigeria iligeuka shubiri ambapo vilio vilitawala upande wa bibi harusi anayesemekana hakufanya uchunguzi kamili kumgundua mwenza wake huyo kabla ya kujitosa kufunga nae pingu za maisha.
Video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii inaonyesha eneo la tukio kuvurugika baada ya viti, maua na mapambo yakiwa yametupwa kila mahali huku waalikwa wakiwa wamesimama kwa mshangao wakiashiria hakuna tena kinachoendelea.
TAZAMA VIDEO CHINI HAPA
Sherehe hiyo iliyokuwa ikifanyika siku ya Jumapili katika jimbo la Edo kusini mwa Nigeria iligeuka shubiri ambapo vilio vilitawala upande wa bibi harusi anayesemekana hakufanya uchunguzi kamili kumgundua mwenza wake huyo kabla ya kujitosa kufunga nae pingu za maisha.
Video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii inaonyesha eneo la tukio kuvurugika baada ya viti, maua na mapambo yakiwa yametupwa kila mahali huku waalikwa wakiwa wamesimama kwa mshangao wakiashiria hakuna tena kinachoendelea.
TAZAMA VIDEO CHINI HAPA