Wandugu naomba mnivumilie lakini nina hoja ya kuijadili. Kwa muda mrefu tumekuwa tukisikia kashfa na tuhuma mbali mbali dhidi ya viongozi wetu na hata wafanya biashara maarufu nchini wakihusishwa na tuhuma au shutuma mbalimbali za kukosa uadilifu na uhujumu uchumi. Kupitia taarifa hizi, wako ambao wamelazimika kuwajibika na wachache kufikishwa mahakamani. Kupitia taarifa hizi, tumeweza hata sisi kutoa michango yetu kupitia kwenye majukwaa mbalimbali likiwemo hili maarufu la JF. Lakini tumewahi kujiuliza uhuru huu wa kuhoji, kushutumu na kushambulia maovu umetokana na nini na umeanza lini.
Kwa ufahamu wangu hli hii imejitokeza kwa upana huu tunaoufurahia baada ya serikali ya awamu ya nne kuingia madarakani na ni matunda ya juhudi binafsi za JK. Katika awamu iliyopita haya yanayojitokeza leo yalikuwepo, tena kwa kiasi cha kutisha lakini tuliyajua kwa undani na ufasaha baada ya awamu hiyo kuondoka. Katika tawala za kidhalimu huko kwa wenzetu, uhuru huu kwa vyombo vya habari na watu binafsi ni ndoto na hata hapa tumeshuhudia watu wakiadhibiwa kiasi hata cha kunyang'anywa uraia kwa kusema kile walichoamini kwamba ni sahihi. Huko nje hali ni mbaya zaidi kwani wapo wanaopoteza maisha wakiusotoea uhuru huu. Hatutaki hilo litokee hapa na nina uhakika halitatokea maana kama ni kutokea lingeshatokea kwani uhuru huo umefikia hata kushambulia maisha binafsi ya rais na familia yake lakini mambo shwari tu.
Mimi ninavyoamini hili ni matunda ya uvumilivu binafsi wa JK na ni vizuri katika hili tumpe sifa yake, maana kama inafikia kwamba hata mafisadi nao wanapata fursa ya kuongea wakati sasa hivi walitakiwa kuwa wameshalala kule segerea au ukonga, basi hakuna fursa kubwa kuliko hiyo. Waswahili wanasema ukimsifia baba yako kwamba anakimbia sana basi umsifie na yule aliyemkimbiza! Naomba kutoa hoja na samahani kwa wale watakaokwazika.
Kwa ufahamu wangu hli hii imejitokeza kwa upana huu tunaoufurahia baada ya serikali ya awamu ya nne kuingia madarakani na ni matunda ya juhudi binafsi za JK. Katika awamu iliyopita haya yanayojitokeza leo yalikuwepo, tena kwa kiasi cha kutisha lakini tuliyajua kwa undani na ufasaha baada ya awamu hiyo kuondoka. Katika tawala za kidhalimu huko kwa wenzetu, uhuru huu kwa vyombo vya habari na watu binafsi ni ndoto na hata hapa tumeshuhudia watu wakiadhibiwa kiasi hata cha kunyang'anywa uraia kwa kusema kile walichoamini kwamba ni sahihi. Huko nje hali ni mbaya zaidi kwani wapo wanaopoteza maisha wakiusotoea uhuru huu. Hatutaki hilo litokee hapa na nina uhakika halitatokea maana kama ni kutokea lingeshatokea kwani uhuru huo umefikia hata kushambulia maisha binafsi ya rais na familia yake lakini mambo shwari tu.
Mimi ninavyoamini hili ni matunda ya uvumilivu binafsi wa JK na ni vizuri katika hili tumpe sifa yake, maana kama inafikia kwamba hata mafisadi nao wanapata fursa ya kuongea wakati sasa hivi walitakiwa kuwa wameshalala kule segerea au ukonga, basi hakuna fursa kubwa kuliko hiyo. Waswahili wanasema ukimsifia baba yako kwamba anakimbia sana basi umsifie na yule aliyemkimbiza! Naomba kutoa hoja na samahani kwa wale watakaokwazika.