Intelligent businessman
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 26,107
- 52,832
GiZA LAANZA KUTAWALA - 1
Matumizi ya nyaraka za vitambulisho na
umuhimu wa kushirikisha jamii katika kupambana na uhalifu.
Watu 17 walikufa ndani ya siku chache, na wengine 23 walijeruhiwa.
Oktoba 2002 wakazi wa jimbo la Washington DC na maeneo ya jirani walijikuta kwenye wakati mgumu wa
matishio ya mauaji, ikiwa ni mwaka mmoja tu tangu kulipuliwa kwa kituo cha biashara cha kimataifa mjini New York. Kila mtu hakudhani kama yupo salama. Mauaji hayo ya kufululiza yalianza asubuhi ya tarehe 2 Oktoba kwa mwanaume wa miaka 55 aliyekuwaa meegesha gari yake maeneo ya Wheaton, Meryland.
Baada ya kufanya manunuzi ndani ya
'Supermarket, James Martin alitoka nje kuelekea mahali alipoegesha gari yake. Mkewe na mtoto wake wakiume mwenye umri wa miaka 11 walikuwa wakimsubiri ndani ya gari. Lakini James Hakufika. Haikujulikana nini kimetokea, bali watu walishtukia tu mtu amedondoka huku akivuja damu nyingi kifuani. Mke wa
James alipiga kelele za kuomba msaada huku akijitahidi kupiga simu kitengo cha huduma za dharura. Haikusaidia. Dakika chache baadaye James Martin alikata roho.
Uchunguzi wa awali ulionesha James alishambuliwa kwa risasi. Mgongoni mwakwe palionekana tundu dogo ilipoingia risasi na tundu kubwa lilionekana kifuani ilipotokea risasi, hii iliashiria kwamba alishambuliwa kwa silaha yenye nguvu kubwa. Ni silaha ya kivita.
Maofisa wa polisi walijitahidi kutafuta
viashiria vya ushahidi wa uhalifu huu ikiwa ni pamoja na maganda ya risasi, lakini hawakupata chochote katika eneo lile.
Ni nani huyo aliyeamua kukatisha maisha ya James Martin, na kwanini aliamua hivyo?
Kabla swali hilo halikupata majibu, asubuhi ya saa 1:40 siku iliyofuata, yaani Oktoba 3, ugumu wa swali uliongezeka. Sunny Buchanan, kijana wa miaka 39
alianguka ghafla na kugalagala wakati akifanya kazi ya kufyeka nyasi kwa kutumia mashine ya kukatia nyasi.
Watu wa karibu walifikiri amejiumiza mwenyewe kwa mashine hiyo. La! Haikuwa hivyo, wala haikuwa ajali. Muuguzi mmoja miongoni mwawa hudumu wa dharura waliofika kumchukua Sunny alisema, hakuwahi kuona mtu akivuja damu vibaya
kama huyo tangu kazi ya kutoa huduma za dharura miaka zaidi ya kumi iliyopita.
Sunny aliuawa kwa risasi iliyotoka
kwenye silaha nzito. Na huo ulikuwa mwanzo tu wa asubuhi ya damu katika kaunti ya Montgomery –Washington DC.
Dakika chache baadaye, saa 2:07 asubuhi, taxi moja iliingia kujaza mafuta kwenye kituo kimoja cha mafuta kando ya barabara ya Connectcut, kilometa takribani 8 kutoka alipouawa Sunny. Mwanamke mmoja kwa jina Caroline naye alikuwa amefika kabla
ya taxi hiyo. Wakati akiweka mafuta, taxi ilikuwa ikisubiri amalize. Ghafla, mlio wa bunduki ukasiskika.
Caroline alipagawa kidogo, lakini alipotazama huku na kule, alimuona dereva wa taxi ile iliyoegeshwa nyuma yake akiwa anatapatapa nyuma ya usukani. Damu nyingi ilikuwa imetapakaa kwenye vioo vya taxi ile. Nini kinaendelea?
