Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,354
- 33,192
Bunduki Mpya ya Marekani Yenye Uwezo Kumlenga Adui Sehemu Aliyojificha
Bunduki mpya ya Marekani XM25 yenye uwezo wa kumtungua adui hata kama amejificha nyuma ya ukuta Monday, June 08, 2009 4:57 PM
Jeshi la Marekani limetengeneza bunduki mpya ambayo ina uwezo wa kumtungua mtu popote pale alipojificha iwe ni nyuma ya ukuta au kwenye mabonde. Picha za bunduki hiyo mwisho wa habari hii. Bunduki hiyo iitwayo XM25 inatumia risasi ambazo hulipuka na kusababisha mvua ya risasi nyingi ndogo ndogo baada ya kwenda umbali uliosetiwa na mtumiaji wa bunduki hiyo.
Jeshi la Marekani litatumia bunduki hizo kuwatungua maadui zao wanaojificha nyuma ya ukuta au kwenye mashimo kwani risasi za bunduki hiyo zikishafika eneo ambalo wamejificha hulipuka na kutoa risasi zingine ndogo ndogo nyingi sana ambazo kuzikwepa ni vigumu sana.
Kwa mfano fikiria mtu amejificha kwenye shimo liliopo nyuma ya mwinuko wa ardhi na kwa mazingira ya kawaida risasi haiwezi kumpata kwa kuwa mwinuko utakuwa kama kinga yake, lakini kwa kutumia bunduki hiyo mpya, risasi itapigwa kwa juu hadi kwenye sehemu ambayo shimo hilo lilipo na itakapofika juu ya shimo hilo italipuka na kutoa risasi ndogo ndogo ambazo zitaelekezwa kwenye shimo hilo.
Bunduki hizo zinatumia mfumo kama wa kompyuta kupiga mahesabu ya sehemu inayotakiwa kulengwa na risasi zake pia zina uwezo wa kupiga mahesabu zimesafiri umbali gani kabla hazijalipuka.
XM25 zimeelezewa na kampuni iliyozitengeneza ya Alliant Techsystems kwamba zitasaidia kupunguza gharama kwani badala ya kurusha bomu ambalo lingerimu maelfu ya dola, bunduki hiyo ikitumika itagharimu dola 20 tu. Bunduki Mpya ya Marekani Yenye Uwezo Kumlenga
Jeshi la Marekani limetengeneza bunduki mpya iitwayo XM25 ambayo ina uwezo wa kumtungua mtu popote pale alipojificha iwe ni nyuma ya ukuta au kwenye mabonde.
Bunduki mpya ya Marekani XM25 yenye uwezo wa kumtungua adui hata kama amejificha nyuma ya ukuta Monday, June 08, 2009 4:57 PM
Jeshi la Marekani limetengeneza bunduki mpya ambayo ina uwezo wa kumtungua mtu popote pale alipojificha iwe ni nyuma ya ukuta au kwenye mabonde. Picha za bunduki hiyo mwisho wa habari hii. Bunduki hiyo iitwayo XM25 inatumia risasi ambazo hulipuka na kusababisha mvua ya risasi nyingi ndogo ndogo baada ya kwenda umbali uliosetiwa na mtumiaji wa bunduki hiyo.
Jeshi la Marekani litatumia bunduki hizo kuwatungua maadui zao wanaojificha nyuma ya ukuta au kwenye mashimo kwani risasi za bunduki hiyo zikishafika eneo ambalo wamejificha hulipuka na kutoa risasi zingine ndogo ndogo nyingi sana ambazo kuzikwepa ni vigumu sana.
Kwa mfano fikiria mtu amejificha kwenye shimo liliopo nyuma ya mwinuko wa ardhi na kwa mazingira ya kawaida risasi haiwezi kumpata kwa kuwa mwinuko utakuwa kama kinga yake, lakini kwa kutumia bunduki hiyo mpya, risasi itapigwa kwa juu hadi kwenye sehemu ambayo shimo hilo lilipo na itakapofika juu ya shimo hilo italipuka na kutoa risasi ndogo ndogo ambazo zitaelekezwa kwenye shimo hilo.
Bunduki hizo zinatumia mfumo kama wa kompyuta kupiga mahesabu ya sehemu inayotakiwa kulengwa na risasi zake pia zina uwezo wa kupiga mahesabu zimesafiri umbali gani kabla hazijalipuka.
XM25 zimeelezewa na kampuni iliyozitengeneza ya Alliant Techsystems kwamba zitasaidia kupunguza gharama kwani badala ya kurusha bomu ambalo lingerimu maelfu ya dola, bunduki hiyo ikitumika itagharimu dola 20 tu. Bunduki Mpya ya Marekani Yenye Uwezo Kumlenga