PatriotMzalendo
Member
- Jan 17, 2011
- 28
- 6
Tangu kikao hiki cha Bunge kilipoanza, nimegundua kuwa wabunge kadhaa wa CCM ni wajinga kupita maelezo. Kwa sababu wanajua wengi wanazidiwa upeo kwa mbali na wabunge wa CHADEMA, wanaona kwamba kuingilia hoja za wabunge wa CHADEMA za mwelekeo wa kitaifa kwa kuomba mwongozo wa spika bila hoja zozote za maana na kulazimisha tafsiri za kanuni ni mbinu yao ya kuvuruga hoja hizo na kupoteza muda wa watoa hoja hao makini wa CHADEMA.
Kwa mfano, Mbunge wa CHADEMA aliposema Rais hana uthubutu wa kubuni mambo makubwa na kutoa mifano hai, ilikera sana mbunge mjinga wa CCM alipoomba mwongozo wa spika na kutumia kanuni inayokataza mbunge kumdhihaki Rais ambacho,kwa tafsiri, hakimkatazi mbunge kuonyesha dosari za kiutendaji za Rais bali kinakataza labda kumwita bungeni Rais Mkwere, Msanii, mtu wa kuchekacheka na kadhalika.
Kibaya ni kwamba hakuna mwongozo wa spika wa kijinga dhidi ya mbunge wa CHADEMA uliokosolewa na naibu spika tofauti na alivyokuwa akifanya Samwel 6. Hawa wabunge wa CCM na spika wao wanapaswa waelewe kuwa hii miongozo ya spika ya kijinga dhidi ya hoja zinazogusa maisha yetu inaongeza umaarufu na upendo wa wabunge wa CHADEMA kwetu na inapoteza kabisa heshima na upendo wetu kwao! Waendelee hivyo hivyo na jibu watalipata 2015.
Kwa mfano, Mbunge wa CHADEMA aliposema Rais hana uthubutu wa kubuni mambo makubwa na kutoa mifano hai, ilikera sana mbunge mjinga wa CCM alipoomba mwongozo wa spika na kutumia kanuni inayokataza mbunge kumdhihaki Rais ambacho,kwa tafsiri, hakimkatazi mbunge kuonyesha dosari za kiutendaji za Rais bali kinakataza labda kumwita bungeni Rais Mkwere, Msanii, mtu wa kuchekacheka na kadhalika.
Kibaya ni kwamba hakuna mwongozo wa spika wa kijinga dhidi ya mbunge wa CHADEMA uliokosolewa na naibu spika tofauti na alivyokuwa akifanya Samwel 6. Hawa wabunge wa CCM na spika wao wanapaswa waelewe kuwa hii miongozo ya spika ya kijinga dhidi ya hoja zinazogusa maisha yetu inaongeza umaarufu na upendo wa wabunge wa CHADEMA kwetu na inapoteza kabisa heshima na upendo wetu kwao! Waendelee hivyo hivyo na jibu watalipata 2015.