Watu wawili walikuwa wameuawa kwa risasi yenyebnguvu ndani ya dakika 31 tu, umbali wa kilometa nane kutoka tukio moja hadi lingine. Na bado haikutosha. Dakika chache baadaye, muuaji alifanya tena kazi yake. Sarah Ramos alikuwa akisubiri usafiri nje ya
makazi ya watu mashuhuri mahali palipoitwa Leisure World. Mwanafunzi huyu wa sheria aliingia Marekani akitokea El Salvadol. Akiwa mwanafunzi wa sheria,
aliamua kufanya kazi za usafi wa ndani ili apate kipato cha kumsaidia kuunganisha siku. Sarah hakujua, si yeye bali roho yake ndiyo ilikuwa ikisubiri safari pale Leisure World. Safari hii hakukusikika mlio
wa bunduki, lakini mashushuda walishtukia mtu amedondoka huku akivuja damu nyingi kichwani na shingoni. Risasi ya kaliba 223 ililengwa kwa Sarah Ramos, ikatoboa paji la uso na kutokea eneo la nyuma ya kichogo, ikapiga kwenye ukuta wa mgahawa uliokuwa karibu na marehemu, ikadondoka sakafuni.
Idara ya dharura ya Montgomery ilikuwa
bize siku hiyo, lakini waliokusudiwa na muuaji wote waliaga dunia. Na bado haikutosha.
Asubuhi hiyohiyo, Lori Luis Rivera alikuwa akifuta vumbi kwenye gari yake eneo la kituo kimoja cha mafuta. Naye alikufa papohapo baada ya kushambuliwa kwa risasi kutoka kwa muuaji asiyeonekana.
Matukio yote matano ya mauaji
yalitokea ndani ya eneo la kilometa za mraba 25 tu, sawa na eneo la upana wa kilometa 5 na urefu wa kilometa 5. Yawezekana pia muuaji aliwashambulia
watu wengine lakini aliwakosa – kutokana na taarifa za kuonekana alama za matundu yaliyosababishwa na risasi kwenye kuta za baadhi ya majengo.
Mauji yote yametokea maeneo ya wazi yanayotumiwa na watu wote. Hakuna misitu mikubwa, hakuna milima, hakuna eneo la kujificha. Huyu muuaji alikuwa wapi?
Maofisa wa upelelezi wasio na sare
walimwagwa kwenye maeneo yote ya matukio ya mauaji kujaribu kupata taarifa zinazoweza kusaidia. Taarifa moja iliyopatikana kutoka kwa shuhuda wa eneo la Leisure World alipouawa Sarah Ramos, ilihusu gari moja jeupe lenye bodi
iliyofunikwa pande zote. Ni gari ambalo
liliondoka ghafla baada ya Sarah kuanguka chini na kuvuja damu. Lakini magari ya aina hiyo yalikuwa mengi ndani ya kaunti ya Montgomery na shushuda hakuweza kukariri namba za gari aliyoiona.
Miili mitano ya marehemu ilichunguzwa kwa umakini. Maofisa wa polisi walitaka kujua asili ya majeraha waliokuwa nayo marehemu – ili wapate picha ya mahali muuaji alipokuwa.
Je! Mdunguaji alishambulia kutoka juu ghorofani, au akiwa ardhini?
Wakati maofisa hao wakikuna vichwa kutafuta majibu ya maswali yao, huku
wakisubiri majibu ya uchunguzi wa kitabibu
muuaji aliwarudisha tena kwenye mshtuko.
Baada ya kuwa ameshambulia asubuhi, mchana alipumzika. Ilipofika usiku muuaji alimuua Pascal Shalom, muhamiaji kutoka Haiti aliyekuwa akivuka barabara eneo la mpaka wa kaunti ya Montgomery.
Asubuhi ya tarehe 4 wakazi wa kaunti ya
Montgomery na jimbo lote la Washington DC waliamka wakiwa na mtazamo mpya. Maisha ya kila mtu yalionekana kuwa hatarini kwani muuaji hakuchagua rika, rangi wala jinsia katika malengo yake.
