Waziri Jerry Silaa unastahili pongezi kwa ubunifu huu!

MTAZAMO

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
19,643
33,433
Kwa niaba yangu binafsi na wana Bunju tunashukuru mno kwa kambi uliyoweka zaidi ya wiki kutatua migogoro ya ardhi na kubwa zaidi ni kubeba timu zima kuhakikisha wananchi wana rasimisha ardhi zao.

Huu ndio ubunifu tunaotamani viongozi wawe nao badala ya kushinda ofisini. Umekuwa mnyenyekevu sana kusikiliza na kutatua changamoto instantly inapowezekana na pia timu yako uliyoambatana nayo imefanya kazi kubwa sana hadi muda wa ziada ili watu warasimishe ardhi zao.

Kupitia zoezi hili zuri nashauri ungeunda kamati makini kila wilaya ziweke kambi ya wiki moja kwa mfumo huu uliofanya Bunju. Matatizo mengi yatatatuliwa na pia wengi watapata hati zao kwa wakati na gharama nafuu.

Nashauri hilo zoezi kila wilaya liwe chini ya wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri na iitwe wiki ya ardhi. Muda utakuwa mdogo lakini matatizo mengi yatapunguzwa.

Mh. Waziri Silaa tunakushukuru sana kwa kazi hii ya mfano huku Bunju na umeacha alama muhimu sana kwetu, Leo ni jumapili lakini upo na wana Bunju kuhitimisha zoezi hili.
Asante sana
 
Hili kwakweli nampongeza, Wengi sana wanaonewa wakifuata sheria, Pesa inawatoa kapa..

Ila kuhusu kutuma watu kuweka kambi, ni nzuri, tatizo tutarudi kule kulee kwenye kuhonga.
 
Maeneo ya Boko kuna nyumba 10+ za wananchi zimezungushiwa ukuta wa matofali na mhe Ridhiwan Kikwete na kuwataka wahame mara moja, akidai ni eneo lake. Mhe. Jerry Slaa amepita na maeneo hayo?
Hahaaaaaa hapo sasa unamfunga kisu cha sime mwenzio shingoni.
 
Aweke mfumo mzuri wa upatikanaji hati kwa wakati,hizo kambi ziwe kwa ajili ya migogoro labda.

Toka 2020 watu tunasubiri hati kama NIDA IDs, kama shida ni rasilimali watu si waajiri!
 
Kupitia zoezi hili zuri nashauri ungeunda kamati makini kila wilaya ziweke kambi ya wiki moja kwa mfumo huu uliofanya Bunju. Matatizo mengi yatatatuliwa na pia wengi watapata hati zao kwa wakati na gharama nafuu.
Kuna tulioporwa ardhi tunaomba afungue dirisha la kupokelea malalamiko maana siyo wote wenye kumfuata Dodoma
 
Labda afukuze hao maafisa ardhi maana asilimia kubwa ndio watengeneza migogoro kisha aajiri wengine
 
Kwa niaba yangu binafsi na wana Bunju tunashukuru mno kwa kambi uliyoweka zaidi ya wiki kutatua migogoro ya ardhi na kubwa zaidi ni kubeba timu zima kuhakikisha wananchi wana rasimisha ardhi zao.

Huu ndio ubunifu tunaotamani viongozi wawe nao badala ya kushinda ofisini. Umekuwa mnyenyekevu sana kusikiliza na kutatua changamoto instantly inapowezekana na pia timu yako uliyoambatana nayo imefanya kazi kubwa sana hadi muda wa ziada ili watu warasimishe ardhi zao.

Kupitia zoezi hili zuri nashauri ungeunda kamati makini kila wilaya ziweke kambi ya wiki moja kwa mfumo huu uliofanya Bunju. Matatizo mengi yatatatuliwa na pia wengi watapata hati zao kwa wakati na gharama nafuu.

Nashauri hilo zoezi kila wilaya liwe chini ya wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri na iitwe wiki ya ardhi. Muda utakuwa mdogo lakini matatizo mengi yatapunguzwa.

Mh. Waziri Silaa tunakushukuru sana kwa kazi hii ya mfano huku Bunju na umeacha alama muhimu sana kwetu, Leo ni jumapili lakini upo na wana Bunju kuhitimisha zoezi hili.
Asante sana
Is that sustainable? and what if I refuse to come to that committee and resort to seek court justice?
 
Back
Top Bottom