Miongoni mwa watu sita walio uawa ndani ya masaa48 walikuwamo wanaume, mwanamke mmoja na mtoto, tena watu hao walikuwa wa matabaka tofauti; wazungu kwa weusi.
Muuaji hakuchagua wa kumuua.
Uchunguzi wa majeraha kwenye miili ya marehemu sasa ulitoa majibu kadhaa. Majeraha yote yalitokana na risasi yenye nguvu iliyorushwa kwa bunduki ya kivita inayotumika kwa udunguaji kutoka mbali.
Yawezekana ni bunduki aina ya Bushmaster. Ni bunduki yenye nguvu kubwa inayoweza kurusha risasi itakayoharibu eneo kubwa la ndani ya mwili ingawa inapoingia huacha katundu kadogo.Taasisi ya taifa ya kuratibu Pombe, Tumbaku na Silaha za Moto ilifanya uchunguzi wake na kugundua kuwa muuaji hakulenga risasi kutoka sehemu ya juu bali usawa wa ardhini. Maana yake, muuaji hakuwa juu ya ghorofa, au juu ya mti, bali alilenga kutoka chini.
Uchunguzi huu hufanywa kwa kutazama majeraha ya wahanga, namna jeraha la
kuingia risasi inavyohusiana na jereha la kutoka kwa risasi. Ikiwa muuaji alikuwa juu ghorofani, bila shaka jeraha la kuingia risasi litakuwa sehemu ya juu ya mwili kuliko
jeraha la kutoka risasi. Lakini kama majeraha yote mawili yapo kwenye usawa au yanakaribiana usawa basi ni wazi muuaji alikuwa ardhini.
Alikuwa wapi? Alikuwa anajificha wapi?
Kutokana na taarifa hiyo, na kwa namna matukio yalivyotokea maeneo tofauti ndani ya muda mfupi, maofisa wa upelelezi waliamini muuaji anatumia usafiri wa gari.
Matumizi ya nyaraka za vitambulisho na
umuhimu wa kushirikisha jamii katika kupambana na uhalifu.
Watu 17 walikufa ndani ya siku chache, na wengine 23 walijeruhiwa.
Oktoba 2002 wakazi wa jimbo la Washington DC na maeneo ya jirani walijikuta kwenye wakati mgumu wa
matishio ya mauaji, ikiwa ni mwaka mmoja tu tangu kulipuliwa kwa kituo cha biashara cha kimataifa mjini New York. Kila mtu hakudhani kama yupo salama. Mauaji hayo ya kufululiza yalianza asubuhi ya tarehe 2 Oktoba kwa mwanaume wa miaka 55 aliyekuwaa meegesha gari yake maeneo ya Wheaton, Meryland.
Baada ya kufanya manunuzi ndani ya
'Supermarket, James Martin alitoka nje kuelekea mahali alipoegesha gari yake. Mkewe na mtoto wake wakiume mwenye umri wa miaka 11 walikuwa wakimsubiri ndani ya gari. Lakini James Hakufika. Haikujulikana nini kimetokea, bali watu walishtukia tu mtu amedondoka huku akivuja damu nyingi kifuani. Mke wa
James alipiga kelele za kuomba msaada huku akijitahidi kupiga simu kitengo cha huduma za dharura. Haikusaidia. Dakika chache baadaye James Martin alikata roho.
Uchunguzi wa awali ulionesha James alishambuliwa kwa risasi. Mgongoni mwakwe palionekana tundu dogo ilipoingia risasi na tundu kubwa lilionekana kifuani ilipotokea risasi, hii iliashiria kwamba alishambuliwa kwa silaha yenye nguvu kubwa. Ni silaha ya kivita.
Maofisa wa polisi walijitahidi kutafuta
viashiria vya ushahidi wa uhalifu huu ikiwa ni pamoja na maganda ya risasi, lakini hawakupata chochote katika eneo lile.
Ni nani huyo aliyeamua kukatisha maisha ya James Martin, na kwanini aliamua hivyo?
Kabla swali hilo halikupata majibu, asubuhi ya saa 1:40 siku iliyofuata, yaani Oktoba 3, ugumu wa swali uliongezeka. Sunny Buchanan, kijana wa miaka 39
alianguka ghafla na kugalagala wakati akifanya kazi ya kufyeka nyasi kwa kutumia mashine ya kukatia nyasi.
Watu wa karibu walifikiri amejiumiza mwenyewe kwa mashine hiyo. La! Haikuwa hivyo, wala haikuwa ajali. Muuguzi mmoja miongoni mwawa hudumu wa dharura waliofika kumchukua Sunny alisema, hakuwahi kuona mtu akivuja damu vibaya
kama huyo tangu kazi ya kutoa huduma za dharura miaka zaidi ya kumi iliyopita.
Sunny aliuawa kwa risasi iliyotoka
kwenye silaha nzito. Na huo ulikuwa mwanzo tu wa asubuhi ya damu katika kaunti ya Montgomery –Washington DC.
Dakika chache baadaye, saa 2:07 asubuhi, taxi moja iliingia kujaza mafuta kwenye kituo kimoja cha mafuta kando ya barabara ya Connectcut, kilometa takribani 8 kutoka alipouawa Sunny. Mwanamke mmoja kwa jina Caroline naye alikuwa amefika kabla
ya taxi hiyo. Wakati akiweka mafuta, taxi ilikuwa ikisubiri amalize. Ghafla, mlio wa bunduki ukasiskika.
Caroline alipagawa kidogo, lakini alipotazama huku na kule, alimuona dereva wa taxi ile iliyoegeshwa nyuma yake akiwa anatapatapa nyuma ya usukani. Damu nyingi ilikuwa imetapakaa kwenye vioo vya taxi ile. Nini kinaendelea?
Watu wawili walikuwa wameuawa kwa risasi yenyebnguvu ndani ya dakika 31 tu, umbali wa kilometa nane kutoka tukio moja hadi lingine. Na bado haikutosha. Dakika chache baadaye, muuaji alifanya tena kazi yake. Sarah Ramos alikuwa akisubiri usafiri nje ya
makazi ya watu mashuhuri mahali palipoitwa Leisure World. Mwanafunzi huyu wa sheria aliingia Marekani akitokea El Salvadol. Akiwa mwanafunzi wa sheria,
aliamua kufanya kazi za usafi wa ndani ili apate kipato cha kumsaidia kuunganisha siku. Sarah hakujua, si yeye bali roho yake ndiyo ilikuwa ikisubiri safari pale Leisure World. Safari hii hakukusikika mlio
wa bunduki, lakini mashushuda walishtukia mtu amedondoka huku akivuja damu nyingi kichwani na shingoni. Risasi ya kaliba 223 ililengwa kwa Sarah Ramos, ikatoboa paji la uso na kutokea eneo la nyuma ya kichogo, ikapiga kwenye ukuta wa mgahawa uliokuwa karibu na marehemu, ikadondoka sakafuni.
Idara ya dharura ya Montgomery ilikuwa
bize siku hiyo, lakini waliokusudiwa na muuaji wote waliaga dunia. Na bado haikutosha.
Asubuhi hiyohiyo, Lori Luis Rivera alikuwa akifuta vumbi kwenye gari yake eneo la kituo kimoja cha mafuta. Naye alikufa papohapo baada ya kushambuliwa kwa risasi kutoka kwa muuaji asiyeonekana.
Matukio yote matano ya mauaji
yalitokea ndani ya eneo la kilometa za mraba 25 tu, sawa na eneo la upana wa kilometa 5 na urefu wa kilometa 5. Yawezekana pia muuaji aliwashambulia
watu wengine lakini aliwakosa – kutokana na taarifa za kuonekana alama za matundu yaliyosababishwa na risasi kwenye kuta za baadhi ya majengo.
Mauji yote yametokea maeneo ya wazi yanayotumiwa na watu wote. Hakuna misitu mikubwa, hakuna milima, hakuna eneo la kujificha. Huyu muuaji alikuwa wapi?
Maofisa wa upelelezi wasio na sare
walimwagwa kwenye maeneo yote ya matukio ya mauaji kujaribu kupata taarifa zinazoweza kusaidia. Taarifa moja iliyopatikana kutoka kwa shuhuda wa eneo la Leisure World alipouawa Sarah Ramos, ilihusu gari moja jeupe lenye bodi
iliyofunikwa pande zote. Ni gari ambalo
liliondoka ghafla baada ya Sarah kuanguka chini na kuvuja damu. Lakini magari ya aina hiyo yalikuwa mengi ndani ya kaunti ya Montgomery na shushuda hakuweza kukariri namba za gari aliyoiona.
Miili mitano ya marehemu ilichunguzwa kwa umakini. Maofisa wa polisi walitaka kujua asili ya majeraha waliokuwa nayo marehemu – ili wapate picha ya mahali muuaji alipokuwa.
Je! Mdunguaji alishambulia kutoka juu ghorofani, au akiwa ardhini?
Wakati maofisa hao wakikuna vichwa kutafuta majibu ya maswali yao, huku
wakisubiri majibu ya uchunguzi wa kitabibu
muuaji aliwarudisha tena kwenye mshtuko.
Baada ya kuwa ameshambulia asubuhi, mchana alipumzika. Ilipofika usiku muuaji alimuua Pascal Shalom, muhamiaji kutoka Haiti aliyekuwa akivuka barabara eneo la mpaka wa kaunti ya Montgomery.
Asubuhi ya tarehe 4 wakazi wa kaunti ya
Montgomery na jimbo lote la Washington DC waliamka wakiwa na mtazamo mpya. Maisha ya kila mtu yalionekana kuwa hatarini kwani muuaji hakuchagua rika, rangi wala jinsia katika malengo yake.
Miongoni mwa watu sita walio uawa ndani ya masaa48 walikuwamo wanaume, mwanamke mmoja na mtoto, tena watu hao walikuwa wa matabaka tofauti; wazungu kwa weusi.
Muuaji hakuchagua wa kumuua.
Uchunguzi wa majeraha kwenye miili ya marehemu sasa ulitoa majibu kadhaa. Majeraha yote yalitokana na risasi yenye nguvu iliyorushwa kwa bunduki ya kivita inayotumika kwa udunguaji kutoka mbali.
Yawezekana ni bunduki aina ya Bushmaster. Ni bunduki yenye nguvu kubwa inayoweza kurusha risasi itakayoharibu eneo kubwa la ndani ya mwili ingawa inapoingia huacha katundu kadogo.Taasisi ya taifa ya kuratibu Pombe, Tumbaku na Silaha za Moto ilifanya uchunguzi wake na kugundua kuwa muuaji hakulenga risasi kutoka sehemu ya juu bali usawa wa ardhini. Maana yake, muuaji hakuwa juu ya ghorofa, au juu ya mti, bali alilenga kutoka chini.
Uchunguzi huu hufanywa kwa kutazama majeraha ya wahanga, namna jeraha la
kuingia risasi inavyohusiana na jereha la kutoka kwa risasi. Ikiwa muuaji alikuwa juu ghorofani, bila shaka jeraha la kuingia risasi litakuwa sehemu ya juu ya mwili kuliko
jeraha la kutoka risasi. Lakini kama majeraha yote mawili yapo kwenye usawa au yanakaribiana usawa basi ni wazi muuaji alikuwa ardhini.
Alikuwa wapi? Alikuwa anajificha wapi?
Kutokana na taarifa hiyo, na kwa namna matukio yalivyotokea maeneo tofauti ndani ya muda mfupi, maofisa wa upelelezi waliamini muuaji anatumia usafiri wa gari.